Kauli ya mwisho ya marehemu rafiki yangu ilikuwa tusi la nguoni. Je, ataenda mbinguni?

Kauli ya mwisho ya marehemu rafiki yangu ilikuwa tusi la nguoni. Je, ataenda mbinguni?

Mtu hunena yaujazao moyo wake maanake yeye matusi ndio yaliyomjaa hata kama asingetamka lakini moyoni mwake yalikuepo hivyo atahukumiwa katika hayo

Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.

Wakolosai 3:8
Waliambiwa Wakolosai, huyo Mmakonde wa Nanjilinji vinamhusu nini?
 
Mithali 26
4 Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Usije ukafanana naye.

5 Umjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake; Asije akawa mwenye hekima machoni pake.

Unataka nikujibu?
🤣🤣🤣🆗
 
Alizan utan , hiii migari mikubwa ya kuheshmu sana
 
Dhambi maana yake ni tendo baya ambalo mtu hufanya kwa kujua ni tendo baya, na anaamua kulifanya kweli. Dhambi Ina vipengele vitatu: kukusaidia, kuamua na kufanya/tenda. Katika mahusiano dhambi hutokea kama wahusika wanalenga kutumiana (exploitation of each other). Kumbuka hapo juu nimesema (dhambi ina madhara kwa mtu mwenyewe, mtu mwingine au jamii). Katika mahusiano ambayo wahusika hawana intention ya kuwa pamoja maisha yao yote, dhambi hutokea kwa sababu wanajihusisha kwenye mahusiano yasiyo ya kweli/yasiyo na kibali machoni pa Mungu/ya kudanganyana na kutumiana kama vyombo vya anasa (fornication, adultery). Kuna athari kwa wahusika na kwa jamii (yaani kutumia viungo vya wahusika kinyume na makusudio yake). Ni kama mtu asiye na madaraka/mamlaka ya kufanya jambo fulani alifanye kama mwenye madaraka/mamlaka nalo. Anayefanya hivyo anatenda kosa (hata kama kufanya hivyo kunamfurahisha au kunawafurahisha baadhi ya watu au hata watu wote maana if one person can make a wrong, even all people can do so). Lazima tujifunze kufanya mambo ambayo tuko authorised/tuna kibali nayo na tukifanya hivi tunafanya ndani ya utaratibu. Kufanya mambo nje ya utaratibu hata kama kufanya hivyo kunamfurahisha mtu, kuna matokeo hasi kwetu wenyewe au kwa watu wengine. Lazima kwenye mahusiano tuji'envolve' kwenye 'genuine relationships' (mahusiano yenye kibali machoni pa Mungu). Hapo tutakuwa tumeepuka dhambi. Hivyo, kabla ya kufanya jambo lolote tujiulize: je, jambo hili lina kibali machoni pa Mungu? Kama jibu ni ndiyo endelea nalo, na kama jibu ni hapana, achana nalo.
Asante sana mkuu, lakini naomba nikuulize kitu, kama mimi na mwenza tumeamua kufurahisha miili yetu na wala hatuna mpango wa mahusiano na kila mmoja wetu analijua hilo sasa hapo dhambi inatoka wapi kwani hakuna anayemdanganya mwenzie, ni kama mtu anapoamua kutoka na malaya, malaya anataka pesa mnunuzi anataka pesa na kila mmoja anaridhia, je hapo pia pana dhambi?
 
Kumama#o ukute alikuwa analitukana lori na wala sio dereva wake 😂😂😂
 
Asante sana mkuu, lakini naomba nikuulize kitu, kama mimi na mwenza tumeamua kufurahisha miili yetu na wala hatuna mpango wa mahusiano na kila mmoja wetu analijua hilo sasa hapo dhambi inatoka wapi kwani hakuna anayemdanganya mwenzie, ni kama mtu anapoamua kutoka na malaya, malaya anataka pesa mnunuzi anataka pesa na kila mmoja anaridhia, je hapo pia pana dhambi?
Tunapoongelea dhambi tunaingia kwenye maadili (moral responsibility). Kuna kufanya jambo morally au immorally. Kufanya jambo morally ni pale unapofanya hilo jambo katika standards zinazokubalika na "jamii" (na hapa jamii inaweza kuwa religious au secular). Kufanya mambo immorally ni pale usipojali matokeo yake. Kwa mfano, ukitoka na malaya na akashika mimba sidhani kama utakubali kuwa baba mzazi wa mtoto atakayezaliwa na kumchukulia mzazi mwenza kama mke wako na mama wa mtoto huyo atakayezaliwa. Sidhani pia akipata shida kutokana na mahusiano yenu utakuwa pamoja naye beneti. Kama huwezi kufanya hivyo, tambua kwamba mahusiano yenu hayana uwajibikaji, bali kutumiana (exploiting each other). Na kufanya hivi hakuna kibali machoni pa Mungu na machoni pa jamii na hiyo ni dhambi. Kumbuka hapo juu (post ya awali) nilisema dhambi ina madhara kwa mhusika au kwa jamii.
 
