Kesi za ndoa na talaka 1,358 zafunguliwa ndani ya miezi 8 Dar es Salaam

Kesi za ndoa na talaka 1,358 zafunguliwa ndani ya miezi 8 Dar es Salaam

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Mashauri ya ndoa na talaka 1,358 yamefunguliwa katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke (IJC), Dar es Salaam katika kipindi cha kuanzia Novemba 2021 hadi Julai, 2022.

Idadi hiyo ni sawa na mashauri 220 yanayofunguliwa kila mwezi kituoni hapo, hali inayoonyesha kuyumba kwa taasisi nyeti ya ndoa, hasa mkoani Dar es Salaam.

Mashauri hayo ni miongoni mwa mashauri 4,267 yaliyofunguliwa katika kipindi hicho, kati ya hayo 2,911 yakihusu mirathi.

Hata hivyo, kituo hicho kimefanikiwa kunusuru ndoa 29 kati ya 80, ambazo wanandoa walifikishana hapo kwa ajili ya kuzivunja.

Naibu Msajili wa IJC, Mary Moyo amesema mashauri yanayoongoza kufunguliwa katika kituo hicho ni ya mirathi ambayo ni 2,911, sawa na asilimia 62 ya mashauri yote, ikifuatiwa na mashauri 1,358 ya ndoa na talaka sawa na asilimia 38.

Kwa upande wa mashauri ya ndoa yaliyofunguliwa katika kipindi hicho, Moyo alisema mashauri yanayoongoza ni ya talaka, wanandoa kuomba kutengana, mgawanyo wa mali baada ya ndoa kuvunjika, matunzo ya watoto na sehemu wanakotakiwa kuishi watoto baada ya wazazi wao kutengana.

Alisema kati ya mashauri 1,358 ya ndoa, mashauri 1,127 ndiyo yaliyosikilizwa na kutolewa maamuzi, huku mashauri 231 yakiwa bado hayajatolewa uamuzi.

“Takwimu hizi ni tangu kituo hiki kilipoanza kutoa huduma Novemba, 2021 hadi Julai 19, 2022 na wanaokuja kupata huduma katika kituo hiki wengi ni wanawake ambao wamekuwa wakifungua kesi za ndoa, talaka, malezi ya watoto na upande wa wajane wamekuwa wakifungua kesi za mirathi,” alisema Moyo.

Kuhusu mirathi, Moyo alisema tayari wasimamizi wa mirathi 2,376, sawa na asilimia 82 wameshateuliwa na mahakama hiyo kukusanya mali na madeni katika kipindi hicho.

Alieleza sababu kubwa ya kituo hicho kupokea kesi nyingi kwa kipindi kifupi ni kutokana na kituo hicho kuhudumia mkoa mzima wa Dar es Salaam.

Tofauti na mahakama nyingine, kituo hicho kina ngazi tano za mahakama kwa pamoja, yaani Mahakama ya Mwanzo, Mahakama ya Wilaya, Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani, jambo ambalo limerahisisha watu kupata huduma kwa urahisi.


Chanzo: Mwananchi
 

Narudi Jasmoni Tegga ☺☺


Hatari sana BigTall


Taasisi ya ndoa Kati ya taasisi nyeti alizoanzisha mwenyezi Mungu mwenyewe imekumbwa na dhoruba kubwa sana.
Tukumbuke katika kila tendo linalotokea liwe baya au zuri ipo roho yenye either nguvu ya ubaya au nguvu ya wema nyuma yake. Ila sasa ni wazi roho ya ubaya imetawala ulimwengu.

Kwa asilimia kubwa sana wazazi wengi tumekua chanzo cha hizi talaka. Nasema hivyo sababu hatulei watoto kwa kuwaandaa kuwa wawakilishi wetu bora na wazazi bora baadae.
Hili linaweza kuwa hatulifanyi kwa kupenda au kwa kujua ila tunalifanya kwa sababu na sisi tulitulipoingia kwenye hii taasisi hatukuwa tumemjua na kumshika Mungu, hatukujua vile tunatakiwa kuishi ili kuwa na uzao wenye baraka baada yetu.

Badala yake tumebaki tunakomaa kusomesha watoto kwa kwa elimu ya kupata vyeti kwa gharama kubwa na baadae kuja kuwapoteza kwa maumivu makubwa kiasi cha hata kutishia kuondoa uhai wetu wenyewe.

Sababu mila na desturi zetu wengi wetu tumeziacha au hata hatuzijui basi tupambane kushikilia imani zetu, tuhakikishe sisi na watoto wetu tunatembea kwenye misingi ya imani zetu.

Tukumbuke sisi wanadamu wote ni mitume wa Mungu na tumetumwa kuja kufanya makusudi ya Mungu kwenye hii dunia. Na kama tumeamua kuwa wazazi ili tuzae watoto basi tusijitoe ufahamu na kujikuta wa kisasa zaidi ya aliyetupa uhai na uzao.

Hukuna aliye fundi wa kulea ila tukishikana na viongozi wetu wa imani, tukaishi kama yanavyotuelekeza maandiko na kuhakikisha watoto wetu tunaambatana nao tunaweza kupunguza haya majanga maana tutaishi kwa taratibu za Mungu kupitia imani zetu, tutachumbia na kuchumbiwa kwa taratibu za Mungu, tutaishi kwa wenza wetu kwa taratibu za imani zetu.

Na ni heri kubwa sana kwamba sheria za nchi zinasaidia kuulinda uhai wetu kwa kuwezesha hili zoezi kuliko kushuhudia vifo kwa sababu watu wamegeukana maadui na wakashindwa kuachana

Cc Maghayo Jasmoni Tegga vita ya ndoa kwa kizazi hiki inaambatana na maadui ambao ni wanandoa wenyewe kwa kupenda Mali kuliko wenza wao, kupenda zinaa, kujihusisha na ushoga na usagaji.

ZABURI 11:3​

"Kama misingi ikiharibika, Mwenye haki atafanya nini?"​

 
Mashauri ya ndoa na talaka 1,358 yamefunguliwa katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke (IJC), Dar es Salaam katika kipindi cha kuanzia Novemba 2021 hadi Julai, 2022.
Kilichobaki ni watu kupelekeana moto tuu. haya mambo ya ndoa tuyaache wajameni.
wanawake hawataki kuolewa basi tuu jamii inataka kulazimisha mambo. wao wanataka hela za wanaume tuu.
 
Mashauri ya ndoa na talaka 1,358 yamefunguliwa katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Temeke (IJC), Dar es Salaam katika kipindi cha kuanzia Novemba 2021 hadi Julai, 2022.

Idadi hiyo ni sawa na mashauri 220 yanayofunguliwa kila mwezi kituoni hapo, hali inayoonyesha kuyumba kwa taasisi nyeti ya ndoa, hasa mkoani Dar es Salaam.

Mashauri hayo ni miongoni mwa mashauri 4,267 yaliyofunguliwa katika kipindi hicho, kati ya hayo 2,911 yakihusu mirathi.

Hata hivyo, kituo hicho kimefanikiwa kunusuru ndoa 29 kati ya 80, ambazo wanandoa walifikishana hapo kwa ajili ya kuzivunja.
Ukifuatilia kwa makini utagundua kuna mkono wa facebook na mitandao mingine ya kijamii kwenye hizi sakata za ndoa

1659346083591.png
 
Back
Top Bottom