Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Kenya Abdallah Hassan, Katibu Mkuu wa kwanza Muislam Wizara ya Elimu, amefariki

Lupwelo,
Hilo kweli linawezekana wala hakuna wasiwasi.

Naingia Maktaba nikuwekee jambo lingine.

''Lakini tuende kielimu. Ninayo ripoti ya mwaka huu. Waliofanya mtihani wa darasa la saba kuingia darasa la tisa, asilimia 71 Waislamu. Asilimia 29 ni wengine.

Walioshinda katika wale asilimia 71 ni asilimia 21. Katika wale 29 walioshinda tena sema mwenyewe.

Katika asilimia 29 waliokwenda shuleni ni asilimia 79.
asilimia 71 waliokwenda darasa la tisa ni asilimia 21.

Sasa kuna moja, ama Waislamu wajinga ama akili yao haifanyi kazi, ama mtu ukiwa Muislamu wewe huna kitu, ama kuna kitu.

Sasa namwomba Waziri anayehusika, anaposema aseme ya kwamba kwa hali ilivyo Waislamu wameumbwa wajinga.

Au kwa hali ilivyo kuna sababu kadha, kadha.

Mwalimu Nyerere alisema zamani ifanywe bidii ya kuwanyanyua waliokuwa chini.

Sasa bidii hii siyo ya kuwanyanyua waliokuwa chini. Bidii hii ni ya kuwakandamiza waliokuwa chini.''

(Mh. Kitwana Kondo Bungeni, Dodoma
Kama ulisoma ukaelewa utafaulu tu haya maswala ya dini kisingizio tu, kuna wasomi wengi tu wakiislamu walisoma wakafaulu ila pia hayo matatizo mlisababisha wenyewe wengi wenu mnaona elimu dunia haina maana at least mmebadilika siku hizi.
 
Kwa sasa marais wote tanzania ni waislam! Unajisikiaje sasa! Roho kwatu
Kolola,
Tatizo si hilo.

Tatizo ni ubaguzi.

Soma historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika uone hali ilikuwaje wakati wa kupigania uhuru.
 
kama ulisoma ukaelewa utafaulu tu haya maswala ya dini kisingizio tu, kuna wasomi wengi tu wakiislamu walisoma wakafaulu ila pia hayo matatizo mlisababisha wenyewe wengi wenu mnaona elimu dunia haina maana at least mmebadilika siku hizi.
Tig,
Unazungumza somo usilolijua.
 
Tig,
Unazungumza somo usilolijua.
may be!!


but wewe nakufahamu kupitia maandiko yako mengi sana, unapenda sana maswala ya udini. kulikuwa na ulazima gani kuanzisha uzi ati katibu mkuu wa kwanza wa wizara ya elimu muislamu! uislamu wake unahusiana nini na utumishi wake serikalini?

hadi leo sijawahi ona mantiki ya dini ya mtu katika uongozi wa taifa ikiwa katiba imejieleza wazi kuwa hii nchi sio ya kidini. Hata rais ,mawaziri wawe wote waislamu ama wapagani ama wakristo as long as wanafanya majukumu yao kwa mujibu wa katiba dini zao hazituhusu hayo ni mambo binafsi.
 
Lupweko,
Hii hapo chini kanitumia msomaji mmoja:

"Nakumbuka Prof. Ndalichako alipokuwa Mkurugenzi wa Elimu kuna skuli moja ya Kiislamu walifelishwa skuli nzima.

Baada ya Waislam kufuatilia ndio Wizara ikaomba radhi na kusema kuna makosa ya bahati mbaya.

Sitasahau kadhia hiyo na zawadi ya Prof. ikawa ni kuwa, "Promoted to a full ministerial post. Minister of education to date."
Mzee Said,
Mume wa Prof ni Muislam. Maajabu!
 
may be!!


but wewe nakufahamu kupitia maandiko yako mengi sana, unapenda sana maswala ya udini. kulikuwa na ulazima gani kuanzisha uzi ati katibu mkuu wa kwanza wa wizara ya elimu muislamu! uislamu wake unahusiana nini na utumishi wake serikalini?

hadi leo sijawahi ona mantiki ya dini ya mtu katika uongozi wa taifa ikiwa katiba imejieleza wazi kuwa hii nchi sio ya kidini. Hata rais ,mawaziri wawe wote waislamu ama wapagani ama wakristo as long as wanafanya majukumu yao kwa mujibu wa katiba dini zao hazituhusu hayo ni mambo binafsi.
Tig,
Bahati mbaya "labda," hujui kuwa nchi yetu Tanzania ina tatizo hili na ndiyo sababu unaandika vitu ambavyo havina ithibati.

