Mkuu, lazima waestablish mazingira kabla ya tukio. Hivyo lazima aulizwe mazingira ya awali kabla ya tukio, kama kuonana na marehemu, milonana wapi, mlikutana vipi, ilikua sehemu gani nk nk.
Hivyo katika maelezo hayo Lulu atakua amesema labda aliitwa na marehemu au alipugiwa simu na marehemu aende kwake. Ataulizwa, aliendaje, kwa miguu au boda boda au taxi au daladala, akisema taxi, ataulizwa anamkumbuka dereva aliempeleka au hamkumbuki, je huyo dereva alimfaham kabla au alimuona siku hiyo.
Sasa yeye alisema alienda na gari yake akiwa anaendesha, hapo akazua jambo jipya, je alikua na leseni, je leseni aliiapata kiuhalali, alipataje leseni huku alikua na umri wa chini ya miaka 17 au alidanganya polisi ili apewe leseni, kudanganya polisi ni kosa kisheria.
Hayo maswali na mengine mengi yanahusiana kabosa na kesi hiyo ya Lulu.