Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Hakuna kuchelewa wala nini. Sehemu pakiwa na ubaguzi utajua tu. Unajua watu ambao hawana fursa ya kurekebisha uzembe waliofanya katika maisha yao wakati wa ujana au utoto huwa wanatafuta visingizio vya kuonyesha kuwa haikuwa wao bali walisababishiwa.

Unajua mtu mvivu wa kufiriki huwa anatengeneza nadharia na kuifanya kuwa ni majibu kamili. Ila ukimwambia akupe evidence utaona anavyotekenyeka na kubadili mikao.

Mimi mtaa nilipokulia kuna watu wa imani za kiislam na kikristo, tulisoma shule moja ya msingi na pia tulienda shule za sekondari tofauti ila zote zinatumia mtaala m'moja wa elimu.

Na tulipomaliza sekondari, kuna ambao walikwenda vyuo vya Tanzania, na wapo waliokwenda nje, mimi sikuwahi kuomba kusoma vyuo vya nje sababu nilikuwa muoga kuishi mbali na familia yangu.

Lakini still nilipokwenda chuo bado nilikutana na wengine na tulisoma wengine walifaulu kunizidi, wengine walikuwa viongozi serikali ya wanafunzi.

Na sasa nimemaliza elimu ya chuo nipo uraiani kupambana na uchumi ila bado nakutana na wenzangu tukiishi maisha katika hali ya ufanano.


Muda wote huu sikuwahi kufikiria kuwa kuna mfumo wa dini ambao unawabania watu baadhi wasiweze kupenya popote na kufanya maisha.

Sasa huwa nashangaa sana nikisikia kuna mtu analalamika kuwa kuna hicho kitu ambacho, mimi na wenzangu tusikione kweli.....?!

Aiseeee kuna watu sijui ni malezi waliopitia, unakuta mtu kalelewa na bibi huko tokea utotoni sasa anavyokuwa mtu mzima anaanza kutafuta wa kumdekea kama alivyodeka kwa bibi.

Maisha sio hisia, maisha ni uhalisia. Yeye sasa kama anaamini kuna udini haya akalage baho, wenzake ndio haoooo tunatafuta maisha tunajenga inchi. Fainali ni uzeeni huko.
Huyu mzee wetu kila alipo yeye ni kuhisi tu wanatendewa uonevu na kubaguliwa wakati mimi nimekuwa na kuishi nao, ila sijawahi kusikia wala kuona wanabaguliwa maana hakuna sehemu kwenye nchi hii unapoambiwa toa cheti cha dini yako ndo uhudumiwe au huo ubaguzi uko huko tu kwenye ngazi za juu?
 
Mzee elimu yako na uzoefu ulionao ni mkubwa sana.

Niombe utupatie maoni yako kuhusu vikundi mbalimbali vya wanaharakati kama Alshababu au Alkaida au Boko haram ili tuweze ongeza ufahamu.

Je, wanaharakati hao wanaotetea Uislamu kwanini wanapigwa vita kila kukicha?

Aksante sana
 
Huyu mzee wetu kila alipo yeye ni kuhisi tu wanatendewa uonevu na kubaguliwa wakati mimi nimekuwa na kuishi nao, ila sijawahi kusikia wala kuona wanabaguliwa maana hakuna sehemu kwenye nchi hii unapoambiwa toa cheti cha dini yako ndo uhudumiwe au huo ubaguzi uko huko tu kwenye ngazi za juu??
Boom...
Hoja ya kuonyesha cheti si hoja ya maana.
 
Inatusaidia nini katika ulimwengu huu wa sasa?
 
Mzee elimu yako na uzoefu ulionao ni mkubwa sana

Niombe utupatie maoni yako kuhusu vikundi mbalimbali vya wanaharakati kama Alshababu au Alkaida au Boko haram ili tuweze ongeza ufahamu.

Je wanaharakati hao wanaotetea Uislamu kwanini wanapigwa vita kila kukicha?

Aksante sana
Uzalendo,
Nina mada nilitoa University of Ibadan mwaka wa 2006 kuhusu ugaidi.

Naingia In Shaa Allah Maktaba kukutafutia.
 
Kulikua na haja gani ya kusema muislamu wa kwanza..acha udini acha inferiority complex..somesheni watoto.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Jiwe,
Haja ilikuja kutokana na yale yaliyotokea katika Wizara ya Elimu pale kwa mara ya kwanza Waislam wawili waliposhika nafasi za juu - Waziri na Katibu Mkuu.

Vurugu kubwa ilitokea kuhitaji majadiliano Dodoma.

Ukiyajua haya?
 
