Ni ushamba tu kufuatilia maisha ya wengine. Ulijuaje yalioko nyumbani kwake kama sio umbea na kufuatiliana.Fuata ushauri wa daktari hivi Ina maana gani una ndoo za plastiki hamsini, majaba kumi mapipa matano familia ya watu sita na kisima cha maji unacho ebu badilika bwana๐๐๐
Sawa mkuuCha kufanya nenda upeleke kwenye nyumba za ibada,wao wanajua wahitaji zaidi
Njoo hapa mtaani kwangu kuna jamaa kila nikipita naye mahali utasikia na hiki ni kiwanja changu. Badala amalize kuendeleza kiwanja kimoja yeye amekazana tu kuongeza vingine, sasa kamahia kununua mashamba.
Katika vitu ambavyo napenda ni muziki, kwahio ukikuta nina redio 3 ndani mwangu kaa kwa kutulia๐๐๐
Duh! Hii hatari sana, inaweza kufikia kipindi akashindwa kuvimudu ata kupalilia majani.
kitu muhimu ni kuwekeza nguvu kwenye kuvimalizia halafu ndio aongeze viwanja vya ziada.
Hawa hayo majabaNi ushamba tu kufuatilia maisha ya wengine. Ulijuaje yalioko nyumbani kwake kama sio umbea na kufuatiliana.
Majirani wenyewe tunaonana kwenye vikao vya mwisho wa mwezi vya ulinzi, napata wapi muda wa kuhesabu ana ndoo ngapi na majaba mangapi, NI USHAMBA NA KUKOSA LA KUFANYA KUNAKUSUMBUA.
Hii hapa siku hizi tumepunguza sana maana gharama za ujenzi zimeongezeka bila kiasi.4. Kupenda kujenga majengo makubwa kuliko uwezo au kuliko idadi ya wanafamilia
Sijajua hasa target ya kufanya hivi hua ni nini, unakuta mtu umejenga nyumba kubwa ambayo hata kuimalizia umeshindwa. Unajenga nyumba ambayo huna uwezo wa kufanya usafi badhi ya sehemu.
Embu funguka kidogo mbona mimi nagawa nguo zangu kila kukicha? Zingine natuma kijijini maninti wanao msaidia mama anawagawia? Nguo nyingine nawatumia wifi zangu. Watoto wa ngugu zangu wa kike almost wote washavaaga nguo zangu embu funguka kidogo maana ninahisi kuna kitu hakiko sawa.Yote umeandika correct mkuu,Kila kitu tuwe na kias.....mi Kuna muda vikinizidia ndan nakusanya navimwaga usiku kwenye mtaa wenye watu wenye mahitaji zaidi yangu nikipita kesho yake hakuna kilichosalia.Nilikuwa na tabia ya kugawa nguo kilichonipata๐ so sikuhizi ndo nafanya ivo
Wacha kunichekesha nimekumbuka siku moja nilikuwa Airport wakati wa ugakuguzi ile tunaingia ndani, mbele yangu alikuwepo mkaka sijawahi ona alikuw na vifu vifuatavyo,Kuna wale wanamiliki simu nne...nyingine kaziweka chumbani tu..
na hao naona wapitie uzi huu
Mkuu hapa umezingua.kitanda kikubwa kuliko ukubwa wa watumiaji
Bora unaewapa ndugu,mi watu Baki walinijibu vibayaEmbu funguka kidogo mbona mimi nagawa nguo zangu kila kukicha? Zingine natuma kijijini maninti wanao msaidia mama anawagawia? Nguo nyingine nawatumia wifi zangu. Watoto wa ngugu zangu wa kike almost wote washavaaga nguo zangu embu funguka kidogo maana ninahisi kuna kitu hakiko sawa.
Na hio inasaidia sana mkuu, juzi nimepigwa Iphone nimepekua kabati nimeibua ka Sony kangu ka mwaka 2017 nakatumia now ๐ ๐ ๐Mtoa uzi ndiyo wale watu wakiingia kwako wakakuta radio 3, anaomba moja.
Kuwa na vitu vingi raha sana. Una simu 3, moja ikipasuka kioo, unabeba nyingine na siyo unaanza kuhangaika kwenda kwa fundi au kununua simu nyingine.
Ungetuambia kilichokupata nasi tuchukue tahadhari mkuu. Mimi bado ninagawa nguo kwa ndugu zangu lakini.Yote umeandika correct mkuu,Kila kitu tuwe na kias.....mi Kuna muda vikinizidia ndan nakusanya navimwaga usiku kwenye mtaa wenye watu wenye mahitaji zaidi yangu nikipita kesho yake hakuna kilichosalia.Nilikuwa na tabia ya kugawa nguo kilichonipata๐ so sikuhizi ndo nafanya ivo
Habari ya wakati huu wakuu?
Naomba nijielekeze moja kwa moja kwenye hii tabia ya watu kupenda kumiliki vitu vingi visivyotumika. Nitavitaja kimoja kimoja lakini sioni mantiki ya wao kufanya hivyo kwa sababu wakati mwingine huishia kutengeneza uchafu.