Tuna tatizo kubwa ni mgawanyo wa madaraka baina ya Waislam na Wakristo kwa kiasi hiki cha 20:80.

Waislam wako nje ya uongozi katika nyanja zote.

Wala huhitaji kufanya utafiti hili liko wazi.
Baraza la mawaziri 23 Waislam ni 3 tu.

Anglia nafasi katika serikali na mashirika ya umma.

Nakujibu kwa kuwa ni wajibu wangu kukufahamisha kile ambacho "labda," akili yako haijaweza kutambua.

Waislam wanatarajia majibu kutoka serikalini si kutoka kwa raia wenzetu ambao wengi wao wananufaika na hali hii.

Haya niandikayo si udini hata kwa mbali ni suala la kutaka haki na usawa.

Kichekesho kikubwa ni pale unapojaribu kuwaingiza ati Wapagani hii leo.

Wapagani walikuwapo wakati TANU inaundwa mwaka wa 1954 kupigania uhuru wa Tanganyika?

Unaijua idadi yao ndani ya serikali na fursa walizonazo?

Jifunze kwanza historia ya uhuru uielewe.

Hili si tatizo la kuandika kichwa kikiwa kitupu na umeghadhibika.

Haya mambo yanahitaji utulivu wa akili na kuuangalia ukweli.

Ungeridhika kuona Baraza la Mawaziri 23 ndani Waislam 20 na Wakristo 3?

Mtu yeyote mwenye akili iliyotimia lazima atajiuliza kwa nini iwe hivi?

Kwa kuhitimisha unasema unanifahamu.

Hapana hunijui.
 
Waisilamu nyie endeleeni kujipa elimu ahera hii ya duniani waachieni wakristu wapambane nayo mzee Mohamed
 
KENYA ABDALLAH HASSAN KATIBU MKUU WA KWANZA MUISLAM WIZARA YA ELIMU AMEFARIKI

Kenya Abdallah Hassan nimemfahamu toka utoto wangu Moshi katika miaka ya 1960.

Siku hizo mimi nikiwa shule ya msingi madarasa ya chini sana yeye alikuwa Mawenzi Secondary School.

Kenya alikwenda Makerere, Uganda nilikuja kujua baadae.

Kenya angefariki na mimi wala nisingenyanyua kalamu yangu kuandika chochote kuhusu yeye kama isingetokea mwaka wa 1987 jambo lililogusa Waislam wengi Tanzania.

Mwaka huo Prof. Kighoma Malima alichaguliwa na Rais Ali Hassan Mwinyi kuwa Waziri wa Elimu.

Hili lilikuwa halijapata kutokea.

Ilikuwa kama vile Rais Mwinyi amevunja mwiko alioweka Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere toka uhuru mwaka wa 1961kuwa nafasi hiyo haishikwi na Muislam.

Baada ya kuwa Waziri wa Elimu Prof. Malima akamchagua Kenya Abdallah Hassan kuwa Katibu Mkuu katika Wizara hiyo.

Prof. alikuwa kapiga msumari wa moto juu ya kidonda.

Wizara ilichafuka na wahariri wa magazeti wakawa wanachonga penseli zao ziandike vizuri.

Kuna watendaji ndani ya wizara waliona kama vile sasa bwawa limeingia luba itakuwa tabu kuogelea kwa raha na salama.

Yaliyotokea sasa ni historia.

Prof. Malima aliondolewa kwenye Wizara ya Elimu baada ya kujadiliwa Dodoma.

Hayo ndiyo yaliyofanya mimi hii leo nimkumbuke kaka yangu Kenya Hassan.

Mola amghufirie dhambi zake na amlipe Pepo ya Firdaus.

Amin.

View attachment 1735030
Mzee wangu Mohamedi Said,Unajua kwamba RAIS wa kwanza Mwanamke wa Tanzania ni Muislamu tena Mzanzibari?Unajua kwamba Mwanamke huyu asingekuwa RAIS wa nchi kama kweli Tanzania kuna udini kama unavofikiri?Nataka leo mimi na wewe tuambizane ukweli,Mtu hawezi kubaguliwa bila yeye mwenyewe kujibagua ama kwa mwenendo wake au kwa mtazamo wake au kwa tabia yake na matendo yake.Ubaguzi wowote huanzia hapa hapo.

