Kwa hiyo Mahakama imeamuru mali ambazo Vicky alikuwa akipinga kuingizwa katika orodha ya mali za marehemu akidai ziliingizwa kimakosa, zijumuishwe katika orodha ya mali za marehemu.
Mali hizo ni nyumba iliyopo kiwanja namba 116 iliyopo Mbweni, Kinondoni jijini Dar es Salaam ambayo alisema walichuma pamoja na nyumba mbili zilizopo huko Mpiji Magoe jijini humo kwenye eneo lenye ukubwa wa hekari 9.5 ambayo alidai ana hisa asilimia 50.
Mbali na hizo, ipo nyumba viwanja namba 387 na 389 iliyopo kitalu D Sinza iliyopo kwa jina lake, nyumba iliyopo Kibamba kwa jina la mtoto wake Gloria Likwelile na viwanja namba 318,319,320 na 321 vilivyopo Mpigi Magoe Ubungo.
Viwanja hivyo vinamilikiwa na kampuni ya Beda Group Limited na Beda Farms Limited ambavyo Vicky alidai kuwa na asilimia 50 ya hisa na pia alipinga gari aina ya Toyota Prado namba T731 CQR na pikipiki Toyota namba MC 588 AHT.