Kibaha: Watu wawili waliotoka jela kwa msamaha wauawa

Kibaha: Watu wawili waliotoka jela kwa msamaha wauawa

Watu wawili waliotoka gerezani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais wameuawa baada ya kukamatwa wakidaiwa kuiba vitu mbalimbali huko kwa Mathiasi mjini, Kibaha mkoani Pwani.

Watu hao walifungwa kwa makosa ya wizi katika kesi ya jinai namba 273/2020 na 260/2020 na walipata msamaha wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 12 mwaka huu kutoka katika gereza la Mkuza mjini Kibaha.

Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Wankyo Nyigesa amesema leo Mei 10, 2021 kuwa watu hao wameuawa Mei 8 alfajiri kwa kupigwa na mawe, mapanga na fimbo na wananchi wenye hasira waliowatuhumu kuhusika kwenye tukio la wizi.

"Hawa watu wametambuliwa ni Ramadhani Mohamed maarufu kwa jina la Seven au Ali (28) mkazi wa kwa Mathiasi na Idd Hamisi maarufu Chuga (30) mkazi wa mtaa Jamaika, wote walikuwa wamerudi uraiani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais," amesema Nyigesa.

Hata hivyo, Kamanda Nyigesa ameshauri wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwa kisingizio cha hasira na badala yake watoe taarifa polisi inapotokea tukio la wizi kwenye maeneo yao, ili watuhumiwa wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Chanzo: Mwananchi
Mkuu Mshana Jr naona Kibaha hawacheki na kima
 
Watu wawili waliotoka gerezani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais wameuawa baada ya kukamatwa wakidaiwa kuiba vitu mbalimbali huko kwa Mathiasi mjini, Kibaha mkoani Pwani.

Watu hao walifungwa kwa makosa ya wizi katika kesi ya jinai namba 273/2020 na 260/2020 na walipata msamaha wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 12 mwaka huu kutoka katika gereza la Mkuza mjini Kibaha.

Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Wankyo Nyigesa amesema leo Mei 10, 2021 kuwa watu hao wameuawa Mei 8 alfajiri kwa kupigwa na mawe, mapanga na fimbo na wananchi wenye hasira waliowatuhumu kuhusika kwenye tukio la wizi.

"Hawa watu wametambuliwa ni Ramadhani Mohamed maarufu kwa jina la Seven au Ali (28) mkazi wa kwa Mathiasi na Idd Hamisi maarufu Chuga (30) mkazi wa mtaa Jamaika, wote walikuwa wamerudi uraiani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais," amesema Nyigesa.

Hata hivyo, Kamanda Nyigesa ameshauri wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwa kisingizio cha hasira na badala yake watoe taarifa polisi inapotokea tukio la wizi kwenye maeneo yao, ili watuhumiwa wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Chanzo: Mwananchi
"A witch will always be a witch" hawajui namna nyingine ya kujipatia riziki mbali na uhalifu. Nadhani jela ndio mahali salama zaidi kwao
 
Kuna jamaa alikaa jela miaka mitano kwa kesi ya wizi wa kutumia bunduki. Baada ya hio miaka alitoka lakini kesi ikawa haijaisha, ikabaki ile ya bunduki.

Basi jamaa akawa anaenda kusikiliza kesi yake kule mahakama ya mwanzo Ilemela na mimi nikawa namuona pale (nilikuwa sitaki hata mazoea nae).

Jamaa msala wa kwanza ulikuwa umeisha kiaina maana hakuna aliekuwa anafuatilia, msala wa pili ikawa bunduki, nao ulikuwa unaelekea kuisha.

Cha ajabu huyu mwamba alirudi tena mzigoni, akaanza tena kuiba!

Wana nzengo walimkamata mchana kweupe wakapiga sana, alipoulizwa ni wa wapi akasema Igoma (alikamatiwa kisesa), hapo wakaona wampe nafasi awajulishe nduguze kwamba anakufa!

Na ikawa hivyo walimuua mchana kweupe.

Nadhan hawa vijana wanaotoka jela wanapaswa kuwekwa special quarantine kwa ajili ya life skills mpya na kuwekwa sawa kisaikolojia.

Matukio ya kutoka jela na kuuwawa yamekuwa mengi mno.
Huko jela wanatakiwa watoke na life skills za kuja ku survive mtaani! Ndio maana wanafunzw kufanya productive activities
 
Mwanangu sudi tulikuwa nae Manzese enzi hizo aliiba akapata msamaha hivyo hivyo

Ila pamoja na msamaha alikuwa akiiba nduguze wanamtoa maana hela na connection walikuwa nazo sema toto lilikuwa jinga

Ila akarudia tena ila safari hii walivyomshika walimpiga ,walimbonda mpka mapumbu walimtoboa mpka na spoku za moto
 
Eeh wazee wa liwezekanalo sasa...lisingoje baadae! Watu wamechafukwa nafsi na haya maisha!
Kuna mitaa flani hapo kwa mathias wengi waliojenga ni wanajeshi,wazee wa suti nyeusi aisee pale hua hawacheleweshi.

