KERO: Masanja Mkandamizaji kutumia Ulokole kinyume na maadili ya Kipentekoste

KERO: Masanja Mkandamizaji kutumia Ulokole kinyume na maadili ya Kipentekoste

Habari ya mda Huu..

Asilimia kubwa ya watu duniani wanaamini uwepo wa Mungu, na uwepo huu wa Mungu umeleta Imani tofauti tofauti za ambazo binadamu huziishi. Na Imani hizi zinaheshimiwa, wapo wenzetu waroma, wakatholiki, wapentekoste, kila imani inataratibu zake na miiko yake inayoheshimiwa na kila muumini wa dini hiyo.


Kwa upande wa wapentekoste, sote twajua namna miiko yao ilivyo hasa katika mavazi, tumeona kwa waroma tumeona kwa waanglikana, zaidi sana hata kwa wenzetu waislamu.Uwepo wa dini hizi umekuwa msaada sana kwa jamii hasa kuibadilisha jamii na hasa vijana kuwa na miiko na heshima.

Lakini siku za hivi karibuni, kumekuwepo na wimbi la vijana wanaokimbilia ulokole lakini matendo yao hayaendani na miiko ya kilokole, bika kupepesa pepesa kumekuwa na celebrity huyu anayefahamika kama "Massanja mkandamizaji" ama "Emmanuel Mgaya" huyu amekuwa akijiita PASTOR.

Kumekuwa na malalamiko mengi hasa toka wa vijana wakilokole wakilalamika mienendo ya celebrity huyu na mavazi yake yasiyoendana na miiko ya kilokole, ki ukweki kuna wakati ukimwona ni kama kijana mwingine tu wa mitaani, kuvaa mlegezo, kusuka nywele, kofia kuvalia nyuma, hivi haviendani na miiko ya kikristo.

Kwenye jamii inaonyesha picha kuwa Anajifichia kwenye mwamvuli wa kipentekoste ili hali si mpentekoste...sasa unamdanganya nani massanja? hata moyo wako ukushuhudie kuwa UNACHOKIFANYA HAKIENDANI NA MAADILI YA KIPENTEKOSTE, KUMBUKA WEWE NI KIOO NA NI MAARUFU, HIVYO EITHER UBADILI NAMNA UNAVYOVAA AU UACHE KUTUMIA ULOKOLE KAMA KIVULI CHA MAOVU!


Unaharibu Taratibu za kipentekoste!


Ujumbe huu ukufikie mahali pote ulipo
92395f03f88a62a17fe2ae4374070d17.jpg
Ujue hadi sasa sijaona hayo maadili ya kipentekoste ktk bibilia, naomba msaada jamani
 
Swala la kuwakwaza wengine sio zuri ....
Tunafundishwa kuwa nakiasi ...tunaambiwa tusikae sana miongongoni na wenye mizaha
 
Acheni kutumika vibaya Mtumishi wa Mungu Masanja mbali ya uchungaji kazi yake nyingine ni msanii wa Commedy kwa hiyo msichanganye mambo. Sidhani hayo mavazi mnayoyalalamikia kama ni kweli lkn huwa anayavaa kanisani, mi ninachokiona wengi wenu hapa mnawivu na mafanikio yake, kwa sababu watu wa kwanza kulalamika kama kweli anakosea wangekuwa viongozi wake wa dini, wala sio nyie. kwa hiyo kwa ushauri wangu acheni majungu kama kweli nyie mmeokoka.
 
kuhusu utajiri wake sina shida kabisa naye, nina shida naye kwenye mavazi na mienendo yake, haiendsni na miiko ya Kikristo kabisa,na ni kama kajifichia kwenye ukristo li afanye yake. kiufupi anawaharibia walokole.


jamaa kaongea point ila kuna watu wanachukulia poa mavazi ni sehemu ya kuonesha heshima na uaminifu.

Huyo jamaa analima mpunga mbarali, na analima kibiashara sio kwa mazoea
 
Acheni kutumika vibaya Mtumishi wa Mungu Masanja mbali ya uchungaji kazi yake nyingine ni msanii wa Commedy kwa hiyo msichanganye mambo. Sidhani hayo mavazi mnayoyalalamikia kama ni kweli lkn huwa anayavaa kanisani, mi ninachokiona wengi wenu hapa mnawivu na mafanikio yake, kwa sababu watu wa kwanza kulalamika kama kweli anakosea wangekuwa viongozi wake wa dini, wala sio nyie. kwa hiyo kwa ushauri wangu acheni majungu kama kweli nyie mmeokoka.
wivu tena, au nawe ni mmoja wao?
 
Hakuna kitu kinaitwa mungu.

