Uchaguzi 2020 Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kusema Wagombea wa Upinzani wasiwachafue wagombea wa chama tawala una lengo la kutaka kuwatisha

Uchaguzi 2020 Kauli ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kusema Wagombea wa Upinzani wasiwachafue wagombea wa chama tawala una lengo la kutaka kuwatisha

Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao.

Ingawa hakuwataja kwa majina wagombea hao, ni dhahiri alikuwa na maana ya wagombea wa Chadema na ACT Wazalendo, ambao kwao CCM ndiyo wanawaona kuwa ni tishio kubwa kwao.

Ni jambo la kushangaza kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa ngazi ya juu wa CCM, kwa kuwa katika kipindi chote cha miaka 5 iliyopita, chama cha CCM "kilijipendelea" kwa kufanya kampeni peke yao, nchi nzima, wakiwachafua na kiwatukana viongozi wenzao wa upinzani, huku wakivipiga marufuku vyama vya upinzani, kutofanya mikutano yoyote ya kisiasa ya kujibu mashambulizi hayo

Sasa inashangaza mno kwa viongozi hao wa upinzani wanapotumia fursa hii waliyoipata wakati huu kufanya kampeni kujieleza, Waziri mkuu anasema wasiwachafue viongozi wa CCM!

Hivi kwa mfano kauli iliyotolewa na kiongozi wa Chadema, ambaye pia ni mgombea wa nafasi ya Urais Tundu Lissu, kuwa Rais Magufuli ametumia nafasi yake ya Urais kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa, huko kijijini kwake Chato na "kulazimisha" kuwa na mbuga yao ya wanyama ya Burigi, kwa Maelezo ya waziri mkuu, ni kumchafua Rais Magufuli?

Ninavyoona Mimi kama raia wa Tanzania, ambaye nina haki ya kutoa maoni yangu, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18(1) uamuzi wa busara kwa viongozi wa CCM ni kwa Rais Magufuli kujitokeza hadharani na kujibu mapigo hayo ni kwanini yeye ameamua kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa kwenye kijiji chake, kinyume cha viongozi waliomtangulia, akina Mwalimu Nyerere, Alli Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, hawajafanya kama yeye, aende kwenye majukwaa ya kisiasa ili atoe maelezo kama maneno aliyoyatoa Tundu Lissu ni ya uwongo. OVA
Uwanja wa ndege Chato ni mali ya rais Magufuli? Mbuga ya wanyama pori Burigi ni mali binafsi ya rais Magufuli? Uwanja wa ndege Chato ni mali ya watanzania wote. Na ni msaada kwa wakazi wa geita maana kama mkoa kulikuwa hakuna uwanja wa ndege. Acha upotoshaji wa kizushi.
 
Kama hawa watawala wetu wangekuwa fair, wangekuwa weshamchukulia hatua za.kisheria siku nyingi tu huyo mtu "wao" Musiba, kutokana na maneno yake ya uzushi, kuwatukana, kuwakashifu na hata kutishia kutaka kuwaua viongozi wa upinzani.

Lakini kwa kuwa huyo Musiba anakumbatiwa na Jiwe, basi kila analolifanya, vyombo vya usalama vimepigwa upofu!
Musiba angekuwa ni muislamu kitambo Sana angeshakuwa jela
 
Hivi Tundu Lisu amemtukana tusi gani Rais Magufuli?

Kuna mambo ambayo wengi, hata baadhi ya wanaCCM hawafurahishwi nayo, tena yanabomoa misingi ya umoja wetu, lazima yasemwe tena kwa ukali kabisa.

Ujenzi wa uwanja mkubwa Chato, hakuna mwenye akili timamu anayeweza kutetea hilo. Uwanja mdogo wa ndege wa kawaida, hakuna ambaye angeshangaa. Ule ni uharibifu wa fedha ya umma. Lakini naambiwa siyo uwanja tu bali taasisi mbalimbali wamelazimishwa kujenga Chato. Hii haileti picha nzuri hata kidogo. Kama kuna watu wanafanya hivyo kwa kutaka kumfurahisha Rais, wajue wanamharibia sana.

