Kaya 644 Magomeni kota zagomea kusaini mkataba kununua nyumba

Kaya 644 Magomeni kota zagomea kusaini mkataba kununua nyumba

Maelekezo ya Magu wakati anaahidi kuzijenga alielekeza waliopo wasiondolewe,

Alitaka maskini wakae nao nyumba nzuri za kisasa.

Nyumba hamkujenga ninyi, kwann mzitolee mate?

Kwann kujitafutia LAANA za kujitakia?

Jengeni zenu hata kule makueni au kule Kiembe samaki mzifanye apartment za biashara.
Tuache kukariri ndugu, tufahamu haya;
1. Aliyesema waendelee kukaa kwenye hizo nyumba ni Rais (wakati huo alikuwa Magufuli) chini ya tamko lake na sio chini ya kanuni na utaratibu. Hivyo Rais mwingine anaweza kutengua/kulipuuzia hilo tamko na hakuna popote pa kwenda kuhoji au kupinga.

2. Tamko la Magufuli lilisema wakazi wote wa hizo nyumba waendelee kukaa humo kwa kuuziwa apartment kabla ya watu wengine. Na hicho ndicho kinachoendelea sasa. Hakuna popote tamko limekiukwa.

Wakazi hao kwa sasa wanapaswa kujenga hoja (kama ipo kweli) kwenye bei ya hizo nyumba kuwa kubwa kuliko uhalisia wa soko. Waje na mifano halisi ya kuonyesha apartment kama hizo, maeneo muhimu hapo Dar zinauzwa kwa bei pungufu ya hiyo. Wasijifiche tena kwenye kivuli cha unyonge, umaskini na siasa, hiyo ni biashara (kuna wabia wamewekeza fedha zao ili kujenga hayo majengo na lazima warejeshe pesa za kwa wakati na faida).

NOTE:
Mimi binafsi naona hizo bei ziko chini zaidi ya soko na ulipaji wako ni nafuu sana, na ikitokea zikatangazwa kuuzwa kwa mtu yoyote kuweza kununua, haitachukua hata wiki moja zote zitakuwa zimeuzwa huenda hata kwa cash.
 
Magufuli hakusema wakazi wa magomeni wakae bure au wajengewe bure.

Na ukweli halisi ni kuwa, sio kila mkazi wa hapo magomeni ni maskini, na Tz ina mamilioni ya maskini kuzidi 'maskini' wa magomeni kota ambao hawana hata uhakika wa chakula sembuse nyumba.

Hivyo umaskini usitumike hapa kama ndio sababu ya kuzing'ang'ania hizo nyumba.
 
View attachment 2508191

Dar es Salaam. Wakazi 644 wa Magomeni Kota wamegomea kusaini mkataba wa kuanza kununua nyumba hizo, kwa madai kwamba bei waliyoletewa sio rafiki na haiendani na hali ya uchumi wao.

Aidha wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aingilie kati kwa kuwa bei ya Serikali iliyowasilishwa ni kati ya Sh48 milioni na Sh56 milioni ni kiwango kikubwa wanachochukulia kama mtego wa kutaka kuwafukuza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa juzi na serikali kupitia kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambaye ni msimamizi wa mradi huo, mkataba huo unaanza kutumika kuanzia Februari 8 mwaka huu hivyo Kaya hizo zinapaswa kusaini kwa bei waliyoletewa.

Mwanasheria wa wakazi hao, Twaha Taslima akisoma barua iliyoandikwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Daud Kandoro, kwenda kwa wakazi hao, jana siku ambayo walifanya kikao mkoani Dar es Salaam, alisema bei iliyowasilishwa na serikali awali ilikuwa ndogo.

“Bei ambayo ilipendekezwa na Serikali awali ilikuwa ni Sh12 milioni hadi Sh17 milioni, iliyotolewa Juni mwaka jana, haikukidhi thamani ya eneo, haikujumuisha faida wala huduma za maeneo yanayozunguka makazi hayo ambayo ni jumuishi,” amesema.

Taslima amesema, "Njia mojawapo ya kuchukua ni kuiomba Serikali au kwenda mahakamani. Bei ya chumba na sebule kwa Sh48. 5 milioni na vyumba viwili na sebule Sh56.8 milioni inaweza isiwe rafiki na mnunuzu asimudu," alisema Taslima.