Amani ni fursa kwa wale wanaoujua ukweli kuwa hakuna mungu. Na ukiona unaitwa kwenye fursa basi jua wewe ndo fursa yenyewe
 
Mjasiliamali huyo.....anachangamkia fursa tu, kwenye vichekesho, uimbaji, kuhubiri, biashara, siasa kote yuko.....anatumia fursa!!
 
masanja kwa level za kuwa pastor/mchungaji inabidi kumchukua miaka mingi sana ili abadilike kwa sababu hata ukisikiliza mahubiri yake yamejaa vijembe, sasa watumishi wa Mungu kazi yao kubwa ni kuwaunganisha watu wawe jamii moja ya taifa la Mungu. lakini huyu jamaa utasikia akihubiri then anamchana mtu mala hata kwenye account huna hata sent mala hata marekani hujawahi kufika

hivyo basi anahiji mentorship kwa mda mrefu ili yale maumivu ya ndani aliyonayo yaishe kwa sababu ukisikia mahubiri yake unajua tu huyu ana maumivu ya ndani
 
Pale unapotafuta amani kwenye mavazi ya watu na sio kutoka kwa Mungu. Mnataka avae kizee na yeye ni pastor kijana?
 
Habari ya mda Huu..

Asilimia kubwa ya watu duniani wanaamini uwepo wa Mungu, na uwepo huu wa Mungu umeleta Imani tofauti tofauti za ambazo binadamu huziishi. Na Imani hizi zinaheshimiwa, wapo wenzetu waroma, wakatholiki, wapentekoste, kila imani inataratibu zake na miiko yake inayoheshimiwa na kila muumini wa dini hiyo.


Kwa upande wa wapentekoste, sote twajua namna miiko yao ilivyo hasa katika mavazi, tumeona kwa waroma tumeona kwa waanglikana, zaidi sana hata kwa wenzetu waislamu.Uwepo wa dini hizi umekuwa msaada sana kwa jamii hasa kuibadilisha jamii na hasa vijana kuwa na miiko na heshima.

Lakini siku za hivi karibuni, kumekuwepo na wimbi la vijana wanaokimbilia ulokole lakini matendo yao hayaendani na miiko ya kilokole, bika kupepesa pepesa kumekuwa na celebrity huyu anayefahamika kama "Massanja mkandamizaji" ama "Emmanuel Mgaya" huyu amekuwa akijiita PASTOR.

Kumekuwa na malalamiko mengi hasa toka wa vijana wakilokole wakilalamika mienendo ya celebrity huyu na mavazi yake yasiyoendana na miiko ya kilokole, ki ukweki kuna wakati ukimwona ni kama kijana mwingine tu wa mitaani, kuvaa mlegezo, kusuka nywele, kofia kuvalia nyuma, hivi haviendani na miiko ya kikristo.

Kwenye jamii inaonyesha picha kuwa Anajifichia kwenye mwamvuli wa kipentekoste ili hali si mpentekoste...sasa unamdanganya nani massanja? hata moyo wako ukushuhudie kuwa UNACHOKIFANYA HAKIENDANI NA MAADILI YA KIPENTEKOSTE, KUMBUKA WEWE NI KIOO NA NI MAARUFU, HIVYO EITHER UBADILI NAMNA UNAVYOVAA AU UACHE KUTUMIA ULOKOLE KAMA KIVULI CHA MAOVU!


Unaharibu Taratibu za kipentekoste!


Ujumbe huu ukufikie mahali pote ulipo
92395f03f88a62a17fe2ae4374070d17.jpg

Mbona kama una chuki binafsi vile. Lete mstari wa biblia unaoonyesha sheria za mavazi hasa ukiwa mlokole. Binafsi nilimuona mchungaji anavuta sigara. nikamuuliza mwanini anavuta sigara? Akanijibu hata kwenye biblia inasema fuata maneno yangu usifuate matendo yangu” nikaishiwa pozi.
 
ila masanja utajiri wake una ukakasi mwingi ngoja siku watamtolea uvivu

Jamani hivi mnjua biashara ngapi anafanya mashanja? Vijana fanyani kazi. Masanja ana mashamba ya mpunga kivao huko vijijini, ana kampuni ya ulinzi hapo Dar na vimgahawa hapo Dar plus na sadaka[emoji16] na alinza biashara kitambo
 
Unaweza ukavaa suruali bwaga kama gunia la mashineni lakini kama moyoni hakuna Mungu ni buree.
Ifact kuvaa milegezo na kusuka kweli inaweza ikatia mashaka ila kuvalia kama hapo kwenye picha sijaona sana ubaya
" Chakula ni kwa tumbo na tumbo ni kwa chakula lakini roho ni kwa Bwana"
Yaani hujaelewa kweli kilichoandikwa au unajitia kichwa ngumu? Ukiambiwa wazinzi hawataingia mbinguni maana yake ni kwamba asiye mzinzi ni mbinguni direct?
 
Back
Top Bottom