DeepPond
JF-Expert Member
- Nov 18, 2017
- 41,728
- 103,997
Ni kijana wa Miaka 25, shahada ya Ualim, ila hakubahatika kupata ajira rasmi.
Amejiajiri kwa kufungua twisheni za mitaani na kabahatika kupata mchumba ambae ni binti wa Miaka 21 ( Ila tayar ana mtoto wa Miaka 3). Amedumu kwenye mahusiano na binti kwa mwaka mmoja tangu Desemba 2020 na Sasa na mwezi Januari 2021 alishika ujauzito wake. Ambapo kwa Sasa anamimba yenye miez 5, kijana akaona afanye mchakato wa kuanza Kuishi rasmi pamoja na binti.
Kaandika barua ya uchumba ukweni imepelekwa na imekubaliwa, majibu yamerudishwa vimeorodheshwa vitu kadhaa na pesa taslim ambazo ukijumlisha inakuja jumla ya 4,600,000 (million 4 na laki 6)
Kijana akazungumza na mshenga kua icho kiwango Ni kikubwa na hawez kabisa kukimudu, mshenga kamshauri asiogope Ayo yanazungumzika na kitapunguzwa Sana watakapoenda kutambulishwa.
Siku ya kutambulishwa maongezi ya punguza yanaendelea, ila Mwisho kabisa wazazi na Ndugu wa MKE wakaishia milioni 2 taslimu (million 1 kwa ajili ya mahari na million 1 Ni faini ya uchafuzi- kuzalisha kabla ya kuoa ). Na mkaja wa mama laki 5 na vitu mchanganyiko vinavyogharimu laki 7. Jumla vyote unapata million 3 na laki 2.
Kijana kasema yeye hicho kiwango hana na hawezi kupata kabisa kwa sasa, kwa kazi anayofanya haimruhusu kabisa kupata kiasi icho. Akasema yeye alijiandaa kwa million 1 na laki 5 kwa Mambo yote.
Mshenga akaliwasilisha kwa Wazee, Wazee wakasema "ilo haliwezekani kijana maana kwenye ukoo wetu hamna mtu ameolewa chini ya million 2 mahari na vitu vyetu, iyo umependelewa kutokana na uchumi Wako Kama alivyotuambiwa na binti yetu"
Kijana akakubali ila akaomba alipe kwa awamu, 1.5million afu baadae atamalizia 1.7million. Wazee Nalo wakakataa kata kata kua hamna cha kupunguza hapo, labda akajipange KWANZA akiwa tayari aje
Kijana amepanik, Ameondoka amemuacha binti kwao na anazunguka uku na kule Anaomba akopeshwe pesa ili akamilishe zoezi. Kaja KWANGU kwetu Kama watu wake wa karibu tumsaidie kwa Hali na mali kakamilisha zoezi lake ili alilokwisha lianza. Kaniomba nimsaidie au nimkopeshe kiasi icho, Kiukweli nafsi yangu imegoma kabisa na nimemwambia kabisa kua yeye Ni rafki yangu ila kumchangia suala Hilo maana naona anajitwika mzigo mkubwa wkt uwezo wake ni mdogo.
Kuna vipaumbele vingi vya Ela ila sio kwa ilo, ila Kama uwezo anao apambane mwenyewe tutamsapoti kwa vingine.
Kijana
Amepambana kwa kuuza baadhi ya vitu vyake vya ndani Kama laptop, dressing table na stendi ya viatu. Jumla vyote kauza kapata laki 5 na 50.
Amepambana tena ameenda Kwenye taasisi flani izi za mitaani ya kukopesha fedha, ameweka bond kiwanja alichaochiwa na marehem mama ake mzazi kwa ajili ya mkopo wa 1.3 million kwa miezi 6. Kaniomba nikamdhamini, na kiroho Safi nimemdhamini na mkopo kapata chap kaenda kumaliza zoezi lake.
