Kesi ya Mirathi ya Dkt. Likwelile: Vicky Kamata ashindwa, mahakama yasema ndoa yao haikuwa halali

Kesi ya Mirathi ya Dkt. Likwelile: Vicky Kamata ashindwa, mahakama yasema ndoa yao haikuwa halali

Mkuu michepuko ni matapeli kwa hivyo ukiamua kua na mchepuko basi uwe na akili zaidi. Mtu wangu wa karibu ana mchepuko sasa mchepuko anaishi kwenye nyumba anajua yake maana kapewa hati fake na alivyomjinga hakuwahi kwenda kulipa kodi ya kiwanja manispaa ili ajue kama hati ni OG. Hati halali inasoma jina la mke halisi. Tuko tumekaa pale kwenye kona tunasubiri siku ya siku.

Nawakumbusha wanaume wenzangu ukiona mwanamke kakubali kua mchepuko na una hela basi huyo kafata hela.
[emoji1][emoji1][emoji38][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji38][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Nimejifunza kitu hapa Tanzania,kua Msajili ndiyo msemaji wa mishwo, yaani Msajili ndiyo kila kitu! Hata huko Mahakamani anatamba Msajili wa Mahakama Kuu!!
... kuna mamlaka za kisheria kwenye sectors mbalimbali kauli zao ndio final! Mkemia Mkuu akisema huu mkojo ulikuwa na traces za madawa ya kulevya hakuna wa kupinga na Mahakama haitakuwa na objection.

Vivyo hivyo NIDA akisema huyu sio raia ndio hivyo! RITA akisema hiki cheti cha ndoa ni feki; that's final! TRA akisema huyu ni mkwepa kodi imekula kwako. TCRA akisema huu mziki haufai kupigwa kwenye media apinge nani? Hospital ikisema huyu kanyongwa ni kazi ya polisi kumtafuta muuaji; etc. etc. etc.

Ndio maana inapingwa sana vyombo hivyo kutumika kisiasa; watawala waovu wanaweza kuvitumia vibaya kuumiza wasiowataka! Vinatakiwa viwe huru kweli kweli mbali kabisa na influences za kisiasa. Hiyo ndio maana yake; ndio maana KATIBA MPYA inatakiwa.
 
... hii sheria ni mbaya iwe kwa mwanamme au mwanamke. Mahusiano ya Vicky na Likwelile hayakuwa siri; yalikuwa open na kila mtu alijua hivyo. Kama mwenye ndoa (huyo mke au hata kama ingekuwa mume) asipojitokeza itajulikana vipi?

Ni wakati sasa wa hii sheria kufanyiwa amendment, kwamba anayehisi kuibiwa mume/mke aandike barua kumtaarifu "mwizi" kwamba anamuibia mkewe/mumewe na (huyo mwizi) akabidhiwe barua chini kiapo cha afisa wa mahakama au kwa utaratibu mwingine wa kisheria utakaowekwa ili kesho na keshokutwa asije kusema sikujua - aambiwe very clearly unaiba mke/mume wa mtu.

Vinginevyo mwenye mke/mume akiamua kukaa kimya ndani ya kipindi ambacho sheria itaweka; "mwizi" asilaumiwe baadaye maana mwenye "mali" haku-declare interest from the beginning kuzuia wizi. Otherwse, hii sheria itasumbua wengi; hawara atakutumia huku akijua ana mke na hataki ujue kwa sababu zake.

