Tatizo lako wewe mawazo yako yote yametawaliwa na neno "Kenya" sijui kwanini, jaribu kuzungusha ubongo wako nyuzi 360.
Huyo jamaa aliyekua na magari ya Summry, hajawahi kuhuza hata gunia moja la mahindi kwa nchi ya Kenya, yeye yupo Sumbawanga, ni zaidi ya Kilometa 2000 hadi Nairobi, gharama ya kusafirisha mahindi toka Sumbawanga ni kubwa sana.
Summry na mikoa yote ya kusini mwa Tanzania, masoko yao yapo DRC, Zambia, Malawi, Zimbabwe na Msumbiji. Nchi ilipiga marufuku kuuza chakula nje ya nchi, ndio sababu wakulima walilalamika, wewe unageuza unasema walizuia kwenda Kenya pekee, wacha kufikiria Kenya kama nchi pekee, Solo la Kenya kwa chakula cha Tanzania, halizidi 10%, DRC ni soko kubwa kwetu kuliko Kenya.
Sent using
Jamii Forums mobile app