Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Dalmine,
Amin kwa sote na Allah ajaalie viongozi wetu wajue kuwa tunajemga fitna kubwa kwa hii hali ambayo siku moja tutakuja kujuta.

Allah awajaalie viongozi na wauone huu ukweli na wafanye marekebisho kwani dhulma inaangamiza.
 

Attachments

  • VID-20210330-WA0083.mp4
    4.4 MB
Salaam Aleykum sheikh Mohamed Said!
Nilisubiri kwa hamu uandike Taazia/Tanzia ya Hayati Magufuli kipenzi cha wanyonge wakiwemo waislamu.
La Pili nilitamani sana Rais wetu ateue waislamu tupu kwenye sehemu zote ili tupunguze kelele za daraja la pili la watanzania.
Ahsanta
 
Salaam Aleykum sheikh Mohamed Said!
Nilisubiri kwa hamu uandike Taazia/Tanzia ya Hayati Magufuli kipenzi cha wanyonge wakiwemo waislamu.
La Pili nilitamani sana Rais wetu ateue waislamu tupu kwenye sehemu zote ili tupunguze kelele za daraja la pili la watanzania.
Ahsanta
Kipuyo,
Hili suala la mimi kuandika taazia ya JPM nimelijibu kuwa sikupata kumfahamu kwa kiwango cha kuweza kumuhadithia.

Suala la kuteua Waislam watupu hii itakuwa dhulma.

Hivi sasa uwiano ni 20:80 katika serikali na hili halipendezi kuwepo kwenye nchi yeyote yenye waumimi wa imani mbili tofauti moja ikahodhi fursa zote.

Ikiwa sasa utakuwa na Tanzania ambayo Wizara ya Elimu yote iko mikononi kwa Waislam hii ni dhulma na kukaribisha fitna.

Kutahadharisha serikali katika kulinda haki na usawa haijapata kuwa kelele.

Nashukuru kwa kutambua kuwa tunalo daraja la kwanza.
 
Kipuyo,
Hili suala la mimi kuandika taazia ya JPM nimelijibu kuwa sikupata kumfahamu kwa kiwango cha kuweza kumuhadithia.

Suala la kuteua Waislam watupu hii itakuwa dhulma.

Hivi sasa uwiano ni 20:80 katika serikali na hili halipendezi kuwepo kwenye nchi yeyote yenye waumimi wa imani mbili tofauti moja ikahodhi fursa zote.

Ikiwa sasa utakuwa na Tanzania ambayo Wizara ya Elimu yote iko mikononi kwa Waislam hii ni dhulma na kukaribisha fitna.

Kutahadharisha serikali katika kulinda haki na usawa haijapata kuwa kelele.

Nashukuru kwa kutambua kuwa tunalo daraja la kwanza.
Daraja la kwanza ni ninyi Waislamu.
Ukisafiri kwa njia ya barabara karibu kona zote za nchi,hoteli zote zilizopo pembezoni mwa barabara kwa ajili ya abiria kupata chochote zinamilikiwa na waislamu,je kwa nn nisiseme ninyi ni raia daraja la kwanza kwa nchi yetu?

Pili,Matajiri wakubwa nchi hii ni ninyi,kwa nn nisiseme ninyi ni raia daraja la kwanza nchi hii?
Tatu,ukitaka kuchinja nyama kwa matumizi ya watu wengi,lazima ichinjwe na muislamu,sasa kwa nn nisiseme nyie ni daraja la kwanza?

Kilichobaki ni nyie kupewa wizara zote ili tutulie
 
Daraja la kwanza ni ninyi Waislamu.
Ukisafiri kwa njia ya barabara karibu kona zote za nchi,hoteli zote zilizopo pembezoni mwa barabara kwa ajili ya abiria kupata chochote zinamilikiwa na waislamu,je kwa nn nisiseme ninyi ni raia daraja la kwanza kwa nchi yetu?

Pili,Matajiri wakubwa nchi hii ni ninyi,kwa nn nisiseme ninyi ni raia daraja la kwanza nchi hii?
Tatu,ukitaka kuchinja nyama kwa matumizi ya watu wengi,lazima ichinjwe na muislamu,sasa kwa nn nisiseme nyie ni daraja la kwanza?

