Asante sana mkuu,maisha ni kupambana Mpaka uitwe boss kuna njia nyingi sana mtu lazima uzipitiepole sana kamanda wewe ni jembe lkn
Pole sana jamaa..hizo kazi ngumu zinahitaji uzoefu na mwili wenye afya..manake pia hao majamaa wanakula sana hawali chakula zaidi ya ugali na makande..Aisee nimeekumbuka na mimi...ukisikia kazi ya kushusha cement wala usisogee.,nakumbuka 2017 nilipita sehemu nikakuta kuna semi nyingi zimepack,,,vijana wakiendelea na kazi za kupakua cement toka kwenye gari mpka store....aaah mm hapo sijala tokea jana afu njaa inauma nikajisemea ngoja nikomae hapa nipate 15000 niishi...duu...nakumbuka nilibeba mifuko 30 wakt hapo nishachoka balaa jasho kila mahali..mda huo speed imepungua miguu inatetemeka balaa..nilivochukua mfuko wa 31 nilidondoka nao na kazi ikaishiaa hapohapo nikapepewa buku mbili nakumbuka ..
Nilichogundua sio swala la nguvu pale ...mana nguvu nilikuwa nazo isipokuwa ni uzoefu
Hapana Mkuu,simjui huyo mtu ila naweza mtetea,Maana kuna mtu nimemsoma na nikakumbukia kuna thread alivyokuwa anajipa mapromo.
Cement sio unga wakawaida ule,ule ni mfuko wa MAWE watu hawajui tunilivochukua mfuko wa 31 nilidondoka nao na kazi ikaishiaa hapohapo nikapepewa buku mbili nakumbuka ..
KUCHUNGA NG'OMBEkuchunga ng'ombe ase
Tulihangaika sana kuktafta,tungekupata usingepona aisee ahahahahahhaKUCHUNGA NG'OMBE
Ilikua Arusha,nilimwambia jamaa flani anitaftie kazi Nilimkuta tu analinda nyumba 1 hivi, nikamuelezea shida yangu ya kazi akaniambia nimpitie kesho atakua ana jibu. basi nikaondoka.
Kesho yake nikarudi,akaniambia imepatikana kazi ya kuchunga ng'ombe unaweza? nikamwambia ukweli sijawahi kuchunga ng'ombe,akanaiambia sio kazi utaelekezwa tu sehemu ya kuwapeleka kwenye malisho kisha unaangalia wasiende kwenye mashamba ya watu.
nikakubaliana nae, akaniambia utakua unakaa hapo hapo (nikafurahi sana) misoto yangu yote guys mimi pakulala huwa sinaga sijawambia ila (ni siri yangu ntawambia kwenye thread zingine) nikisema naenda home huwa naendaga wapi.
Basi bana tutoke huko, nilipoambiwa ntakua nalala hapo hapo nikafurahi sana nikajua hapa nitakua nimepga ndege wawili kwa jiwe 1, yani ntakua nime solve tatizo la msosi na pili ntakua nimepata sehemu ya kuishi.
Basi jamaa akaniambia itabidi leo tushinde wote hapa ili badae nikitoka hapa nikupeleke,nikamwambia hamna shida tukashinda wote hiyo siku usiku mzma asubuhi yake tukatoka akanipeleka kwa boss, ni Muarusha yule mzee.
Nikafika nikakaribishwa mchana muda wa kula ukafika wakaleta "loshorooo" Hili ni jina la chakula cha kimasai/waarusha huchanganya maindi na maziwa fresh sjui, nikaletewa, kiukweli sikiwezagi mimi hiki kitu muda mrefu tu.
Nakijua maana mimi ni "mkazi wa arusha" hivyo naijua kabisa Loshoroo na siiwezi nishaitest nikatapkaga,basi ilivyoletwa nikapewa Nikawambia Hapana niko vizuri nimeshba kabisa, Hapo sijala nmesema hivyo nikivuta muda wa usiku watapka aina ingine ya chakula ntakula,basi jioni jioni akaja kijana wa huyo mzee akaniambia twende anipeleke sehemu wanazolisha akanionyeshe na njia ya kupitisha ng'ombe.
