mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,897
- 18,477
- Thread starter
-
- #61
Embu nukuu wewe hiyo standing order tuisome hapa wote...Taratibu za serikali nazijua sana!! Mimi ni mumishi wa umma mstaafu!! Niliajiriwa katika utumishi wa umma mwaka 1986 baada ya kuhitimu chuo kikuu cha Dar, na nimestaafu mwaka 2019!! Kinachofanyika sio taratibu za utumishi wa umma bali uhuni. Taratibu za utumishi wa umma zinaongozwa na Government standing orders toleo la 2009 na marekabisho yake ya mwaka 2011!! Huo utaratibu wa mtu kuripoti kazini kwa wito rasmi halafu unarudishwa nyumbani bila kuhudumiwa kwa lolote ni uhuni wa watu!! Naomba unukuu hapa waraka wowote rasmi wa serikali unaoelekeza hivyo!!
😂😅 sasa mbona unajichanganya mwenyew tena... Unapewa vipi barua wakat tayar ulipata barua ya ajira... Halafu sasa ukitaka twende kwa utaratibu basi yeye ndiye alipaswa kuandika barua ya kukiri kufika kituoni na kuruhusiwa kurudi nyumban kusubiri taratibu nyingine za kikazi... Vijana msi complicate mambo ya kiserikali hayahitaji papara, by the way hakuna wa kuwazurumu stahiki zenu...Ukisharipoti ni ajira imekamilika. Hizo ni taratibu tu.
Ilipaswa kumpa hata barua kuwa ameripoti na sasa wanakamilisha taratibu nyingine arudi tarehe fulani.
Huyu akianza kazi Ofisi yake wajipangeJamaa unajua kulalamika unaandika gazette wewe unachembe chembe ya umbea
Haiwezekani kukubaliana na uonevu eti kwa kuwa tu umepata ajira!! huu ni utumishi ni utumishi wa umma na haikubaliki watu kujifanyia utaratibu unaonyanyasa na kutesa watu!! Mtu aliitwa kwa vitisho kuwa ukichelewa nafasi yako atapewa mwingine! lakini alivyoripoti bado anazungushwa, hilo halikubaliki!
HujitambuiKukiwa hakuna ajira kelele mkipata kelele. Mama kanyaga twende
Naona naongea na mtu anayedai anajua taratibu kumbe hata standing order zinazoongoza kwenye utumishi hana habari nazo na hajui mahali pa kuzipata!Embu nukuu wewe hiyo standing order tuisome hapa wote...
Watu wateseke wasiseme au?. We waweza kuwa n miongoni mwa watesaji wa vjana wa watu!. Wapeni vjana wa watu posho zao zikawasaidie kuanza maisha.Kukiwa hakuna ajira kelele mkipata kelele. Mama kanyaga twende
Kumbe alisikika mpumbavu mmoja HR; nlifikiri n ww ulokuwa unaongea pumba.Naomba nijibu kama ifuatavyo....unakuwa bado hujaingizwa kwenye mfumo, na mpaka uingizwe kwenye mfumo anaweza kuchukua mwezi au ndani ya miezi miwili ili upate mshahara wako, ili upate mshahara wako inabidi utumishi wa approve taarifa zako, kwa kuzikagua kiundani ili tusipate udanganyifu......kwa kuwa hakuna bajeti Yako ya kujikimu kwa mda ule,ndio maana tunakwambia kuwa kakae kwanza nyumbani mpaka tukupigie simu....jamani sio kwa ubaya,maana hakuna wa kukulisha hapa mjini.....kama hamuamini kawaulize walimu wanavyopata ajira,wanakaa zaidi ya mwezi ndio wanaingiziwa mshahara wao..muda wote huwa wanahudumiw na wakuu wa shule mpaka wanapopata mishahara Yao kwa mara ya kwanza.....alisikika HR mmoja wa michango.
ukuda ndio nini?Mleta mada anachembechembe za ukuda kazini.
Bora hata tumseme waziri husika, hivi mama/rais atafanyia vitu vingapi vidogo vya namna hii, hata km rais ni taasisi, lakini mengine yanapswa kuishia wizara husika.Nimwombe mama Samia alifuatilie hili maana ni mateso makubwa wanayoyapitia waajiriwa wapya usione wamekaa kimya!!
