TANZIA Kibaha Vijijini: Diwani Mteule wa CCM Kata ya Kikongo afariki pamoja na wajukuu zake wawili baada ya nyumba yao kuchomwa moto

TANZIA Kibaha Vijijini: Diwani Mteule wa CCM Kata ya Kikongo afariki pamoja na wajukuu zake wawili baada ya nyumba yao kuchomwa moto

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Kibaha. Diwani mteule wa CCM kata ya Kikongo Kibaha vijijini Fatuma Ngozi pamoja na wajukuu zake wawili wamefariki baada ya kuungua kwa moto wakiwa ndani ya nyumba.

Nyumba ya diwani huyo imeungua moto usiku wa kuamkia leo Novemba 9, 2020.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Wankyo Nyigesa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

"Nipo kwenye kikao, najua unaulizia tukio la moto huko Kikongo ni kweli na watu wangu wapo eneo la tukio toka alfajiri wakifatilia chanzo, nitazungumza baadaye mchana kikao kitakuwa kimeisha," amesema.

Chanzo:
Mwananchi

mo.jpg
 
Diwani mteule Kata ya Kikongo Kibaha Vijijini (CCM), Fatuma Ngozi na wajukuu zake wawili wamekufa baada ya nyumba yake kuchomwa moto usiku wa kuamkia leo, Kamanda wa Polisi Pwani, Wankyo Nyigesa amethibitisha. #MwananchiUpdates

Tanzania tunakoelekea ni giza nene.
 
Tunapoenda wenye akili walishaona, haya ni matokeo tu

or else itakuwa michezo yao michafu wenye nchi hii sio Wananchi

R. I. P
 
Back
Top Bottom