Madanga wasichekwe; bali kuwe na taratibu za kijamii za kuwasaidia kwani nao ni watoto wetu na sehemu ya jamii. Cc: Victoire, Mamndenyi, Joanah, Sky Eclat, FaizaFoxy, Zurie, et. al. tieni neno hapa; leo kwa Vicky, kesho kwenu!
Kwahiyo vibaka wa mali za watoto wapate upenyo wa kuchukua mali,majambazi wa mali za watoto wakatafute zao...wanaume tujiongeze sio kuacha watoto wakiporwa jasho letu na hawa majambazi
 
Kosa kubwa la Vicky ni kuwanyanyasa watoto wa marehemu! Angekula nao vizuri wala yasingemkuta haya. Tatizo ni tamaa ya kutaka kumiliki mali peke yake huku watoto wakiteseka. Hakujifunza kwa K-Lyn?
Ndio shida ya wanawake wengi, hawajui kula na vipofu, yaan angejipendekeza kwa watoto yasingetokea haya
 
Lakini si ana mtoto na huyo marehemu? Wakati mwingine tuache vingine vitupite. Kama amezaa nae na ni watoto halali wa huyo mzee wanastahili pia.

Na kama mali imeandikwa jina langu huwezi kuiweka kwenye mali za marehemu. Maana nikisoma vielelezo kuna mali hapo inaonesha imeandikwa kwa jina la Vick. Tusishabikie sana maana hakuna msafi hapa. Basi tu za kwetu hazijulikani.
Aliambiwa athibitishe mali zake kwa kuweka viambatanisho, mtoto wa vicky na likwelile yeye yumo kwenye hesabu ila sio Vicky, aliwanyanyasa sana watoto wa Marehemu
 
Kwahiyo vibaka wa mali za watoto wapate upenyo wa kuchukua mali,majambazi wa mali za watoto wakatafute zao...wanaume tujiongeze sio kuacha watoto wakiporwa jasho letu na hawa majambazi
... marehemu hakuwa muwazi kwa "kibaka"; alitaka amchezee akijua ataacha msala nyuma. Lau kweli ingelijulikana mapema mambo yangelikuwa tofauti.
 
Kosa kubwa la Vicky ni kuwanyanyasa watoto wa marehemu! Angekula nao vizuri wala yasingemkuta haya. Tatizo ni tamaa ya kutaka kumiliki mali peke yake huku watoto wakiteseka. Hakujifunza kwa K-Lyn?
Muache tamaa pesa huwa hazitoshi
 
Lakini si ana mtoto na huyo marehemu? Wakati mwingine tuache vingine vitupite. Kama amezaa nae na ni watoto halali wa huyo mzee wanastahili pia.

Na kama mali imeandikwa jina langu huwezi kuiweka kwenye mali za marehemu. Maana nikisoma vielelezo kuna mali hapo inaonesha imeandikwa kwa jina la Vick. Tusishabikie sana maana hakuna msafi hapa. Basi tu za kwetu hazijulikani.
Yaani ikibainika kuna mali Vicky alipewa kimyakimya na marehemu zitataifishwa sio halali kwake, hata kama amazaa nae huyo ni sawa na mwizi ameiba mali za watu na anastaili hata kufungwa
 
Vinginevyo mwenye mke/mume akiamua kukaa kimya ndani ya kipindi ambacho sheria itaweka; "mwizi" asilaumiwe baadaye maana mwenye "mali" haku-declare interest from the beginning kuzuia wizi. Otherwse, hii sheria itasumbua wengi; hawara atakutumia huku akijua ana mke na hataki ujue kwa sababu zake.
si kweli, umewaza kibinafsi sana, huwezi ukaiingia kichwakichwa kwenye mto ukiwa unavuka na usichukue tahadhari ikiwa kuna mamba au la.

dr. Likwelile hakuwa raia wa kawaida, alikuwa katibu mkuu wizara ya fedha na mhadhiri mwandamizi wa uchumi UDSM. Ukizingatia kuwa hata Vicky kamata ni msomi wa kiwango cha digrii ya uzamili (kama nakumbuka vizuri) alipaswa kujua marital status ya likwelile.

Na katika hali ya kawaida, mwanaume au mwanamke wakikutana kwa mara ya kwanza hicho ndicho huwa kitu cha kwanza kuuliza.
 
Back
Top Bottom