Kilichobaki ni nyie kupewa wizara zote ili tutulie
Kipuyo,
Tafadhali pitia post za nyuma ujue maudhui ya mjadala huu.
 
Kiongozi ebu elezea hiyo dhulma bas japo kidogo na sisi vijana tuzijue..mana naskia huwa waislam wanalalamika wanafanyiwa dhulma..ni zipi hizo?
 
Lupweko,
Hii hapo chini kanitumia msomaji mmoja:

"Nakumbuka Prof. Ndalichako alipokuwa Mkurugenzi wa Elimu kuna skuli moja ya Kiislamu walifelishwa skuli nzima.

Baada ya Waislam kufuatilia ndio Wizara ikaomba radhi na kusema kuna makosa ya bahati mbaya.

Sitasahau kadhia hiyo na zawadi ya Prof. ikawa ni kuwa, "Promoted to a full ministerial post. Minister of education to date."
Huwa mnalishwaga sumu huko nyie..haha..hv wazir mzima aanze kuhangaika na matokea na shule ya kiislam ili iweje labda?? Wacheni kulalamika mzee..somesheni watoto elimu dunia wacheni kuwachanganyia na lugha za kiarabu ndo mana wanashindwa kumudu darasan..
 
Kiongozi ebu elezea hiyo dhulma bas japo kidogo na sisi vijana tuzijue..mana naskia huwa waislam wanalalamika wanafanyiwa dhulma..ni zipi hizo?
J,
Inaelekea umeingia umeukuta mjadala uko mbali.

Soma post za nyuma taratibu.
 
Huwa mnalishwaga sumu huko nyie..haha..hv wazir mzima aanze kuhangaika na matokea na shule ya kiislam ili iweje labda?? Wacheni kulalamika mzee..somesheni watoto elimu dunia wacheni kuwachanganyia na lugha za kiarabu ndo mana wanashindwa kumudu darasan..
J,
Pitiable post za nyuma hayo yote uliyoandika hapa nimeyaeleza.

Nakusihi jambo dogo.

Jiepushe na kauli za kudhani kuwa unajua.

Ukifanya hivyo huenda ukajifunza mengi kutoka kwangu.
 
Msamehe bure,uzee umemfanya asahau mengi
KAULIZA MWENYE KUULIZA ITAKUWAJE HISTORIA MPYA INAYOANDALIWA IKIFANANA NA HII HISTORIA YA SASA?

Historia ya Tanganyika na kwa makusudi nataka nianze na hii kwa kuwa mimeitafiti na kuandika kitabu ambacho naamini sote tunakifahamu.

Umuhimu wa historia hii unasimama kwenye historia ya kudai uhuru chini ya TANU.
Chuo Cha CCM Kivukoni kilichapa kitabu cha historia ya TANU mwaka wa 1981.

Kitabu hiki kilichapwa baada ya Abubakar Ulotu kuandika historia ya TANU kutoka mswada ulioanza kuandikwa na Abdul Sykes na Dr. Wilbard Kleruu labda mwaka wa 1962.

Uandishi wa kitabu hiki uliingia katika matatizo na Abdul Sykes akajitoa kazi ikakamilishwa na Dr. Kleruu peke yake.

Tatizo katika utafiti huu lilikuwa kwanza nafasi ya baba yake Abdul, Mzee Kleist Sykes katika uasisi wa African Association mwaka wa 1929.

Tatizo jingine likawa nafasi ya Abdul Sykes katika TAA baada ya kifo cha baba yake mwaka wa 1949.
Halafu pakawa na tatizo la Julius Nyerere.

Nini mchango wake katika kuunda TANU?

Abdul alipojitoa katika uandishi wa historia hii ikawa kwa uamuzi ule umetoa fursa kwa waliobakia kuandika historia waliyoitaka wao.
Abdul Sykes akafutwa kwenye historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Mswada huu haukuchapwa na ukawa Maktaba ya TANU Mtaa wa Lumumba na hivi ndivyo ulivyoangukia mikononi kwa Abubakar Ulotu na yeye akachapa kitabu kwa jina lake.

Historia iliyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni haina tofauti na ile "aliyoandika," Abubakar Ulotu.
Miaka ikapita.