Mwenyekiti wa Wakazi wa Magoneni Koti, George Abel, amesema kwamba bei zilizokokotolewa siyo rafiki kwa wakazi hao, licha ya Serikali kuongezewa mkataba wa kulipa na kuishi kutoka miaka 10 hadi 15.

Amesema kuwa bei hiyo inatakiwa kila mkazi alipie Sh300,000 kwa mwezi hivyo kwa mwaka ni Sh3.6 milioni akisema kiasi hicho ni kikubwa ikizingatiwa baadhi ya wakazi tayari ni wazee na wastaafu.

"Tumepokea barua hii ikiwa zimebaki siku tatu tu kwamba tusaini mkataba wa manunuzi, tukutane tujadiliane kabla ya tarehe 8, Februari, mwaka huu, hizi bei si rafiki haziendani na hali za wakazi walio wengi," amesema Abel.

Mmoja wa wakazi wa nyumba hizo, Salama Goronga (65), amesema barua hiyo iliyosomwa kwao, ikionyesha bei hiyo imewahuzunisha kwa kuwa haiendani na hali zao kimaisha.

"Mimi nina wajukuu, na iliposomwa barua machozi tu yameanza kunitoka hiyo pesa nitatoa wapi, nitaondoka hapa niende wapi," amesema Salama.

Mkazi mwingine, Mwajuma Hamisi (82), amesema ana watoto wawili wa walioolewa ndio wanaomtunza kwa kumnunulia chakula na mahitaji mengine, hivyo itawawia vigumu leo hii waanze kumtafutia kodi mara atakapoondoka kwenye makazi hayo kutokana na kushindwa kulipia.

"TBA wanaotaka hizo nyumba, leo bei hii, kesho hii, tutalipaje mimi mzee, wanitoe hapa si aibu kwangu, mamilioni hayo nitayatoa wapi," amesema Mwajuma.

Alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi kutoka idara ya miliki TBA, Said Mndeme amesema “Masuala hayo aulizwe mkuu wa taasisi ndiye anayejua,” amesema.

Mwananchi
Kama bei ya 48m siyo sahihi, hiyo wananchi wanayotaka ya 17m itakuwaje sahihi?
Magu naye àlikuwa laghai, eti kufungiwa umeme 27k, nyumba za magomeni kotaz 17m
 
View attachment 2508191

Dar es Salaam. Wakazi 644 wa Magomeni Kota wamegomea kusaini mkataba wa kuanza kununua nyumba hizo, kwa madai kwamba bei waliyoletewa sio rafiki na haiendani na hali ya uchumi wao.

Aidha wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aingilie kati kwa kuwa bei ya Serikali iliyowasilishwa ni kati ya Sh48 milioni na Sh56 milioni ni kiwango kikubwa wanachochukulia kama mtego wa kutaka kuwafukuza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa juzi na serikali kupitia kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambaye ni msimamizi wa mradi huo, mkataba huo unaanza kutumika kuanzia Februari 8 mwaka huu hivyo Kaya hizo zinapaswa kusaini kwa bei waliyoletewa.

Mwanasheria wa wakazi hao, Twaha Taslima akisoma barua iliyoandikwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Daud Kandoro, kwenda kwa wakazi hao, jana siku ambayo walifanya kikao mkoani Dar es Salaam, alisema bei iliyowasilishwa na serikali awali ilikuwa ndogo.

“Bei ambayo ilipendekezwa na Serikali awali ilikuwa ni Sh12 milioni hadi Sh17 milioni, iliyotolewa Juni mwaka jana, haikukidhi thamani ya eneo, haikujumuisha faida wala huduma za maeneo yanayozunguka makazi hayo ambayo ni jumuishi,” amesema.

Taslima amesema, "Njia mojawapo ya kuchukua ni kuiomba Serikali au kwenda mahakamani. Bei ya chumba na sebule kwa Sh48. 5 milioni na vyumba viwili na sebule Sh56.8 milioni inaweza isiwe rafiki na mnunuzu asimudu," alisema Taslima.

Mwenyekiti wa Wakazi wa Magoneni Koti, George Abel, amesema kwamba bei zilizokokotolewa siyo rafiki kwa wakazi hao, licha ya Serikali kuongezewa mkataba wa kulipa na kuishi kutoka miaka 10 hadi 15.

Amesema kuwa bei hiyo inatakiwa kila mkazi alipie Sh300,000 kwa mwezi hivyo kwa mwaka ni Sh3.6 milioni akisema kiasi hicho ni kikubwa ikizingatiwa baadhi ya wakazi tayari ni wazee na wastaafu.

