Kero: Mahari sasa yageuzwa chanzo cha kipato

Kero: Mahari sasa yageuzwa chanzo cha kipato

DeepPond

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2017
Posts
41,728
Reaction score
103,997
Ni kijana wa Miaka 25, shahada ya Ualim, ila hakubahatika kupata ajira rasmi.

Amejiajiri kwa kufungua twisheni za mitaani na kabahatika kupata mchumba ambae ni binti wa Miaka 21 ( Ila tayar ana mtoto wa Miaka 3). Amedumu kwenye mahusiano na binti kwa mwaka mmoja tangu Desemba 2020 na Sasa na mwezi Januari 2021 alishika ujauzito wake. Ambapo kwa Sasa anamimba yenye miez 5, kijana akaona afanye mchakato wa kuanza Kuishi rasmi pamoja na binti.

Kaandika barua ya uchumba ukweni imepelekwa na imekubaliwa, majibu yamerudishwa vimeorodheshwa vitu kadhaa na pesa taslim ambazo ukijumlisha inakuja jumla ya 4,600,000 (million 4 na laki 6)

Kijana akazungumza na mshenga kua icho kiwango Ni kikubwa na hawez kabisa kukimudu, mshenga kamshauri asiogope Ayo yanazungumzika na kitapunguzwa Sana watakapoenda kutambulishwa.

Siku ya kutambulishwa maongezi ya punguza yanaendelea, ila Mwisho kabisa wazazi na Ndugu wa MKE wakaishia milioni 2 taslimu (million 1 kwa ajili ya mahari na million 1 Ni faini ya uchafuzi- kuzalisha kabla ya kuoa ). Na mkaja wa mama laki 5 na vitu mchanganyiko vinavyogharimu laki 7. Jumla vyote unapata million 3 na laki 2.

Kijana kasema yeye hicho kiwango hana na hawezi kupata kabisa kwa sasa, kwa kazi anayofanya haimruhusu kabisa kupata kiasi icho. Akasema yeye alijiandaa kwa million 1 na laki 5 kwa Mambo yote.

Mshenga akaliwasilisha kwa Wazee, Wazee wakasema "ilo haliwezekani kijana maana kwenye ukoo wetu hamna mtu ameolewa chini ya million 2 mahari na vitu vyetu, iyo umependelewa kutokana na uchumi Wako Kama alivyotuambiwa na binti yetu"

Kijana akakubali ila akaomba alipe kwa awamu, 1.5million afu baadae atamalizia 1.7million. Wazee Nalo wakakataa kata kata kua hamna cha kupunguza hapo, labda akajipange KWANZA akiwa tayari aje

Kijana amepanik, Ameondoka amemuacha binti kwao na anazunguka uku na kule Anaomba akopeshwe pesa ili akamilishe zoezi. Kaja KWANGU kwetu Kama watu wake wa karibu tumsaidie kwa Hali na mali kakamilisha zoezi lake ili alilokwisha lianza. Kaniomba nimsaidie au nimkopeshe kiasi icho, Kiukweli nafsi yangu imegoma kabisa na nimemwambia kabisa kua yeye Ni rafki yangu ila kumchangia suala Hilo maana naona anajitwika mzigo mkubwa wkt uwezo wake ni mdogo.

Kuna vipaumbele vingi vya Ela ila sio kwa ilo, ila Kama uwezo anao apambane mwenyewe tutamsapoti kwa vingine.

Kijana
Amepambana kwa kuuza baadhi ya vitu vyake vya ndani Kama laptop, dressing table na stendi ya viatu. Jumla vyote kauza kapata laki 5 na 50.

Amepambana tena ameenda Kwenye taasisi flani izi za mitaani ya kukopesha fedha, ameweka bond kiwanja alichaochiwa na marehem mama ake mzazi kwa ajili ya mkopo wa 1.3 million kwa miezi 6. Kaniomba nikamdhamini, na kiroho Safi nimemdhamini na mkopo kapata chap kaenda kumaliza zoezi lake.