Kwa nionavyo mimi,Waislamu wachache ambao mmebahatika kaupata ilimu mmeshindwa kuwatendea haki waislamu wenzenu kwa kuwainua na badala yake mmebaki kulaumu na kulalamika mkitaka kubebwa na mbeleko.Wewe ni mzee,Nataka sasa unambie Je unafikiri kwamba Kuteuliwa kwa Malima kuwa waziri wa elimu kulikuwa ni kwa sababu ya dini yake?Je unafikiri kuondolewa katika nafasi hiyo kulikuwa ni kwa sababu ya dini yake?

Kwamba aliyemteu alikuwa mwinyi muislamu mwenzake na aliyemtengua ni Mwinyi muislamu mwenzake na mnataka kusingizia ubaguzi wa kidini?HAPANA MZEE wangu ,umegahfiirika katika hili na katika mengi.Labda mimi sijakuelewa nia na mantiki yako hasa ni nini,kwani maandiko yako yamesheheni mambo mazuri mengi ambayo yanatufaa wengi bila kujali dini zetu ingawa kwa kweli huwa nakuonea huruma sana unapoharibu ujumbe wako mwanana kwa kuingiza UISLAMU as if it is a PRIME.

Kubali kataa mzee wangu hata kama unaitaka pepo na umeamua kutumia kalamu yako kuwatetea waislamu bado hujanishawishi kwamba kuna ubaguzi wa serikali dhidi ya waislamu hapana,Ninachojua ni kwamba kuna ukosefu wa mwamko katika jamii kubwa ya waislamu na wachache wenye muamko hawawahamsishi wenzao wawe na mwamko sijui ni kwa nini.

Wote mnajifanya ni victims,hata wale ambao mna wajibu wa kubadili narative kama wewe.Niseme tu labda ni kwa sababu ya tabia na imani zenu za kutupiana majini n.k. mnajikuta mnaogopana na kutokupendana.Au ni kwa sababu imani yenu inawafanya mtamani mngekuwa waarabu nanyi mnaamini kwamba ninyi ni sawa na waarabu na mnaufahamu uislamu kuliko waarabu wenye QURANI yao.

Ombi langu kwako;Nipe wasifu wa Kighoma Malima na utendaji wake katika kipindi hicho kifupi alipokuwa waziri wa ELimu pamoja na huyo katibu wake.Niambe mageuzi waliyoleta katika elimu ambayo yalileta TIJA nami nitakubaliana nawe kwamba hao ni waislamu Murua,Pembeni ya hapo TUSEME tu aliyekuwa KATIBU Mkuu wa ELIMU ameifariki Dunia nasi tutamwombea DUA NJEMA KWA MUUMBA

Samahani kama nimekuwa Offensive,Ila naumia sana wasomi kama ninyi mnapotumia Dini na Imani kujenga BIAS katika Jamii huku mkiacha hata kuchukua hatua ndogo tu kuhamasisha watu wenu wainuke na kukua.

MODS napendekeza Nyuzi ZOTE za HUYU MZEE wetu zihamishiwe JUKWAA la DINI ili anagalau tunavozisoma tusoma kama historia ya harakati za WAISLAMU wa TANZANIA kudai usawa kutoka kwa MAKAFIRI.

Ashakum si matusi,Unisamehe kama nimekosa adabu ila kama kuna lenye kujenga lipokee na pale nilipokosea nikosoe.IT IS NOT PERSONAL and I will keep reading YOU.
 
Tig,
Bahati mbaya "labda," hujui kuwa nchi yetu Tanzania ina tatizo hili na ndiyo sababu unaandika vitu ambavyo havina ithibati.

Tuna tatizo kubwa ni mgawanyo wa madaraka baina ya Waislam na Wakristo kwa kiasi hiki cha 20:80.

Waislam wako nje ya uongozi katika nyanja zote.

Wala huhitaji kufanya utafiti hili liko wazi.
Baraza la mawaziri 23 Waislam ni 3 tu.

Anglia nafasi katika serikali na mashirika ya umma.

Nakujibu kwa kuwa ni wajibu wangu kukufahamisha kile ambacho "labda," akili yako haijaweza kutambua.

Waislam wanatarajia majibu kutoka serikalini si kutoka kwa raia wenzetu ambao wengi wao wananufaika na hali hii.

Haya niandikayo si udini hata kwa mbali ni suala la kutaka haki na usawa.

Kichekesho kikubwa ni pale unapojaribu kuwaingiza ati Wapagani hii leo.

Wapagani walikuwapo wakati TANU inaundwa mwaka wa 1954 kupigania uhuru wa Tanganyika?

Unaijua idadi yao ndani ya serikali na fursa walizonazo?

