KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

KESI YA MAUAJI: Utetezi wa Elizabeth Michael (Lulu) ndani ya mahakama kuu

japo wananchi wenzangu mnashangilia huyu binti kufungwa, me niko against na nyie, ingawa hata sio fan wake,lakini namhurumia sana,jela sio sehemu nzuri kabisa,mimi niliwahi kukaa lock up masaa kadhaa tu,mpaka leo nina adabu zote...tuombe Mungu tu mahakama ionyeshe huruma zake tuendelee kuwa nae uraiani..maana kesi yenyewe imemkalia vibaya,halafu marafiki zake nao ni kama wamemtenga vile..dah!namhurumia sana kiukweli
Watu wamemezeshwa sumu mkuu...si rahisi kukuelewa maana wanachokitaka wanakijua wenyewe
 
Ataangukaje mwenyewe na wakati aliweza kumfukuza nabkumzuia bi Lulu akiwa amejifunga taulo na taulo halikumdondoka.Huyu binti alposema jamaa alikuwa na tabia ya kupiga kila akilewa kajichanganya,atakjwa alijipanga.muda mrefu kumuwahi kabla hajampiga,hapo she was malicious.
 
Nafikiri angekubali kuwa walikuwa wanasukumana hivyo bahati mbaya akaanguka Kanumba,kesi ingekuwa manslaughter mwisho umri ungembeba na kuachiwa akarudi home kula bata kama kawa.
 
Pamoja na yote haya mimi nabet kwamba dogo anashinda hii kesi ya msingi,sababu kwanza alikuwa under 18 kipindi hicho na hii ilishathibitika mahakamani,pili marehemu alimshambulia lulu na alikuwa amelewa na panga kwel lilikuwepo eneo LA tukio na lulu alitibiwa majeraha ya shambulio,Tatu chumbani walikuwa wawili tu hii inafanya kusiwe na WA kupinga kauli ya lulu kuhusu kilichoendelea huko wakiwa wawili tu,nne amekana kuhusika kwa namna yoyote hata kumsukuma amesema hakumsukuma Bali marehemu alianguka mwenyewe kwa ulev na pirika zake za kutoa vichapo.dogo anashinda hii kesi Bila shida labda ubaki msala WA leseni ambao ni issue ndogo tu ukilinganisha na kesi ya msingi.hapa hata mzigo naweka WA kutosha Nina uhakika hii betting inatoa kabisa
 
japo wananchi wenzangu mnashangilia huyu binti kufungwa, me niko against na nyie, ingawa hata sio fan wake,lakini namhurumia sana,jela sio sehemu nzuri kabisa,mimi niliwahi kukaa lock up masaa kadhaa tu,mpaka leo nina adabu zote...tuombe Mungu tu mahakama ionyeshe huruma zake tuendelee kuwa nae uraiani..maana kesi yenyewe imemkalia vibaya,halafu marafiki zake nao ni kama wamemtenga vile..dah!namhurumia sana kiukweli
Akithibitika ana hatia asondekwe tuu,waache kutafuta sifa nyiingi wakati bado wadogo,namwangalia Tunda naye asipoangalia ataishia hivi hivi.
 
Aman iwe nanyi wapendwa

Niko hapa mahakaman nikifatilia kwa karibu hii kes ya lulu

Moja ya vitu vinavyoniacha hoi ni maswali ya majaji wa hapa mahakam

Jaji lumanyika anaonekana kumukazia sana lulu tofaut na majaji wengine nahis huyu jaji atakuwa msukuma

Kamtwanga swali lulu kuhusu lesen ya gar lulu kasema alikuwa na lesen kipindi hicho

Akamurudia tena ieleze mahakama kama lesen yako ilikuwa halal, lulu akajichanganya akasema sikuwa na lesen

Mtanange bado unaendelea

Kwa kes ninanyoiona lulu lazima ale miala si chin ya kumi na tano

Bado niko hapa makaman mazee

LONDON BABY
Rumanyika ni wahaya na mama Kanumba ni muhaya
Hata hivyo sio ukabila bali ni taratibu za sheria tu
Km alisema aliendeshaa gari wkt anadai hakuwa na umri wa miaka 18 ambao kisheria ndio unaruhusu kuwa na leseni lzm ajichanganye
 
Lumanyika ni mhaya na mama wa Marehemu Kanumba ni Mhaya pia, kwaiyo utakuwa umepata majibu mkuu.
 