Ila baada ya kijana kuondoka NIMEBAKI NA MASWALI YAFUATAYO KICHWANI:

1. mahari Ni malipo ya shukrani kwa wazazi kwa kumtunza vema binti yao.
-Inakuaje kijana alazimishwe kulipia mahari kubwa kwa binti ambae alimkuta bila bikra?
Kibaya Zaid binti alishazalishwa kabla.

2. Inakuaje kijana atozwe faini ya uchafuzi wakati binti mwenyewe tayar alikua keshazalishwa hapo awali na binti tayar alikua na mtoto mkubwa? Maana Ake iyo mimba ya jamaa inakua ni mimba ya pili kwa uyo binti?

3. Wazee inakuaje wang'ang'anie binti yao hawezi kuolewa na kijana bila kumaliza kabisa mahari wakati wanaona kabisa kijana uwezo wake kiuchumi Ni mdogo?

4. Wamechukua hatua gani kwa kijana aliemzalisha binti yao hapo kabla ya kulipa mahari?

5. Wazee, je Binti yao amegeuka bidhaa ya kuuzwa kiasi kwamba lazima awekewe kiwango maalum Cha gharama za kuolewa rasmi, na isipofikiwa Basi haiwezekani? Yaani eti "Hakuna binti yetu yoyote ameolewa kwa mahari chini ya mil 3"

6. Kijana anajiskiaje anapokua na mke ndani ambae ameingia madeni na gharama za kuuza vitu vyake kwa hasara ili mradi amuoe? Yaan una MKE ambae umepata kwa gharama,madeni na Maumivu makali sana?

7. Itakuaje endapo atashindwa kurejesha Deni ndani ile miez 6 na kiwanja Cha urithi kichukluliwe kisa Ela ya ule mkopo ulienda kulipia mahari ya kuoa MKE?

8. Binti alishindwa Nini kusimama na mwanaume wake kusimama na yeye pamoja kumtetea dhidi ya Wazee wenye tamaa ya Ela ya mahari?

Kiukweli, ili suala limeniacha na sintofahamu nyingi kwa jamii zetu hizi kuhusu ustaarabu na mtizamo wao Kwenye suala Zima la Utoaji wa mahari.
 
Muoaji na wakwe zake wote hawana akili.

binti wa Miaka 21 ( Ila tayar ana mtoto wa Miaka 3).
million 1 kwa ajili ya mahali na million 1 Ni faini ya uchafuzi- kuzalisha kabla ya kuoa )
Binti mwenyewe ni mchafu alizaa akiwa na miaka 18 tena nje ya ndoa.

Wazazi wengine bhana sijui ata wanaujinga gan vichwan mwao, mtu kaamua kuficha aibu ya mtoto wao ila bado wanamuona mjinga
 
Mkishakubaliana wawili mbebane kwa sh ngapi hiyo imetosha,wazaz watapanga wapangavyo mwanaume komaa na kile mlichokubaliana na mwenza.Kwa mfano mimi nilimwambia toa million moja mwenzangu akakubali,ivo walivyopanga milion 4 yao mshikaji alikomaa sana sema wazazi wangu nao naona walivuta cha Arusha sikuhiyo walimbana mpaka wakamminya 2 ml.

Tukaona si mbaya sana kuliko hiyo 4.Unajua mambo haya hayatakiwi uangalie leo tu na sifa kede za kulipiwa mahari kubwa inatakiwa utazame na kesho yatakapokukuta nawe kwa wanao.
 
Muoaji na wakwe zake wote hawana akili.



Binti mwenyewe ni mchafu alizaa akiwa na miaka 18 tena nje ya ndoa.