Mwaka wa 1998 mimi nikachapa kitabu cha maisha ya Abdul Sykes kitabu kilichoeleza historia ya TANU na harakati za kudai uhuru.
Kitabu hiki kilipindua historia ya TANU juu chini.

Kitabu kilimleta Abdul Sykes na Hamza Mwapachu kama chanzo cha kuundwa kwa TANU na harakati za uhuru.

Kadhalika kitabu katika hili kitabu kikamleta Chief David Kidaha Makwaia katika juhudi za kutafuta kiongozi wa kuongoza harakati za kudai uhuru.

Kuna watu hawakuridhika na kitabu hiki hasa kwa kuwa kilionyesha mchango mkubwa wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Watu hawa wakataka kiandikwe kitabu kuonyesha mchango wa Julius Nyerere katika kuunda TANU.
Kitabu hiki kipo sokoni hivi sasa.

Swali la kujiuliza ni hili.

Je kuna mapya ndani ya kitabu hiki ambayo yanabadilisha yaliyomo kwenye historia ya TANU iliyokwisha andikwa?

Tutegemee nini katika historia hii mpya inayotayarishwa hivi sasa?

Gide...
Katika makala hiyo hapo juu umeona dalili la mtu aliyepotemza utambuzi?

Hii makala iko hapa JF nimeiweka muda mfupi uliopita.
 
KENYA ABDALLAH HASSAN KATIBU MKUU WA KWANZA MUISLAM WIZARA YA ELIMU AMEFARIKI

Kenya Abdallah Hassan nimemfahamu toka utoto wangu Moshi katika miaka ya 1960.

Siku hizo mimi nikiwa shule ya msingi madarasa ya chini sana yeye alikuwa Mawenzi Secondary School.

Kenya alikwenda Makerere, Uganda nilikuja kujua baadae.

Kenya angefariki na mimi wala nisingenyanyua kalamu yangu kuandika chochote kuhusu yeye kama isingetokea mwaka wa 1987 jambo lililogusa Waislam wengi Tanzania.

Mwaka huo Prof. Kighoma Malima alichaguliwa na Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa Waziri wa Elimu.

Hili lilikuwa halijapata kutokea.

Ilikuwa kama vile Rais Mwinyi amevunja mwiko alioweka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere toka uhuru mwaka wa 1961kuwa nafasi hiyo haishikwi na Muislam.

Baada ya kuwa Waziri wa Elimu Prof. Malima Rais Mwinyi akamchagua Kenya Abdallah Hassan kuwa Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.

Rais alikuwa kapiga msumari wa moto juu ya kidonda.

Wizara ilichafuka na wahariri wa magazeti wakawa wanachonga penseli zao ziandike vizuri.

Kuna watendaji ndani ya wizara waliona kama vile sasa bwawa limeingia luba itakuwa tabu kuogelea kwa raha na salama.

Yaliyotokea sasa ni historia.

Prof. Malima aliondolewa kwenye Wizara ya Elimu baada ya kujadiliwa Dodoma.

Hayo ndiyo yaliyofanya mimi hii leo nimkumbuke kaka yangu Kenya Hassan.

Mola amghufirie dhambi zake na amlipe Pepo ya Firdaus.

Amin.

View attachment 1735030
Wanaokuheshimu kwa udini unaoeneza wa shida vichwani mwao.
 
Wanaokuheshimu kwa udini unaoeneza wa shida vichwani mwao.
Bila...
Ujuzi wangu uko katika political history na nimeandika vitabu kadhaa vilivyochapwa na publishers mashuhuri duniani.

Ninayoandika ni haya unayosoma hapa.
Catalogue za vitabu hivi ni Islam, Politics.

Ikiwe wewe unaona kitabu cha Abdul Sykes ni kitabu cha udini hii ni bahati mbaya sana kwako.

Vyuo Vikuu ulimwenguni vinavyosomesha African History wanakitumia kama "corrective history."

Wanasomesha kitabu hiki kujua ukweli na hali halisi.

Wewe unaona udini.
Mimi sina tatizo na hilo.

Angalia uzi huu unafuatiliwa na watu wangapi.
 
Kichuguu,
Muhimu ni yale ambayo Prof. Malima aligundua yanafanyika ndani ya Wizara ya Elimu na akaandika taarifa kwenda kwa Rais.