Jifunze kwanza historia ya uhuru uielewe.

Hili si tatizo la kuandika kichwa kikiwa kitupu na umeghadhibika.

Haya mambo yanahitaji utulivu wa akili na kuuangalia ukweli.

Ungeridhika kuona Baraza la Mawaziri 23 ndani Waislam 20 na Wakristo 3?

Mtu yeyote mwenye akili iliyotimia lazima atajiuliza kwa nini iwe hivi?

Kwa kuhitimisha unasema unanifahamu.

Hapana hunijui.
Mzee wangu,Unatetea haki za waislamu,ARISE and SHINE.Inuanenei ninyi wenye kwa kupeana Maarifa na kuungana Mkono.Mjenge tabia ya kutokuwababgua wengine kwani,Ukiona mnahisi kuwa mnabaguliwa basi jua kabisa kuwa nanyi ni wabaguzi mmezidiwa keti.OVA.Najua hoja yangu inaweza kuwa si sawa lakini sitaki kabisa kusikia kwamba KIGEZO cha kuwa waziri ni DINI.In short ni kwamba DINI ni personal issu huko SERIKALINI hamuendi kuhubiri DINI mnaenda kuchapa KAZI.SO KAMA UNAFIKIRI KUWA MUISLAMU NI KIGEZO CHA KUWA WAZIRI basi NENDA KULE ZENJI AMBAKO KUNA WAKRISTO LAKINI SIDHANI HATA KAMA KUNA MKRISTO AMBAYE ANAONGOZA SHEHIA.Acheni kujazana ujinga kuwa mnaonewa na kubaguliwa ilihali mnajibagua wenyewe.
 
Mzee wangu Mohamedi Said,Unajua kwamba RAIS wa kwanza Mwanamke wa Tanzania ni Muislamu tena Mzanzibari?Unajua kwamba Mwanamke huyu asingekuwa RAIS wa nchi kama kweli Tanzania kuna udini kama unavofikiri?Nataka leo mimi na wewe tuambizane ukweli,Mtu hawezi kubaguliwa bila yeye mwenyewe kujibagua ama kwa mwenendo wake au kwa mtazamo wake au kwa tabia yake na matendo yake.Ubaguzi wowote huanzia hapa hapo.

Kwa nionavyo mimi,Waislamu wachache ambao mmebahatika kaupata ilimu mmeshindwa kuwatendea haki waislamu wenzenu kwa kuwainua na badala yake mmebaki kulaumu na kulalamika mkitaka kubebwa na mbeleko.Wewe ni mzee,Nataka sasa unambie Je unafikiri kwamba Kuteuliwa kwa Malima kuwa waziri wa elimu kulikuwa ni kwa sababu ya dini yake?Je unafikiri kuondolewa katika nafasi hiyo kulikuwa ni kwa sababu ya dini yake?

Kwamba aliyemteu alikuwa mwinyi muislamu mwenzake na aliyemtengua ni Mwinyi muislamu mwenzake na mnataka kusingizia ubaguzi wa kidini?HAPANA MZEE wangu ,umegahfiirika katika hili na katika mengi.Labda mimi sijakuelewa nia na mantiki yako hasa ni nini,kwani maandiko yako yamesheheni mambo mazuri mengi ambayo yanatufaa wengi bila kujali dini zetu ingawa kwa kweli huwa nakuonea huruma sana unapoharibu ujumbe wako mwanana kwa kuingiza UISLAMU as if it is a PRIME.

Kubali kataa mzee wangu hata kama unaitaka pepo na umeamua kutumia kalamu yako kuwatetea waislamu bado hujanishawishi kwamba kuna ubaguzi wa serikali dhidi ya waislamu hapana,Ninachojua ni kwamba kuna ukosefu wa mwamko katika jamii kubwa ya waislamu na wachache wenye muamko hawawahamsishi wenzao wawe na mwamko sijui ni kwa nini.

Wote mnajifanya ni victims,hata wale ambao mna wajibu wa kubadili narative kama wewe.Niseme tu labda ni kwa sababu ya tabia na imani zenu za kutupiana majini n.k. mnajikuta mnaogopana na kutokupendana.Au ni kwa sababu imani yenu inawafanya mtamani mngekuwa waarabu nanyi mnaamini kwamba ninyi ni sawa na waarabu na mnaufahamu uislamu kuliko waarabu wenye QURANI yao.

