Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Kazi nilizowahi zifanya na zikanishinda kwenye utafutaji

Kwamba kukaa lindoni ukaona ni kifo lkn hujaona kifo kutembea njiani saa 8 au 9 usiku. Na hukuwaza ulikuwa tayari unakata tiketi ya segerea kwa kuondoka lindoni na kuacha mali ulizokabidhiwa? Ila nahisi hapa kwenye ulinzi hujanyoosha maelezo
sawa
 
Sitosahau kazi ya upagazi kubeba mizigo Kilimanjaro, wale wote maPorter wa Kilimanjaro nawasalimu.

Rafiki yangu alikufa kifo cha kusikitisha nikawa naogopa kumpa taarifa mke wake na mtoto wao alikuwa mdogo. Maiti ilipelekwa singida kwa mazishi. kazi ilikuwa ngumu mno. mzigo ni kilo 20 tu lakin mazingira yalikuwa mabaya mabovu usipime. kuna watu wanatafuta mlo wao kwa taabu sana. Mungu wabariki watu wale. niliki maisha yale baada ya kupata Dollar 80 iyo ilikuwa ni kazi yangu ya mwisho na kampuni ya ZARA TOURS
 
Sitosahau kazi ya upagazi kubeba mizigo Kilimanjaro, wale wote maPorter wa Kilimanjaro nawasalimu.

Rafiki yangu alikufa kifo cha kusikitisha nikawa naogopa kumpa taarifa mke wake na mtoto wao alikuwa mdogo. Maiti ilipelekwa singida kwa mazishi. kazi ilikuwa ngumu mno. mzigo ni kilo 20 tu lakin mazingira yalikuwa mabaya mabovu usipime. kuna watu wanatafuta mlo wao kwa taabu sana. Mungu wabariki watu wale. niliki maisha yale baada ya kupata Dollar 80 iyo ilikuwa ni kazi yangu ya mwisho na kampuni ya ZARA TOURS
Rafiki yako alikafaje hiko Kifo kibaya??tafadhali tupe news Mkuu tujifunze
 
Sitosahau kazi ya upagazi kubeba mizigo Kilimanjaro, wale wote maPorter wa Kilimanjaro nawasalimu.

Rafiki yangu alikufa kifo cha kusikitisha nikawa naogopa kumpa taarifa mke wake na mtoto wao alikuwa mdogo. Maiti ilipelekwa singida kwa mazishi. kazi ilikuwa ngumu mno. mzigo ni kilo 20 tu lakin mazingira yalikuwa mabaya mabovu usipime. kuna watu wanatafuta mlo wao kwa taabu sana. Mungu wabariki watu wale. niliki maisha yale baada ya kupata Dollar 80 iyo ilikuwa ni kazi yangu ya mwisho na kampuni ya ZARA TOURS
vanus porter mwenzako huyu
 
Sitosahau kazi ya upagazi kubeba mizigo Kilimanjaro, wale wote maPorter wa Kilimanjaro nawasalimu.

Rafiki yangu alikufa kifo cha kusikitisha nikawa naogopa kumpa taarifa mke wake na mtoto wao alikuwa mdogo. Maiti ilipelekwa singida kwa mazishi. kazi ilikuwa ngumu mno. mzigo ni kilo 20 tu lakin mazingira yalikuwa mabaya mabovu usipime. kuna watu wanatafuta mlo wao kwa taabu sana. Mungu wabariki watu wale. niliki maisha yale baada ya kupata Dollar 80 iyo ilikuwa ni kazi yangu ya mwisho na kampuni ya ZARA TOURS
tueleze hali ilikuwaje pale ulipofika kwenye lile jiwe la kubusu
 
Sitosahau kazi ya upagazi kubeba mizigo Kilimanjaro, wale wote maPorter wa Kilimanjaro nawasalimu.

Rafiki yangu alikufa kifo cha kusikitisha nikawa naogopa kumpa taarifa mke wake na mtoto wao alikuwa mdogo. Maiti ilipelekwa singida kwa mazishi. kazi ilikuwa ngumu mno. mzigo ni kilo 20 tu lakin mazingira yalikuwa mabaya mabovu usipime. kuna watu wanatafuta mlo wao kwa taabu sana. Mungu wabariki watu wale. niliki maisha yale baada ya kupata Dollar 80 iyo ilikuwa ni kazi yangu ya mwisho na kampuni ya ZARA TOURS

Mwaka gani ilikua
 
tueleze hali ilikuwaje pale ulipofika kwenye lile jiwe la kubusu
Tunaitaga breakfast kwasababu ukiamka asubuhi na wenge lako unakutana na huo mlima mkali si mchezo, usipokuwa makini unaweza kuporomoka ukapasua kichwa kwenye majabali makubwa

Mwisho wa hiyo hill ndo kuna sehemu inaitwa jiwe la kubusu, hilo jiwe lazima ulikumbatie huku umebeba mzigo wako hakuna namna ndo maana pakaitwa jiwe la kubusu
IMG_20210826_081833.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa ndo wanaitwa ma-porter aka wagumu wanatembea hapo mlimani cruiser cha mtoto.