Kuna mambo ambayo Rais Magufuli itabidi ayafafanue:

1) Uwanja mkubwa wa ndege Chato
2) Taasisi nyingi za serikali kulazimika kujrnga Chato na siyo Geita au Bukoba
3) Wateule wengi kutoka kanda moja
4) Wanafamilia au ndugu wa karibu kupewa nafasi kubwa za serikali

Pengine ana sababu za msingi. Kama ndivyo, afanye ufafanuzi. Bila kufanya hivyo, tuhuma za upendeleo, visasi na ubaguzi, zitaendelea kumwandama.

Mfahamu kuwa kuna mikoa mingi, tena yenye maendeleo binafsi mazuri kwa miaka mingi, hakuna kitu chochote kikubwa cha maana kikichofanyika awamu hii.

Sent using Jamii Forums mobile app
Jibu ni rahisi sana.
Ukiacha mikoa ya ukanda wa pwani, kaskazini,kusini na Kati sehemu kubwa iliyo na idadi kubwa ya watu ni maeneo yanayozunguka ziwa Victoria.
Katika maeneo hayo ndiko kuna fursa nyingi za kiuchumi kwa maana ya ukaribu na nchi za maziwa makuu (Rwanda, Burundi, Uganda, DRC, )
Huduma muhimu maeneo hayo zilisahaulika,kwa kuwa wengi wa watu walienda maeneo hayo kama watafutaji tu na si wakazi (kwenye uvuvi, madini na ufugaji).
Ukanda ule unajumuisha maeneo yafutayo:-
Biharamulo,Chato,Nkome,Muleba,Kakonko,Ushirombo,Nzera,Sengerema,Keza,Nyakasanza,Nyabugombe,Ushetu,Malongwe,Mbogwe kwa pamoja yanaweza kutengeneza Mkoa wa kiutawala kama ilivyo Arusha.(Kuna madini,utalii,fursa za biashara nchi jirani,)
Binafsi naona serikali imechelewa kupeleka madaraka ya kimkoa maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo nao wajivunie Utanzania wa kweli.
Wengi tunapinga sababu tu ya fikra za kibaguzi, ubinafsi na choyo kwa maendeleo hasa kwenye maeneo ya pembezoni mwa nchi kuwa eti tukifanya tutawanufaisha watu wengine.
Haiwezekani na haitowezekana maeneo ynayochangia pato watu wake waachwe bila maendeleo si vizuri.
Kujengwa uwanja wa ndege wa Chato ni fursa ya kukuza biashara na kuimalisha utalii katika ukanda wa maziwa makuu, Chato kijiographia iko sawa sawa na wilaya ya Nyamagana, Mwanza na ni karibu na maeneo mengine katika nchi za maziwa makuu.
Maeneo yale zipo biashara nyingi na hivyo ni muhimu kupeleka huduma, anayetaka kuamini atembelee Buselesele/Katoro (tumia hata Google Map)
Nitaendelea baadae....
 
Jiwe hata kama akishinda kwa zile mbinu zake za kishetani lazima aoge matusi kipindi chote cha kampeni
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
taja tusi moja tu ambalo lisu alishawahi kumtukana magufuli. moja tu
 
