ivan1212
JF-Expert Member
- Mar 4, 2019
- 932
- 2,441
Inaendelea mkuu, kuwa na subiraMbona imeishia hapa?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Inaendelea mkuu, kuwa na subiraMbona imeishia hapa?
Atanibariki kwa nyakati zake Jo wala usihofuPokea baraka za Mungu.
Mungu ibariki CHADEMATuko pamoja
Ajapata posho ya buku 7 ila yupo kwenye foleniNakuona Jo![]()
Huyu Madenge naye anaingia 'kikaangoni'.Shahidi mfupi amevaa kaunda[emoji3][emoji3]
Kwamba wakimfunga utaacha hiyo tabia yako ya kumchungulia bibi yako akiwa chooni.Wamfunge tu mbona ushahidi wa jamhuru umeenyooka hivyo. Kuliko hata ule wa Sabaya wa kuunga unga naa gundi. Kama hii kesi ni ya uwongo niamini kesi ya namna gani. Technologia aidanganyi bhana
Mnasumbua tu mahakana
YeleuwiiKwamba wakimfunga utaacha hiyo tabia yako ya kumchungulia bibi yako akiwa chooni.
Ni aibu sana na inashangaza na kufikilisha ni kipi kiliwapa jeuri IGP na Samia kuizungumzia hii kesi kua ushahidi wanao..Hii kesi inavyoendelea upande wa serikali wamebaini upande wa utetezi wamejipanga sana.
Ni tofauti na walivyokua wakidhani.
Jinsi kesi inavyoendelea wanazidi kubaini wamekurupuka.
Shahidi jana kutofika ni moja ya dalili.
Ngoja tuone leo.
hawa askari walikuwa wanatunga hadithi ambayo ilikosa uhariri......project ya hovyo kabisa....kibaya sana WANACHEZEA FEDHA ZA WANANCHI WAZI WAZI.....TUNAKATWA MITOZO wanachezea fedha kulipana lipana kwenye kesi ya maigizoumenikumbusha mzee wa tubongeee kamilioni nasema tubongeee mungu baba...tubongeee
Binafsi nmekuelewaWamfunge tu mbona ushahidi wa jamhuru umeenyooka hivyo. Kuliko hata ule wa Sabaya wa kuunga unga naa gundi. Kama hii kesi ni ya uwongo niamini kesi ya namna gani. Technologia aidanganyi bhana
Mnasumbua tu mahakana
@ TAJIRI Tanzanate. Hebu kuwa na hekima. Kama umetumwa MBOWE afungwe basi nenda niambie jaji Artie hukumu.Kwani lazima upaste hii comment kwenye kila uzi? Acha undezi dogo
Huyu TAJIRI JIWE NI mpuuzi Tu. Maana hauoni ukweli. AnakeraMaoni ya tajiri jiwe.
Kamnajisi Chief Mkwawa,Jaji: Kabila
Shahidi: Mheh
Jua kali sana viwanja hivi vya mahakama.Baada ya jana kuahirishwa, Kesi ya mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe inaendelea kuunguruma leo mahakamani. Jana kesi iliahirishwa kutokana shahidi kupata dharura ya kiafya na upande wa utetezi haukutoa kikwazo chochote kwenye sababu hiyo. Jaji aliahirisha mpaka leo. Kuwa nami.
==============
Jaji ameingia.
