Sawa, inawezekana muongo, lakini muongo kuhusu nini?
Inawezekana alikuwa na leseni ya bandia, akasema alikuwa na leseni, akajishtukia leseni haikuwa halali, akachomoa, akadanganya kuhusu leseni.
Hilo halimaanishi kadanganya kuhusu kuua.
Kwamba kakataa alikuwa namahusiano na Komba inawezekana anadanganya, huyu mtoto mdogo, Komba mtu mzima alikuwa na mkewe na watoto wakubwa kuliko Lulu. Sasa msichana kama Lulu akikataa ukweli kwamba alikuwa na uhusiano na jibaba inawezekana anadanganya, lakini je, kudanganya kuhusu uhusiano huo kunamaanisha kwamba yeye ni muuaji?
Ningeona contradiction ina nguvu zaidi kama ingeweza kuhusishwa moja kwamoja na kesi ya mauaji, siyo habari za kumharibia character tu. Mtu yeyote ukimuweka katika microscope utakuta mapungufu, huyu ana mchepuko, huyu hajalipa kodi, huyu anampiga mkewe, huyu mlevi mbwa, lakini, kama tunazungumzia kesi ya mauaji, kitu muhimu ni ushahidi wa kesi ya mauaji, si hizi habari nyingine. Unless zinaingia moja kwa moja katika kesi ya mauaji.
Kama Kanumba angefariki katika ajali ya gari ambalo Lulu alikuwa anaendesha, hapo habari za leseni ya Lulu ingekuwa very relevant.
Lakini haikuwa ajali ya gari, suala la leseni ya Lulu linakuja vipi? Sisemi kwamba halihusiki, inawezekana linahusika (sijafuatilia kesi kwa karibu). Ningependa kujua tu, linahusikaje?
Ukimchukua mtu yeyote na kuanza kumdai risiti za nguo zake zote alizonunua katika miak 10 iliyopita, utakuta kuna nguo kibao hana risiti.
Je, hilo linatosha kusema huyu ni mkwepa kodi na hivyo anaweza kuua tu?