KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

Kinachoniacha na maswali mengi ni mpenzi wako kuanguka na kuonekana kama anatapatapa halafu wewe uwashe gari na kuelekea beach..

Hapa kuna jambo!
Yaaap hapo ndipo hata Mimi napata ukakasi kidogo...anachojaribu kukifanya Lulu ni kuepusha mazingira ambayo yatonesha aligusana na Steve...
 
Siku ya leo umefanya kazi ya kukuingizia kipato juu ya uzao wako?
 
Kujichanganya sio suala LA elimu mkuu,si suala LA uongo na usahaulifu,ukiongea kwel tupu ukanyoosha maelezo ilivyokuwa hakuna sehemu utajichanganya
 
Kama ni hivyo, wanampa grounds za ku appeal kwamba hakimu alikuwa biased kwa kuanza kuuliza maswali ya waendesha mashitaka.
Hapana, hakimu anaweza kumuuliza mtu swali lolote na wakati wowote, hakimu anaweza kukataa swali au akamodify swali wakati wowote.

Mambo ya kisheria ya ajabu sana mkuu. Hapo hakimu hajatenda kosa lolote, sema ndio hivyo ameuliza swali litakalowapa waendesha mashitaka red light ili wao nao wapuge hapo hapo kummaliza kabisa.

Ukijichanganya tu kwenye cross examination, maelezo yako yote uliyotoa yanaweza kua discredited na ukajikuta kwenye matatizo hasa kama wewe ndie mwenye kesi, ikiwa ni shahidi basi ushahidi wake unatupiliwa mbali kabisa.

Natamani hata nikapate ka certificate ka sheria aisee. Sheria tam sana.
 
Hakimu haruhusiwi kuuliza swali litakalomvunjia mtu haki zake za kikatiba, akifanya hivyo anaweza kusababisha mistrial.
 

Sioni uhusiano wa Lulu kujichanganya kuhusu leseni ya kuendesha gari na kifo cha Kanumba.

Sioni ni kivipi kujichanganya huko kuhusu leseni kutaathiri matokeo ya hiyo kesi.
 
Hakimu haruhusiwi kuuliza swali litakalomvunjia mtu haki zake za kikatiba, akifanya hivyo anaweza kusababisha mistrial.
Nakupata mkuu.

Ila nadhani kwenye hili hakimu hakua nje ya mipaka ili kuweka kesi sawa sawa maana umri wa Lulu ulikua na mashaka kipindi kile cha kifo cha Kanumba.

Nadhani pia hata kwenye utetezi wake Lulu kuna sehemu atakua kazungumzia umri wake kipindi hicho au kwenye maelezo ya awali kutakua na sehemu ya umri wake wakati kitendo hicho kinatokea.

Niliona jana mahala pia kua alieleza kua alienda kwa Kanumba na gari, hivyo unaona ni mambo yanayohusiana na tukio. Maana lazima uulizwe ulifikaje kwa jamaa, akasema alienda akiwa anaendesha gari, hapo akazua jambo lingine.

Ndio maana hakimu ametaka kuweka kumbukumbu sawa, kama lienda na gari anaendesha, je alikua na leseni, je aliipataje kama alikua chini ya miaka 18, alidanganya polisi, kama alidanganya atakua kadanganya mangapi?

Lulu akikutana na mwanasheria mzuri wa cross examination hachomoki, aombe wamuwekee wanasheria mazwazwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…