Ombi langu kwako;Nipe wasifu wa Kighoma Malima na utendaji wake katika kipindi hicho kifupi alipokuwa waziri wa ELimu pamoja na huyo katibu wake.Niambe mageuzi waliyoleta katika elimu ambayo yalileta TIJA nami nitakubaliana nawe kwamba hao ni waislamu Murua,Pembeni ya hapo TUSEME tu aliyekuwa KATIBU Mkuu wa ELIMU ameifariki Dunia nasi tutamwombea DUA NJEMA KWA MUUMBA

Samahani kama nimekuwa Offensive,Ila naumia sana wasomi kama ninyi mnapotumia Dini na Imani kujenga BIAS katika Jamii huku mkiacha hata kuchukua hatua ndogo tu kuhamasisha watu wenu wainuke na kukua.

MODS napendekeza Nyuzi ZOTE za HUYU MZEE wetu zihamishiwe JUKWAA la DINI ili anagalau tunavozisoma tusoma kama historia ya harakati za WAISLAMU wa TANZANIA kudai usawa kutoka kwa MAKAFIRI.

Ashakum si matusi,Unisamehe kama nimekosa adabu ila kama kuna lenye kujenga lipokee na pale nilipokosea nikosoe.IT IS NOT PERSONAL and I will keep reading YOU.
Andoza,
Huna sababu ya kunitaka radhi kwani hujanikosea kitu.

Tatizo ni umeghadhibika na hili ni jambo la kawaida nakutananalo kila siku katika mjadala huu.

Mimi si mtaalamu wa dini elimu yangu yote ni sekula na nimeaandika mengi katika papers na vitabu na kuhadhiri vyuo kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani katika political history ya Tanganyika.

Nimesahihisha historia ya uhuru wa Tanganyika kupitia kitabu changu, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," Minerva Press London, 1998.

Ikiwa hiki si kitabu cha dini vipi makala zangu ziwekwe Jukwaa la Dini kama ulivyopendekeza?

Angalia catalogue ya Library of Congress uone hiki kitabu kimewekwa kwenye category gani.

Ikiwa hupendi makala zangu kuwapo Jukwaa la Historia dawa ni kutozifungua.

Waislam wanasubiri majibu kutoka serikalini si kwa raia wenzao kwa nini hali imekuwa hivi licha ya wao kueleza tatizo hili kwa miaka mingi sasa.
 
Zama za wagalatia zimeshakwisha, sasa ni zamu za maamuma. Mzee Said utanawiri sana na makala zako za kihistoria zenye mbegu ya kidini ndani yake. Huenda ukatoboa fresh zamu hii.
 
Zama za wagalatia zimeshakwisha, sasa ni zamu za maamuma. Mzee Said utanawiri sana na makala zako za kihistoria zenye mbegu ya kidini ndani yake. Huenda ukatoboa fresh zamu hii.
Zanzibar...
Unadhani wazee wangu waliunda TANU kupigania uhuru wa Tanganyika kwa kutatizika na dhiki zao binafsi katika chakula, mavazi nk?

Babu yangu Salum Abdallah katika maisha yake ya kupambana na dhulma za ukoloni aliongoza migomo mitatu mikubwa kati ya mwaka wa 1947 na 1960 akiwa kiongozi.

Mgomo uliotia fora na utadumu katika kumbukumbu ya historia ya Tanganyika ni mgomo wa Railways wa mwaka wa 1960 uliodumu siku 82.

Salum Abdallah alikuwa katika kamati ya siri ya kuunda TANU kati ya mwaka wa 1953 - 1954 na mwaka wa 1955 aliunda Tanganyika Railways African Union (TRAU) akiwa Mwenyekiti Muasisi, Christopher Kassanga Tumbo akiwa Katibu.

Kipi kinachokupelekea wewe udhani mimi nahangaishwa na tumbo langu?

Hayo ni matusi dhidi yangu mimi hapa natoa mawazo yangu kama mwananchi kwa kutegemea kuwa nitasikika na viongozi wetu.

Acha serikali itoe majibu.
 
Magufuli Angekua muislam sa hizi ungekua umeshaandika tazia (sina uhakika kama nimeandika vizuri)Mzee ni muandishi na mchambuzi wa maswala ya kihistoria lakini tatizo lako unaendekeza mno udini mzee wangu sasa unakua kama mwanaharakati wa kidini zaidi tunashindwa kuwa huru kwenye mabandiko yako
 
Magufuli Angekua muislam sa hizi ungekua umeshaandika tazia (sina uhakika kama nimeandika vizuri)Mzee ni muandishi na mchambuzi wa maswala ya kihistoria lakini tatizo lako unaendekeza mno udini mzee wangu sasa unakua kama mwanaharakati wa kidini zaidi tunashindwa kuwa huru kwenye mabandiko yako
Dude...
Hili la kutoandika taazia ya Rais Magufuli ni kuwa sikuwa namfahamu kwa kiasi cha kuweza kumwandika.

