Kesi ya Mbowe: Ushauri wa Mbatia kwa Rais Samia

Kesi ya Mbowe: Ushauri wa Mbatia kwa Rais Samia

mbatia aache unafiki, Kuna mashekhe wa uamsho wengine mpaka leo bado wapo ndani,mbona hakutoka nje aongelee hili, leo huyu mpuuz mmoja kaswekwa ndani kwa kuleta taharuki ametoa pua yake kwenye media,angekuwa mtetez Basi angebalance hapo tungemuelewa, otherwise ni utopolo tu !!
Sio kila kesi ni za mchongo.Ya Mbowe sababu ushahidi umeonekana angalau kiasi.Hizo nyingine hazijasikika hata kuanza.Utalinganishaje?Hii ni mbinu inayotumiwa ili kupandikiza mbegu za kidini na kikabila ili focus ya kudai haki ipotezwe
 
Sio kila kesi ni za mchongo.Ya Mbowe sababu ushahidi umeonekana angalau kiasi.Hizo nyingine hazijasikika hata kuanza.Utalinganishaje?Hii ni mbinu inayotumiwa ili kupandikiza mbegu za kidini na kikabila ili focus ya kudai haki ipotezwe

Yawezekana zao za michongo wanazijua.

Ukweli mchungu, kwa hali ilivyo na bila katiba ya haki: polisi, magereza na mahakamani - ni mwendo wa ukiukwaji wa haki za binadamu tu.
 
Ndugu MpendaTz , ni kweli watu wengi na dunia karibu yote imeshaona kuwa hapo hakuna kesi bali ni watawala wachache kuitumia mahakama kukomoa wapinzani wao kisiasa....

Na kwa hiyo, na kwa lugha rahisi ni kusema kuwa, huu ni mchezo wa siasa tu uliopewa sura ya "UJINAI" na jinai anageuziwa mtu mwingine aonekanaye kikwazo kwa mambo ya watawala....

LAKINI WAFANYEJE SASA? Maana hata Rais Samia Suluhu mwenyewe bila shaka ameshaelewa kuwa, ni KWELI AMEDANGANYWA kwenye hili naye bila kujua akaingia mkenge...?

Mimi nina hakika ANALO LA KUFANYA lakini lililo na gharama za kulipa KISIASA. Na hapo ndipo ugumu ulipo. Kwamba aumeze UONGO wake au ASHUPAZE shingo ivunjike..?

UONGO WAKE kwa sababu alishautangazia ulimwengu kuwa Freeman Mbowe ni gaidi na mhalifu na wenzake anaoshirikiana nao tayari walishahukumiwa kifungo cha jela huku ukweli ukiwa kinyume chake...!!

Aidha, kesi iko mahakamani lakini cha ajabu Rais Samia Suluhu na wenzake huko serikalini na CCM completely wameshashindwa kujenga msingi wa UGAIDI na UHALIFU wa Freeman Mbowe na hakuna hata mmoja aliyekwisha hukumiwa jela kama Rais Samia na Polisi wake wanavyodai....!!
Alivyokua anamnanga jpm kwenye clip alizokua anatayarisha na yule mchaga mwenzake mwenezi wake alishakua na uhakika kama samia na magufuli sio kitu kimoja au la? 🤔 Maana ingekua mimi ndio samia kwa uongo na uzushi ule ningekushughulikia tu. 🙄
 
Alivyokua anamnanga jpm kwenye clip alizokua anatayarisha na yule mchaga mwenzake mwenezi wake alishakua na uhakika kama samia na magufuli sio kitu kimoja au la? 🤔 Maana ingekua mimi ndio samia kwa uongo na uzushi ule ningekushughulikia tu. 🙄

Una maana ni mambo ya chuki binafsi kazini?
 
Kumbuka ndani ya siku 100 za kwanza Samia:-
1. Alimfungulia Akaunti zake zote
2. Kesi ya Mdude Chadema ya kubambikizwa ikaisha in favour ya Mdude Mahakama ya Mbeya
3. Kesi ya rufaa ya mauaji ya Akwilina ambayo Mahakama ya Kisutu wali wa convict akina Mbowe ilipinduliwa kwa akina Mbowe kushinda kurudushiwa Hela zao
4. Yule baradhuli wa Hai, Ole Sabaya aliyemsumbua sana Mbowe na wafanya biashara alifunguliwa mashtaka.

Nimekutajia hayo manner tu ili ujiulize kama akili ya Mbowe ilikuwa sawasawa au alivuta BANGI kwa kuanza KUMDHARAU Rais kwenye mitandao, mikutanoni na kwa kupitia Mdude Chadema aliyesema; "na huyo Mama yenu nitamnyoa kwa wembe uleule uliomnyoa mtangulizi wake"

Kaeni kimya tuonyeshane makali
Hapa ndipo tunapotea njia, hivi watu hugombea uongozi ili kupata nafasi ya kuonyeshana makali? Ni lini tutakuwa na ustaarabu wa kukaa pamoja kupanga mipango ya maendeleo kwa Taifa letu?
 
