Kesi ya Halima Mdee na wenzake, vigogo waliogushi nyaraka wote kuanikwa

Kesi ya Halima Mdee na wenzake, vigogo waliogushi nyaraka wote kuanikwa

CHADEMA akili KUBWA siku zote...huwa nawashangaa watu wanaoibeza ...UJASUSI Katika chama kwa maslahi ya TAIFA..

Kizimbani ama Kufuta kesi na kurudi kwenye misingi ya KATIBA
Mtabaki kujisifu hivyo hivyo hadi mtanyanganywa hadhi ya chama kikuu Cha upinzani.Wapi Umoja Party wahi haraka
 
Gazeti la Raia Mwema limeandika kuwa kesi iliyofunguliwa na kina Mdee na wenzake 18 itafungua boksi ambalo limeficha siri kubwa la ‘vigogo’ waliohusika na sakata zima la wabunge 19 wa viti maalumu waliokuwa wanachama wa Chadema.

Gazeti hilo linasema mchakato mzima unaihusisha Ikulu, vigogo kutoka Tume ya Uchaguzi akiwemo Mkurugenzi wa NEC Mahera, vigogo kutoka Bunge akiwemo Spika na katibu wa bunge, vigogo kutoka ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa.

Kwa upande wa Chadema wao wanasema wamefurahi kesi hii kufunguliwa kwa sababu wanazo nyaraka za kutosha watakazoziwasilisha mahakamani na kwa umma ambazo zitaishangaza dunia, wanaujua mchezo wote nani alihusika nani aliandaa hayo majina 19, nani aliandika removal order ya Nusrat na nani yuko nyuma yao kwa sasa. Kikosi cha mawakili wa chama kiko tayari kitawaanika wote waliohusika kwa vile wao kama chama hawana cha kupoteza.

Kwa habari zaidi soma gazeti la leo la Raia Mwema.

View attachment 2228860
Ndicho nilichokuwa nakitaka, hata kama huyo Mwenyekiti wenu Mboye amehusika haukumiwe kwa mujibu wa Sheria.
 
nakukumbusha …mwenye Mamlaka ya kuithibitishia Mahakama kuwa Sahihi iliyopo kwny hiyo barua kuwa ni ya John Mnyika au laa sio Mnyika mwenyewe wala Chadema
"Fomu za kudhaminiwa kwa hawa wabunge 19, zilitoka wapi na zilikuwa za chama gani? Maana fomu halisi (original) za kudhaminiwa za CHADEMA hadi leo zipo ofisini.” - Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara
 
Chadema waliomba tume ya uchaguzi nakala ya orodha iliyowasilishwa bungeni ili kumjua aliyesaini. Tume ikakataa [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Safari hii kupitia mawakili wa CDM, kwa amri ya mahakama, hiyo nakala itatolewa.
 
Mbona mashitaka mengine huwa yanapelekwa na mawakili wa CHADEMA? KWANINI hili mnaloita kuwa Halima amefoji hamjawahi kwenda hata kulalamika kituo cha polisi wala kukusudia kushitaki?
Usiwe na haraka, majibu utayapata.
 
Mimi naona Kubenea akitumia Gazeti hili kwa niaba ya Chadema ili kuwatisha kina Mdee wafute kesi kabla ya vigogo wa Chadema hawajaumbuka kuhusu Signature iliyoko kwenye nyaraka zao huko Mahakamani.

Nani alisaini nyaraka za kina Mdee kwenda NEC na Bungeni?
Tusubiri.
 
Back
Top Bottom