Kwa Waislam, hukumu zetu ni Allah ajuwaye, hakuna binadam ajuwaye. Wajibu wetu ni kufanya toba.
Yesu asema, Mimi ndimi njia Kweli na Uzima.

Hakikisha TOBA inapita kwake.

Bila kufanya hivyo, mbingu mtaishia kuisikia tu ndugu Islams!!
 
(Soma ufunuo 21:8) watukanao wako kwenye kundi la " wachukizao", destiny Yao ni kuzimu kwenye gereza la muda, Kisha JEHANUM milele na milele.

Ikiwa hujampa Yesu maisha Yako fuatisha Sala hii,

EE MUNGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO, NINAKUKIRI WEWE KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU, ULIANDIKE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA UZIMA, NIPE UWEZO WA KUISHI MAISHA MATAKATIFU, DHAMBI ISINISHINDE, UOVU USINISHINDE, ULEVI USINISHINDE, NINAOMBA HAYO KUPITIA JINA LA YESU KRISTO ALIYE BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YANGU. AAMEN
 
Yesu asema, Mimi ndimi njia Kweli na Uzima.

Hakikisha TOBA inapita kwake.

Bila kufanya hivyo, mbingu mtaishia kuisikia tu ndugu Islams!!
Hajakosea, kabisa. Ukimfata yeye unakuwa Muislam, ndiyo kazi ya mitume yote, ndiyo njia zetu wao.

hayo mengine ni porojo zako gtu, yeye mwenyewe alikuwa anamuonba Mwenyezi Mungu wake na wako. Au umezisahau aya nikukumbushe?
 
Hajakosea, kabisa. Ukimfata yeye unakuwa Muislam, ndiyo kazi ya mitume yote, ndiyo njia zetu wao.

hayo mengine ni porojo zako gtu, yeye mwenyewe alikuwa anamuonba Mwenyezi Mungu wake na wako. Au umezisahau aya nikukumbushe?
Hizo uziitazo porojo achana nazo.

Yesu ndiye njia pekee kweli na Uzima, ukimwamini ,njia Yako kwenda Mbinguni ni guaranteed.

Yesu alikuja duniani Kwa Kila kiumbe, Islam, Pagani,Myunani, myahudi, mjaluo, mwarabu, msambaa, nk nk

Ubarikiwe 🙏
 
Mwaka jana rafiki yangu akiwa amepakiza familia yake kwenye gari binafsi alipata ajali ba kufariki hapohapo.

Kwa ufupi ni kwamba kuna lori lilifeli break likawa linakuja kasi upande wake yeye akidhani ni mbwembwe za dereva wa lori

Lori lilipomkaribia akatoa tusi ile anamalizia herufi o tu, lori likamgonga upande wake na kufariki hapohapo.

Mimi sikuwepo nilihadithiwa na waliokuwemo kwenye gari.

Sasa wale wafia dini huyu mtu siku ya kiana atakuwa upande upi?

Ni amri ipi ya Mungu inasema usitukane?
Hukumu ni za Mungu
 
Hizo uziitazo porojo achana nazo.

Yesu ndiye njia pekee kweli na Uzima, usimwamini ,njia Yako kwenda Mbinguni ni guaranteed.

Yesu alikuja duniani Kwa Kila kiumbe, Islam, Pagani,Myunani, myahudi, mjaluo, mwarabu, msamaha, nk nk

Ubarikiwe 🙏
Mbona unapingana na Yesu na Biblia?

Mathayo 15:24 Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.”


Tukuamini wewe au Yesu wa kwenye Biblia?
 
Ila honestly hivi vitu tunafundishwa sio poa.....

Muda si mrefu kijana wangu kaja ananiambia "mama siku ya mwisho ya kiama watu wote tutasimama kutakua na moto, ambae haji moto utamfata na hapo tutasimama kwa miaka elf tano"

nikamjibu tu "mwanangu nenda kaoge sasa"

Ni nini hiki lakini
Hofu ndiyo mtaji mkubwa wa dini..
Mtoto mdogo tayari ana 'nightmares' badala ya kufurahia dunia na kuwa na natumaini na future.
 
Mwaka jana rafiki yangu akiwa amepakiza familia yake kwenye gari binafsi alipata ajali ba kufariki hapohapo.

Kwa ufupi ni kwamba kuna lori lilifeli break likawa linakuja kasi upande wake yeye akidhani ni mbwembwe za dereva wa lori

Lori lilipomkaribia akatoa tusi ile anamalizia herufi o tu, lori likamgonga upande wake na kufariki hapohapo.