"Tumepokea barua hii ikiwa zimebaki siku tatu tu kwamba tusaini mkataba wa manunuzi, tukutane tujadiliane kabla ya tarehe 8, Februari, mwaka huu, hizi bei si rafiki haziendani na hali za wakazi walio wengi," amesema Abel.

Mmoja wa wakazi wa nyumba hizo, Salama Goronga (65), amesema barua hiyo iliyosomwa kwao, ikionyesha bei hiyo imewahuzunisha kwa kuwa haiendani na hali zao kimaisha.

"Mimi nina wajukuu, na iliposomwa barua machozi tu yameanza kunitoka hiyo pesa nitatoa wapi, nitaondoka hapa niende wapi," amesema Salama.

Mkazi mwingine, Mwajuma Hamisi (82), amesema ana watoto wawili wa walioolewa ndio wanaomtunza kwa kumnunulia chakula na mahitaji mengine, hivyo itawawia vigumu leo hii waanze kumtafutia kodi mara atakapoondoka kwenye makazi hayo kutokana na kushindwa kulipia.

"TBA wanaotaka hizo nyumba, leo bei hii, kesho hii, tutalipaje mimi mzee, wanitoe hapa si aibu kwangu, mamilioni hayo nitayatoa wapi," amesema Mwajuma.

Alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi kutoka idara ya miliki TBA, Said Mndeme amesema “Masuala hayo aulizwe mkuu wa taasisi ndiye anayejua,” amesema.

Mwananchi
watangaze kwa raia wote tukanunue pale waone kama hazitaisha ndani ya siku moja.
 
Chumba kimoja na sebule mtu akinunue Kwa ML 50?

WOSIA wa mahehemu haufuatwi!!!

Ukiona NCHI , Mungu ameruhusu atawale mtoto au ......... Anataka KUTUADHIBU.

Tuombe TOBA na REHEMA juu ya nchi yetu.

Aaaamen.
Gharama ya nyumba inategemea vitu vingi na siyo vyumba tu. Hizo nyumba mimi sizijui lakini kwa kutumia tu akili ya kuzaliwa, nadhani milioni 48 ni resonable price. Serikali inaweza kuwasaidia kwa kuwapa muda wa kulipa uwe miaka 20 na pia kuwapa uhuru wa kuziuza iwapo wanataka. Yaani hata kama amelipa nusu ya bei na akataka kuuza, basi aruhusiwe kuuza na anayeinunua ndiye awe na jukumu la kumalizia deni lililobaki.
 
Maelekezo ya Magu wakati anaahidi kuzijenga alielekeza waliopo wasiondolewe,

Alitaka maskini wakae nao nyumba nzuri za kisasa.

Nyumba hamkujenga ninyi, kwann mzitolee mate?

Kwann kujitafutia LAANA za kujitakia?

Jengeni zenu hata kule makueni au kule Kiembe samaki mzifanye apartment za biashara.
Nyumba zilizojengwa kwa kodi ya wananchi wote ina laana kutoka kwa nani. Wale waliambiwa wakae miaka 5 bure baada ya hiyo miaka kuisha mi nafikiri serikali ingetangaza kuziuza zile nyumba kwa bei ya soko. Mtanzania yoyote mwenye uwezo apewe fursa wakiwemo na walioko ndani ya nyumba husika. Zile ni kodi zetu watu wasitake dezo kisa wanajua kuongea na kulalamika. Hii serikali iwe serious na mambo yake siyo kila malamiko ni ya kusikiliza.
 
Wakazi wengi wa kota huwa ni wagumu sana kuhama. Fatilia kota zootee wanapotakiwa kutoka huwa hawakubali kirahisi na kutaka kuuziwa kwa bei yoyote,wakiletewa bei matokeo ndo kama haya ya wa uzi huu
Utasikia mimi nimezaliwa hapa, nimekulia hapa nimeoa naishi hapa, nina wajukuu wanaishi hapa mnataka mnitoe mnipeleke wapi? Wakati baba angu ananza kazi alikuwa anaishi hapa
 
Tuache kukariri ndugu, tufahamu haya;
1. Aliyesema waendelee kukaa kwenye hizo nyumba ni Rais (wakati huo alikuwa Magufuli) chini ya tamko lake na sio chini ya kanuni na utaratibu. Hivyo Rais mwingine anaweza kutengua/kulipuuzia hilo tamko na hakuna popote pa kwenda kuhoji au kupinga.