Ila baada ya kijana kuondoka NIMEBAKI NA MASWALI YAFUATAYO KICHWANI:
1. mahari Ni malipo ya shukrani kwa wazazi kwa kumtunza vema binti yao.
-Inakuaje kijana alazimishwe kulipia mahari kubwa kwa binti ambae alimkuta bila bikra?
Kibaya Zaid binti alishazalishwa kabla.
2. Inakuaje kijana atozwe faini ya uchafuzi wakati binti mwenyewe tayar alikua keshazalishwa hapo awali na binti tayar alikua na mtoto mkubwa? Maana Ake iyo mimba ya jamaa inakua ni mimba ya pili kwa uyo binti?
3. Wazee inakuaje wang'ang'anie binti yao hawezi kuolewa na kijana bila kumaliza kabisa mahari wakati wanaona kabisa kijana uwezo wake kiuchumi Ni mdogo?
4. Wamechukua hatua gani kwa kijana aliemzalisha binti yao hapo kabla ya kulipa mahari?
5. Wazee, je Binti yao amegeuka bidhaa ya kuuzwa kiasi kwamba lazima awekewe kiwango maalum Cha gharama za kuolewa rasmi, na isipofikiwa Basi haiwezekani? Yaani eti "Hakuna binti yetu yoyote ameolewa kwa mahari chini ya mil 3"
6. Kijana anajiskiaje anapokua na mke ndani ambae ameingia madeni na gharama za kuuza vitu vyake kwa hasara ili mradi amuoe? Yaan una MKE ambae umepata kwa gharama,madeni na Maumivu makali sana?
7. Itakuaje endapo atashindwa kurejesha Deni ndani ile miez 6 na kiwanja Cha urithi kichukluliwe kisa Ela ya ule mkopo ulienda kulipia mahari ya kuoa MKE?
8. Binti alishindwa Nini kusimama na mwanaume wake kusimama na yeye pamoja kumtetea dhidi ya Wazee wenye tamaa ya Ela ya mahari?
Kiukweli, ili suala limeniacha na sintofahamu nyingi kwa jamii zetu hizi kuhusu ustaarabu na mtizamo wao Kwenye suala Zima la Utoaji wa mahari.
Amejiajiri kwa kufungua twisheni za mitaani na kabahatika kupata mchumba ambae ni binti wa Miaka 21 ( Ila tayar ana mtoto wa Miaka 3). Amedumu kwenye mahusiano na binti kwa mwaka mmoja tangu Desemba 2020 na Sasa na mwezi Januari 2021 alishika ujauzito wake. Ambapo kwa Sasa anamimba yenye miez 5, kijana akaona afanye mchakato wa kuanza Kuishi rasmi pamoja na binti.
Kaandika barua ya uchumba ukweni imepelekwa na imekubaliwa, majibu yamerudishwa vimeorodheshwa vitu kadhaa na pesa taslim ambazo ukijumlisha inakuja jumla ya 4,600,000 (million 4 na laki 6)
Kijana akazungumza na mshenga kua icho kiwango Ni kikubwa na hawez kabisa kukimudu, mshenga kamshauri asiogope Ayo yanazungumzika na kitapunguzwa Sana watakapoenda kutambulishwa.
Siku ya kutambulishwa maongezi ya punguza yanaendelea, ila Mwisho kabisa wazazi na Ndugu wa MKE wakaishia milioni 2 taslimu (million 1 kwa ajili ya mahari na million 1 Ni faini ya uchafuzi- kuzalisha kabla ya kuoa ). Na mkaja wa mama laki 5 na vitu mchanganyiko vinavyogharimu laki 7. Jumla vyote unapata million 3 na laki 2.
Kijana kasema yeye hicho kiwango hana na hawezi kupata kabisa kwa sasa, kwa kazi anayofanya haimruhusu kabisa kupata kiasi icho. Akasema yeye alijiandaa kwa million 1 na laki 5 kwa Mambo yote.