Jibu ni rahisi sana.
Ukiacha mikoa ya ukanda wa pwani, kaskazini,kusini na Kati sehemu kubwa iliyo na idadi kubwa ya watu ni maeneo yanayozunguka ziwa Victoria.
Katika maeneo hayo ndiko kuna fursa nyingi za kiuchumi kwa maana ya ukaribu na nchi za maziwa makuu (Rwanda, Burundi, Uganda, DRC, )
Huduma muhimu maeneo hayo zilisahaulika,kwa kuwa wengi wa watu walienda maeneo hayo kama watafutaji tu na si wakazi (kwenye uvuvi, madini na ufugaji).
Ukanda ule unajumuisha maeneo yafutayo:-
Biharamulo,Chato,Nkome,Muleba,Kakonko,Ushirombo,Nzera,Sengerema,Keza,Nyakasanza,Nyabugombe,Ushetu,Malongwe,Mbogwe kwa pamoja yanaweza kutengeneza Mkoa wa kiutawala kama ilivyo Arusha.(Kuna madini,utalii,fursa za biashara nchi jirani,)
Binafsi naona serikali imechelewa kupeleka madaraka ya kimkoa maeneo hayo ili wananchi wa maeneo hayo nao wajivunie Utanzania wa kweli.
Wengi tunapinga sababu tu ya fikra za kibaguzi, ubinafsi na choyo kwa maendeleo hasa kwenye maeneo ya pembezoni mwa nchi kuwa eti tukifanya tutawanufaisha watu wengine.
Haiwezekani na haitowezekana maeneo ynayochangia pato watu wake waachwe bila maendeleo si vizuri.
Kujengwa uwanja wa ndege wa Chato ni fursa ya kukuza biashara na kuimalisha utalii katika ukanda wa maziwa makuu, Chato kijiographia iko sawa sawa na wilaya ya Nyamagana, Mwanza na ni karibu na maeneo mengine katika nchi za maziwa makuu.
Maeneo yale zipo biashara nyingi na hivyo ni muhimu kupeleka huduma, anayetaka kuamini atembelee Buselesele/Katoro (tumia hata Google Map)
Nitaendelea baadae....
sawa je bunge lilipitsha? sawa je tenda/kandarasi ilitangazwa? sawa je palikuwa na uwazi wa kumpata mkandarasi? sawa je kwanini basi isiwe mwanza ambako tayari kuna uwanja iwe chato?
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Watanzania ni waelewa ni mwisho wa magufuli sasa
 
Awamu hii wamejenga tabia ya kusifiana, imefikia mahali wamejisahau wanadhani kampeni ni sehemu ya kuwasifia CCM.
ati mkuu wa wilaya anaenda kukagua choo kilichojengwa kwa nguvu za wananchi badala ya kuwasifia wananchi kwakujitolea anasema namshukuru raisi JPM kwa juhudi zake mfyuuuuuu? kwani yye alibeba tofali pale mfyuuuuuu
 
Serikali ya CCM wana mambo ya kishenzi sana.
Wanakwambia vizuri "Uhuru unao LAKINI" maneno yanayofata mbele ya hiyo lakini yanabana uhuru wote, ni sawa na kumwambia mtu, unaweza kula hii keki lakini hutakiwi kutumia mdomo wala mkono, ile kwa macho. Ni ujinga ambao hau-make sense. Huyu aliyejaliwa ni mbaya kuliko hata jiwe basi tu mchukulieni poa kwa kua hua haongei.
Yaleyale ya jiwe "maendeleo hayana vyama" kesho yake "mmemchagua wa upinzani kamuombeni huyohuyo maendeleo". Words from kiongozi wa nchi hahaha! watu wanapewa cheo na wananchi wanakaa wanajisahau wanahisi wamegeuka miungu. AH
Hahaaaaaa............ 😁 😛
 
Habari kubwa kwenye magazeti ya Leo ni kauli aliyoitoa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ya kuwapiga mkwara mzito, wagombea wa vyama vya upinzani kuwa wasitumie majukwaa ya kisiasa katika kipindi hiki cha kampeni kuwachafua wagombea wenzao.

Ingawa hakuwataja kwa majina wagombea hao, ni dhahiri alikuwa na maana ya wagombea wa Chadema na ACT Wazalendo, ambao kwao CCM ndiyo wanawaona kuwa ni tishio kubwa kwao.

Ni jambo la kushangaza kauli hiyo kutolewa na kiongozi wa ngazi ya juu wa CCM, kwa kuwa katika kipindi chote cha miaka 5 iliyopita, chama cha CCM "kilijipendelea" kwa kufanya kampeni peke yao, nchi nzima, wakiwachafua na kiwatukana viongozi wenzao wa upinzani, huku wakivipiga marufuku vyama vya upinzani, kutofanya mikutano yoyote ya kisiasa ya kujibu mashambulizi hayo

Sasa inashangaza mno kwa viongozi hao wa upinzani wanapotumia fursa hii waliyoipata wakati huu kufanya kampeni kujieleza, Waziri mkuu anasema wasiwachafue viongozi wa CCM!