Experience ya ule mwendo wa kutembea mlimani itakufanya ujue vizuri matumizi ya gear zote 5 za kwenye gari

Gear no 1 hutumika wakati wa kupanda mlima mkali, yaani unageuka gari kabisa na discipline inakuepo hakuna cha race wala nini ni mdogo mdogo

Gear no 2 utakutana na kilima kimeanza kulainika ndo hapo kidogo unavuta wese

Gear no 3 hapo kwa sadala kidogo unapiga story na wana

Gear no 4 na 5 ndo kabisa unachanganya mwendo wese la kutosha uwahi camp kabla wageni hawajakukuta njiani, maana yule guide wa mlima na wageni huwa wanakuwa wa mwisho kufika camp, sasa guide akikukuta njiani ni matusi kilo 7 anakuambia
“ww malaya kaza hiyo sifuri huku hakuna shangazi wala mjomba mpaka saivi hujafika camp unakata viuno na bag la wageni”

Gear no 1 pia hii hutumika wakati wa kushuka mlima hapa ndo utaimba haleluya ni kheri kupanda kuliko kushuka maana kunakuwa na mteremko mkali sana na umebeba mzigo hapo mgongoni yaani miguu inakosa balance kabisa swala la kuanguka na mzigo wako kama tembo ni kawaida sababu ya utelezi maana sehemu nyingi za kushuka huwa zimezungukwa na forest hivyo mvua mvua zinakuwepo through out the seasons
IMG_20210826_103346.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilipewa kazi ya kulinda sehemu karibia na chichi na lacasa chica tulikuwa na kajumba chetu yani ka post tulikuwa wawili

Malaya wakitoka kujiuza chichi wanakuja kujistiri kwenye kibanda maana kurudi mwenyewe saa tisa usku ni mushkeli

Malipo yao ilikuwa ni kuwala mbususu kipindi kile mimi nilikuwa muoga ila mzee ambaye nilikuwa naye ndio zilikuwa pigo zake

Mzee alikufa na ukimwi nikabaki mwenyewe ile kazi nikaipiga chini siku malaya walivyopigana visu kwenye ugomvi wao kwakua waliuana kwenye post yangu ikawa crime scene plus kuchukuliwa maelezo na kuwa shahidi nilikoma
Mkuu hebu andaa thread ya hiki kistory ulichomokaje kwenye hii case?
 
Hawa ndo wanaitwa ma-porter aka wagumu wanatembea hapo mlimani cruiser cha mtoto.

Experience ya ule mwendo wa kutembea mlimani itakufanya ujue vizuri matumizi ya gear zote 5 za kwenye gari

Gear no 1 hutumika wakati wa kupanda mlima mkali, yaani unageuka gari kabisa na discipline inakuepo hakuna cha race wala nini ni mdogo mdogo

Gear no 2 utakutana na kilima kimeanza kulainika ndo hapo kidogo unavuta wese

Gear no 3 hapo kwa sadala kidogo unapiga story na wana

Gear no 4 na 5 ndo kabisa unachanganya mwendo wese la kutosha uwahi camp kabla wageni hawajakukuta njiani, maana yule guide wa mlima na wageni huwa wanakuwa wa mwisho kufika camp, sasa guide akikukuta njiani ni matusi kilo 7 anakuambia
“ww malaya kaza hiyo sifuri huku hakuna shangazi wala mjomba mpaka saivi hujafika camp unakata viuno na bag la wageni”

Gear no 1 pia hii hutumika wakati wa kushuka mlima hapa ndo utaimba haleluya ni kheri kupanda kuliko kushuka maana kunakuwa na mteremko mkali sana na umebeba mzigo hapo mgongoni yaani miguu inakosa balance kabisa swala la kuanguka na mzigo wako kama tembo ni kawaida sababu ya utelezi maana sehemu nyingi za kushuka huwa zimezungukwa na forest hivyo mvua mvua zinakuwepo through out the seasonsView attachment 2327765

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu umetisha sana, hivi kuna wanawake ma porter? Hao jamaa daaa, huruma sana , jamaa kama wakimbizi miziko hadi kichwana maisha hayako fair.
 
