Kibatala awataka Ndugai na Mahera mahakamani

Kibatala awataka Ndugai na Mahera mahakamani

Huna akili kwani Ndugai aliwapitisha kama watoto wake au kama Spika??

Kwani kahama na ofisi yake??

Si kuna spika mwingine??

Wakati mwingine utumie ubongo badala ya miguu kufikiri.
Spika anaweza kufanya maamuzi ya kukiuka Katiba. Je, naibu spika anaweza kumzuia!? Kwenye kesi ya yule Professor aliyekuwa balozi nchini Italia, mbona Marehemu Mkapa alipanda kizimbani makamani? Kwani Rais Kikwete hakuwepo au Marehemu Mkapa alihama na ofisi!?
 
Spika anaweza kufanya maamuzi ya kukiuka Katiba. Je, naibu spika anaweza kumzuia!? Kwenye kesi ya yule Professor aliyekuwa balozi nchini Italia, mbona Marehemu Mkapa alipanda kizimbani makamani? Kwani Rais Kikwete hakuwepo au Marehemu Mkapa alihama na ofisi!?
Hizi ni kesi tofauti.

Jaribu kwanza kuzifahamu ndio uzilinganishe.
 
Spika wa sasa ndio aliwaapisha? Ndugai na kiherehere chake ili kumfurahisha yule shujaa wenu uchwara ndio anatakiwa akajibu maswali mahakamani.
Aliwaapisha kama Ndugai au kama Spika??
 
Spika anaweza kufanya maamuzi ya kukiuka Katiba. Je, naibu spika anaweza kumzuia!? Kwenye kesi ya yule Professor aliyekuwa balozi nchini Italia, mbona Marehemu Mkapa alipanda kizimbani makamani? Kwani Rais Kikwete hakuwepo au Marehemu Mkapa alihama na ofisi!?
Hayo Majinga ya uvccm hayajitambui hata uyafundishe vipi mkuu. Ndio maana Magu aliyapiga 20000/ kwa kuwapa vitambulisho feki vya machinga na bado alipo kufa wakamwita shujaa. Unaweza kuona tuna wajinga kiasi gani lakini pia Mkaguzi mkuu wa mahesabu alithitisha 1.5 tirioni zimepotelea Ofisini kwa Magu pia.
 
..msishangilie kabla ya wakati

..huwezi kujua maamuzi ya Jaji yatakuwa nini?

..upo uwezekano wa Jaji kukataa kuwaita Ndugai na Mahera kama mashahidi ktk kesi.

..kama mtakumbuka ktk kesi ya Mh.Mbowe Jaji alikataza jina la Mh.Hussein Mwinyi kutajwa mahakamani, au kumuita kama shahidi wa upande wa washtakiwa.

Cc The Palm Beach. Erythrocyte

Kabisa ulichosema. Kwenye ile kesi ya Mbowe ndio niliidharau mahakama jumla. Ushahidi uliokuwa unatolewa na upande wa serikali ilikuwa una udhaifu wa wazi, cha ajabu mahakama ilikuwa inatoa maamuzi kinyume kabisa na ushahidi. Sitegemei lolote la maana kwenye hizo mahakama zilizopoteza uadilifu wake.
 
Wakili Peter Kibatala amesema atawahitaji aliyekuwa spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai na aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Dkt. Charles Mahera ili wahojiwe kuhusu wabunge 19 walioapishwa kwa tiketi ya CHADEMA.

Kibatala amesema ni lazima viongozi hao wahojiwe kwa kuwa ndio waliowapitisha na kutoa kaulinza kuwalinda kwa hali youote ili wabaki bungeni.

Kati ya maswali ambayo Kibatala atapenda kuuliza ni pamoja na mbunge mmoja kuapishwa japo hakupitia mchakato wa uchaguzi.

Dkt. Mahera atatakiwa kueleza alipoipata barua ya majina wakati katibu wa chadema aliikana barua hiyo.

Pia majina ya wabunge hayakutangazwa kama utaratibu unavyohitaji.