Kesi inatajwa
Robert Kidando anatambulisha Jopo lake
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Tulimanywa Majige
Peter Kibatala anatambulisha Jopo la mawakili wa utetezi
Peter Kibatala
John Malya
Fredrick Kiwhero
Dickson Matata
Idd Msawanga
Nashon Nkungu
Maria Mushi
Khadija Aron
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri lina kuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja Tupo tayari kuendelea
Wakili wa Serikal: Mmoja anatoka kwenda Kumfuata
Jaji: upande wa Utetezi
Wakili Peter Kibatala: Na sisi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi Wenu?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ameenda Kufuatwa Anaingia Shahidi Mfupi Kavaa Kaunda
Jaji: Majina yako
Shahidi: SSP Sebastien Madembwe
Jaji: umri
Shahidi: 46
Jaji: Kabila
Shahidi: Mhehe
Jaji: Shughuli zako
Shahidi: Afisa wa Polisi
Jaji: Dini yako
Shahidi: Mkrito
Shahidi: Mimi SSP sebastian Madenge Naapa Kwamba Ushahidi nitakaotoa ni Kweli tupu Eeeh Mwezi Mungu nisaidie
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shahidi Ataongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla
Wakili wa Serikali: Shahidi umesema Majina yako kwa ukamilifu ni nani
Shahidi: SSP sebastian Madenge
Wakili wa Serikali: Unaishi Wapi
Shahidi: Iyumbu Kule Dodoma
Wakili wa Serikali: Mkazi wa Dodoma tangu lini
Shahidi: Mwezi wa Nane 2020
Wakili wa Serikali: Kabla ya hapo ulikuwa unaishi Wapi
Shahidi: Nilikuwa naishi Muongo la Ndege Ukonga, Nikiwa Ofisa wa Polisi Makao Makuu, iliyokuwa Makao Makuu Dar es Salaam
Wakili wa Serikali: Uliajiliwa lini kama Polisi
Shahidi: 02 Mwezi 09 Mwaka 1999
Wakili wa Serikali: Katika Jeshi la Polisi Upo kamisheni gani
Shahidi: Nipo kamisheni ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai
Wakili wa Serikali: Kitengo Gani
Shahidi: Udhibiti na Usajili wa Silaha
Wakili wa Serikali: Kwa Kizungu Mnaitaje
Shahidi: Arms Management and Registration Unit
Wakili wa Serikali: Kitengo hilo kina husika na Nini
Shahidi: Usajili wa Silaha za Raia Utoaji wa Leseni za Kumiliki silaha Kibali Vya Kuingiza Silaha Nchini Vibali Vya Usafirishaji wa Silaha na Risasi Hapa Nchini
Shahidi: Vibali Vya Upotoshaji wa Silaha zinazoenda Nchi mbalimbali kupitia Kwetu Tunatoa Vibali Vya Uuzaji wa Silaha na Risasi Yote yanahusiana na Usajili wa Silaha Tunahusika pia na Nchi Mbalimbali katika Udhibiti wa Silaha katika Kutekeleza Mikataba ya kikanda na Kimataifa
Wakili wa Serikali: Umesema Usajili wa Kiraia Je Unamaanisha Nini Shahidi: Ni zile Silaha zilizoruhusiwa Kwa Mujibu wa Sheria namba 02 ya Mwaka 1995 Sheria imetaja Silaha zinazoruhusiwa ni Pistol, Riffles, Short gun na Silaha yoyote ambayo Bodi ya Udhibiti wa Silaha itapendekeza iingie Miongoni Mwa silaha za Kiraia
Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji, Silaha Nyingine ni Gobole
Wakili wa Serikali: Silaha Ndogo na nyepesi Fafanua hapo
Shahidi: Udhibiti Wa Silaha hizi tunazomiliki za Kiraia, Silaha Ndogo Ndogo ni zile ambazo Mtumiaji ni Mtu Mmoja. Kwa Mfano AK47 ni Silaha Ndogo Lakini Silaha Nyepesi yani Light Weapon ni Ile ambayo inatumika kwa Urahisi
Wakili wa Serikali: Kwenye Kitengo wewe ni nani
Shahidi: Ni Mrajisi Wa Leseni za Bunduki
Wakili wa Serikali: Kwa Kizungu
Shahidi: ni CEO arms Register
Wakili wa Serikali: Majukumu yako wewe ni Yapi
Shahidi: Ni Kuhakikisha kwamba napokea Maombi yote ya Waombaji wanataka Kumiliki silaha, Yaliyopitishwa na Kamati za Ulinzi na Usalama Kuanzia ngazi ya mtaa ambalo Mwombaji anaishi, Kata, Wilaya na Kamati ya Ulinzi na Usalama Ya Mkoa
Wakili wa Serikali: Jukumu la Pili..?