Miaka flani hapo moro nasoma chuo cha ujenzi,
Life ngumu,nikashauriwa na jamaa yangu kwanini usiuze hata miwa inalipa...

Nikatafuta jamaa anauza miwa anipe hints, akuwa mchoyo wa michongo.Akanipa maelekezo yote.
Enzi zile wanakodi baiskel kulikua hamna boda,
Mtaji ulikua buku 15 tu.

Nikakodi baiskeli yangu huyooo nikakitafuta chuo cha SUA,nikakipita nikanyonga ngwinjo kuelekea ni "kauzeni" kama sijakosea...majina mengi nimesahau..
Niliendesha baiskeli zaidi ya masaa 2,
Kila ninaposimama kuulizia naambiwa ni hapo mbele..
Unasonga tu hufiki,hatimaye kuna ka mtaa nikafika nikaelekezwa mbele kidogo kuna kijumba.

Nikakuta kuna wazee wakarimu kweli,wakanipa kijana anipeleke shambani sasa...

Ebooo ikabidi niwaulize bado hatujafika?wakasema sio mbali ni hapo tu...nikajiuliza hii hapo tu si ndio ile naambiwa toka kule mwanzo na sikua nafika,Nikasema nishafika mpaka hapa wacha nijipe moyo...

Mana sikua nimezoea kufanya kazi ngum wala kuendesha baiskeli masafa marefu,miguu ilikua inatetemeka na kuchoka kwa umbali mrefu.

Tulitembea tena na baiskel kwa mda,mpaka tunafika sehem kuna kijumba mbele kuna kijinjia si kijinjia hasa ni ki mfereji...

Tukawacha baiskeli na ndala zangu tukaanza fata hicho ki mfereji...
Baada ya mwendo mbele tulikuta shamba kubwa sana la miwa....

Tulipofika dogo akaita mara kadhaa,kuna mzee akaitika akasema niko huku.

Tukasalimiana na mzee nikakaribishwa shamba kwa ukarimu.
Nikaulizwa nataka miwa ya bei gani,nikasema ya buku 10,akasema sawa unaweza kukata,mana mimi nimebanana nina miwa naanda muda si mrefu inakuja kuchukuliwa..

Nikasema naweza,nikapewa panga.

Nikauliza nikate mingapi,
"Niko busy kijana kata unayoweza kubeba"

Wee tamaa ikaniingia nikasahau safari ya nilikotoka.
Miwa ilikua ni mingi mno mingine iko chini tu ni kukataa tu,hapo moyoni nikasema kama ni hivi nitatoboa mapema.

Nikakata mizigo miwili mikubwa ya haja kwa msaada wa dogo [emoji38].

Kimbembe kwenye kubeba kuifikisha njiani baiskeli ilipo sasa.
Kwanza miwa ni mirefu na minene,pili ukibeba mingi inanesanesa na kukuyumbisha.

Mjomba ilibidi niigawe mara nne na bado nilifika kwenye baiskeli kwa tabu sana.
Nikajisemea tabu gani hiii..

Kwenye kuifunga kwenye baiskeli sasa ni mingi haikutosha ikabidi mingine ibaki,mzee anacheka tu...

Kimbembe kingine kuikokota hio baiskel ni shughuli...
Ki ukweli nilifika mjini ila miwa mingine mingi niliacha njiani kidogo niitupe yote.nisije nikafa bure na niliyokuwa nayo kwenye baiskel niliikatakata vipande vipande mana ni mirefu ilikua inanesanesa inasababisha baiskeli kuyumba. .

Sikuwahi kurudi tena na sitarudi.
Tamaa mbaya sana.[emoji28]

#MaendeleoHayanaChama
 
Miaka flani hapo moro nasoma chuo cha ujenzi,
Life ngumu,nikashauriwa na jamaa yangu kwanini usiuze hata miwa inalipa...

Nikatafuta jamaa anauza miwa anipe hints, akuwa mchoyo wa michongo.Akanipa maelekezo yote.
Enzi zile wanakodi baiskel kulikua hamna boda,
Mtaji ulikua buku 15 tu.