Rais alishtuka na akajua kuwa anakabiliwa na tatizo kubwa hajapata kukutananalo.
Taarifa hii ya Prof. Malima iliibiwa na kuvujishwa kwenye magazeti.

Taarifa hii ilikuwa kwenye agenda ya kikao cha Dodoma ambacho Nyerere alihudhuria.
Kwa unyeti wa agenda hii ilionekana bora isijadiliwe.

Ndugu yangu wewe unanufaika na mfumo huu ulioko na hili linakufanya ukatae kutaka kuujua kweli.

Je, ulikuwa unayajua haya?

Aliyeiba taarifa ile ya Prof. Malima kwa Rais alifahamika na hakufanywa lolote zaidi alipongezwa.

Nakuwekea hapo chini picha ya Rais Ali Hassan Mwinyi na watendaji wake.
Prof. Malima ni huyo mstari wa mbele wa kwanza kushoto.

View attachment 1738342

Kuna vitu nilivyokwisha andika kuhusu profesa malima kudanganya watu kuwa yeye ndiye alieanzisha utaratibu wa wanafunzi kutumia namba kwenye mitihani ili waislamu wasionewe na wao wakakubali. Wote waliokubali kuwa Malima ndiye aliyeanzisha utaratibu ule itakuwa ni wale ambao hawakuwahi kufanya mitihani hiyo kwani matumizi ya namba kwenye mitihani yaliachwa na mkoloni, na wala utaratibu huo haukuwahi kubadilishwa. Malima akatia uwongo kuwa watoto wenye majina ya kiislamu walikuwa wanafelishwa, na hiyo ikampa wafuasi ambao walikuwa hawajui mitihani ile ilikuwa inatungwa na kusahihishwaje.

Usahihisjai wa matokeo ya darasa la saba ulikuwa unafanywa na waalimu wa misingi huo huko mikoani ambapo kila swali lilikuwa lisahahishiwa na grupu la waalimu wachache tu; na grupu hilo lilikuwa halijui swali jingine mwanafunzi huyo kafanya nini. Mitihani ya darasa la 12 ilikuwa inasahahihishwa na kundi la waalimu wa shule za sekondari kwa utaratibu kama huo huo wa darasa la saba. Mitihani mingi ya darasa la 14 ilikuwa isahahihishwa na waalimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam. Sasa maofisa wa wizara wangeingiliaje matokeo ya usahihishaji wa mitihani hiyo na kuwafelisha watoto wa kiislamu tu?

Hata hivyo, yeye akiwa pale Wizarani, je alibadilisha nini? Je alipofukzwa Wizara ya fedha ilikuwa pia ni kwa sababu ya Nyerere kumchukia kwa vile ni mwislamu?

Malima hata historia yake ya kwenda kusoma marekani ninaijua na niliwahi kuiweka hapa; safari yake ya kwanza ilikuwa ni kuombewa na Nyerere kutoka kwenye conncetions alizokuwa nazo wakati huo. Malima asingekuwa hapo alipofikia bila Nyerere kumpeleka Marekani kwa mara ya kwanza wakati akiwa Katibu wa TANU Rufiji. Babu alimfukuza Malima pale wizara ya Mipango kwa vile alisema alikuwa incompetent, ndipo Nyerere aakampeleka UDSM kama profesa. Alipoanza juhudi za kurudi kwenye siasa, ni Nyerere aliyempigia debe sana mwaka 1981, na baadaye kumfanya kuwa waziri wa mipango - akaleta SAP ambayo haikusaidia kujenga uchumi bali blah blah tu.

Kwa vile malima alikuwa incompetent kweli kama alivyosema Babu, hakuna la maana alilofanya kwenye kila position aliyopewa hadi ikafikia hata mwisho Mwinyi naye akamfukuza wizara ya fedha. Chuo kikuu pale alipotoa professorial inaugural lecture yake ya "Political Economy of Devaluation in Developing Countries" wataalamu wote wa uchumi walijiuliza huyu ni profesa gani.

Kutokana na Malima kufilisika kimawazo, ndiyo akaona akakimbilia siasa za dini, na njia pekee ya kuwapata wafuasi wenye mlengo wa dini ni kumshambulia nyerere. Kwa waislamu wa aina hiyo ukishamshambulia Nyerere kuwa alikuwa anapiga vita uislamu, unawapata wengi sana, na ndiyo siasa za watu wa namna hiyo.
 