Tukaondoka tunatembea nakunywa maji tu ku clear njaa,nina hasira kulia nataka sina wakumlilia basi tukaenda akanionyesha tukarudi, Usiku ukafika nikasubiri msosi nione nini kitapkwa ili nile, Muda wa kula umefika
naletewa tena Loshoroooo, yewoomiiiiiiiiii... ki ukweli hiyo siku nilijua nini maana ya maisha ni safari ndefu, nikasema hapa sina namna acha nijaribu tu ntafanyaje sasa,kupga tu mdomoni Nikarudsha chenchi tapikaaa sanaaaa, hadi nikawashtua wenyeji, wakaniuliza vipi unaumwa? nikawambia hapana...
Akatokea mtoto wa kike wa huyo mzee ni mkubwa kbsa kama mmama akasema mtengenezeeni uji hebu, kimoyo moyo nikasema ashukuriwe Mungu, uji ukatengenezwa nikaona wanataka kuweka maziwa kwenye UJI, Nikawambia hapana Hapana usiweke maziwa "wamasai na maziwa sijui wana nini",basi nikatengenezewa uji nikaupiga wote,Usiku ukaisha kwa usalama.
Kesho yake kazn sasa,natakiwa kutoa ng'ombe kwenda kuchunga,Kijana ninaetakiwa kwenda nae kama mwenyeji wangu mjukuuu wa huyo mzeee "katoroka" kaenda kucheza huko,basi nikaambiwa niende tu kuchunga maana jana si nilishaonyeshwa pakuwapeleka.
Nikiwa natoa ng'ombe zizini naona maandalizi ya Loshorooo ya mchana ikiandaliwa,maana yake nikirudi kuchunga nakutana na loshoroo,sawa nikatoa ng'ombe na fimbo yangu nikawa na wa swaga mdogo mdogo,naongea nao road "nyieee rudi huku" tandika sana fimbo ng'ombe viburi kweliii wanahangaika haoooo
Nikafika eneo la kulisha nikawaacha wakawa wanaendelea kula,hapo kurudsha ng'ombe ni jioni,kumbuka nimeamka asubuhi sijala kitu,nmekaaa pale uwanjan nawaangalia ng'ombe, nililia sana hiyo siku,Nililia mpaka kwikwi..
kama ni sikuweza jinyonga ile siku hapa duniani hamna kitu itafanya niondoe uhai wangu tena,ni moja ya siku nilikaa nikijitafakari sanaaa maisha haya mpaka lini,shida hizi mpaka lini, Naendelea kuwaza ila njaa inauma nikaona mimi ninapoelekea ntachinja ng'ombe wa watu nile nyama.
Nikaamka nikajinyooosha nikifkiria nkirudi home nakutana na loshorooo tena Hapana siwezi, nikatupa fimbo kuleee nikawaaga ng'ombe (nikawambia wanangu leo mtarudi wenyewe home) Nikapita na hamsini zangu, mimi huyooooo.... (huko nyuma sijui kilichoendelea) ila kuchunga kukaishia hapo..
Mshahara niliahidiwa 20,000 kwa mwezi, niliukubali kabisa ila kazi ikawa sio riziki.
Ndugu yangu ng'ombe wenu kila nilipokua nikiwaangalia napata wazo la kuchinja au kuuzaTulihangaika sana kuktafta,tungekupata usingepona aisee ahahahahahha
Hiyo kazi kuna kijana wangu alinyatia kwenda kuiba nguo zake ili atorokeee kwani aliona atakufaa!!amefanya kazi toka saa 12 asubuhi hadi saa 3 usiku anaona hakuna hata dalili ya mzigo kuisha!!akaona isiwe tabu .bora nusu shali kuliko shari kamili!!nguo ni zako ila unazinyatiaKUBEBA ZEGE
Kwenye site ya ujenzi kituo cha watoto Sam Nujoma road, aisee hiyo kazi acha kabisa. Niliishia siku moja tu nikaenda zangu viwandani Mikocheni
Elfu 20 kwa mwezi duuh?sio poah!KUCHUNGA NG'OMBE
Ilikua Arusha,nilimwambia jamaa flani anitaftie kazi Nilimkuta tu analinda nyumba 1 hivi, nikamuelezea shida yangu ya kazi akaniambia nimpitie kesho atakua ana jibu. basi nikaondoka.
Kesho yake nikarudi,akaniambia imepatikana kazi ya kuchunga ng'ombe unaweza? nikamwambia ukweli sijawahi kuchunga ng'ombe,akanaiambia sio kazi utaelekezwa tu sehemu ya kuwapeleka kwenye malisho kisha unaangalia wasiende kwenye mashamba ya watu.
nikakubaliana nae, akaniambia utakua unakaa hapo hapo (nikafurahi sana) misoto yangu yote guys mimi pakulala huwa sinaga sijawambia ila (ni siri yangu ntawambia kwenye thread zingine) nikisema naenda home huwa naendaga wapi.
