KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

Lulu kuogopa kupigwa na kanumba endapo angeanguka kunaniambia kilichosababisha Kanumba kuanguka ni kupigwa na Lulu.

Kuna rumors zilisemaga kuwa baada ya tukio alipewa lifti na Alikiba. Huweza kuta Alikiba alimpiga Kanumba na kumkimbiza Lulu.

Mimi si mtaalamu sana.
 
Nimesoma maelezo hayo kama ndivyo alivyoeleza basi asubiri mvua zake kadhaa.inaonyesha kuna kitu kikubwa kimejificha.Hasa kuhusu hilo panga.je Lulu alikuwa mtu wa kumshikia panga kweli.je Aunt Ezekieli umshikie nini? SMG?
 
USHAHIDI ALIOUTOA LULU MAHAKAMANI KUHUSU KIFO CHA KANUMBA

Msanii wa filamu, Elizabeth Michael (22) amejitetea katika kesi ya kuuwa bila kukusudia katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Katika utetezi wake, Lulu amesema anakumbuka siku ya tukio ilikuwa Ijumaa ya April 6/2017 ambapo aliahidiana na rafiki zake kwamba wangetoka usiku.

Amesema kuwa asubuhi ya siku hiyo alienda kuonana na rafiki zake maeneo ya Mikocheni, ambapo pia alikuwa akiwasiliana na Kanumba.

"Marehemu alikuwa ni msanii mwenzangu lakini pia nilikuwa naye na mahusiano naye ya kimapenzi,".

Lulu alisema kuwa marehemu Kanumba alikuwa hapendi kumuona akitoka, hivyo hadi siku ya tukio hakutaka kumwambia kwamba atatoka na rafiki zake.

"Hata hivyo ilipofika saa 6 kasoro usiku, nilimpigia simu Kanumba na kumwambia nataka nitoke na rafiki zangu, hivyo nitapitia nyumbani kwake nimuage,".

Lulu amesema alienda hadi nyumbani kwa marehemu, ambapo ni Sinza Vatican na akamwambia akikaribia atampigia simu.

" Nilipompigia tena simu akanambia anataka kwenda kuoga, hivyo kama nikifika nipitilize hadi chumbani maana hataweza kupokea simu, ".

Lulu amesema kuwa alipofika nyumbani aliingia mpaka chumbani, ambapo alimkuta Kanumba akiwa kwenye dressing table akipaka mafuta kwenye nywele, huku akiwa anakunywa pombe aina ya Jack Daniel.

Amesema kuwa kutokana na chumba hicho kutokuwa na sehemu ya kukaa, aliamua kukaa kitandani huku akisalimiana na marehemu.

"Baada ya muda kidogo simu ya Kanumba ikaita ambapo alikuwa akiongea na Charles Baba akimuuliza kama ataenda kwenye muziki wa bendi usiku huo, ambapo Kanumba alimwambia anamalizia kujiandaa anakuja,ambapo na mimi nikamwambia nataka nitoke na rafiki zangu,".

Lulu amesema kuwa baada ya kumwambia Kanumba kuwa anataka kutoka alianza kuumuliza anataka kwenda wapi.

" Nilimjibu kuwa nataka nitoke na rafiki zangu twende Disco mimi sipendi muziki wa Dansi kwani nj kama wakizee, lakini yeye alikuwa hataki badala yake anataka twende wote kwenye dansi,".

Lulu ameeleza kuwa wakati akiendelea kuongea na Kanumba, simu yake ikawa inaita ambapo aliogopa kupokea mbele ya Kanumba kwa sababu alihisi rafiki zake wanampigia, hivyo endapo wangemuuliza kuhusu suala la kutoka basi Kanumba angesikia.

Kutokana na hali hiyo, Lulu alisema kuwa aliamwambia Kanumba kwamba anataka akachukue Maji ya kunywa jikoni.

"Nikiwa naelekea kuchukia Maji nilipokea simu, ambapo nikaanza kuongea na rafiki zangu kwamba wasubiri nitatoka, lakini wakati nakata simu Kanumba alikuwa ananifatilia kwa nyuma na kuanza kuniuliza naongea na nani,

" Niliogopa kumwambia kwa sababu ningemwambia naongea na rafiki zangu kuhusu kutoka angenipiga, nikaanza kumtania kwa kumwambia unanifata hadi jikoni kujua naongea na nani,".

Akiendelea na ushahidi wake, Lulu amesema kuwa Kanumba alikuwa akimuuliza anaongea na nani huku akimfata, na akiwa katika hali ya kukasirika ambapo yeye akawa anarudi nyuma.

"Wakati wote huo alikuwa katika hali ya kulewa, hivyo wakati ananifata nikahisi anataka kunipiga na mimi nikawa nazidi kurudi nyuma nikafungua mlango na nikatoka hadi nje,".

Amesema kuwa aliamua kutoka nje akiamini kwamba Kanumba asingeweza kumfata kwa sababu alivaa taulo na alikuwa tumbo wazi, hivyo angeona aibu na angeshindwa kumfata kulingana na umaarufu wake.

" Hata hivyo aliendelea kunifata, ambapo alinikimbiza hadi getini na akatoka hadi nje ya geti akiwa peku peku,".

Lulu amebainisha kuwa kutokana na hali hiyo aliamua kukimbia hadi lilipo gofu la baa ya Vatican ambayo ilikuwa haifanyi Kazi kwa wakati huo.