Mfumo wa wapi huo?. Subsistance allowance inakuwa inafanya kazi gani au ni kutokana na kutokuelewa kanuni za utumishi wa umma hivyo unataka kuaminisha umma kuwa ndivyo ilivyo?.Ukipata placement kitu Cha muhim ni kwenda kuripoti kituo Cha KAZI. Taratbu za vyeti zikiisha inabidi urudi ulikotoka na uendelee kutafta pesa zako had utakapopigiwa simu. Kuna watu hikaa hata mwez mzma na sehm Kisha ndo wanapigiwa simu.
Na huo ndio mfumo ulivo.
Kama kweli wewe ni mastaf utakua una stress huelewiNaona naongea na mtu anayedai anajua taratibu kumbe hata standing order zinazoongoza kwenye utumishi hana habari nazo na hajui mahali pa kuzipata!
Mimi yalinikuta kwenye ofisi Moja za mamlaka Fulani nilipo riport TU wakaniambia tutakuita baada ya week Moja ,ukapita mwezi nikaenda na suruali nyeusi na shati zuri la chama Cha mapinduzi na kofia,nilipowauliza na majibu hayaeleweki nikaenda office za CCM mkoa nikaonana na mwenyekiti wa ccm.Kesho yake nilipigiwa simu ni riport mapema na nilionyeshwa ofisi yangu nikapiga miaka 4 nikapata internal transfer .Inawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine! Hii inmfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!! Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!! Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar. Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watun na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!! Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa! Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!
Kuwa na utu mbwa ww ajira ni haki yao hii serikali imejengwa kwa kodi za babu zaoKukiwa hakuna ajira kelele mkipata kelele. Mama kanyaga twende
Taasisi nyingi ukiripoti ndo wanachukua vyeti vyako wanapeleka necta kuhakiki.. baada ya hpo ndo uingizwe kwenye payroll.. so taasisi hiz muda huu wanapenda kukuambia urudi watakuita hadi watakapoona tayari umeingizwa Kwa payroll na uhakiki umekamilika... Taasisi zenye uwezo wanaweza kukuretain ubaki huku wakikusuprt kidogo, zingne wanaona huo ni mzigo so nenda tutakuita.. ni vizuri Pia kuomba maelezo kwanin urudi nyumbani wakati ndo umeripoti???usikae kimyaaaInawezekanaje watu wapange utaratibu ambao siyo rafiki kwa waajiriwa wapya? Iko hivi: Ukipangiwa ajira na sekretarieti ya ajira kwa maana ya kufaulu usaili, unapewa barua ya kuripoti kazini ndani ya siku 14 vinginevyo nafasi yako atapewa mwingine! Hii inmfanya mwajiriwa atafute nauli hata kwa kukopa toka huko aliko na kusafiri hadi kituo alichopangwa. Akifika huko wanakagua vyeti vyake halisi, na kujaza taarifa zake binafsi kisha huambiwa RUDI NYUMBANI NA TUKIKAMILISHA TARATIBU ZA AJIRA TUTAKUITA KWA SIMU!! Hapo wameshamaliza na unatoka ofisini bila hata senti moja! Hawajali utalala wapi na utakula wapi na usalama wako ni upi! na utasafiri vipi na utarudi tena vipi!! Niliposikia kwa mara ya kwanza kwa mtu aliyekuwa amepangiwa halmashauri moja huko tabora sikuamini kuwa huo ndio utaratibu!! Nilifikiri ni roho mbaya tu ya wahusika huko halmashauri ya tabora!! Juzi juzi kuna dogo alipata nafasi katika moja ya manispaa za Dar. Naye aliporipoti alipokelewa na kukaguluiwa vyeti vyake na kujaza fomu za personal particulars na kuambiwa arudi hadi atakapopigiwa simu! Ni wiki nimepita sasa na bado hajapigiwa simu na anajibanza tu kwa watun na hajui hadi lini!! Huu utaratibu una usumbufu sana!! Ninachofahamu watu huitwa wakati serikali imeshafanya maandalizi tayari ya kuwapokea na kuwahudumia!! Yaani kijana amesota na interview kibao kwa gharama kubwa sana ya nauli, malazi na chakula, sasa ameitwa kwenye ajira bado anasoteshwa! Niwaulize nyie mnaowafanyia hivyo wenzenu mnajua masaibu wanayopambana nayo wanaposubiria? Wengine wanalala kwenye vituo vya mabasi kwa kukosa pesa za gesti na nauli ya kurudi tena nyumbani hawana! Tafadhali angalau siku wanaporipoti wapeni zile posho za kujikimu zilizopo kisheria ili ziwalinde wanaposubiria!