2. Tamko la Magufuli lilisema wakazi wote wa hizo nyumba waendelee kukaa humo kwa kuuziwa apartment kabla ya watu wengine. Na hicho ndicho kinachoendelea sasa. Hakuna popote tamko limekiukwa.

Wakazi hao kwa sasa wanapaswa kujenga hoja (kama ipo kweli) kwenye bei ya hizo nyumba kuwa kubwa kuliko uhalisia wa soko. Waje na mifano halisi ya kuonyesha apartment kama hizo, maeneo muhimu hapo Dar zinauzwa kwa bei pungufu ya hiyo. Wasijifiche tena kwenye kivuli cha unyonge, umaskini na siasa, hiyo ni biashara (kuna wabia wamewekeza fedha zao ili kujenga hayo majengo na lazima warejeshe pesa za kwa wakati na faida).

NOTE:
Mimi binafsi naona hizo bei ziko chini zaidi ya soko na ulipaji wako ni nafuu sana, na ikitokea zikatangazwa kuuzwa kwa mtu yoyote kuweza kununua, haitachukua hata wiki moja zote zitakuwa zimeuzwa huenda hata kwa cash.
Ndo nasema jengeni zenu Kwa pesa mlizikopa na mzifanye za biashara mpate faida.

Hizo Zina maelekezo ya marehemu kuwa wapewe hao maskini waliopo kipaumbele.

Sasa kuwapandishia Bei Ili muwafukuze, hizo ni HILA.
 
Ndo nasema jengeni zenu Kwa pesa mlizikopa na mzifanye za biashara mpate faida.

Hizo Zina maelekezo ya marehemu kuwa wapewe hao maskini waliopo kipaumbele.

Sasa kuwapandishia Bei Ili muwafukuze, hizo ni HILA.
HILA kutoka kwa nani, hela iliyotumika kujenga hizo nyumba lazima zirudi msitake dezo kila mtu apambane ili kupata kilicho kizuri.
 
View attachment 2508191

Dar es Salaam. Wakazi 644 wa Magomeni Kota wamegomea kusaini mkataba wa kuanza kununua nyumba hizo, kwa madai kwamba bei waliyoletewa sio rafiki na haiendani na hali ya uchumi wao.

Aidha wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan aingilie kati kwa kuwa bei ya Serikali iliyowasilishwa ni kati ya Sh48 milioni na Sh56 milioni ni kiwango kikubwa wanachochukulia kama mtego wa kutaka kuwafukuza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyowasilishwa juzi na serikali kupitia kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambaye ni msimamizi wa mradi huo, mkataba huo unaanza kutumika kuanzia Februari 8 mwaka huu hivyo Kaya hizo zinapaswa kusaini kwa bei waliyoletewa.

Mwanasheria wa wakazi hao, Twaha Taslima akisoma barua iliyoandikwa na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Daud Kandoro, kwenda kwa wakazi hao, jana siku ambayo walifanya kikao mkoani Dar es Salaam, alisema bei iliyowasilishwa na serikali awali ilikuwa ndogo.

“Bei ambayo ilipendekezwa na Serikali awali ilikuwa ni Sh12 milioni hadi Sh17 milioni, iliyotolewa Juni mwaka jana, haikukidhi thamani ya eneo, haikujumuisha faida wala huduma za maeneo yanayozunguka makazi hayo ambayo ni jumuishi,” amesema.

Taslima amesema, "Njia mojawapo ya kuchukua ni kuiomba Serikali au kwenda mahakamani. Bei ya chumba na sebule kwa Sh48. 5 milioni na vyumba viwili na sebule Sh56.8 milioni inaweza isiwe rafiki na mnunuzu asimudu," alisema Taslima.

Mwenyekiti wa Wakazi wa Magoneni Koti, George Abel, amesema kwamba bei zilizokokotolewa siyo rafiki kwa wakazi hao, licha ya Serikali kuongezewa mkataba wa kulipa na kuishi kutoka miaka 10 hadi 15.

Amesema kuwa bei hiyo inatakiwa kila mkazi alipie Sh300,000 kwa mwezi hivyo kwa mwaka ni Sh3.6 milioni akisema kiasi hicho ni kikubwa ikizingatiwa baadhi ya wakazi tayari ni wazee na wastaafu.

"Tumepokea barua hii ikiwa zimebaki siku tatu tu kwamba tusaini mkataba wa manunuzi, tukutane tujadiliane kabla ya tarehe 8, Februari, mwaka huu, hizi bei si rafiki haziendani na hali za wakazi walio wengi," amesema Abel.