Kuna vitu nilivyokwisha andika kuhusu profesa malima kudanganya watu kuwa yeye ndiye alieanzisha utaratibu wa wanafunzi kutumia namba kwenye mitihani ili waislamu wasionewe na wao wakakubali. Wote waliokubali kuwa Malima ndiye aliyeanzisha utaratibu ule itakuwa ni wale ambao hawakuwahi kufanya mitihani hiyo kwani matumizi ya namba kwenye mitihani yaliachwa na mkoloni, na wala utaratibu huo haukuwahi kubadilishwa. Malima akatia uwongo kuwa watoto wenye majina ya kiislamu walikuwa wanafelishwa, na hiyo ikampa wafuasi ambao walikuwa hawajui mitihani ile ilikuwa inatungwa na kusahihishwaje.

Usahihisjai wa matokeo ya darasa la saba ulikuwa unafanywa na waalimu wa misingi huo huko mikoani ambapo kila swali lilikuwa lisahahishiwa na grupu la waalimu wachache tu; na grupu hilo lilikuwa halijui swali jingine mwanafunzi huyo kafanya nini. Mitihani ya darasa la 12 ilikuwa inasahahihishwa na kundi la waalimu wa shule za sekondari kwa utaratibu kama huo huo wa darasa la saba. Mitihani mingi ya darasa la 14 ilikuwa isahahihishwa na waalimu wa chuo kikuu cha Dar es salaam. Sasa maofisa wa wizara wangeingiliaje matokeo ya usahihishaji wa mitihani hiyo na kuwafelisha watoto wa kiislamu tu?

Hata hivyo, yeye akiwa pale Wizarani, je alibadilisha nini? Je alipofukzwa Wizara ya fedha ilikuwa pia ni kwa sababu ya Nyerere kumchukia kwa vile ni mwislamu?

Malima hata historia yake ya kwenda kusoma marekani ninaijua na niliwahi kuiweka hapa; safari yake ya kwanza ilikuwa ni kuombewa na Nyerere kutoka kwenye conncetions alizokuwa nazo wakati huo. Malima asingekuwa hapo alipofikia bila Nyerere kumpeleka Marekani kwa mara ya kwanza wakati akiwa Katibu wa TANU Rufiji. Babu alimfukuza Malima pale wizara ya Mipango kwa vile alisema alikuwa incompetent, ndipo Nyerere aakampeleka UDSM kama profesa. Alipoanza juhudi za kurudi kwenye siasa, ni Nyerere aliyempigia debe sana mwaka 1981, na baadaye kumfanya kuwa waziri wa mipango - akaleta SAP ambayo haikusaidia kujenga uchumi bali blah blah tu.

Kwa vile malima alikuwa incompetent kweli kama alivyosema Babu, hakuna la maana alilofanya kwenye kila position aliyopewa hadi ikafikia hata mwisho Mwinyi naye akamfukuza wizara ya fedha. Chuo kikuu pale alipotoa professorial inaugural lecture yake ya "Political Economy of Devaluation in Developing Countries" wataalamu wote wa uchumi walijiuliza huyu ni profesa gani.

Kutokana na Malima kufilisika kimawazo, ndiyo akaona akakimbilia siasa za dini, na njia pekee ya kuwapata wafuasi wenye mlengo wa dini ni kumshambulia nyerere. Kwa waislamu wa aina hiyo ukishamshambulia Nyerere kuwa alikuwa anapiga vita uislamu, unawapata wengi sana, na ndiyo siasa za watu wa namna hiyo.
Inside 10,
Maudhui ya uzi huu si Prof. Malima wala Julius Nyerere.

Ukitaka tuwazungumze watu hawa wafungulie uzi mpya mimi nitakuja In Shaa Allah.

Nina mswada nimekamilisha kuhusu historia hii.

Prof. Malima kuwa mtu asiyejiweza yaani "incompetent," kisha awe alma mater wa Princeton University ambayo ni Ivy League ni vitu visivyoingia akilini na ukweli huu ni mbali kuwa akiwa mwanafunzi Mzumbe alikuwa akiongoza katika hesabu.