Shahidi: Kuyakagua Maombi hayo niliyoyapokea ilikuina kama Yana Vigezo kwa Mujibu wa Sheria, Licha ya Kwamba Maombi hayo yatakuwa yamepitishwa kwenye Kamati nilizozitaja Na Kwamba Maombi Yaliyokodhi Vigezo huendelea Kuya Shughulikia Ngazi inayofuata
Maombi Yaliyokidhi Vigezo nayarudisha yalikotoka Kutoa Vibali Vya Uuzaji wa Silaha hapa Nchini, Kibali cha Usafirishaji WA Silaha hapa Nchini na Upitishaji Vibali kwenda Nchi Jirani hasa wanatumia Bandari yetu Tunatoa Vibali Vya Kutunza Silaha (Warehouse License)
Shahidi: Tunatoa silaha Gunsmith Lisence (Kibali Cha Kufanyia Matengenezo silaha kwa Raia endapo itapata hitilafu Na Pia kutoa Leseni kwa wale waonataka Kumiliki Silaha Kutunza Kumbukumbu ya Silaha na Wamiliki wote ambao wamesajiliwa
La Mwisho ni Kupokea Maombi ya Kiuchunguzi pale silaha Inapo okotwa Ili tuweze Kuangalia Kwenye Data Base Kama Silaha hiyo imesajiliwa Au lah
Wakili wa Serikali: Mbali na Maombi hayo, Maombi Mengine huja kwa Namna gani
Shahidi: Ninapozumgumzia Uchunguzi no Uchunguzi wa Taarifa
Yoyote inayohitajika kwa ajili ya Shughuli ya Kiupelelezi, Ni Kitengo Kinacho Support Upelelezi katika Maswala ya Silaha
Wakili wa Serikali: Moja ya Jukumu umesema kutoa Vibali au Leseni za Umiliki wa Silaha Je Mchakato Ukoje Utaratibu wa Mpaka Mtu apewe Leseni
Shahidi: Wa Kwanza ni Kupokea Maombi ambayo yamepitishwa katika Kamati za Ulinzi na Usalama
Wakili wa Serikali: Kabla ya Hilo anaanza na Jambo gani Shahidi Ni Kununua Silaha, anaweza Kununua Katika Vyanzo Vitatu 1. Kwenye Duka ambalo wamepewa Leseni ya Kuuza Silaha (Lisenced Dealer)
2. Kwa Kununua kwa Mtu aliyekuwa anamiliki hiyo silaha Kihalali kwa kuandikishiana Mkataba wa Kisheria Na Kama Silaha ya Mirathi basi Kikao cha Ndugu wa Marehemu Kitakaa chini ya Mwenyekiti ambaye atakuwa amepitishwa na Mahakama Kwamba ni Msimamizi wa Mirathi kwamba ni nani wa Kuirithi Silaha hiyo Endapo wataamua Basi Mrithi anaweza Kumiliki Mwenyewe Kwa Utaratibu wa Kisheria au Kuuza Lakini Mrithi atahakikishq Kwamba Mteja anaye Muuzoa anamkabidhi Nyaraka zote za Mirathi pamoja na Mkataba walioandikishana Kisheria
3. Muombaji anaeleza Kununua Nje ya Nchi kwa Kuomba Kibali cha Kuingiza Hiyo silaha Nchini (Import Lisence) iwe Bandarini au Uwanja wa Ndege TASAKI ndiye atahusika Ku Clear hiyo silaha na Kuhifadhi wakati Muhusika ataendelea na Taratibu za Kuomba Kumiliki Silaha Hiyo
Shahidi: Kwa hiyo katika Vyanzo Vyote VitatuSilaha utatakiwa kuwa Kwenye Ghala, yeye atakuwa na Nyaraka za Mauziano ili ziweze Kumsaidia kama attachments katika Maombi yake Zipo fomu za Umiliki wa Silaha Kwa Mujibu wa Sheria na Kanuni zinaitwa Fomu A
Mwombaji hupaswa kuzijaza na Kuambatisha Nyaraka zote zinazoomyesha Chanzo cha Silaha hiyo Ata attach Fomu za Silaha hiyo, Kama Mfanya Biashara basi Leseni ya Biashara, Kitambulisho Cha Taifa na Nyaraka yoyote ile itakayodhibitisha Anamatishio Kutokana na Kazi anayofanya
Wakili wa Serikali: Inaambatana na nini hiyo fomu Ni lazima Kuwa muhtasari Kuanzia Ngazi ya Mtaa, Kata, Wilaya na Mkoa Wakili wa Serikali: Kingine?