Mwezi uliopita nimeandika taazia ya Jim Mdoe.

Huyu si Muislam.

Jim Mdoe alikuwa Muanglikana kutoka Bonde.

Soma nilichosema kuhusu Jim Mdoe:

Thread 'Kwaheri kaka yangu, mzungumzaji wangu Jimmy Mdoe' Kwaheri kaka yangu, mzungumzaji wangu Jimmy Mdoe

Taazia ya Arthur Mambeta aliyekuwa mwanasoka wa sifa katika miaka ya uchezaji wake:

 
Andoza,
Huna sababu ya kunitaka radhi kwani hujanikosea kitu.

Tatizo ni umeghadhibika na hili ni jambo la kawaida nakutananalo kila siku katika mjadala huu.

Mimi si mtaalamu wa dini elimu yangu yote ni sekula na nimeaandika mengi katika papers na vitabu na kuhadhiri vyuo kadhaa Afrika, Ulaya na Marekani katika political history ya Tanganyika.

Nimesahihisha historia ya uhuru wa Tanganyika kupitia kitabu changu, "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika," Minerva Press London, 1998.

Ikiwa hiki si kitabu cha dini vipi makala zangu ziwekwe Jukwaa la Dini kama ulivyopendekeza?

Angalia catalogue ya Library of Congress uone hiki kitabu kimewekwa kwenye category gani.

Ikiwa hupendi makala zangu kuwapo Jukwaa la Historia dawa ni kutozifungua.

Waislam wanasubiri majibu kutoka serikalini si kwa raia wenzao kwa nini hali imekuwa hivi licha ya wao kueleza tatizo hili kwa miaka mingi sasa.
Naendelea kusisitza kwamba unayoheshima yako kama mwanazuoni na Unao wajibu wako kama Muislam.Je unataka sasa Serikali ikujibu nini tofauti na majibu tunayokupa wananchi wenzako?Raia wenzako ambao sisi sote kwa pamoja ni Watanzania?Unafikri serikali itafanya kwa matakwa ya dini fulani?Unafikiri wanaopewa nyadhifa wanapewa kwa sababu ya DINI zao?

Ndugu yangu yumkini hujui,ila historia inaonesha kwamba kila mahali ambapo waislamu walipewa cheo hata kidogo walionesha kiwango kikubwa sana cha ubaguzi wa dini.Walishindwa kuonesha utofauti wao kiutendaji.Nafikri tukubali tukatae ukweli ni kwamba Waislamu Tanzania hawabaguliwi na katika hali ya kawaida kabisa hizo takwimu zako unazoleta za kwamba kuna waislamu wachache katika nyadhifu naweza kuziita ni uchochezi tena mbaya sana.Kama kuna Muislamu mwenye kigezo na amenyimwa fursa kwa sababu ya imani yake basi anayo haki ya kulalamika na kulaumu la hakuna basi tuache kuleta chokochoko.Pelekeni watoto wenu shule.Mnaona JINSI TANZANIA ILIVO NJEMA pamoja na ninyi waislamu kuwanyanyasa wanawake,Tanzania imemuinua mwanamke muislamu kuwa RAIS wa TANZANIA.Kama sivyo sijui mpewe nini.Labda tuweke aya za QURAN kwenye sarafu zetu,Na kufanya KIARABIA KUWA LUGHA YA TAIFA?
 
Huna busara, Mchochezi
MTV,

UCHOCHEZI WA MAKARATASI YA ALLY SYKES KWA WAAFRIKA WA TANGANYIKA: KISA CHA ALLY SYKES NA AMRI KWEYAMBA KACHERO WA SPECIAL BRANCH 1953

Ilikuwa katika miaka ya 1980s wakati huo nafanya utafiti wa kitabu cha Abdul Sykes ni yangu ikiwa kuandika historia ya TANU kupitia Nyaraka za Sykes.

Nimekuta nyaraka iliyokuwa imechapwa kwa ''cyclostyle,'' juu imeandikwa ''Kwa Waafrika Wote wa Tanganyika.''

Ujumbe uliokuwapo ni kuwataka Waafrika wote wa Tanganyika wajiunge na TAA kwani kuna jambo kubwa linakuja.

Nilikuwa naandika katikati ya juma na siku ya Jumamosi ndiyo siku kama nilikuwa na maswali nakwenda ofisini kwa Ally Sykes kupata majibu na maelezo mengine.