Mwizi akijichanganya ni imeisha hioooo.
 
Wanafiki, wakiwa kwenye media wanasema hivyo lakini wakifika kwenye matukio wakaona wezi wanapumua wanaelekeza lawama kwa wananchi kwanini wanafanya kazi nusunusu

[emoji23][emoji23][emoji23] sa ulitaka wawasaidie wezi? Ukiona hivyo ujue nao wamewachoka. Mtu anaiba, anafungwa, anapewa msamaha wa rais, anatoka kifungoni kurudi uraiani, anaiba tena [emoji848][emoji848]. Hapo lazima raia walaumiwe kwa kufanya kazi nusu nusu [emoji23]
 
Kuna mitaa flani hapo kwa mathias wengi waliojenga ni wanajeshi,wazee wa suti nyeusi aisee pale hua hawacheleweshi.

Mwizi akijichanganya ni imeisha hioooo.
Mkuu Shukrani za dhati kwa hili dokezo 'hint'. Sasa nitaenda maeneo hayo kuiba maksudi tu hili nichangamshe na kupasha martial art skills zangu ambazo kwa muda sasa zimepoa.
 
"A witch will always be a witch" hawajui namna nyingine ya kujipatia riziki mbali na uhalifu. Nadhani jela ndio mahali salama zaidi kwao
Wanauwezo mkubwa kukwepa makosa yao mbele yamahakama nandomana hukmbana na adhabu ndogo ,pia askari mchukua maelezo nae hua anaweza pigwa chenga yamwili kwenye maelezo....

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu Shukrani za dhati kwa hili dokezo 'hint'. Sasa nitaenda maeneo hayo kuiba maksudi tu hili nichangamshe na kupasha martial art skills zangu ambazo kwa muda sasa zimepoa.
Hahah karibu mkuu,pale watu wanamiliki vyuma vya moto viwili viwili per house.

Ile unafanya tu Mae Geri,Choku Zuki,Mawashi Geri utakutana risasi ya kichwa ubongo wote chini.
 
Mmojawapo wa waliouliwa
IMG-20210510-WA0015.jpg
 
Jeshi letu la Polisi linapaswa kuteketeza Vijiwe vyote vya Uvutaji na uuzaji wa Bangi ambavyo kimsingi mdio mazalia ya uhalifu wa kila aina.

kufanyike msako maalum seriously tutateketeza kabisa uhalifu mitaani.

Mamlaka zinazo toa mapendekezo ya Misamaha kwa wafungwa iwe makini sana ktk kupendekeza majina ya wanao paswa kupewa msamaha wa Rais. uadilifu na umakini ni muhimu sana wakati wa zoezi.
 
Watu wawili waliotoka gerezani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais wameuawa baada ya kukamatwa wakidaiwa kuiba vitu mbalimbali huko kwa Mathiasi mjini, Kibaha mkoani Pwani.

Watu hao walifungwa kwa makosa ya wizi katika kesi ya jinai namba 273/2020 na 260/2020 na walipata msamaha wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Aprili 12 mwaka huu kutoka katika gereza la Mkuza mjini Kibaha.

Kamanda wa Polisi Mkoani Pwani Wankyo Nyigesa amesema leo Mei 10, 2021 kuwa watu hao wameuawa Mei 8 alfajiri kwa kupigwa na mawe, mapanga na fimbo na wananchi wenye hasira waliowatuhumu kuhusika kwenye tukio la wizi.

"Hawa watu wametambuliwa ni Ramadhani Mohamed maarufu kwa jina la Seven au Ali (28) mkazi wa kwa Mathiasi na Idd Hamisi maarufu Chuga (30) mkazi wa mtaa Jamaika, wote walikuwa wamerudi uraiani hivi karibuni kwa msamaha wa Rais," amesema Nyigesa.

Hata hivyo, Kamanda Nyigesa ameshauri wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi kwa kisingizio cha hasira na badala yake watoe taarifa polisi inapotokea tukio la wizi kwenye maeneo yao, ili watuhumiwa wakamatwe na kufikishwa katika vyombo vya sheria.

Chanzo: Mwananchi
Sio mbaya huo ndio msamaha wa wananchi
 
Back
Top Bottom