Hivi kwa mfano kauli iliyotolewa na kiongozi wa Chadema, ambaye pia ni mgombea wa nafasi ya Urais Tundu Lissu, kuwa Rais Magufuli ametumia nafasi yake ya Urais kujenga kiwanja cha ndege cha kimataifa, huko kijijini kwake Chato na "kulazimisha" kuwa na mbuga yao ya wanyama ya Burigi, kwa Maelezo ya waziri mkuu, ni kumchafua Rais Magufuli?

Ninavyoona Mimi kama raia wa Tanzania, ambaye nina haki ya kutoa maoni yangu, kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 18(1) uamuzi wa busara kwa viongozi wa CCM ni kwa Rais Magufuli kujitokeza hadharani na kujibu mapigo hayo ni kwanini yeye ameamua kujenga uwanja wa ndege wa kimataifa kwenye kijiji chake, kinyume cha viongozi waliomtangulia, akina Mwalimu Nyerere, Alli Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete, hawajafanya kama yeye, aende kwenye majukwaa ya kisiasa ili atoe maelezo kama maneno aliyoyatoa Tundu Lissu ni ya uwongo. OVA
Siasa Safi, Elimu na Afya=Maendeleo, Siasa Safi sio matusi bali sera zenye kuamsha hisia za wapiga kura.
 
Musiba angekuwa ni muislamu kitambo Sana angeshakuwa jela
Siyo dini ndiyo inayomlinda huyo kivuruge.

Bali ukweli ni kuwa yupo "karibu sana" na Jiwe, ndiyo imekuwa kinga yake kubwa, hadi vyombo vya sheria vinamuogopa!
 
sawa je bunge lilipitsha? sawa je tenda/kandarasi ilitangazwa? sawa je palikuwa na uwazi wa kumpata mkandarasi? sawa je kwanini basi isiwe mwanza ambako tayari kuna uwanja iwe chato?
Kupanga ni kuchagua.
Kuhusu tenda sijui
Kuhusu uwazi wa tenda sijui
Kuhusu kwanini isiwe Mwanza, jibu ni Umbali wa kimkoa swala hapa ni kutengeneza Mkoa mwingine utakaofanana na Arusha/Kilimanjaro.
Full stop (fursa zipo za kutosha)
Mbona wao wa huko hawalalamikii mafungu ya mapesa yaliyojenga na yanaendelea kujenga maeneo mengine?
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.
Sasa akijaharibia sio vizuri kwetu sie ccm.
Ww unataka ajijenge. TAGA mwenzetu vp ww?
 
Kupanga ni kuchagua.
Kuhusu tenda sijui
Kuhusu uwazi wa tenda sijui
Kuhusu kwanini isiwe Mwanza, jibu ni Umbali wa kimkoa swala hapa ni kutengeneza Mkoa mwingine utakaofanana na Arusha/Kilimanjaro.
Full stop (fursa zipo za kutosha)
Mbona wao wa huko hawalalamikii mafungu ya mapesa yaliyojenga na yanaendelea kujenga maeneo mengine?
asante kwa kukiri ukweli. kiongozi yeyete msafi hufuata taratibu zilizowekwa.
 
Tutawasema tu na yako mengi kweli kweli!! Wasubiri dawa inachemka jikoni! Mpaka wajumbe cheche
 
Majaliwa analeta upendeleo wa wazi kabisa, kama alikua na nia njema angesema kabisa both CCM na wapinzani wasichafuane.
 
Wafanye kampeni za kistaarabu maana wengine wanafikiri wakitukana watanzania ndio wanawaelewa na muuache kumsemasema magufuli..


Semeni mgombea wenu
 
Nchi haijengwi kwa matusi au dharau, ni muhimu kujenga utamaduni wa kushindana kwa hoja za maendeleo. Mfano Lis anapomdharau na kumtusi Dkt Magufuli unadhani anamfurahisha nani zaidi ya kujiharibia? Watanzania ni waelewa.

Hajamtusi bali ana expose madhambi yake
 
Back
Top Bottom