Mshenga akaliwasilisha kwa Wazee, Wazee wakasema "ilo haliwezekani kijana maana kwenye ukoo wetu hamna mtu ameolewa chini ya million 2 mahari na vitu vyetu, iyo umependelewa kutokana na uchumi Wako Kama alivyotuambiwa na binti yetu"
Kijana akakubali ila akaomba alipe kwa awamu, 1.5million afu baadae atamalizia 1.7million. Wazee Nalo wakakataa kata kata kua hamna cha kupunguza hapo, labda akajipange KWANZA akiwa tayari aje
Kijana amepanik, Ameondoka amemuacha binti kwao na anazunguka uku na kule Anaomba akopeshwe pesa ili akamilishe zoezi. Kaja KWANGU kwetu Kama watu wake wa karibu tumsaidie kwa Hali na mali kakamilisha zoezi lake ili alilokwisha lianza. Kaniomba nimsaidie au nimkopeshe kiasi icho, Kiukweli nafsi yangu imegoma kabisa na nimemwambia kabisa kua yeye Ni rafki yangu ila kumchangia suala Hilo maana naona anajitwika mzigo mkubwa wkt uwezo wake ni mdogo.
Kuna vipaumbele vingi vya Ela ila sio kwa ilo, ila Kama uwezo anao apambane mwenyewe tutamsapoti kwa vingine.
Kijana
Amepambana kwa kuuza baadhi ya vitu vyake vya ndani Kama laptop, dressing table na stendi ya viatu. Jumla vyote kauza kapata laki 5 na 50.
Amepambana tena ameenda Kwenye taasisi flani izi za mitaani ya kukopesha fedha, ameweka bond kiwanja alichaochiwa na marehem mama ake mzazi kwa ajili ya mkopo wa 1.3 million kwa miezi 6. Kaniomba nikamdhamini, na kiroho Safi nimemdhamini na mkopo kapata chap kaenda kumaliza zoezi lake.
Ila baada ya kijana kuondoka NIMEBAKI NA MASWALI YAFUATAYO KICHWANI:
1. mahari Ni malipo ya shukrani kwa wazazi kwa kumtunza vema binti yao.
-Inakuaje kijana alazimishwe kulipia mahari kubwa kwa binti ambae alimkuta bila bikra?
Kibaya Zaid binti alishazalishwa kabla.
2. Inakuaje kijana atozwe faini ya uchafuzi wakati binti mwenyewe tayar alikua keshazalishwa hapo awali na binti tayar alikua na mtoto mkubwa? Maana Ake iyo mimba ya jamaa inakua ni mimba ya pili kwa uyo binti?
3. Wazee inakuaje wang'ang'anie binti yao hawezi kuolewa na kijana bila kumaliza kabisa mahari wakati wanaona kabisa kijana uwezo wake kiuchumi Ni mdogo?
4. Wamechukua hatua gani kwa kijana aliemzalisha binti yao hapo kabla ya kulipa mahari?
5. Wazee, je Binti yao amegeuka bidhaa ya kuuzwa kiasi kwamba lazima awekewe kiwango maalum Cha gharama za kuolewa rasmi, na isipofikiwa Basi haiwezekani? Yaani eti "Hakuna binti yetu yoyote ameolewa kwa mahari chini ya mil 3"
6. Kijana anajiskiaje anapokua na mke ndani ambae ameingia madeni na gharama za kuuza vitu vyake kwa hasara ili mradi amuoe? Yaan una MKE ambae umepata kwa gharama,madeni na Maumivu makali sana?
7. Itakuaje endapo atashindwa kurejesha Deni ndani ile miez 6 na kiwanja Cha urithi kichukluliwe kisa Ela ya ule mkopo ulienda kulipia mahari ya kuoa MKE?
8. Binti alishindwa Nini kusimama na mwanaume wake kusimama na yeye pamoja kumtetea dhidi ya Wazee wenye tamaa ya Ela ya mahari?
Kiukweli, ili suala limeniacha na sintofahamu nyingi kwa jamii zetu hizi kuhusu ustaarabu na mtizamo wao Kwenye suala Zima la Utoaji wa mahari.