Nikakodi baiskeli yangu huyooo nikakitafuta chuo cha SUA,nikakipita nikanyonga ngwinjo kuelekea ni "kauzeni" kama sijakosea...majina mengi nimesahau..
Niliendesha baiskeli zaidi ya masaa 2,
Kila ninaposimama kuulizia naambiwa ni hapo mbele..
Unasonga tu hufiki,hatimaye kuna ka mtaa nikafika nikaelekezwa mbele kidogo kuna kijumba.

Nikakuta kuna wazee wakarimu kweli,wakanipa kijana anipeleke shambani sasa...

Ebooo ikabidi niwaulize bado hatujafika?wakasema sio mbali ni hapo tu...nikajiuliza hii hapo tu si ndio ile naambiwa toka kule mwanzo na sikua nafika,Nikasema nishafika mpaka hapa wacha nijipe moyo...

Mana sikua nimezoea kufanya kazi ngum wala kuendesha baiskeli masafa marefu,miguu ilikua inatetemeka na kuchoka kwa umbali mrefu.

Tulitembea tena na baiskel kwa mda,mpaka tunafika sehem kuna kijumba mbele kuna kijinjia si kijinjia hasa ni ki mfereji...

Tukawacha baiskeli na ndala zangu tukaanza fata hicho ki mfereji...
Baada ya mwendo mbele tulikuta shamba kubwa sana la miwa....

Tulipofika dogo akaita mara kadhaa,kuna mzee akaitika akasema niko huku.

Tukasalimiana na mzee nikakaribishwa shamba kwa ukarimu.
Nikaulizwa nataka miwa ya bei gani,nikasema ya buku 10,akasema sawa unaweza kukata,mana mimi nimebanana nina miwa naanda muda si mrefu inakuja kuchukuliwa..

Nikasema naweza,nikapewa panga.

Nikauliza nikate mingapi,
"Niko busy kijana kata unayoweza kubeba"

Wee tamaa ikaniingia nikasahau safari ya nilikotoka.
Miwa ilikua ni mingi mno mingine iko chini tu ni kukataa tu,hapo moyoni nikasema kama ni hivi nitatoboa mapema.

Nikakata mizigo miwili mikubwa ya haja kwa msaada wa dogo [emoji38].

Kimbembe kwenye kubeba kuifikisha njiani baiskeli ilipo sasa.
Kwanza miwa ni mirefu na minene,pili ukibeba mingi inanesanesa na kukuyumbisha.

Mjomba ilibidi niigawe mara nne na bado nilifika kwenye baiskeli kwa tabu sana.
Nikajisemea tabu gani hiii..

Kwenye kuifunga kwenye baiskeli sasa ni mingi haikutosha ikabidi mingine ibaki,mzee anacheka tu...

Kimbembe kingine kuikokota hio baiskel ni shughuli...
Ki ukweli nilifika mjini ila miwa mingine mingi niliacha njiani kidogo niitupe yote.nisije nikafa bure na niliyokuwa nayo kwenye baiskel niliikatakata vipande vipande mana ni mirefu ilikua inanesanesa inasababisha baiskeli kuyumba. .

Sikuwahi kurudi tena na sitarudi.
Mwamba richie ze best inaonekana kule kauzeni Ni wakulima wazuri Sana wa miwa hasa kuanzia pale Magadu kwenda mbele kule Mzinga
 
Mi nilikuwa naosha vyombo restaurant huko ugaibuni
Nimeosha vyombo ila hapa hapa bongo na haikunishinda,ni 1 ya kazi ambazo kupitia hiyo kazi mafanikio yangu mzizi wake ni hiyo kazi.

Ni kazi yangu ya kwanza iliyonifundisha mengi sana maana hapo kazini kulikua na jiko hivyo nimejua vitu vingi sana kupitia hapo,ila nilikaribishwa kama "muosha vyombo" tena wakati napewa kazi boss aliniuliza "unaweza sugua masufuria yale makubwa" akanipointia yale masufuria ya sherehe,yakang'aaa kama mapya?

nikamwambia shaka ondoa naomba kazi boss,akasema pita karoni Anza kazi nikuone,Nilisugua sufuria aliporudi akauliza,nani kanisaidia kuzisugua,wafanyakazi wakamwambia "huyo sharo wako hapo" kasugua,Nikaajiriwa rasmi kama muosha vyombo.

Kazi niliiipenda nilijivunia mnooo,japo wakati naianza niliianza kwa ugumu na shida sana,si rahisi kama ninavyoandika na kusmulia hapa.

Ki ufupi upambanaji ule wenyewe wenyewe niliuanza kwenye kibarua hicho,Godoro langu la kwanza,kodi yangu ya cghumba cha kwanza DAR nilipata hela kupitia kazi hiyo.

