Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Kesi ya Abdallah Zombe: Mashitaka, hatia, hukumu na yanayojiri

Hii serikali ni ya ajabu sana,wanataka kukata rufaa ya nini? waendelee tu na mambo yao mengine,huu mchezo nadhani walishau-plan siku nyingi sana na walikuwa wanaelewa fika wanachofanya,pamoja na kwamba wanasema kuwa wanataka kukata rufaa bado naona kama ni kiini macho fulani wanasema hivyo ili kutupumbaza tuone kweli wanajali lakini ukweli unabaki pale pale wala hawajali,wanachotaka ni kuendela kutumia kodi za wananchi kujinufaisha na kujitajirisha.
 
Wakuu,hivi punde nimetonywa na kiongozi mmoja kutoka katika Wizara ya Mambo ya Ndani (Ni mtu ninayeheshimu maneno yake) sababu iliyopelekea zombe kuachiwa mbali na hukumu ya jaji ilivyosema.

Ni kwamba katika hukumu hiyo Jaji aliitwa na Serikali na kuagizwa hakutane wakuu wa wizara ya mambo ya ndani ili kutazama mambo makuu yafuatayo kabla ya hukumu.

Ni kuwa mfumo wa jeshi la polisi nchini tanzania uendeshwa klwa maagizo yasiyo kwenye maandishi yahani IGP,RPC,RCO nk hutoa maagizo ya mdomo kwa walioko chini yao.

hivyo katika tukio la akina zombe ndivyo ilivyofanyika kwa maana kuwa ilidaiwa kuwa wale waliotekeleza mauaji waliagizwa na wa,kubwa wao.

Lakini ni kuwa iwapo washtakiwa chini ya zombe au zombe mwenyewe wangehukumiwa asdhabu yoyote basi utaratibu wa polisi wa kufanya kazi kwa maagizo ya mdogo,simu nk ungekuwa umefutwa rasmi hali ambayo serikali iliona inaweza kuleta tatizo katika uendeshaji wa jeshi la polisi nchini.

hapa ni kwamba OCD hasingeweza kumpigia simu koplo na kuagiza kumkamata mwizi fulani mpaka yawepo maandishi.

nimeamua niweke hapa ili baadhi yetu tujue hilo,au kama kuna mwenye habari zaidi kuhusu kilichojiri katika kikao hicho wamwage hapa !

JUU kabisa umesema una chanzo cha uhakika toka wizara ya Mambo ya ndani. halafu mwishoni unatuomba wenye habari Zaidi tumwage, kwanini usiulize huyu huyu wa Mambo ya ndani?

Mahakama za Tanzania na majaji bado waiheshimu sana fani yao. kama wizara ya Mambo ya ndani ilikuwa inaweza kufanya hivyo kwanini isingemsaidia Zombe akae nje kuliko kuwa ndani kwa miaka karibu mitatu na miezi kadhaa?

Liyumba alikamatwa na Kweka ambaye ni ndugu na mama Mkapa huwezi kumsikia Kweka ameshatolewa anaendelea kusota ni LIYUMBA AMATUS.
Ndugu HABARI yako ni uongo mkubwa.Jaji aitwe wizara ya ndani au unakusudia Hakimu wa mahakama ya Kisutu?
 
Wakuu,hivi punde nimetonywa na kiongozi mmoja kutoka katika Wizara ya Mambo ya Ndani (Ni mtu ninayeheshimu maneno yake) sababu iliyopelekea zombe kuachiwa mbali na hukumu ya jaji ilivyosema.

Ni kwamba katika hukumu hiyo Jaji aliitwa na Serikali na kuagizwa hakutane wakuu wa wizara ya mambo ya ndani ili kutazama mambo makuu yafuatayo kabla ya hukumu.