Shahidi: Hati ya Tabia Njema inayotolewa na Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha
Kibatala: SAMAHANI Mheshimiwa Jaji Naomba Kwanza Kumuombea Wakili Jeremiah Mtobesya Aweze Kuingia Kwenye Orodha yetu Ambaye kachelewa Kwa sababu nilizotoa Mwanzoni Baada ya hayo nitaomba Sasa Wakili Mtobesya aweze kusema alichotaka
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Shahidi hana Maelezo katika Kifurushi cha Comito Kwa hiyo Ushahidi wake Hauwezi Kuingia Kwa Mujibu wa Kifungu cha 246 cha CPA Hakuna Maelezo yake, na Nimeulizana na Wenzangu Kama Upande wa Mashtaka Uliomba Mwanzoni Ombi lolote nimeambiwa Hapana
Mahakama Kimyaaaaaaa!
Upande wa mashtaka ni kama wamebutwa fulani hivi.
Mtobesya: Mheshimiwa Jaji Tutaomba Pia Maelekezo endapo Wenzetu watafanya Kwa Usahihi, Vipi kuhusu Ushahidi ambao Shahidi ameshaanza kuutoa hapa Mahakamani?
Mtobesya: Na ninataatifiwa hapa na kaka yangu, shahidi anatakiwa aondoke na ushahidi wake tuendelee na ushahidi Mwingine kwa Sababu hawawezi kupata faida baada ya sisi kusema kama wao hawakuomba mwanzoni Mawakili wa Serikali: Wananong'onezana Jaji anainama na kuandika
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ombi hilo halina mashiko yoyote ya kisheria
Jaji: maombi au pingamizi
Wakili wa Serikali: Ahaaa pingamizi, halina mashiko yoyote ya kisheria Sababu limeletwa katikati ya ushahidi Wa PW6 kinyume na sheria
Na Kama wangekuwa na hoja hiyo walitakiwa kufuatilia mapema, Lakini kwa wakili ambaye hakufuatilia tangu mapema proceedings hizi, Hoja yetu ya Pili ni kwamba Shahidi huyu aliorodheshwa tangu Kipindi Cha Committal Proceedings na anasomeka Kama Shahidi namba 23 tangu Mahakama Ya Hakimu Mkazi Kisutu Na hata katika Barua yetu ya 11 August 2021
Wakili wa Serikali: Ukurasa wa 32 na Jina lake linaonekana Katika 23 Labda lile neno S liondoke isomeke Sebastian
Wakili wa Serikali: Lakini Substance ilikuwa Committed na Ilisomwa Katika Mwenendo wa Shauri hilo katika Proceedings za Tarehe 23/8 Siku ambazo COMMITTAL Proceedings zilifanyika Na Jina lake limeandikwa sebastian Madembwe SSP
Lakini pia Katika Ile list ya Exhibit katika Ukurasa wa 33 Nyaraka Anayokuja Kuzungumzia imekuwa Litsted pale Namba 18 Ambayo pia imesainiwa na Sebastian Madembwe SSP nilikuwa Committed na Substance yake ilisomwa
Kwa hiyo kwa namna yoyote ile Hatukutakiwa Kuleta Ombi kupitia Kifungu cha 289 cha CPA ili Shahidi huyu aweze Kutoa Ushahidi Wake.. Na tunasema Pia Matakwa ya Rule 8 Sub 2 ya The Economic and Organized Crime Control (Corruption and Procedure Rules ya 2016),