MOSHI HOTEL/MANZESE-TIP TOP
 
Kuna vijana nawajua wanna pataga kazi za kuswaga punda kuwatoa singida, mantra kuwa nafuu kuja kuwauza wilaya za geita wanatembea njiani usiku na mchana wiki 2 ,,,, mmoja aliponea kukiwa na fisi usiku, ILA siku hzi kwa sehemu kafanikiwa anamaisha safiii tuuu, kashaacha kuswaga punda, mvumikivu hula mbivu
 
Nishafanya ukonda
Nishazibua choo
Nishakata michongoma
Nishachukuaga kazi ya kupiga rangi
Nlipopewa advance nkala kona.
Nishauza mazagazaga tx market kinondoni.....enzi hizo wazungu,wageni wakumwaga pale dokoni

Vp niendeleee


Ova
 
Wakati nasoma O level nilikuwa najipikia vimaandazi usiku asubuhi napeleka dukani.
Siku moja usiku nikawa napikia ndani bahati mbaya umeme ukakatika nikawa natumia mshumaa.
Akaingia mdogo wangu kuubeba mshumaa sijui hata alikuwa anaenda kutafuta nini muda ule nilikuwa nimemaliza kupika mafuta nimeipua nimeyaweka chini.
Sijui ilikuwaje nikawa nasimama nitoke pale bahati mbaya nikagusa yale mafuta yakamwagika nikateleza nikaanguka nikaungua mana bado yalikuwa yamoto.

Nimefanya biashara ya mkaa sasa yale magunia yanapangwa kwenda juu ili kushusha gunia lazima upande kwenye kitu ili uweze kuyafikia uvute ile uweze kumimina kwaajili ya wateja wa reja reja.
Siku zote napanda nashusha wala sioni tabu ila sometimes unatumia hata dkk10 kuvuta mpaka lifike chini mana unakuta kwenye kupangwa limebanwa na lenzie so lazima utumia akili na nguvu litoke.
Nna ndoo yangu kubwa huwa naigeuza napanda napambania kombe hadi linashuka na muda mwingine anakuja mteja anabeba na pikipiki lakini dereva hataki kuchafuka hivo unapambana kushusha halafu kulipakia mnasaidiana.
Siku hiyo nimepanda vizuri nikaanza kuvuta sijui nilibugi wapi nilianguka nikaangukia mkono ukateguka nikabaki najiuguza wiki nzima.

Kulima ni kazi kiukweli nikiona mtu ni mkulima hasa wa jembe la mkono namheshimu sana.
Nikiwa advance tulipewa adhabu waliovuta ya kupanda mchicha mpaka uvune ndio adhabu inaisha.
Hapo sijawahi kulima na kwetu hatuna hata shamba mbaya zaidi tukapewa sehemu ambayo ilikuwa imeota ukoka halafu watu wanapatumia pia kama njia palikuwa pagumu ukipiga jembe linadunda.
Aisee sitasahau huyo mwalimu alikuwa akija akikuta mmegusa kidogo anawatoa darasani wenzenu wanasoma nyie mnalima.
Nililima lakini sisogei wala sioni dalili ya kusogea.Tulikuwa na Headgirl wetu alikuwa anapiga kazi basi akija kutusimamia anatusaidia kidogo.Nimelima nasema hapa naweka mbegu naambiwa bado umetifua juu juu tu bado jembe linatakiwa kufika chini.
Mpaka tunakuja kumwaga mbegu mikono imeota malengelenge hadi yamepasuka yanauma balaa.
Part iliyobaki ilikuwa sio ngumu kunyeshea japo maji yalikuwa ya tabu ila bora kufuata maji mbali kuliko kulima.Mwasandende huko ulipo punguza ubabe usio na maana,chuki na upendeleo.

Hapo napofanyia biashara jirani yangu anauza cement.
Akaja mteja anataka mifuko minne ya cement abebewe mpaka eneo lake la kazi.
Changamoto ikawa mbebaji mana boda aliitwa akagoma anataka elfu nne akapunguza mpaka tatu lakini mteja akagoma.
Kuna mama jirani anauza mboga mbaga akauliza atalipwa sh ngapi akaambiwa elfu mbili akakubali.
Kazi yangu ikawa kumsaidia kuweka kichwani na alipaona ni karibu na ukweli ni karibu sema mziki wa uzito wa cement.
Kabeba trip zote ile ya mwisho akajikuta kaingia period ghafla.Kilichomfanya abebe aongezee hela akalipe kibati.
 
Back
Top Bottom