Akithibitika ana hatia asondekwe tuu,waache kutafuta sifa nyiingi wakati bado wadogo,namwangalia Tunda naye asipoangalia ataishia hivi hivi.
jaribu kumuombea mwenzio walau kikombe hiki kimwepuke...umri wake mdogo sana kiukweli kulinganisha na haya mashtaka yanayomkabili
 
japo wananchi wenzangu mnashangilia huyu binti kufungwa, me niko against na nyie, ingawa hata sio fan wake,lakini namhurumia sana,jela sio sehemu nzuri kabisa,mimi niliwahi kukaa lock up masaa kadhaa tu,mpaka leo nina adabu zote...tuombe Mungu tu mahakama ionyeshe huruma zake tuendelee kuwa nae uraiani..maana kesi yenyewe imemkalia vibaya,halafu marafiki zake nao ni kama wamemtenga vile..dah!namhurumia sana kiukweli
hamna kesi pale,

kwani itabidi wathibitishe kamuua kivipi,kampiga makonde,ama kamnyonga au wakisema kamsukuma ,itatakiwa eye witness aliemuona lulu akimsukuma kanumba,

maelezo ya lulu yako supported na circumsitantial evidence kama kukutwa panga pembeni ya kitanda,kukutwa chupa ya pombe chumbani na kama daktari walimpima kilevi marehemu yote yatachangia kuonyesha lulu hana hatia,
kwa uzoefu wangu
 
Sawa, inawezekana muongo, lakini muongo kuhusu nini?

Inawezekana alikuwa na leseni ya bandia, akasema alikuwa na leseni, akajishtukia leseni haikuwa halali, akachomoa, akadanganya kuhusu leseni.

Hilo halimaanishi kadanganya kuhusu kuua.

Kwamba kakataa alikuwa namahusiano na Komba inawezekana anadanganya, huyu mtoto mdogo, Komba mtu mzima alikuwa na mkewe na watoto wakubwa kuliko Lulu. Sasa msichana kama Lulu akikataa ukweli kwamba alikuwa na uhusiano na jibaba inawezekana anadanganya, lakini je, kudanganya kuhusu uhusiano huo kunamaanisha kwamba yeye ni muuaji?

Ningeona contradiction ina nguvu zaidi kama ingeweza kuhusishwa moja kwamoja na kesi ya mauaji, siyo habari za kumharibia character tu. Mtu yeyote ukimuweka katika microscope utakuta mapungufu, huyu ana mchepuko, huyu hajalipa kodi, huyu anampiga mkewe, huyu mlevi mbwa, lakini, kama tunazungumzia kesi ya mauaji, kitu muhimu ni ushahidi wa kesi ya mauaji, si hizi habari nyingine. Unless zinaingia moja kwa moja katika kesi ya mauaji.

Kama Kanumba angefariki katika ajali ya gari ambalo Lulu alikuwa anaendesha, hapo habari za leseni ya Lulu ingekuwa very relevant.

Lakini haikuwa ajali ya gari, suala la leseni ya Lulu linakuja vipi? Sisemi kwamba halihusiki, inawezekana linahusika (sijafuatilia kesi kwa karibu). Ningependa kujua tu, linahusikaje?

Ukimchukua mtu yeyote na kuanza kumdai risiti za nguo zake zote alizonunua katika miak 10 iliyopita, utakuta kuna nguo kibao hana risiti.

Je, hilo linatosha kusema huyu ni mkwepa kodi na hivyo anaweza kuua tu?
Umeandika kiubinadamu ila sio kisheria
 
Maelezo yake yanaonyesha kabisa kuwa yanauongo kujichanganya huku ndio matatizo ya mtoto kuvamia mambo makubwa kuliko umri wako wakiambiwa wanakwambia wivu sasa umri huo unamilili wanaume wakubwa badala ya kuwa ndani unajisomea wewe uko kwa mabwana kina mama kweli ndio wa kulaumiwa kwa malezi bado huyo gigy money
 
hivi muda wotehuo yuko nje alikosa hata wanasheria wakumpa madesa ya kutema mahakamani?tatizo la huyu binti nadhani ni amekosa watu wa kumuongoza katika maisha yake,kesi kama hii anaenda kizembe zembe hivyo mahakamani,watamla kichwa shauri zake
 
Back
Top Bottom