Sam,
Udini ni kule kueleza kuwa walikuwapo watu katika watendaji wa Wizara ambao hawakupendezewa na kuwa na Waziri na Katibu Mkuu Waislam?

Tafadhali nifahamishe.
Mzee wangu,

Kiongozi akiwa wa dini fulani hilo linasaidia nini ??
 
Kulikua na haja gani ya kusema muislamu wa kwanza..acha udini acha inferiority complex..somesheni watoto.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Jiwe...
Sababu ni kwa kuwa hujui.

Naingia Maktaba nitakuwekea taarifa itakayokuthibitishia kuwa tatizo si kuwa watoto hawapelekwi shule.

Jiwe hebu tazama hii taarifa hapo chini:

''Lakini tuende kielimu.

Ninayo ripoti ya mwaka huu.
Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu.

Asilimia 29 ni wengine.
Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21.

Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe.
Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79.

Katika asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21.

Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu.

Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga.

Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha.
Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini.

Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini.
Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini.''

(Hotuba ya Mh. Kitwana Selemani Kondo Bungeni, Dodoma 1999)
 
Twaisubiri kwa hamu kubwa
Uzalendo...
Kama nilivyoahidi paper yangu ni hiyo hapo chini.

ISLAM, TERRORISM AND AFRICAN DEVELOPMENT​


ISLAM, TERRORISM AND AFRICAN DEVELOPMENT
8th– 10th FEBRUARY 2006

Venue
University of Ibadan Conference Centre
Organised by Department of Arabic and Islamic Studies

UNIVERSITY OF IBADAN
NIGERIA

‘TERRORISM’ IN EAST AFRICA
The Tanzanian Experience

Speaker

Mohamed Said


1617025969972.png

Mstari wa pili kutoka mbele wa kwanza kulia aliyevaa kanzu nyeupe na kofia ni mimi Mohamed Said Salum Abdallah nikifuatilia mjadala Chuo Kikuu Cha Ibadan, Nigeria.
 
We jamaaa ni mshmba sana udini umekujaa kila siku uislam uislam. Tatizo ndugu zako wakacha elimu wakakimbilia madrasa na bahati mbaya teuzi zinaangalia elimu dunia na sio madrasa.
Enjai...
Waislam walikuwa wanajenga Chuo Kikuu mwaka wa 1968.
Mradi huu ukahujumiwa.

Je, hii ni sura ya watu wasiothamini elimu?
Kuna mengi hamyajui lakini hamjakubali kuwa hamyajui.
 
Udini udini udini

Ova
Mrangi,
Historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ndivyo ilivyokuwa ingawa leo hii wewe inakukera pengine kwa ugeni wa Dar es Salaam, au kwa kutokuwa wa kizazi kile au kwa kukosa kuwa na waliopigania uhuru huko utokako au ndani ya familia yako.

Hii ndiyo inakupa shida unalalamika kwa nini Uislam, Waislam, Uislam katika historia hii?
Nimekutolea kipande hiki kutoka Maktaba:

DINI ILIVYOTUMIKA KUWAUNGANISHA WATANGANYIKA DHIDI YA UKOLONI
SEHEMU YA KWANZA: MWANZO WA HARAKATI 1950

Utangulizi
Nami nasubiri patulie In Shaa Allah nataka niandike jinsi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alivyochaguliwa kuongoza harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika katika kikao cha watu watatu Nansio, Ukerewe nyumbani kwa Hamza Kibwana Mwapachu mwaka wa 1953 na moja ya sifa kubwa iliyotajwa ni dini yake.

Wazalendo hao wote watatu waliokubaliana kumkabidhi Baba wa Taifa uongozi walikuwa Waislam, mmojawapo akiwa Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika).

Kisha nitaeleza vikao vyote vya dua alivyoshiriki Baba wa Taifa pamoja na Waislam katika kumlilia Allah awape msaada Watanganyika washinde dhulma zote za Waingereza na Allah alikubali dua ya wenye kudhulumiwa.

Ndipo ninapouliza nini kimetokea?

1617053964244.png
 
KENYA ABDALLAH HASSAN KATIBU MKUU WA KWANZA MUISLAM WIZARA YA ELIMU AMEFARIKI

Kenya Abdallah Hassan nimemfahamu toka utoto wangu Moshi katika miaka ya 1960.

Siku hizo mimi nikiwa shule ya msingi madarasa ya chini sana yeye alikuwa Mawenzi Secondary School.

Kenya alikwenda Makerere, Uganda nilikuja kujua baadae.

Kenya angefariki na mimi wala nisingenyanyua kalamu yangu kuandika chochote kuhusu yeye kama isingetokea mwaka wa 1987 jambo lililogusa Waislam wengi Tanzania.