Wabunge 19 wamefungua mashtaka ya kufukuzwa uanachama bila kufuata itaratibu
Hii kesi inaenda kumuumbua mnyika na mbowe hivi unafikiri hao kina dada ni wajinga mpaka walazimieshe kesi? Mnyika ndiyo alipeleka majina angekuwa hajapeleka angeshaga fungua kesi muda mrefu ya kufojiwa kwa sahihi yake kwanini Yuko kimya? Kibatala kafichwa hajui anakuja kuropoka tu hapa eti anamtaka ndugai nawaambiaga kibatala siyo mwema kwa chadema hata Sheria hazijui anatumia umaarufu tu ndiyo maana hata kesi ya mbowe ilimshinda ashukuru viongozi wa dini waliomuombea kwa mama akaachiwa angepata aibu ya mwaka na uwakili angeacha
 
Watoe majina kwenda kwenye bunge la majizi ya kura? Hiyo 2020 hakukuwa na uchaguzi, bali maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura.
Kama mbowe munaemuona kama Mungu wenu kakubali uchaguzi kuwa Halali wewe ni nani mpaka ubishe?
 
Kama mbowe munaemuona kama Mungu wenu kakubali uchaguzi kuwa Halali wewe ni nani mpaka ubishe?

Kwakuwa we ulikuwa unamuona dhalimu ni mungu, basi unadhani na kila mtu anamuona Mbowe ni mungu pia. Ule ukhanithi wa 2020 acha kama Mbowe angesema ulikuwa sahihi, hata mama yake Mbowe angesema ulikuwa huru tungemuona mzandiki tu. Ule uhayawani ulikuwa wazi peupe. Huhitaji kuaminishwa na yoyote kwa jambo lililokuwa wazi vile.
 
Wakili Peter Kibatala amesema atawahitaji aliyekuwa spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai na aliyekuwa Mkurugenzi wa Uchaguzi Dkt. Charles Mahera ili wahojiwe kuhusu wabunge 19 walioapishwa kwa tiketi ya CHADEMA.

Kibatala amesema ni lazima viongozi hao wahojiwe kwa kuwa ndio waliowapitisha na kutoa kaulinza kuwalinda kwa hali youote ili wabaki bungeni.

Kati ya maswali ambayo Kibatala atapenda kuuliza ni pamoja na mbunge mmoja kuapishwa japo hakupitia mchakato wa uchaguzi.

Dkt. Mahera atatakiwa kueleza alipoipata barua ya majina wakati katibu wa chadema aliikana barua hiyo.

Pia majina ya wabunge hayakutangazwa kama utaratibu unavyohitaji.

Wabunge 19 wamefungua mashtaka ya kufukuzwa uanachama bila kufuata itaratibu

Kitendo Cha kugombea majimboni Halafu unarudi Tena kutaka viti maalum kutawaondoa haraka kwenye kesi.
 
Naomba niulize swali kwa manguli wa sheria hapa jukwaani......

Nadhani kesi ya msingi ni wakina Halima Mdee dhidi ya CHADEMA wakipinga kuvuliwa uanachama wao bila kufuata utaratibu wa chama.......madai ya Kibatala kwa Ndugai ni kwanini aliwaapisha kina Halima UBUNGE Hali ya kuwa hawakuwa halali.....na kuhusu mwenyekiti wa time ya uchaguzi ya kupokea barua ya majina ya akina Halima hali ya kuwa hayakuwa na baraka za chama...... nadhani hizi ni hoja mbili tofauti na hazihusiani na kesi ya msingi iliyopo mahakamani kwa sasa....Mimi si mjuzi wa masuala ya sheria bali ni mtazamo wangu.....ningependa manguli wa sheria hapa jukwaani wanifafanulie kwa faida ya wengi.....natanguliza shukrani zangu za dhati......
 
..msishangilie kabla ya wakati

..huwezi kujua maamuzi ya Jaji yatakuwa nini?

..upo uwezekano wa Jaji kukataa kuwaita Ndugai na Mahera kama mashahidi ktk kesi.

..kama mtakumbuka ktk kesi ya Mh.Mbowe Jaji alikataza jina la Mh.Hussein Mwinyi kutajwa mahakamani, au kumuita kama shahidi wa upande wa washtakiwa.

Cc The Palm Beach. Erythrocyte

Lazima waitwe Kama mashahidi. Maana hawana vyeo kwa sasa
 
Back
Top Bottom