Basi bana tutoke huko, nilipoambiwa ntakua nalala hapo hapo nikafurahi sana nikajua hapa nitakua nimepga ndege wawili kwa jiwe 1, yani ntakua nime solve tatizo la msosi na pili ntakua nimepata sehemu ya kuishi.
Basi jamaa akaniambia itabidi leo tushinde wote hapa ili badae nikitoka hapa nikupeleke,nikamwambia hamna shida tukashinda wote hiyo siku usiku mzma asubuhi yake tukatoka akanipeleka kwa boss, ni Muarusha yule mzee.
Nikafika nikakaribishwa mchana muda wa kula ukafika wakaleta "loshorooo" Hili ni jina la chakula cha kimasai/waarusha huchanganya maindi na maziwa fresh sjui, nikaletewa, kiukweli sikiwezagi mimi hiki kitu muda mrefu tu.
Nakijua maana mimi ni "mkazi wa arusha" hivyo naijua kabisa Loshoroo na siiwezi nishaitest nikatapkaga,basi ilivyoletwa nikapewa Nikawambia Hapana niko vizuri nimeshba kabisa, Hapo sijala nmesema hivyo nikivuta muda wa usiku watapka aina ingine ya chakula ntakula,basi jioni jioni akaja kijana wa huyo mzee akaniambia twende anipeleke sehemu wanazolisha akanionyeshe na njia ya kupitisha ng'ombe.
Tukaondoka tunatembea nakunywa maji tu ku clear njaa,nina hasira kulia nataka sina wakumlilia basi tukaenda akanionyesha tukarudi, Usiku ukafika nikasubiri msosi nione nini kitapkwa ili nile, Muda wa kula umefika
naletewa tena Loshoroooo, yewoomiiiiiiiiii... ki ukweli hiyo siku nilijua nini maana ya maisha ni safari ndefu, nikasema hapa sina namna acha nijaribu tu ntafanyaje sasa,kupga tu mdomoni Nikarudsha chenchi tapikaaa sanaaaa, hadi nikawashtua wenyeji, wakaniuliza vipi unaumwa? nikawambia hapana...
Akatokea mtoto wa kike wa huyo mzee ni mkubwa kbsa kama mmama akasema mtengenezeeni uji hebu, kimoyo moyo nikasema ashukuriwe Mungu, uji ukatengenezwa nikaona wanataka kuweka maziwa kwenye UJI, Nikawambia hapana Hapana usiweke maziwa "wamasai na maziwa sijui wana nini",basi nikatengenezewa uji nikaupiga wote,Usiku ukaisha kwa usalama.
Kesho yake kazn sasa,natakiwa kutoa ng'ombe kwenda kuchunga,Kijana ninaetakiwa kwenda nae kama mwenyeji wangu mjukuuu wa huyo mzeee "katoroka" kaenda kucheza huko,basi nikaambiwa niende tu kuchunga maana jana si nilishaonyeshwa pakuwapeleka.
Nikiwa natoa ng'ombe zizini naona maandalizi ya Loshorooo ya mchana ikiandaliwa,maana yake nikirudi kuchunga nakutana na loshoroo,sawa nikatoa ng'ombe na fimbo yangu nikawa na wa swaga mdogo mdogo,naongea nao road "nyieee rudi huku" tandika sana fimbo ng'ombe viburi kweliii wanahangaika haoooo
Nikafika eneo la kulisha nikawaacha wakawa wanaendelea kula,hapo kurudsha ng'ombe ni jioni,kumbuka nimeamka asubuhi sijala kitu,nmekaaa pale uwanjan nawaangalia ng'ombe, nililia sana hiyo siku,Nililia mpaka kwikwi..
kama ni sikuweza jinyonga ile siku hapa duniani hamna kitu itafanya niondoe uhai wangu tena,ni moja ya siku nilikaa nikijitafakari sanaaa maisha haya mpaka lini,shida hizi mpaka lini, Naendelea kuwaza ila njaa inauma nikaona mimi ninapoelekea ntachinja ng'ombe wa watu nile nyama.
