mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,897
- 18,477
- Thread starter
- #61
Naomba nieleweke: Mimi sikatai mtu kuambiwa asubiri taratibu za ajira zikamilike na aingizwe kwenye pay roll ya saerikali. Ninachokataa ni mtu kutokulipwa gharama ya nauli aliyotumia kuitikia wito wa kuripoti ndani ya siku 14, na pia kutokulipwa nauli ya kurudi nyumbani akasubirie taratibu za kukamilisha ajira. Hiyo imesababisha watu wateseke mjini!! Safari ya kuitikia wito ni rasmi lazima ilipwe kikamilifu kwa mujibu wa taratibu za serikali!! Huko nyuma hata kuja kwenye usaili ilikuwa unarudishiwa nauli na posho ya siku angalau mbili kwenye kituo cha usaili. Sisemi ifanyike hivyo sasa lakini hata la kuitikia wito rasmi wa ajira mtu asilipwe!!! Hapana huu ni uhuni!!