Mimi sikuwepo nilihadithiwa na waliokuwemo kwenye gari.

Sasa wale wafia dini huyu mtu siku ya kiana atakuwa upande upi?

Ni amri ipi ya Mungu inasema usitukane?
Kwamba alisema kumam.ako...!
Manake angesema mkyu...nd u Ingeishia na u
 
Mbona unapingana na Yesu na Biblia?

Mathayo 15:24 Yesu akajibu, “Sikutumwa ila kwa watu wa Israeli waliopotea kama kondoo.”


Tukuamini wewe au Yesu wa kwenye Biblia?
(Mark 16:15-16)

Yesu huyo huyo asema " Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri INJILI Kwa Kila kiumbe.

Aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa.

BIBLIA haijipingi, usikubali kuzeeka na Ujinga. Kibali kuomba ufundishwe Ili uelewe.

Yesu alikuja Kwa ajili ya Ulimwengu mzima.

Waislamu msipomwamini Yesu, njia pekee ya Uzima, mtaenda kuzimu, Kisha JEHANUM direct.

Aamen!!
 
(Mark 16:15-16)

Yesu huyo huyo asema " Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri INJILI Kwa Kila kiumbe.

Aaminiye na kubatizwa ataokoka, asiyeamini atahukumiwa.

BIBLIA haijipingi, usikubali kuzeeka na Ujinga. Kibali kuomba ufundishwe Ili uelewe.

Yesu alikuja Kwa ajili ya Ulimwengu mzima.

Waislamu msipomwamini Yesu, njia pekee ya Uzima, mtaenda kuzimu, Kisha JEHANUM direct.

Aamen!!
Wacha porojo, nishike maneno yako niwache ya Biblia?

Tena hapo ndiyo umejibamiza kabisa.

Injili ipi hiyo manyoisambaza?


Hapo Sasa.
 
Tunapoongelea dhambi tunaingia kwenye maadili (moral responsibility). Kuna kufanya jambo morally au immorally. Kufanya jambo morally ni pale unapofanya hilo jambo katika standards zinazokubalika na "jamii" (na hapa jamii inaweza kuwa religious au secular). Kufanya mambo immorally ni pale usipojali matokeo yake. Kwa mfano, ukitoka na malaya na akashika mimba sidhani kama utakubali kuwa baba mzazi wa mtoto atakayezaliwa na kumchukulia mzazi mwenza kama mke wako na mama wa mtoto huyo atakayezaliwa. Sidhani pia akipata shida kutokana na mahusiano yenu utakuwa pamoja naye beneti. Kama huwezi kufanya hivyo, tambua kwamba mahusiano yenu hayana uwajibikaji, bali kutumiana (exploiting each other). Na kufanya hivi hakuna kibali machoni pa Mungu na machoni pa jamii na hiyo ni dhambi. Kumbuka hapo juu (post ya awali) nilisema dhambi ina madhara kwa mhusika au kwa jamii.
Mkuu mimi nadhani kusema dhambi moja kwa moja tunazungumzia swala la imani, na tukisema maadili hapo tunakuwa tunahusisha jamii. Mfano, kumtamani mwanamke ni dhambi (kwa wakristo) hata kama umemtamani kimya kimya pasi jamii kujua. So hapo hakuna madhara kwa jamii. Kutompisha mtu mzima sit akae siyo maadili mazuri kwa jamii lakini siyo dhambi. Sijui nimeeleweka
 
Mkuu mimi nadhani kusema dhambi moja kwa moja tunazungumzia swala la imani, na tukisema maadili hapo tunakuwa tunahusisha jamii. Mfano, kumtamani mwanamke ni dhambi (kwa wakristo) hata kama umemtamani kimya kimya pasi jamii kujua. So hapo hakuna madhara kwa jamii. Kutompisha mtu mzima sit akae siyo maadili mazuri kwa jamii lakini siyo dhambi. Sijui nimeeleweka
Hapa nimechukulia tusi lililotolewa na mtu ambaye aliona gari linaacha njia yake na kumfuata aliko na kisha kumhonga na kumuua. Mleta hii mada alisema alimsikia alitoa tusi ambalo after all limezoeleka sana na wakati mwingine hata kupoteza maana tusi na kuwa tu 'loose expression'. Mimi nikasema mlengwa hakusikia (hakuna madhara) na hata kuangalia tusi lenyewe huenda hata siyo tusi kwa maana halisi ya tusi. Tusi ni pale mtu anapolenga kuumiza feelings za mtu mwingine au kumshushia heshima. Unapomuumiza feelings za mtu au kumshushia heshima unamuathiri huyo mtu na kwa vile unafanya kwa makusudi (maana ungeweza kujizuia) unakuwa umetenda dhambi (umeharibu uhusiano wako na Mungu na mtu mwenzako).
 
Back
Top Bottom