Nikaamka nikajinyooosha nikifkiria nkirudi home nakutana na loshorooo tena Hapana siwezi, nikatupa fimbo kuleee nikawaaga ng'ombe (nikawambia wanangu leo mtarudi wenyewe home) Nikapita na hamsini zangu, mimi huyooooo.... (huko nyuma sijui kilichoendelea) ila kuchunga kukaishia hapo..
Mshahara niliahidiwa 20,000 kwa mwezi, niliukubali kabisa ila kazi ikawa sio riziki.
Hahaaaa! Mkuu umenikumbusha mbali sana, kuna kampuni inajihusisha na ujenzi wa minara ya mawasiliano, nikaenda kuomba kazi wakasema kuwa rigger lazima uende training na kozi ni ya wiki moja na gharama yake ni dola 400! na ofisi itakulipia, mimi poa, kwanza sinema lilianza hapo kwenye trining kuna bonge la mnara unatakiwa kupanda, nikapambana nikamaliza kozi fresh, nikaenda site sasa(USINIPIGIE SIMU NIPO SITE)ki ukweli malipo yake ni mazuri kwa siku ni 50, 000!!mnara wenye urefu wa mita 72!Nakumbuka nilivyokuwa mlinzi kwenye mgodi fulani aisee kuwasimamia mafundi juu ya mnara sehemu moja inaitwa knelson kwenye uchenjuaji wa dhahabu nilipata kizunguzungu.Ikabidi nimcheki mkubwa wangu kwenye radiocall aje mwenyewe kusimamia aisee!
Hahaaaaaa.Kuna siku nipo maskani nishachoka zanguu,akaja jamaa akasema anaeweza kuchezea mavi twende kuna kazi huko,,
Nikamuuliza kazi gani? akasema mwenye nyumba anataka chemba ya choo tuchote mavi yote na ndooo tukamwage kwenye shamba lake ili ile chemba iongezwe urefu yani pale ilipo ifukuliwe zaidi kwenda chini..
ila huwezi kufukua zaidi bila kutoa kinyesi chote, tukamwambia si aite tu gari ya kunyonya mavi inyonye, Akasema njia ya kufika kwake gari ya mavi haifiki na hata wakifosi gharama ni kubwa mno inafika 1m na huyo mzee hiyo hela hana..
hivyo mzee katoa ofa ya watu kuchota mzgo wote na ndoo na kwenda kuumwaga huko shambani kwake, Tukauliza OFA yake sh ngapi?
Jamaa akasema kazi tunaifanya watu wa 4 tu mzee kasema atatoa 100,000 kwa kila mtu,jamaa mmoja akasema mwambie aongeze walau iwe 150,000 tukapge kazi, nazama chumvini nalamba inye live na ulimi sembuse hiyo harufu inishinde? mwambie aongeze dau...
Jamaa akavuta simu kwa mshua akamwambia vijana wa kazi wamepatikana ila wanasema 100k haitoshi waongeze 50k iwe 150k, mzee akajibu Sawa njooni.
Jamaa akasema oyaa mshua kakubali, Huyo mwingine akawambia sasa sikilizeni hapa tunaenda nunua mafuta ya Taaa kidumu cha lita 5 tunamwaga mwaga mule kwenye chemba mote Harufu inakata kazi tunapga freshi..
Kusikia hivyo tukaona jamaa katoa idea nzuri sana,kweli haooo hadi kwa mangi tukanunua mafuta ya taaa haooo safari ikaanza kwenda site.
Tumefika tukaenda kwenye chemba, ilikua tayari ishabomolewa lile zege la juu hivyo limebaki shimo pana tu unaona inye live live,mafinyo finyo live live, Jamaa akamwaga mafuta ya taaa pwaaaaaa koteee..
Tukaletewa ndooo kila mtu na ndoo yake,gloves kazi ikaanza nikadumbukiza nikachota ndoo ya kwanza nikatoa,jamani jamani jamani nilienda kumwaga shambani nikapitiliza huko huko sikurudi nyuma tena.
Asee inye isikieni tu,ile 150,000 nikaona wala isinipe presha mimi,na niikose tu siwezzi chezea gwede gwede kama vile ni rost... nimeondoka nimefika maskani nasimulia waliobaki,nusu saa haijaisha namuona mwenzangu mwingine huyu hapa karudi, aaah weee kuna kazi za kufanya bwana sio kazi ya kuchezea tope la binadamu..
