Kazi bado ngumu: Mawakili wa Mbowe waweka pingamizi jipya, Mahakama yakubali kulisikiliza

Kazi bado ngumu: Mawakili wa Mbowe waweka pingamizi jipya, Mahakama yakubali kulisikiliza

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Leo_Sept.Mosi%2C_2021_Mhe_%40freemanmbowetz_akifurahi_jambo_na_Mawakili_wanaomtetea_katika_kes...jpg

Kama ulidhani hii kesi ni lelemama basi unapaswa kujitafakari upya , wakati baadhi ya mamluki wakishangilia kutupwa kwa pingamizi lililohoji uhalali wa Mahakama ya uhujumu uchumi na rushwa kusikiliza kesi ya Ugaidi, Mawakili wa Mbowe wameweka pingamizi ambalo wasomi wengi walikuwa wanalisubiri, la KUPINGA HATI YA MASHITAKA KUTOKIDHI VIGEZO NA MASHARTI YA KISHERIA, kukosewa kwa hati hii kunatokana na uwezo mdogo na umbumbumbu wa Wanasheria wa serikali ,mara zote imesemwa sana kuhusu uwezo wa watu hawa.

Jino_kwa_jino.jpg

=====

Leo Septemba Mosi, 2021 Mawakili upande wa utetezi wameweka pingamizi lingine kuhusu hati ya mashtaka, wamedai kuwa imekosa vigezo vya kisheria na upande wa Serikali wameomba Ijumaa Septemba 3, 2021 kuja na majibu.

Mahakama hiyo imeridhia ombi hilo na kuahirisha kesi hadi Ijumaa.
 
Kushindana kisheria na wenye nguvu wasiofuata sheria, kupata matokeo chanya ni ndoto. Save energy, jipange
 
😁😁😁😁...hili pia litatupwaHa
Uamuzi wa Ijumaa ni kwa judge kuwaambia wanasheria wa serikali wairekebishe hiyo hati ya mashtaka ili ikizi vigevo vya kisheria, vinginevyo, kesi itatupiliwa mbali kama haikizi vigezo hivyo vya kisheria kama wanavyodai waweza pingamizi...
 
Sijui ni kwa nini mapingamizi haya hayakuja pamoja:

1. Kuhoji uhalali- limetupwa
2. Hati ya mashtaka kutokukidhi matwaka ya kisheria kama mahakama ingekubaliana na serikali.. ni mchezo wa paka na pacha kwa sasa.
 
Pingamizi za aina hiyo hazina tija yoyote. Sana sana zinachelewesha tu kesi ya msingi, kwasababu hata kesi ikitupwa mtuhumiwa anaweza kukamatwa tena na kesi ikafunguliwa upya. That may not buy you even 15 minutes of freedom. Ukitoka tu mahakamani polisi wanakudaka tena!
 
Pingamizi za aina hiyo hazina tija yoyote. Sana sana zinachelewesha tu kesi ya msingi, kwasababu hata kesi ikitupwa mtuhumiwa anaweza kukamatwa tena na kesi ikafunguliwa upya. That may not buy you even 15 minutes of freedom. Ukitoka tu mahakamani polisi wanakudaka tena!
Atachukuliwa na Mabalozi kama vile TL akivyopelekwa Airport na msafara wa mabalozi kadhaaa
 
Back
Top Bottom