Alivyokua anamnanga jpm kwenye clip alizokua anatayarisha na yule mchaga mwenzake mwenezi wake alishakua na uhakika kama samia na magufuli sio kitu kimoja au la? 🤔 Maana ingekua mimi ndio samia kwa uongo na uzushi ule ningekushughulikia tu. 🙄
Jitahidi kujiweka huru kifikra bila kutaja mtanzania mwenzako kwa kabila lake au dini yake. Utavuna amani itakayo kuepusha na ajali za kifikra ili akili isikwame kwenye hilo tope, weka 4WD kichwani.
 
1. Mh. Mbatia ni mwenyekiti wa chama cha siasa chenye usajili wa kudumu.
2. Mh. Mbatia amewahi kuwa mbunge wa kuchaguliwa kwa haki kabisa jimboni kwake.
3. Mh. Mbatia amewahi kuwa mbunge wa kuteuliwa na rais.
4. Mh. Mbatia ni mtanzania alikuwa swahiba wa mwendazake
5. Mh. Mbatia ana mawazo huru kuhusiana na kesi hii kama waungwana wengine walivyo.
6. Mh. Mbatia ana akili timamu.
7. Mh. Mbatia ni msomi mhitimu wa vyuo vikuu ndani na nje ya nchi.
8. Mh. Mbatia ni mume na baba wa watu.
9. Mh. Mbatia ana kula kwake.
10. Nk, nk.

Heshima gani zaidi wengine mnazo kumzidi Mh. Mbatia?

Mtu anaweza kuwa na vyote hivyo na bado akakosa heshima
👣👣👣👣
 
Ukiliwazia sana hili jambo linalomhusu Freeman Mbowe unashindwa kuona mwanga wa sababu ya yanayoendelea, inakua kama kuna hisia za chuki binafsi. Seems as if there is an old personal issue between Mbowe and the President. Huyu Mama hakuna aliyemtegemea kuwa Raisi, nahisi kuna waliowahi kumkejeli huko nyuma sasa huwezi jua neno lilimfikia likiwa limekorogewa sumu gani. Maana sisi waswahili na sisi, mhh..... Maana najiuliza kwanini watu wengi namna hii na hata dunia nzima inahoji hili jambo lakini haileti badiliko lolote? There is something wrong somewhere!
Huyo mwanamama anatafuta pa kutokea baada ya kulikoroga. Vuta subira kidogo utaona sarakasi zitakazofuata.

Hii haiondoi ukweli kwamba hana siha ya uongozi.
 
Rais wetu kama laiti angekuwa na hekima, japo ndogo sana, asingeruhusu kesi za kutengenezwa kama hizi ziwepo kwenye utawala wake.
Unachosahau ni kwamba hizo kesi anazo matarajio ya kujinufaisha nazo. CHADEMA nitishio sana kwake na chama chake.

Kwa hiyo ikiwezekana kuondoa tishio hilo kupitia hizo kesi ndiyo nafuu kwake.
 
mbatia aache unafiki, Kuna mashekhe wa uamsho wengine mpaka leo bado wapo ndani,mbona hakutoka nje aongelee hili, leo huyu mpuuz mmoja kaswekwa ndani kwa kuleta taharuki ametoa pua yake kwenye media,angekuwa mtetez Basi angebalance hapo tungemuelewa, otherwise ni utopolo tu !!
Mbona alishawatetea sana.. Hukusikia?
 
mbatia aache unafiki, Kuna mashekhe wa uamsho wengine mpaka leo bado wapo ndani,mbona hakutoka nje aongelee hili, leo huyu mpuuz mmoja kaswekwa ndani kwa kuleta taharuki ametoa pua yake kwenye media,angekuwa mtetez Basi angebalance hapo tungemuelewa, otherwise ni utopolo tu !!
Taharuki ipi wewe uliyezaliwa bila uelewa ?! . Kutaka katiba ya wote ni taharuki !!. Nani atashangaa Tz kuwa masikini kama aina yako ndiyo raia waliopo !!
 
Mtu anaweza kuwa na vyote hivyo na bado akakosa heshima
👣👣👣👣

Au tufanye wewe una heshima zaidi kuliko huyu 😁😁.

Hapo tuko vizuri sasa?
 
Au tufanye wewe una heshima zaidi kuliko huyu 😁😁.

Hapo tuko vizuri sasa?

Hayo ni maoni yako

Hujafungwa kufanya au kuwaza chochote unachokipenda lakini hakuna unayewaza kumlazimisha kukubali unachopenda au kuwaza

Kwani ubongo wango si umeubeba mwenyewe kichwani kwako!?
 
Hoja ya Mbatia inawakera sana wapambanaji nuksi.

Au nasema uongo mama D

Akiwa mpambanaji kwako haitoshi!?

Kila mtu ana mtazamo wake kwa vitu kutokana na uelewa wake

Akikupambania wewe inatosha😂😂😂😂
 
Hayo ni maoni yako

Hujafungwa kufanya au kuwaza chochote unachokipenda lakini hakuna unayewaza kumlazimisha kukubali unachopenda au kuwaza

Kwani ubongo wango si umeubeba mwenyewe kichwani kwako!?

Kwa hakika hakuna unapolazimishwa lolote zaidi ya kukuitisha kama vipi:

"Kujikita kwenye hoja za watu badala ya kuanza kutafuta heshima zao kwa tochi."

Hoja ya Mbatia ni kuwa kesi ya Mbowe ni jumba bovu.

Au nasema uongo?
 
Back
Top Bottom