Nilifanya kazi ya ulinzi majambazi wakavamia wakaua walinzi mi nikakamatwa kwa kosa la kwanini mimi nipone na wenzangu wafe
Nilikimbia kazi ya kushusha mizigo kwenye store ya kiwanda fulani.
Kwenye hicho kiwanda Kuna kitengo kinaitwa finance Sasa walikuwa wamebandika tangazo wanahitaji Kuajiri vijana 10 so kutokana na jina la kitengo nikashawishika kuomba kuajiriwa Kwa Imani kuwa kazi zitazokuwa zinafanyika pale zitarelate na mambo ya finance ili kujiakikishia kuwa napata hiyo nafasi nikaenda kuoongea na mshua fulani ili hakikishe connection hainipiti pembeni.
Picha linaanza tunapelekwa general store ya hiyo kampuni Kwa hiyo sisi ndio tutakuwa full responsible Kushusha mizigo yote inayoingia kwenye hiyo kampuni na kweli kampuni inapokea mizigo sio kitoto kuanzia cement, chokaa, Nondo, mabati, mbolea, dawa za kilimo in short ni general store haswa.
Sasa task yetu ya kwanza ilikuwa Kushusha mbolea Toka kwenye scania mzee nilikomaa Kushusha tumemaliza tunaona scania nyingine inaingia zile za kufuta na kontena mbili ilikuwa na cement wahuni wakaniambia Mimi ndio niwe nawatishwa aisee niliona Bora kubeba kuliko kuwatishwa sababu walikuwa wako chapu kinoma nikaomba kubeba wakakubali tunakaribia kumaliza tunaona nje ya Fensi scania nyingine inakuja na yenyewe cement nikaanza kugiveup wahuni wananiambia Kuna siku magari yanakuwa hayaji Kwa hiyo zipo siku tutarelax.
Nilipiga Ile kazi Kwa siku tatu sikuchukua malipo kwani walikuwa wanalipa baada ya wiki mbili na malipo was 3500 per day bila ya kujali uzito wa kazi wa siku husika.
Na wanakuwa wakali kinoma wanapenda kazi zao ziwe perfect bila ya kujali mazingira ya utendaji wa kazi na maslahi ya mfanyakazi.Hao watu ni wauaji
Ngoma kama hiyo nilimshuhudia mwamba mmoja wa tanesco akikata motoHahaaaa!!mkuu umenikumbusha mbali sana, kuna kampuni inajihusisha na ujenzi wa minara ya mawasiliano, nikaenda kuomba kazi wakasema kuwa rigger lazima uende training na kozi ni ya wiki moja na gharama yake ni dola 400!na ofisi itakulipia, mimi powa, kwanza sinema lilianza hapo kwenye trining kuna bonge la mnara unatakiwa kupanda, nikapambana nikamaliza kozi fresh, nikaenda site sasa(USINIPIGIE SIMU NIPO SITE)ki ukweli malipo yake ni mazuri kwa siku ni 50, 000!!mnara wenye urefu wa mita 72!!!nilipanda niaanza kusikia kama sauti ya maraika wananiambia karibu kwetu kwa baba!!upepo unapiga mluzi halafu ni kisiwani huko, pande zote ni maji tu!!ki ukweli kilichofuata sikujua nilijikuta nipo kivulini chini napewa huduma ya kwanza!!kumbe nilikata moto nusu.Ila sikukata tamaa, nilipambana hadi nikazoea kabisa, ila siku ile daaa!!!ni kazi ngumu kwa mwanzoni ila ukiisha izoea ni nyepesi sana yenye malipo mazuri, ila zingitia maharti yote ya ki usalama, utaifurahia.
Ni za hatari sana, lakini ukizingatia kutumia vile vifaa vya usalama unavyokuwa navyo hasa mkanda, shockabsorbers, work positioning, miaka yote utakuwa salama na utaifurahia kazi yako, na mimi ndio vilivyoniokoa hivyo, kwani baada ya kupoteza fahamu nilibaki pale pale nina ning'inia hadi nikapata msaada!!na ni kazi zenye matukio machache sana ya ajari kulinganisha na zile za chini ya ardhi!!Ngoma kama hiyo nilimshuhudia mwamba mmoja wa tanesco akikata moto
Kapanda kwenye msitm sijui alijichanganya nini yule jamaa akapolochoka kutoka juu mpka chini akatua kwa kukaa tulisikia mtu anaguna tu MMHHH!! Akakata moto
Kazi nyingne sio poa