Ni kuwa mfumo wa jeshi la polisi nchini tanzania uendeshwa klwa maagizo yasiyo kwenye maandishi yahani IGP,RPC,RCO nk hutoa maagizo ya mdomo kwa walioko chini yao.

hivyo katika tukio la akina zombe ndivyo ilivyofanyika kwa maana kuwa ilidaiwa kuwa wale waliotekeleza mauaji waliagizwa na wa,kubwa wao.

Lakini ni kuwa iwapo washtakiwa chini ya zombe au zombe mwenyewe wangehukumiwa asdhabu yoyote basi utaratibu wa polisi wa kufanya kazi kwa maagizo ya mdogo,simu nk ungekuwa umefutwa rasmi hali ambayo serikali iliona inaweza kuleta tatizo katika uendeshaji wa jeshi la polisi nchini.

hapa ni kwamba OCD hasingeweza kumpigia simu koplo na kuagiza kumkamata mwizi fulani mpaka yawepo maandishi.

nimeamua niweke hapa ili baadhi yetu tujue hilo,au kama kuna mwenye habari zaidi kuhusu kilichojiri katika kikao hicho wamwage hapa !

Hiki ni kichekesho kingine. Zombe anajulikana kwa ubabe na uuaji!!! Usiniambie nithibitishe, sitafanya ila ukweli ndiyo huo!!!! Ni watu wangapi ambao enzi zao walikuwa wanafanyiwa uhalifu, askari wanakuja kwako wanajua una hela wanazichukua na kukufungualia kesi??? Ni wangapi ambao wamechukuliwa magari yao huku wakibambikizwa kesi ni wezi wa magari??? Ni wangapi walibambikizwa kesi kwa kuwa hawakufikisha mgao wa ujambazi kunakotakiwa??? Let us be realistic!!!! Nijuavyo mimi huu wizi wa high profile unahusisha vigogo wengi askari, hata hili la Zombe, hayuko peke yake na nina amini kabisa walipokuwa ndani kuna vigogo walikuwa wanacheza dili kwa niaba yao. Hata uniambie kuwa eti mashtaka yalifunguliwa kidhaifu na kuwa eti ni ushahidi dhaifu, si kweli, ni namna ambavyo walipanga, full stop.
 
Kazi kweli kweli! Kama huyo aliyekupa habari ni mtu wa "kuheshimika" nafikiri wanasheria wetu wanatakiwa kubadili kazi! Bora kupambana na askari wa jiji wakiwa wamebeba bidhaa mikononi kuliko kufanya kazi wanayoifanya inayowadhalilisha hivi!

Duh! Kazi kubwa!
 
Binadamu tunacheza na mungu,lakini ole wao kama ni kweli waliua na sasa wako huru,basi mungu atahukumu kwa haki na wala si wa haraka,yatima walioachwa wameumbwa na mungu na watahangaika kwa kadri shetani atakavyoona inafaa,lakini jicho la huruma la mungu litaona na litajibu.
 
Wakuu,hivi punde nimetonywa na kiongozi mmoja kutoka katika Wizara ya Mambo ya Ndani (Ni mtu ninayeheshimu maneno yake) sababu iliyopelekea zombe kuachiwa mbali na hukumu ya jaji ilivyosema.

Ni kwamba katika hukumu hiyo Jaji aliitwa na Serikali na kuagizwa hakutane wakuu wa wizara ya mambo ya ndani ili kutazama mambo makuu yafuatayo kabla ya hukumu.

Ni kuwa mfumo wa jeshi la polisi nchini tanzania uendeshwa klwa maagizo yasiyo kwenye maandishi yahani IGP,RPC,RCO nk hutoa maagizo ya mdomo kwa walioko chini yao.

hivyo katika tukio la akina zombe ndivyo ilivyofanyika kwa maana kuwa ilidaiwa kuwa wale waliotekeleza mauaji waliagizwa na wa,kubwa wao.