Wazazi wengine bhana sijui ata wanaujinga gan vichwan mwao, mtu kaamua kuficha aibu ya mtoto wao ila bado wanamuoba mjinga
Ni KERO sana, unabaki unajiuliza huu Ni ustaarabu wa namna gani kwa jamii yetu
 
Mkishakubaliana wawili mbebane kwa sh ngapi hiyo imetosha,wazaz watapanga wapangavyo mwanaume komaa na kile mlichokubaliana na mwenza.Kwa mfano mimi nilimwambia toa million moja mwenzangu akakubali,ivo walivyopanga milion 4 yao mshikaji alikomaa sana sema wazazi wangu nao naona walivuta cha Arusha sikuhiyo walimbana mpaka wakamminya 2 ml.Tukaona si mbaya sana kuliko hiyo 4.Unajua mambo haya hayatakiwi uangalie leo tu na sifa kede za kulipiwa mahari kubwa inatakiwa utazame na kesho yatakapokukuta nawe kwa wanao.
Safi Sana,
mabinti wengi hawaangalii kesho yao.

Sipati picha kijana wa watu Maumivu Kama Ayo alopata Kwenye mahali, Afu binti ndo alete za kuleta kwny Ndoa.

Itakua Yale Yale ya GUNIA MBILI ZA MKAA mtu anachomwa Moto kisa visirani na vinyongo moyoni.
 
Mwanadamu hawezi kubakia salama kwa kuongozwa na hisia peke yake kwani hisia zinaziba nafasi ya akili kufanya kazi......ndio maana aliyezama kwenye mapenzi anafanya mambo anayoyaona ya kawaida lakini walio nje ya penzi wanamuona amerukwa na akili......

Kitu pekee kinacho mtenganisha mwanaume na mvulana ni matumizi sahihi ya akili badala ya emotions.......
Huyo kijana akifikia kwenye hatua ya UANAUME akili zitamjia na kujiona mjinga sana....

maamuzi ya huyo kijana yameegemea kwenye emotions pekee na ndio maana nafsi yake ikashindwa kuhimiri presha za jambo hilo......akija kwenye uhalisia atajikuta amefanya maamuzi yasiyoendana na uhalisia wa uchumi wake......na hilo jambo litazaa majuto makuu siku za usoni.........

NB;
Ukiona jambo la khiyari unatumia nguvu kulifanikisha......achana nalo....
 
Kuna baadhi ya Makabila kipengele cha Mahari huwa hairuhusiwi kutolewa yote, kama waliandika mahari ni milioni 1 unaweza kutoa nusu na inakubalika. Wanadai ukilipa mahari yote ni sawa umemnunua Binti yao na haruusiwi kurudi kwao. Ila hivyo vikolokolo vingine vyote (Faini, Mkaja wa Mama etc) huwa vinalipiwa ela yote au upeleke vitu husika vilivyoandikwa kwenye barua. Hii inahitaji umpate mshenga mzuri wa kuongea na kupanga hoja.

Huyo mwalimu tayari ameshapachika ujauzito, hawakustahiki kumfanyia hivyo kwa kuwa pia tayari alishazalishwa na mtu mwingine hivyo thamani yake nayo imepungua.

Ningekuwa mimi kwenye hali ya namna hiyo tayari ana ujauzito wangu, ningewaachia Binti yao kisha nawaambia tutarudi mwakani tunaenda kujipanga upya halafu sirudi tena maana vitu vingine vinatia hasira.

Aisee!. Binti tayari ameshakuwa Singo Mother halafu wanataka kumuongezea tatizo lingine.
 
Mkishakubaliana wawili mbebane kwa sh ngapi hiyo imetosha,wazaz watapanga wapangavyo mwanaume komaa na kile mlichokubaliana na mwenza.Kwa mfano mimi nilimwambia toa million moja mwenzangu akakubali,ivo walivyopanga milion 4 yao mshikaji alikomaa sana sema wazazi wangu nao naona walivuta cha Arusha sikuhiyo walimbana mpaka wakamminya 2 ml.Tukaona si mbaya sana kuliko hiyo 4.Unajua mambo haya hayatakiwi uangalie leo tu na sifa kede za kulipiwa mahari kubwa inatakiwa utazame na kesho yatakapokukuta nawe kwa wanao.
Sidhani kama dada zangu waliolewa kwa hata milion 1 maana wengi ni chin ya laki 8 .
 
Back
Top Bottom