1. Mabegi/mafurushi makubwa kwenye safari
Utakuta safari ni ya siku tatu lakini kafungasha begi ambalo hata hawezi kulibeba. Yaani kwenye begi kaweka vitu au nguo ambazo hawezi kuzitumia kwenye hiyo safari yake.
2. Makabati makubwa na vyombo vingi
Hapa sasa ndio vita ilipo. Unakuta familia ya watu wanne wana kabati la vyombo milango mitatu, vyombo navyo ni vingi sana. Unakuta kuna vyombo havijawahi kutumika karibia mwaka mzima, ukiuliza kwa nini utaambiwa ni vyombo vya wageni. ushauri wangu kama una familia ndogo weka kabati la mlango mmoja lenye vyombo vichache au makabati ya jikoni pekee yanatosha.
3. Kukaa na vitu visivyotumika
Sambamba na hilo kuna kasumba ya kurundika vitu visivyotumika ndani ya nyumba au chumba. Ninaamini kukaa na kitu ambacho hukitumii ni matumizi mabaya ya nafasi.
Unakuta mtu una godoro ambalo haulitumii ummelikunja limekaa kabatini. Una nguo ambazo hujazivaa miaka miwili ila zinakujazia kabati.
4. Kupenda kujenga majengo makubwa kuliko uwezo au kuliko idadi ya wanafamilia
Sijajua hasa target ya kufanya hivi hua ni nini, unakuta mtu umejenga nyumba kubwa ambayo hata kuimalizia umeshindwa. Unajenga nyumba ambayo huna uwezo wa kufanya usafi badhi ya sehemu.
Matokeo yake unalazimika kuwa na wasaidizi kama wawili ili kuifanyia usafi, au wakati mwingine ukarabati unakushinda kwa sababu ya gharama kubwa ya ukarabati.
5. Mrundikano mkubwa wa vitu ndani ya nyumba
Unakuta nyumba ina fenicha nyingi kupitiliza kiasi kwamba baadhi ya fenicha zinachakaa au muonekano wake unakua ni wa kizamani sana. Kutokana na uwingi wake inakua ngumu kuziboresha. Au mpangilio wa vitu unafanya nyumba ikose mvuto.
6. Kufanya sherehe kubwa kuzidi uwezo
Unakuta mtu anafunga ndoa anaandaa sherehe kubwa kuliko uwezo wake. Matokeo yake baada ya sherehe inakua ni dhiki kuu. Madeni kama yote mbali na madeni ndoa za siku hizi hazikai sana unaishia kupata stress.
7. kitanda kikubwa kuliko ukubwa wa watumiaji
Hapa napo siku hizi ni changamoto, unakuta mtu mwili mdogo lakini anataka kulala kwenye 6 kwa 6. wakati wangeweza kulala ata kwenye 4 kwa 6 na chenji ikabaki.
Ushauri wangu
Napendekeza watu wawe na vitu muhimu tu. Vitu visivyohitajika ndani ya nyumba visitumike. Usikae na fenicha zisizokua na kazi kwa mawazo kwamba kuna siku kitapata kazi. Pangilia mambo yako vizuri, kuwa na vitu vichache unavyoweza kuvimudu na kuvitunza. Kwa mfano vyombo vya ndani viwe angalau mara tatu ya idadi ya wanafamilia. Kwa mfano familia ya watu wan ne muwe na sahani 12 tu. Kukaa na vyombo ambavyo vinaweza kumaliza miezi 6 bila kuoshwa ni uchafu.
Tumia vyombo vikiisha ondoa nunua vingine, furahia maisha. usiishi maisha ya gharama kuzidi uwezo wako. ukipata wageni wakirimu kwenye vyombo vya kila siku, tusiishi maisha feki, tuishi uhalisia wetu.
Nawasilisha.
View attachment 2270607
Gawa Kwa ndugu inatosha....niliibiwa vibaya tuUngetuambia kilichokupata nasi tuchukue tahadhari mkuu. Mimi bado ninagawa nguo kwa ndugu zangu lakini.
Tatizo kubwa tunafanya vitu kwa tamaa!Sisi bado ni wajima. Ndiyo maana nyumba nyingi hazipendezi hata kama ni ya kisasa. Hatujui kufanya nyumba ipendeze.
Wenzetu huko mbele hadi wana kampuni maalumu za kurudisha makazi katika ubora wake. Mtu akishazidiwa na mikorokocho anawakodi jamaa. Utaona hata vitu vya mitumba, si kwamba wanatuhurumia saaana bali ni kusafisha makazi yao. Sisi ndiyo jalala lao. Imagine tunaletewa hadi vyombo vya jikoni na vya kulia vya mtumba. Sasa unavinunua,unajaza home kwako.
Mada hii iendane na ununuzi wa vitu rahisirahisi mradi tu kujaza nyumba. Mfano,mavyombo ya plastiki kibao. Hii ni akili mbovu.
Asante kwa mada nzuri