Wakuu,hivi punde nimetonywa na kiongozi mmoja kutoka katika Wizara ya Mambo ya Ndani (Ni mtu ninayeheshimu maneno yake) sababu iliyopelekea zombe kuachiwa mbali na hukumu ya jaji ilivyosema.
Ni kwamba katika hukumu hiyo Jaji aliitwa na Serikali na kuagizwa hakutane wakuu wa wizara ya mambo ya ndani ili kutazama mambo makuu yafuatayo kabla ya hukumu.
Ni kuwa mfumo wa jeshi la polisi nchini tanzania uendeshwa klwa maagizo yasiyo kwenye maandishi yahani IGP,RPC,RCO nk hutoa maagizo ya mdomo kwa walioko chini yao.
hivyo katika tukio la akina zombe ndivyo ilivyofanyika kwa maana kuwa ilidaiwa kuwa wale waliotekeleza mauaji waliagizwa na wa,kubwa wao.
Lakini ni kuwa iwapo washtakiwa chini ya zombe au zombe mwenyewe wangehukumiwa asdhabu yoyote basi utaratibu wa polisi wa kufanya kazi kwa maagizo ya mdogo,simu nk ungekuwa umefutwa rasmi hali ambayo serikali iliona inaweza kuleta tatizo katika uendeshaji wa jeshi la polisi nchini.
hapa ni kwamba OCD hasingeweza kumpigia simu koplo na kuagiza kumkamata mwizi fulani mpaka yawepo maandishi.
nimeamua niweke hapa ili baadhi yetu tujue hilo,au kama kuna mwenye habari zaidi kuhusu kilichojiri katika kikao hicho wamwage hapa !