Mwaka huo Prof. Kighoma Malima alichaguliwa na Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa Waziri wa Elimu.

Hili lilikuwa halijapata kutokea.

Ilikuwa kama vile Rais Mwinyi amevunja mwiko alioweka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere toka uhuru mwaka wa 1961kuwa nafasi hiyo haishikwi na Muislam.

Baada ya kuwa Waziri wa Elimu Prof. Malima Rais Mwinyi akamchagua Kenya Abdallah Hassan kuwa Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.

Rais alikuwa kapiga msumari wa moto juu ya kidonda.

Wizara ilichafuka na wahariri wa magazeti wakawa wanachonga penseli zao ziandike vizuri.

Kuna watendaji ndani ya wizara waliona kama vile sasa bwawa limeingia luba itakuwa tabu kuogelea kwa raha na salama.

Yaliyotokea sasa ni historia.

Prof. Malima aliondolewa kwenye Wizara ya Elimu baada ya kujadiliwa Dodoma.

Hayo ndiyo yaliyofanya mimi hii leo nimkumbuke kaka yangu Kenya Hassan.

Mola amghufirie dhambi zake na amlipe Pepo ya Firdaus.

Amin.

View attachment 1735030
malima na kenya walipokuwa Wizara ya elimu walileta mabadiliko gani ya maana unayokumbuka ambayo unaamini yaliondoa unachoita "dhulma." Miaka nenda rudi tunajua kuwa shule nyingi za kiislamu zimekuwa zinafanya vibaya sana wakati shule nyingi za kikatoliki zikifanya vizuri sana.

Tatizo siyo wizara wala rais bali tatizo ni mfumo wa ufundishaji. Nakumbuka marehemu Dr Omar Juma wakati akiwa makamu wa rais aliwahi kuhutubia kikao fulani cha maulidi kwa kuhimiza waislamu kupeleka watoto shule na kutumia muda wa ziada kwenye masomo ya dini badala ya kutumia muda mwingi kwenye masomo ya dini na kuifanya shule kama kitu cha ziada. Bila kubadilisha mfumo huo, hata kama utapata rais, waziri wa elimu, katibu mkuu wa elimu, na wakurugenzi wote wizara ya elimu ambao ni wasilamu, tatizo hiyo la inequity katia elimu halitatoweka!
 
malima na kenya walipokuwa Wizara ya elimu walileta mabadiliko gani ya maana unayokumbuka ambayo unaamini yaliondoa unachoita "dhulma." Miaka nenda rudi tunajua kuwa shule nyingi za kiislamu zimekuwa zinafanya vibaya sana wakati shule nyingi za kikatoliki zikifanya vizuri sana.

Tatizo siyo wizara wala rais bali tatizo ni mfumo wa ufundishaji. Nakumbuka marehemu Dr Omar Juma wakati akiwa makamu wa rais aliwahi kuhutubia kikao fulani cha maulidi kwa kuhimiza waislamu kupeleka watoto shule na kutumia muda wa ziada kwenye masomo ya dini badala ya kutumia muda mwingi kwenye masomo ya dini na kuifanya shule kama kitu cha ziada. Bila kubadilisha mfumo huo, hata kama utapata rais, waziri wa elimu, katibu mkuu wa elimu, na wakurugenzi wote wizara ya elimu ambao ni wasilamu, tatizo hiyo la inequity katia elimu halitatoweka!
Kichuguu,
Muhimu ni yale ambayo Prof. Malima aligundua yanafanyika ndani ya Wizara ya Elimu na akaandika taarifa kwenda kwa Rais.

Rais alishtuka na akajua kuwa anakabiliwa na tatizo kubwa hajapata kukutananalo.
Taarifa hii ya Prof. Malima iliibiwa na kuvujishwa kwenye magazeti.

Taarifa hii ilikuwa kwenye agenda ya kikao cha Dodoma ambacho Nyerere alihudhuria.
Kwa unyeti wa agenda hii ilionekana bora isijadiliwe.

Ndugu yangu wewe unanufaika na mfumo huu ulioko na hili linakufanya ukatae kutaka kuujua kweli.

Je, ulikuwa unayajua haya?

Aliyeiba taarifa ile ya Prof. Malima kwa Rais alifahamika na hakufanywa lolote zaidi alipongezwa.

Nakuwekea hapo chini picha ya Rais Ali Hassan Mwinyi na watendaji wake.
Prof. Malima ni huyo mstari wa mbele wa kwanza kushoto.

20210330_070423.jpg
 
Back
Top Bottom