Mmoja wa wakazi wa nyumba hizo, Salama Goronga (65), amesema barua hiyo iliyosomwa kwao, ikionyesha bei hiyo imewahuzunisha kwa kuwa haiendani na hali zao kimaisha.

"Mimi nina wajukuu, na iliposomwa barua machozi tu yameanza kunitoka hiyo pesa nitatoa wapi, nitaondoka hapa niende wapi," amesema Salama.

Mkazi mwingine, Mwajuma Hamisi (82), amesema ana watoto wawili wa walioolewa ndio wanaomtunza kwa kumnunulia chakula na mahitaji mengine, hivyo itawawia vigumu leo hii waanze kumtafutia kodi mara atakapoondoka kwenye makazi hayo kutokana na kushindwa kulipia.

"TBA wanaotaka hizo nyumba, leo bei hii, kesho hii, tutalipaje mimi mzee, wanitoe hapa si aibu kwangu, mamilioni hayo nitayatoa wapi," amesema Mwajuma.

Alipoulizwa Kaimu Mkurugenzi kutoka idara ya miliki TBA, Said Mndeme amesema “Masuala hayo aulizwe mkuu wa taasisi ndiye anayejua,” amesema.

Mwananchi
hyo gharama sidhani kama kuna 40% ya wapangaji wataweza kuilipa maana hapi tu service charge ya 30k watu hawezi ku afford

wengi wanaokaa humo wamepangishwa na watu maana wahusika wengi wanakaa nje ya magomeni kama chanika,mbagala n.k

tena na kuna wengine wamepiga bei kabisa flat zao humo,inshort magomeni kota ni jipu ambalo linasubiria kulipuka tutayaona na kuyaskia mengi sana it's just matter of time
 
Ndo wabongo tulivyo huwa hatuna future plans zaidi ya kupenda dezo. Hapo walitakiwa wawe na mijengo yao kuliko kuishi kizazi na kizazi kwa kupanga na kuja kutoa lawama zisizo na kivhwa kwa serikali
Utasikia mimi nimezaliwa hapa, nimekulia hapa nimeoa naishi hapa, nina wajukuu wanaishi hapa mnataka mnitoe mnipeleke wapi? Wakati baba angu ananza kazi alikuwa anaishi hapa
 
Serikali haijitambui inataka kufanya nini.

Inauza nyumba zake kwa sababu haitaki kujihusisaha na umiliki wa nyumba, halafu hapo hapo inajenga nyumba na kujirudisha kulekule ilikokataa.

Hivi serikali yetu inaelewa inataka kufanya nini?
 
hyo gharama sidhani kama kuna 40% ya wapangaji wataweza kuilipa maana hapi tu service charge ya 30k watu hawezi ku afford

wengi wanaokaa humo wamepangishwa na watu maana wahusika wengi wanakaa nje ya magomeni kama chanika,mbagala n.k

tena na kuna wengine wamepiga bei kabisa flat zao humo,inshort magomeni kota ni jipu ambalo linasubiria kulipuka tutayaona na kuyaskia mengi sana it's just matter of time
Kama kuna uozo huo, ina naana serikali yenye kuona kila pahala, imekuwaje kwa jambo hilo ikaingia upofu?

Basi wangelipiga utepe na kufanya sensa ya dharula kwa wakazi waliopo na kuanza mazungumzo na hao.

Ujanja janja huo wa kizamani haufai sana kwenye mali za umma.
 
Ndo nasema jengeni zenu Kwa pesa mlizikopa na mzifanye za biashara mpate faida.

Hizo Zina maelekezo ya marehemu kuwa wapewe hao maskini waliopo kipaumbele.

Sasa kuwapandishia Bei Ili muwafukuze, hizo ni HILA.
Ndugu jitafakari upya, umeandika vitu vya ajabu ajabu tupu.
Hapa tunazungumzia mustakabari wa nchi yetu na sio matamko ya Marehemu (Magufuli).

Zile nyumba hazikuwa mali ya Magufuli, hivyo rejea ya matamko yake haina maana yoyote.

Zile nyumba zimejengwa kwa kodi za watanzania wote, na sio kwa pesa binafsi za Magufuli au pesa za wakazi wa Magomeni Kota.

Kanuni, taratibu na masharti ya serikali kuzingatia soko na biashara za upangishaji lazima zifuatwe.
 
Back
Top Bottom