Kisha huyu mtu asiyejiweza akawa mhadhiri Idara ya Uchumi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kisha Waziri wa Fedha.

Jitulize ondoa ghadhabu pitia post za nyuma nisome kwa utulivu angalia naeleza nini.

Tatizo lililokuwako Wizara ya Elimu limefahamika vyema kwa taarifa ya Prof. Malima kwa Rais Mwinyi.

Hiki ndicho kisa cha chuki dhidi yake.

Wizara ya serikali iligeuzwa kuwa mahali pa kunufaisha jamii moja dhidi ya nyingine.

Na hata walipokutana Dodoma kuhusu suala hili kwa uzito na unyeti wa suala hili Nyerere aliamua lisijadiliwe.

Unadhani mimi niko hapa kufanya mchezo?

Fungua uzi wa Prof. Malima na Nyerere In Shaa Allah nitakuja kusomesha na nyote mtanufaika na nitakayoeleza.
 
Prof. Malima kuwa mtu asiyejiweza yaani "incompetent," kisha awe alma mater wa Princeton University ambayo ni Ivy Leaguebni vitu visivyoingia akilini na ukweli huu ni mbali kuwa akiwa mwanafunzi Mzumbe alikuwa akiongoza katika hesabu.

Kisha huyu mtu asiyejiweza akawa mhadhiri Idara ya Uchumi Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Kuwa Alma Mater wa Princeton ambayo iko kwenye ivy league siyo hoja; kuna wengi waliosoma Yale, Princeton, MIT, Harvard, Pennynsylvania na shule kadhaa amabazo ni za ivy league ambao ni intellectually failure kabisa - Trump ni mmojawapo!. Wewe uliwahi kusoma Ph.D thesis yake? Je theisis hiyo ilitoa publications ngapi? Kwa list ya publications zake zote pale UDSM zilikuwa ni zile opinionated kuhusu mikopo na world bank, siyo zenye research based evidence. Niliahsoma maandishi yake mengi sana tangu nikiwa mwanafuzi wa UDSM; huyu jamaa alikuwa shallow sana. Ukitaka assessement nzuri zaid kuhusu depth ya malima mwulize Professor Issa Shivji au Professor Samwel Wangwe wakuambie.

Kwa Malima aliyewahi kupewa madaraka mbalimbali serikalini, haitakiwi kusema kuwa alisoma chuo fulani kwa hiyo ni superman, anatakaiwa aonyeshe matokeo ya elimu aliyopata huko kama kweli alielimika. Ana bahati mbaya kuwa alipewa uwanja wa kuonyesha uwezo wake akashindwa.

Inawezekana hujui kuwa Baada ya Malima kutoka Marekani alipangiwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchumi na Mipango ambayo ilikuwa inaongozwa na Abdulrhaman Babu. Huyu Babu ndiye aliyesema kuwa Malima ni incompetent kuongoza uchumi wa nchi ! siyo maneno yangu

Kutokana na Babu kumkataa kama Katibu mkuu wa wizara yake- wote walikuwa ni waislamu, ndipo Nyerere akampelekea UDSM kuwa Associate Professor kwa sababu mshahara aliokuwa nao kama Katibu Mkuu ulikuwa ni ngazi hiyo. Malima hakuwahi kuwa Lecturer akafanya research za kupanda kuwa au Senior Lecturer; alitoka wizarani na kuwa Associate Professor wa UDSM moja kwa moja kwa maagizo ya Nyerere. Kwa hiyo yeye kuwa Professor wa UDSM kwa kupewa position siyo blanket la kuficha udhaifu wake. Kuna watu wanaitwa adjunct professor nao wanaweza kufundisha chuo kikuu, hujui hilo?
 
Kichuguu,
Tuko pale pale nimesema ufunguliwe uzi wa Prof. Malima maudhui ya uzi huu uko wazi.

Nimetabasamu kidogo ulipomtaja Prof. Issa Shivji kuwa naweza kupata yakini kutoka kwake.

Prof. Issa Shivji tunafahamiana vyema.

Wakati yeye, Prof. Saida Othman na Dr. Ng'wazi Kamata wanaandika kitabu cha Julius Nyerere Prof. Shivji alinihoji hasa kuhusu Nyerere na uhusiano wake na wazee wangu.

Nilimweleza kila kitu na nikatoa nyaraka na picha.