Takwa hili la Kisheria lilitekelezwa na Mahakama. Iwe Jina ama Substance ya Ushahidi Anaotoa Leo hii hakuna Kitu Kipya kama Ambavyo wakili anajaribu Kuonyesha Mahakama yako Tukufu Na Kama hali Iko hivyo hakuna Haja Wa Kutoa Amri yoyote ile Kutokana na Ushahidi ambao Umeolewa na Shahidi Kwa sababu Shahidi Yupo Sahihi Kwa Mujibu wa sheria Hivyo Mheshimiwa Jaji tunaomba hilo Pingamizi ulitupilie Mbali ili Shahidi wetu aweze Kuendelea na Ushahidi Wake
Jaji anaandika Kidogo
Mtobesya: Kwanza Kabisa Wenzangu wameni attack, Personally Sikuwepo Kwenye Proceedings tangu Mwanzo, Mimi Kuchelewa Kufika sidhani kunaweza Kuathiri. Sisi tunachofanya hapa ni Kuisaidia Mahakama Kufanya Shughuli Zake Kwa Mujibu wa Sheria
Mtobesya: Nimesema Kwenye Committal Documents hakuna Ushahidi wa shahidi i huo. Substance inaongelea mambo matatu. 1. MAJINA Ingawa yamekosa hatuna Shida na hilo, 2 Cheti atakachotoa na 3. Hakuna Kile ambacho "Ataongea nini Mbele ya Mahakama"
Mtobesya: Tumeongea mara Nyingi kuhusu hili Kuwa kuna Sababu Ipo ya Kumpatia Mtu Nyaraka za Ushahidi kupitia Committal, Na Wasipokuwa wamefanya Upo Mlango Mwingine wa wao Kuomba kupitia Kifungu cha 289 Criminal Procedure Act
Wakili wa Serikali: Kama namwelewa Mtobesya anazumgumzia % Documents kutosomwa
Jaji: kama nimekuelewa umesema haipo kwenye Committal Bandle!
Mtobesya: Nimesema haipo kwenye Committal bundle kwa maana hiyo haijakidhi matakwa hayo ya kwenye 246 CPA
Jaji: Umeridhika na line yake ya argument sasa
Wakili wa Serikali: Hapana Sikubaliani na Mtobesya. Yeye ana argue kwamba haijasomwa, Maana akianza kujielekeza kwenye mengine na mengine inakuwa siyo sawa
Jaji: Hoja yao ni Kwamba argue kwa namna ambayo umeletea pingamizi
Mtobesya: Kwasababu Haipo ina maana haijasomwa, na kwa sababu haijasomwa inakiuka sheria aliyosoma Kaka yangu Kidando ya uhujumu uchumi na makosa ya uchumi ya mwaka 2016 Kingine Kaka Yangu anasema P. O imeletwa Kinyume na Sheria Kwa sababu Ilishapitwa
Hiyo siyo Sawa, Jambo lolote linaweza Kuibuliwa pale tu tunapoona tunaenda Kinyume na Sheria, tunalo hilo Jukumu Kama Wawakilishi wa wateja wetu na Pia kama Maafisa wa Mahakama Kwa hiyo kama ilivyoombwa Mwanzoni Mahakama Itoe Maelekezo na Kukidhi Matakwa YA Sheria. Ni hayo tu
Jaji anainama na kuandika kidogo
Jaji: Mmesikia hoja zote, Naomba nipate muda na mimi Tutarudi tena hapa saa tano na robo.. Anasimama na kutoka nje ya chumba cha mahakama
Kichwa maji sana.Wamfunge tu mbona ushahidi wa jamhuru umeenyooka hivyo. Kuliko hata ule wa Sabaya wa kuunga unga naa gundi. Kama hii kesi ni ya uwongo niamini kesi ya namna gani. Technologia aidanganyi bhana
Mnasumbua tu mahakana