Nilipomwonyesha nyaraka ile Ally Sykes nilimuona kachangamka na kafurahi sana.

Akanambia kuwa nyaraka ile ilimletea matatizo makubwa.

Siku hiyo ndiyo aliponihadithia kisa cha yeye kuitwa na kusakwa kama mchochezi.

Ally Sykes anasema baada ya kuwa na uhakika kuwa mwaka wa 1954 kwenye Mkutano Mkuu wa TAA wanaunda TANU yeye alipewa kazi ya kuandika na kusamabaza makaratasi ya kuhamasisha Waafrika kujiunga kwa wingi na TANU ili chama kikiundwa kiwe na wanachama wa kutosha.

Ally Sykes alikuwa na mashine ya kudurufu nyumbani kwake Mtaa wa Kipata.

Mkabala wa nyumba hii alikuwa anaishi baba yangu Said Salum.

Katika baraza hiyo ya nyumba aiyokuwa anaishi baba yangu alikuwa Mzee Kitwana akishona nguo na cherehani yake ya Singer.

Wazee wangu hawa wameona haya yote kwa macho yao mawili.

Ally Sykes akawa sasa anachapa makaratasi haya ya mwito kwa Waafrika kujiunga na TAA kisha anawapa vijana maalum waliokuwa wanafanyakazi katika treni za Reli ya Kati na wao wakawa kwa siri kubwa wanazisambaza kila stesheni kuanzia Morogoro, Dodoma, Tabora hadi Mwanza na Kigoma.

Special Branch wakawa na taarifa kuwa kuna makaratasi ya uchochezi yanasambazwa kwa Waafrika.

Ikawa sasa kuna msako mkubwa wa kutafuta mashine hii na mchapaji wa makaratasi hayo ya uchochezi.

Haukupita muda Special Branch wakajua kuwa mashine ya makaratasi ya uchochezi iko Mtaa wa Kipata nyumbani kwa Ally Sykes na yeye ndiye mchapaji wake.

Ndani ya TAA bila uongozi kufahamu walikuwa na makachero wawili waliokuwa wanapeleka taarifa zote za TAA serikalini - Alexander Thobias na Ali Mwinyi Tambwe.

Kipindi hiki President wa TAA alikuwa Julius Nyerere na Vice President Abdulwahid Sykes, Joseph Kasella Bantu akiwa Secretary General.

Amri Kweyamba akaweka mtego wa kumnasa Ally Sykes.

Mtego ukafyatuka siku moja mchana.

Ndugu yangu MTV,
Hebu niambie unaamini kuwa Ally Sykes alikuwa mchochezi?

Vipi kuhusu Julius Nyerere, Abdul Sykes na Kasella Bantu na wao pia kama viongozi wa TAA tuwaite pia wachochezi?

Mimi natokana na wazee wangu waliounda TANU na naijua vizuri historia ya kupigania haki na madhila yake.

Sishangai kuniona sina busara na "mchochezi."

Kisa ni kuwa natafuta haki na usawa.

Haya yaliwakuta wazee wangu waliopigania uhuru wa Tanganyika kutafuta hayo.

Picha hiyo hapo chini Ally Sykes na mimi ofisini kwake Mtaa wa Makunganya miaka mingi nyuma.

1616927047091.png
 
Naendelea kusisitza kwamba unayoheshima yako kama mwanazuoni na Unao wajibu wako kama Muislam.Je unataka sasa Serikali ikujibu nini tofauti na majibu tunayokupa wananchi wenzako?Raia wenzako ambao sisi sote kwa pamoja ni Watanzania?Unafikri serikali itafanya kwa matakwa ya dini fulani?Unafikiri wanaopewa nyadhifa wanapewa kwa sababu ya DINI zao?

Ndugu yangu yumkini hujui,ila historia inaonesha kwamba kila mahali ambapo waislamu walipewa cheo hata kidogo walionesha kiwango kikubwa sana cha ubaguzi wa dini.Walishindwa kuonesha utofauti wao kiutendaji.Nafikri tukubali tukatae ukweli ni kwamba Waislamu Tanzania hawabaguliwi na katika hali ya kawaida kabisa hizo takwimu zako unazoleta za kwamba kuna waislamu wachache katika nyadhifu naweza kuziita ni uchochezi tena mbaya sana.Kama kuna Muislamu mwenye kigezo na amenyimwa fursa kwa sababu ya imani yake basi anayo haki ya kulalamika na kulaumu la hakuna basi tuache kuleta chokochoko.Pelekeni watoto wenu shule.Mnaona JINSI TANZANIA ILIVO NJEMA pamoja na ninyi waislamu kuwanyanyasa wanawake,Tanzania imemuinua mwanamke muislamu kuwa RAIS wa TANZANIA.Kama sivyo sijui mpewe nini.Labda tuweke aya za QURAN kwenye sarafu zetu,Na kufanya KIARABIA KUWA LUGHA YA TAIFA?
Andoza,
Nimekusoma.
 