Lakini ni kuwa iwapo washtakiwa chini ya zombe au zombe mwenyewe wangehukumiwa asdhabu yoyote basi utaratibu wa polisi wa kufanya kazi kwa maagizo ya mdogo,simu nk ungekuwa umefutwa rasmi hali ambayo serikali iliona inaweza kuleta tatizo katika uendeshaji wa jeshi la polisi nchini.

hapa ni kwamba OCD hasingeweza kumpigia simu koplo na kuagiza kumkamata mwizi fulani mpaka yawepo maandishi.

nimeamua niweke hapa ili baadhi yetu tujue hilo,au kama kuna mwenye habari zaidi kuhusu kilichojiri katika kikao hicho wamwage hapa !
"Mr Rutunga,am very sorry to tell you that,the kind of fools you intended to fool are all wise men + women,so stop fooling pipo vinginevyo you'll b fooling unfooled"
 
Sasa wakuu ndo tunakwisha kabisa na tz yetu mana kama tulipokuwa tunapaamini watatoa haki mahakama ndo hivyo wameanza mambo tusiyoyaelewa..haiingii akilini jaji kusema kuwa shahidi aliyesema alimwona mwenzake akiwapiga risasi kule msituni..na eti kwa kuwa huyo aliyepiga risasi hajakamatwa basi hawezi kuhukumu mtu ambaye hajakamatwa..kwa hiyo jaji anakubali kuwa mtu aliuawa kweli na kuna watu waliona kwa macho yao na inaonekana waliridhia hasa wale wakubwa walioenda huko msituni..kwanini basi hakutoa hata adhabu ya vifungo vya maisha kwa wale wote ambao alijiridhisha kuwa walishuhudia vfo vikitendeka na bado mbele yake wamekanusha? Inasikitisha kwani kama muhimili huu umeanza kukosa dira na wakati tuna masikitiko na muhimili wa bunge kuelekea kubaya hasa baada ya spika kutishiwa kunyang'anywa kadi na kuahidi kuwabeba mfisadi ili aendelee kuwa spika..watanzania hatuna pa kukimbilia mana muhimili wa kwanza serikali ndo ulishachoka toka siku nyingi..tumebaki kama watoto yatima..watu watauwawa na polisi na mafisadi watakula nchi kama wawezavyo huku wakishangiliwa..mungu ibariki tanzania
 
attachment.php

Je hii ni haki jamani?
 
kwa maneno yako inawezekana kuwa kweli kwa nchi yetu ambayo viongozi wetu ni maskini mpaka kwenye kufikiria.
 
Jamani labda huyu Zombe ana tatizo la kisaikolojia, asaidiwe!!! Isije kuwa damu ya wale marehemu inamsumbua, anahitaji maombezi !!!
 
Magazeti yalimnukuu hata mke wa Zombe kuwa hataki waandishi waende nyumbani kwake. Hayo yote ni kuhaha kwa umwagaji damu za watu wasio na hatia. Yetu macho.
 
Zombe ana kazi kubwa sana ya kuishi na jamii,kimtizamo inaonekana ni mtu mkorofi sana na mwenye roho mbaya kupindukia.Kwa wale watu wa Tanga wana jua na maanisha nini.
 
Huyu Zombe anapata wapi confo ya kumpiga mtu punde baada ya kuepuka kitanzi? au kesi ile ilikuwa mchezo wa kuigiza, alishahakikishiwa na 'wenye nchi' kuwa hakuna 'tatizo'?
 
Huyu Zombe anapata wapi confo ya kumpiga mtu punde baada ya kuepuka kitanzi? au kesi ile ilikuwa mchezo wa kuigiza, alishahakikishiwa na 'wenye nchi' kuwa hakuna 'tatizo'?
Kila kitu kina wezekana kwenye hii nchi mkuu.
 
Zombe ana confo dunia nzimaa wajuaa....maana anajuaa maovu ya wenzake wote wakubwa....lazima awe na confo...hata huko keko alikuwa ana confo hadi kumzidii mkuu wa gereza uliza......
 
Huyu shule yake (both formal and informal) inaonekana kuwa ndogo, au vipi?
 
Back
Top Bottom