Kesi za mauaji zinavyowasumbua mahabusu na wafungwa wengi

Kesi za mauaji zinavyowasumbua mahabusu na wafungwa wengi

Notorious thug

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2021
Posts
2,817
Reaction score
10,667
Nakumbuka kipindi nilipokuwa mahabusu na hatimaye mfugwa nilikutana na mahabusu wengi waliokuwa wanasubiri hatima ya kesi zao. Wengi wamekuwa kama vichaa au kuchoka kimwili kwa muda mrefu wanaosubiri hukumu yao.

Nilikutana na mzee aliyekaa mahabusu toka 2008 anasubiri hukumu ya kumuua mkewe hakika huyu mzee anasikitisha sana haswa usiku huwa anapiga kelele nyingi kama kuota au hali ya kuweweseka.

Kwa hali ilivyo kesi za mauaji iwe uliua au umesingiziwa kwa uzoefu nilioupata pale wengi wanaoshtakiwa kesi hizi zimekuwa ngumu sana kwao na kuwaathiri kimwili na kisaikolojia. Wengi wamepigwa sana na askari kipindi cha upelelezi miguu kuvunjwa mikono kuvunjwa wengi wanachechemea na majeraha makubwa mwilini na kutengwa na ndugu zao hakika wanakua kwenye kipindi kigumu sana.

Ombi langu kubwa ni kwa askari kukamilisha upelelezi mapema na wapate haki zao mapema, wengi wanafia ndani bila kuhukumiwa

Mahakama ziangalie pale na division ya kuhukumu kesi za mauaji tu zimekuwa nyingi na wengi wanaishia rumande miaka 10-15 bila kupata hukumu.
 
Jaji Mkuu anataarifa hii? Kwamba kesi zinacheleweshwa? Kuna sababu gani ya kumshikilia mtu kwa kesi ya mauaji kwa miaka 15 kama upelelezi umeshindikana bunge litunge sheria ya jaji kuwaachia Mahabusu waliokaa miaka 5 Mahabusu wakisubiri upelelezi ukamilike.
 
Hahaha
Kesi hizi zinachelewa sababu ya kutumia mida mwingi kuendesha kesi za akina Mbowe

Jaji Mkuu anataarifa hii? Kwamba kesi zinacheleweshwa? Kuna sababu gani ya kumshikilia mtu kwa kesi ya mauaji kwa miaka 15 kama upelelezi umeshindikana bunge litunge sheria ya jaji kuwaachia Mahabusu waliokaa miaka 5 Mahabusu wakisubiri upelelezi ukamilike.
Wasaidizi wake wamelala binafsi namshukuru hayati Magufuli alienda butimba kujionea hali na waliosingiziwa walitolewa kwa chifu hangaya sijui kama atakumbuka kwenda gereza lolote
 
Hahaha



Wasaidizi wake wamelala binafsi namshukuru hayati Magufuli alienda butimba kujionea hali na waliosingiziwa walitolewa kwa chifu hangaya sijui kama atakumbuka kwenda gereza lolote
Tatizo hapa ni wasaidizi, inaonekana hawatoshi basi tuwapigie kelele kwamba viatu vyao haviwatoshi
 
Yaani hii nchi shida kweli majitu yamepewa dhamana kazi ni kunenepesha matumbo na kazi yanafanya Kwa speed ya kunyonga,
Hawa viongozi wetu nadhani hawana uchungu na wananchi I wish siku litokee li dictator lipindue serikali na litie Wanaccm wote Kuanzia mwenyekiti wao ndani katika magereza kuzimu ya hapa bongo bila kusomewa mashtaka miaka kama 20 Hivi Ili iwe funzo,
Maana hii nchi ishachakaa tunaiburuza tu hakuna vitu vya maana tunafanya Wala kufanyia kazi haki za msingi za raia wao wakijichotea Kwa urefu wa kamba zao baaasi!
 
Nakumbuka kipindi nilipokuwa mahabusu na hatimaye mfugwa nilikutana na mahabusu wengi waliokuwa wanasubiri hatima ya kesi zao. Wengi wamekuwa kama vichaa au kuchoka kimwili kwa muda mrefu wanaosubiri hukumu yao.

Nilikutana na mzee aliyekaa mahabusu toka 2008 anasubiri hukumu ya kumuua mkewe hakika huyu mzee anasikitisha sana haswa usiku huwa anapiga kelele nyingi kama kuota au hali ya kuweweseka.

Kwa hali ilivyo kesi za mauaji iwe uliua au umesingiziwa kwa uzoefu nilioupata pale wengi wanaoshtakiwa kesi hizi zimekuwa ngumu sana kwao na kuwaathiri kimwili na kisaikolojia. Wengi wamepigwa sana na askari kipindi cha upelelezi miguu kuvunjwa mikono kuvunjwa wengi wanachechemea na majeraha makubwa mwilini na kutengwa na ndugu zao hakika wanakua kwenye kipindi kigumu sana .

Ombi langu kubwa ni kwa askari kukamilisha upelelezi mapema na wapate haki zao mapema, wengi wanafia ndani bila kuhukumiwa

Mahakama ziangalie pale na division ya kuhukumu kesi za mauaji tu zimekuwa nyingi na wengi wanaishia rumande miaka 10-15 bila kupata hukumu.
Kesi za mauaji murder case ni serious sana hata kwenye nchi maskini z nazoendelea zenye weak judiciary system.
 
Hahaha



Wasaidizi wake wamelala binafsi namshukuru hayati Magufuli alienda butimba kujionea hali na waliosingiziwa walitolewa kwa chifu hangaya sijui kama atakumbuka kwenda gereza lolote
Kwa kweli itungwe sheria, mtu kakaa mahabusu miaka mi5 na upelelezi haujakamilika basi jaji apewe nguvu kisheria kumwachilia huru mahabusu
 
Nakumbuka kipindi nilipokuwa mahabusu na hatimaye mfugwa nilikutana na mahabusu wengi waliokuwa wanasubiri hatima ya kesi zao. Wengi wamekuwa kama vichaa au kuchoka kimwili kwa muda mrefu wanaosubiri hukumu yao.

Nilikutana na mzee aliyekaa mahabusu toka 2008 anasubiri hukumu ya kumuua mkewe hakika huyu mzee anasikitisha sana haswa usiku huwa anapiga kelele nyingi kama kuota au hali ya kuweweseka.

Kwa hali ilivyo kesi za mauaji iwe uliua au umesingiziwa kwa uzoefu nilioupata pale wengi wanaoshtakiwa kesi hizi zimekuwa ngumu sana kwao na kuwaathiri kimwili na kisaikolojia. Wengi wamepigwa sana na askari kipindi cha upelelezi miguu kuvunjwa mikono kuvunjwa wengi wanachechemea na majeraha makubwa mwilini na kutengwa na ndugu zao hakika wanakua kwenye kipindi kigumu sana .

Ombi langu kubwa ni kwa askari kukamilisha upelelezi mapema na wapate haki zao mapema, wengi wanafia ndani bila kuhukumiwa

Mahakama ziangalie pale na division ya kuhukumu kesi za mauaji tu zimekuwa nyingi na wengi wanaishia rumande miaka 10-15 bila kupata hukumu.
Damu ya mtu lazima uweweseke tu,pole kamanda kwa kufungwa,ila jina hilo libadilishe mkuu
 
Back
Top Bottom