Mzee wangu Mohamedi Said,Unajua kwamba RAIS wa kwanza Mwanamke wa Tanzania ni Muislamu tena Mzanzibari?Unajua kwamba Mwanamke huyu asingekuwa RAIS wa nchi kama kweli Tanzania kuna udini kama unavofikiri?Nataka leo mimi na wewe tuambizane ukweli,Mtu hawezi kubaguliwa bila yeye mwenyewe kujibagua ama kwa mwenendo wake au kwa mtazamo wake au kwa tabia yake na matendo yake.Ubaguzi wowote huanzia hapa hapo.

Kwa nionavyo mimi,Waislamu wachache ambao mmebahatika kaupata ilimu mmeshindwa kuwatendea haki waislamu wenzenu kwa kuwainua na badala yake mmebaki kulaumu na kulalamika mkitaka kubebwa na mbeleko.Wewe ni mzee,Nataka sasa unambie Je unafikiri kwamba Kuteuliwa kwa Malima kuwa waziri wa elimu kulikuwa ni kwa sababu ya dini yake?Je unafikiri kuondolewa katika nafasi hiyo kulikuwa ni kwa sababu ya dini yake?

Kwamba aliyemteu alikuwa mwinyi muislamu mwenzake na aliyemtengua ni Mwinyi muislamu mwenzake na mnataka kusingizia ubaguzi wa kidini?HAPANA MZEE wangu ,umegahfiirika katika hili na katika mengi.Labda mimi sijakuelewa nia na mantiki yako hasa ni nini,kwani maandiko yako yamesheheni mambo mazuri mengi ambayo yanatufaa wengi bila kujali dini zetu ingawa kwa kweli huwa nakuonea huruma sana unapoharibu ujumbe wako mwanana kwa kuingiza UISLAMU as if it is a PRIME.

Kubali kataa mzee wangu hata kama unaitaka pepo na umeamua kutumia kalamu yako kuwatetea waislamu bado hujanishawishi kwamba kuna ubaguzi wa serikali dhidi ya waislamu hapana,Ninachojua ni kwamba kuna ukosefu wa mwamko katika jamii kubwa ya waislamu na wachache wenye muamko hawawahamsishi wenzao wawe na mwamko sijui ni kwa nini.

Wote mnajifanya ni victims,hata wale ambao mna wajibu wa kubadili narative kama wewe.Niseme tu labda ni kwa sababu ya tabia na imani zenu za kutupiana majini n.k. mnajikuta mnaogopana na kutokupendana.Au ni kwa sababu imani yenu inawafanya mtamani mngekuwa waarabu nanyi mnaamini kwamba ninyi ni sawa na waarabu na mnaufahamu uislamu kuliko waarabu wenye QURANI yao.

Ombi langu kwako;Nipe wasifu wa Kighoma Malima na utendaji wake katika kipindi hicho kifupi alipokuwa waziri wa ELimu pamoja na huyo katibu wake.Niambe mageuzi waliyoleta katika elimu ambayo yalileta TIJA nami nitakubaliana nawe kwamba hao ni waislamu Murua,Pembeni ya hapo TUSEME tu aliyekuwa KATIBU Mkuu wa ELIMU ameifariki Dunia nasi tutamwombea DUA NJEMA KWA MUUMBA

Samahani kama nimekuwa Offensive,Ila naumia sana wasomi kama ninyi mnapotumia Dini na Imani kujenga BIAS katika Jamii huku mkiacha hata kuchukua hatua ndogo tu kuhamasisha watu wenu wainuke na kukua.

MODS napendekeza Nyuzi ZOTE za HUYU MZEE wetu zihamishiwe JUKWAA la DINI ili anagalau tunavozisoma tusoma kama historia ya harakati za WAISLAMU wa TANZANIA kudai usawa kutoka kwa MAKAFIRI.

Ashakum si matusi,Unisamehe kama nimekosa adabu ila kama kuna lenye kujenga lipokee na pale nilipokosea nikosoe.IT IS NOT PERSONAL and I will keep reading YOU.
Huyu mzee wetu ana udini sana.
 
Back
Top Bottom