"Wakati tukio likiendelea umeme ulikatika, ambapo mimi niliingia hadi kwenye ghofu hilo na kujificha, lakini Kanumba alinifata hadi nilipojificha na kuanza kunipiga makofi ya uso,".

Amesema kuwa baada ya kumpiga alimshika mikono na kuanzia kumburuza kutoka nje hadi kumuingiza ndani, ambapo alimuingiza hadi chumbani kwake kisha kufunga mlango na funguo, kisha kumrusha kitandani.

"Baada ya kunitupa kitandani, aliinama chini na kuchukua Panga ambapo akaanza kunipiga nalo kwenye ubapa hasa maeneo ya mapajani, kutokana na mimi nilikuwa natapatapa ambapo nilijiziba uso ili asiweze kunikata huku nikipiga kelele za kuomba msaada,

*wakati akinipiga alikuwa akilalamika kwamba kwanini naongea na simu na mwanaume mwingine mbele yake,".

Lulu amebainisha kuwa wakati Kanumba akimpiga alikuwa katika hali ya jazba na kuema kwa haraka.

" Ghafla nikasikia sauti ya Panga limedondoka chini, pia nikasikia sauti kama ya mtu amekabwa, ambapo nilitoa mikono na kuona ameanguka kwa kujigonga kichwani kwenye ukuta, kisha akawa kama mtu anayetapatapa ambapo alirudi tena nyuma na kujigonga ukutani,,".

Lulu amesema kuwa kutokana na hali hiyo, aliinuka kutoka kitandani na kukimbilia chooni kwa ajili ya kujificha, huku akiwa anapiga kelele za kuomba msaada.
 
Lulu kuogopa kupigwa na kanumba endapo angeanguka kunaniambia kilichosababisha Kanumba kuanguka ni kupigwa na Lulu.

Kuna rumors zilisemaga kuwa baada ya tukio alipewa lifti na Alikiba. Huweza kuta Alikiba alimpiga Kanumba na kumkimbiza Lulu.

Mimi si mtaalamu sana.
Yaani we hata uelewi kinachoendelea.....Seth Bosco ambae ni mdogo wa Kanumba anakwambia ndani walikuwa watu watatu na Lulu mwenyewe anathibitisha hivyo.
 
japo nilikuwa sikapendi kalulu yaani leo tumbo la uzazi limenishika haswa.EE mwenyezi Mungu naomba umsaidie huyu mtoto asifungwe.please father wewe ni mwingi wa huruma na REHEMA
hapo Mungu hausiki sheria ndo itachukua mkondo wake

kama hana hatia tutakua nae uraiani ila kama vingine tusubiri stori nyingine tu
 
Nasikia Lulu alikua anamuhudumia mama Kanumba akachoka mama akaona alihamshe dude tena
 
Usiwe mwepesi kunyoshea mwenzako kidole, hii dunia hakuna mkamilifu ndugu, ni kwa vile hapo umejificha kwenye keyboard ndio maana mapovu yanakutoka tu, ila una mengi ya gizani pengine kuliko huyo Lulu

Alafu umekazania ooooh Lulu alikua anakazwa na Komba, sasa cha ajabu nin hapo?? Lulu si wa kike? Ulitaka akazwe na ngedele bse kukazwa na Komba imekuuma sana!

Au ulitaka ukazwe wewe
Umeongea point mkuu...hii dunia hakuna mjanja asee

Lulu ana nyodo na maneno fulani ya shombo but kwa hili janga namuombea asee
 
hamna kesi pale,

kwani itabidi wathibitishe kamuua kivipi,kampiga makonde,ama kamnyonga au wakisema kamsukuma ,itatakiwa eye witness aliemuona lulu akimsukuma kanumba,

maelezo ya lulu yako supported na circumsitantial evidence kama kukutwa panga pembeni ya kitanda,kukutwa chupa ya pombe chumbani na kama daktari walimpima kilevi marehemu yote yatachangia kuonyesha lulu hana hatia,
kwa uzoefu wangu
Kuna sehemu anasema marehemu alimpigapiga na mapanga mapajani, maana yake kulikuwa na contact, yaani walishikana... Hapo ndipo kesi ya kujibu inapoanzia.
 
Ulitaka aende wapi? Na Kanumba alitakiwa akalee katoto kakue ktk misingi mema ya kumcha Mungu ila yeye akawa anakakomaza na kukaraghai

Lulu is innocent
Kwa nn asikimbilie kwao kwa mama ake eti aende kupunga upepo Coco apunguze stress mtoto Gan huyo anawaza Coco wakati anajua kuna ktu kimetokea ambacho Si cha kawaida kwake....
 
japo wananchi wenzangu mnashangilia huyu binti kufungwa, me niko against na nyie, ingawa hata sio fan wake,lakini namhurumia sana,jela sio sehemu nzuri kabisa,mimi niliwahi kukaa lock up masaa kadhaa tu,mpaka leo nina adabu zote...tuombe Mungu tu mahakama ionyeshe huruma zake tuendelee kuwa nae uraiani..maana kesi yenyewe imemkalia vibaya,halafu marafiki zake nao ni kama wamemtenga vile..dah!namhurumia sana kiukweli
Mm sitak afungwe Ila naona utetezi wake utamfunga
 
Back
Top Bottom