Hawa ndo wanaitwa ma-porter aka wagumu wanatembea hapo mlimani cruiser cha mtoto.
Experience ya ule mwendo wa kutembea mlimani itakufanya ujue vizuri matumizi ya gear zote 5 za kwenye gari
Gear no 1 hutumika wakati wa kupanda mlima mkali, yaani unageuka gari kabisa na discipline inakuepo hakuna cha race wala nini ni mdogo mdogo
Gear no 2 utakutana na kilima kimeanza kulainika ndo hapo kidogo unavuta wese
Gear no 3 hapo kwa sadala kidogo unapiga story na wana
Gear no 4 na 5 ndo kabisa unachanganya mwendo wese la kutosha uwahi camp kabla wageni hawajakukuta njiani, maana yule guide wa mlima na wageni huwa wanakuwa wa mwisho kufika camp, sasa guide akikukuta njiani ni matusi kilo 7 anakuambia
“ww malaya kaza hiyo sifuri huku hakuna shangazi wala mjomba mpaka saivi hujafika camp unakata viuno na bag la wageni”
Gear no 1 pia hii hutumika wakati wa kushuka mlima hapa ndo utaimba haleluya ni kheri kupanda kuliko kushuka maana kunakuwa na mteremko mkali sana na umebeba mzigo hapo mgongoni yaani miguu inakosa balance kabisa swala la kuanguka na mzigo wako kama tembo ni kawaida sababu ya utelezi maana sehemu nyingi za kushuka huwa zimezungukwa na forest hivyo mvua mvua zinakuwepo through out the seasons
View attachment 2327765
Sent using
Jamii Forums mobile app