Kwa ufupi niliwapa hazina yote kuhusu Nyerere niliyokuwanayo Maktaba.

Hapa mimi nasimama.

Kasome kitabu cha Nyerere na angalia Prof. Issa Shivji kaandika nini kuhusu mimi.

Kwa kuwa tuko katika suala la elimu nitakueleza nini Prof. Shivji kaandika kuhusu Waislam.

Nyerere aliivunja EAMWS mwaka wa 1968 na kuunda BAKWATA wakati EAMWS inajenga Chuo Kikuu Cha Waislam na yeye ndiye aliyeweka jiwe la msingi.

Prof. Shivji ameandika kuwa EAMWS ilikuwa inajenga Islamic Centre sio Chuo Kikuu.

Nilisikitika sana.

Prof. Shivji kaandika hivi ili isionekane kuwa Nyerere ana mkono katika kurudisha nyuma maendeleo ya Waislam katika elimu.

Naamini umenielewa.
Haya ndiyo matatizo tuliyonayo.

20210331_073712.jpg
 
Kichuguu,
Tuko pale pale nimesema ufunguliwe uzi wa Prof. Malima maudhui ya uzi huu uko wazi.

Nimetabasamu kidogo ulipomtaja Prof. Issa Shivji kuwa naweza kupata yakini kutoka kwake.

Prof. Issa Shivji tunafahamiana vyema.

Wakati yeye, Prof. Saida Othman na Dr. Ng'wazi Kamata wanaandika kitabu cha Julius Nyerere Prof. Shivji alinihoji hasa kuhusu Nyerere na uhusiano wake na wazee wangu.

Nilimweleza kila kitu na nikatoa nyaraka na picha.

Kwa ufupi niliwapa hazina yote kuhusu Nyerere niliyokuwanayo Maktaba.

Hapa mimi nasimama.

Kasome kitabu cha Nyerere na angalia Prof. Issa Shivji kaandika nini kuhusu mimi.

Kwa kuwa tuko katika suala la elimu nitakueleza nini Prof. Shivji kaandika kuhusu Waislam.

Nyerere aliivunja EAMWS mwaka wa 1968 na kuunda BAKWATA wakati EAMWS inajenga Chuo Kikuu Cha Waislam na yeye ndiye aliyeweka jiwe la msingi.

Prof. Shivji ameandika kuwa EAMWS ilikuwa inajenga Islamic Centre sio Chuo Kikuu.

Nilisikitika sana.

Prof. Shivji kaandika hivi ili isionekane kuwa Nyerere ana mkono katika kurudisha nyuma maendeleo ya Waislam katika elimu.

Naamini umenielewa.
Haya ndiyo matatizo tuliyonayo.

View attachment 1739219
Historia za namna hii hazitakupa raha maisha yako yote! Kuna historia nzr na za kurithi siyo hizi!! Kila jema!
 
Historia za namna hii hazitakupa raha maisha yako yote! Kuna historia nzr na za kurithi siyo hizi!! Kila jema!
Saimile,
Hakuna siku nilifurahi kama siku nilipokikamata kitabu changu mkononi kikitokea London kwa publisher mwaka wa 1998.

Hakuna siku nilifurahi kama siku baada ya kufanya mhadhara University of Iowa baada ya Prof. Jonathan Glassman kunisikia pale pale akanialika nikatoe mhadhara chuoni kwake Northwestern University, Evanston, Chicago.

Hiki chuo ndiyo kinaongoza ulimwenguni katika ufundishaji wa African History.

Katika kunishukuru Glassman aliiambia hadhira kuwa nimeandika historia ambayo wengi hawakuwa wanaifahamu.

Abdul Sykes alikuwa kaondolewa kabisa katika historia ya Tanganyika licha kuwa ndiye aliyempokea Nyerere na kumsaidia kuchukua uongozi wa TAA 1953 na 1954 wakaunda TANU.

Mimi ninafuraha kubwa kuona kuwa nimewarudisha wazee wangu wote katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika baada ya kufutwa.

Wewe unaungua roho kwa kuwa labda kwenu hamna historia kama hii yangu unapata shida kuona Waislam walivyokuwa mstari wa mbele kupambana na ukoloni.

1617462083144.png
 
Back
Top Bottom