Uchaguzi 2020 Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kusema Wagombea wa Upinzani wasiwachafue wagombea wa chama tawala una lengo la kutaka kuwatisha

Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Mi mwenyewe ni pro-Magufuli na obviously nitampigia kura come October.

Linapokuja suala la campaign wacha vyama vimseme na "vimchafue" Magufuli maana huu ndo mda wake.

Tatizo watawala wa nchi hii ni thin-skinned, wamezoea kusifiwa na kupongezwa kiasi kwamba any slight criticism kwao wanaiona ni tusi.

Maana ya kujenga nchi imara na inayojitambua ni pamoja na kuwaachia watanzania wenyewe wachuje pumba na mchele. CCM tangi 2015 mnajipigia campaign waziwazi, mnashindwa nini kuvumilia wenzenu kupiga campaign kwa namna zao? Mambo aliyoyafanya Magu hayatoshi kumuuza?
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Lisu anaongea facts
Jiwe ndio anatoaga màtusi majukwaani..
Acheni vitisho
 
Kassim Majaliwa anaelewa ni nini maana ya kampeni?
Kampeni ni kuongea sera zako sio mtu. Ndio Maana media hazitaki kutangaza vitu vyake upinzani haeaongelei sera wanaongelea Watu
 
Hivi yale maneno ya boss mkubwa, kwamba wapinzani wakichumua madaraka watavunja madaraja na kuyauza kama skrepa... SIYO KUWACHAFUA WAPINZANI..!?? Au uchafu ni upande mmoja!?
Kweli kabisa......

Hivi kwa tafsiri yao CCM, kuchafuliwa ni kwa upande mmoja tu pale wapinzani wanaopokosoa viongozi wa CCM, lakini wakati huo huo viongozi wa CCM wakiwatukana na kuwachafua viongozi wa upinzani ni ruksa?
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao...
Hivi yale maneno ya boss mkubwa, kwamba wapinzani wakichumua madaraka watavunja madaraja na kuyauza kama skrepa... SIYO KUWACHAFUA WAPINZANI..!?? Au uchafu ni upande mmoja!?
Wameanza wenyewe kuwachafu wapinzani mtu kweli unaweza kuvunja nyumba yako? nafananisha daraja km kitu muhimu km nyumba maana bila daraja huwezi kupiga hatua
 
Kweli kabisa......

Hivi kwa tafsiri yao CCM, kuchafuliwa ni kwa upande mmoja tu pale wapinzani wanaopokosoa viongozi wa CCM, lakini wakati huo huo viongozi wa CCM wakiwatukana na kuwachafua viongozi wa upinzani ni ruksa?
Halafu,

Hawa wa CCM hawachafuliwi, bali wanakumbushwa uchafu walioufanya wakiwa madarakani... kwa mfano, kusema JPM aliuza nyumba za serikali kwa utaratibu alioutumia ni kumchafua..!?

Au kusema JPM alisema tupige mbizi kati ya Kigamboni na Ferri ni kimchafua!? Kwani hakuyasema au..!?
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Matusi gani hayo?

Taja hayo matusi hapa siyo unakazana tu matusi matusi.

Umesahau watu walimwita mwenzao faru joni bungeni mkawa mnakenua tu.?
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Kwani akisema Rais kajenga uwanja was ndege Chato katukana? Akisema kujenga miundombinu kulianza toka enzi za mjerumani aliyejenga ikulu, Kambarage aliyejenga viwanda, reli ya Tazara, Mkapa aliyefanya mengi Kama ulisikia aliyofanya hivi majuzi, Kikwete aliyejenga UDOM Ni tusi gani hapo? Kwamba vyama vya upinzani vimeminywa Ni tusi?
 
Mi mwenyewe ni pro-Magufuli na obviously nitampigia kura come October.

Linapokuja suala la campaign wacha vyama vimseme na "vimchafue" Magufuli maana huu ndo mda wake...
Umesema ukweli kwa asilimia 100

Mimi nimekuwa nikijiuliza hivi "media house" ya nchi hii imeona hilo tamko la Waziri mkuu, ndiyo habari Kuu?

Ni kwanini "wameziepa" taarifa Kuu, ya mapokezi makubwa sana ya Maalim Seif huko Zanzibar na mafuriko ya wakazi wa Singida, wakati wakimpokea mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Tundu Lissu?
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Kwani akijiharibia si ndio vizuri mshinde kwa kishindo. Mi nasema Lissu aendelee kupiga spana tu.
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Hivi Tundu Lisu amemtukana tusi gani Rais Magufuli?

Kuna mambo ambayo wengi, hata baadhi ya wanaCCM hawafurahishwi nayo, tena yanabomoa misingi ya umoja wetu, lazima yasemwe tena kwa ukali kabisa.

Ujenzi wa uwanja mkubwa Chato, hakuna mwenye akili timamu anayeweza kutetea hilo. Uwanja mdogo wa ndege wa kawaida, hakuna ambaye angeshangaa. Ule ni uharibifu wa fedha ya umma. Lakini naambiwa siyo uwanja tu bali taasisi mbalimbali wamelazimishwa kujenga Chato. Hii haileti picha nzuri hata kidogo. Kama kuna watu wanafanya hivyo kwa kutaka kumfurahisha Rais, wajue wanamharibia sana.

Kuna mambo ambayo Rais Magufuli itabidi ayafafanue:

1) Uwanja mkubwa wa ndege Chato
2) Taasisi nyingi za serikali kulazimika kujrnga Chato na siyo Geita au Bukoba
3) Wateule wengi kutoka kanda moja
4) Wanafamilia au ndugu wa karibu kupewa nafasi kubwa za serikali

Pengine ana sababu za msingi. Kama ndivyo, afanye ufafanuzi. Bila kufanya hivyo, tuhuma za upendeleo, visasi na ubaguzi, zitaendelea kumwandama.

Mfahamu kuwa kuna mikoa mingi, tena yenye maendeleo binafsi mazuri kwa miaka mingi, hakuna kitu chochote kikubwa cha maana kikichofanyika awamu hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.

Kama serikali ilitakia kuanza na wakina musiba

And unakumbuka jinsi kibajaji alivyokuwa anamtukana lowasa? Tena matusi makubwa ya kumdhalilisha mbona hakuna mtu alikemea....

Hata mkapa aliwahi kusema wapinzani ni malofa Hilo ni tusi pia

So kwa Sasa watulie tu
 
Hivi matusi ni yapi?

Lugha za kuchafuana, kuuziana ni jambo la kawaida ktk kampeni.

Maana kama haupo focused lazima utoke kwenye mstari.

Na sisi wananchi tunahitaji viongozi ambao wapo focused hata wawe challenged vipi.
 
Kampeni ni kuongea sera zako sio mtu
Ndio Maana media hazitaki kutangaza vitu vyake upinzani haeaongelei sera wanaongelea Watu
Kusema kuwa tutajenga misingi bora ya maamuzi ya matumizi ya fedha ya umma, na siyo kama ilivyo sasa ambapo Rais anaamua kujenga uwanja mkubwa wa ndege kijijini kwake, siyo sera?

Lazima unapotaka kuleta kitu kipya, uelezee kilichopo, mapungufu yake, na wewe utakavyofanya tofauti?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…