Kibiti mpaka laana ya Cabo Delgado: Part II

Kibiti mpaka laana ya Cabo Delgado: Part II

Abu Dardai Jongo yeye alikuwa na pikipiki. Alikuwa anfanya kazi ya kusafirisha watu toka mto Ruvuma mpaka Montepuez. Kitambo fulani, akaenda Macomia. Aliporejea, wenzake wanasema hakuwa tena yule Abu walokuwa wanamfahamu.
Hii inanikumbusha kituko cha Juzi juzi wakati Mwenezi Paul Makonda anafanya ziara Mkoa wa Rukwa Nkasi kuna afisa mmoja alituhumiwa Kufafirisha Wahamiaji haramu.
Tuhuma zile za yule mzee ambaye alidai ana ushahidi alihusisha maafisa wa polisi na Uhamiaji.

Je huenda hizi ndio mbinu watu hao wanavushwa?

Tuwe makini sana
 
MKIRU sasa hivi ni tulivu, kenge hao wakijitokeza tena huko mama awapeleke kuzimu wakatulie huko. Ni washenzi sana
 
Uko ndio tunapoelekea unafikiri vijana wanapenda kukalishwa bila ajira zozote za kueleweka.

Vijana wa JKT wanarudishwa majumbani wale wasio na watu wa kuwashika mkono lakini watoto wa wakubwa ni mwendo wa kupigiwa simu tu za maelekezo na kuitwa.

Maafande wanajibu shit kuwa jeshi halitoi ajira etii muwe wazalendo hakuna uzalendo kwenye njaa.

Watoto wao wanawaweka kwenye system chap madogo wengine wanarudishwa kwao, madogo wengine wenye mioyo mepesi huishia kujinyonga.

Ubaya JKT wanaorudishwa kitaa wanazidi kuwa wengi na kitaa pakavu balaa life lime tight.

Hawa watu wanahitaji tu supplier wa silaha kuanzisha vikundi vya kiasi na ubaya nchi yetu rasilimali inazo tena za kutosha za kupigania.

Huwezi wapa vijana mafunzo utegemee watakuwa humble maisha yao yote huku wakiona viongozi wa chama na serikali na maafande wao pekee wakila mema ya nchi na kulindana.

JKT wanatengeneza bomu la vikundi vya kiasi sio vya kigaidi ni suala la muda serikali ijitafakari sana namna wanavyo iongoza hii Tanzania.

Watu wanaumia ndani kwa ndani tena hasa vijana kitu ambacho ni kibaya sana.

Hawa watu wanahitaji supplier tu wa silaha maana kama chuki dhidi ya serikali wanazo hawaitaji wa kuwaambia hiki na hiki kibaya serikali imefanya na inafanya.
Wishful thinking.

Ni miaka mingapi tangu mafunzo ya JKT kwa vijana yaanze? Ni wangapi waliopitia hayo mafunzo walipata ajira? Wangapi hawakupata?

Ukiijua JKT (JWTZ) vizuri, utaacha hizi ndoto za mchana.
 
Kabla ya kuendelea, turejelee kauli aliyoitoa Colonel Lionel Dyck, mkurugenzi wa jeshi binafsi la DAG ambaye mkataba wake wa kutoa msaada wa anga pale Msumbiji ulitamatika tarehe 6, April 2021.

View attachment 3004739

Alipohojiwa, alisema kauli hii; "Mungu, wasaidie watu wale."

Akimaanisha watu wa Msumbiji aliowaacha katika tabu. Tabu ambazo hakusimuliwa na mtu bali alizishuhudia yeye mwenyewe katika oparesheni yake nchini humo.

Na sisi pia tunaishi hapa. Eeh Mungu wasaidie watu wale (wa Msumbiji). Lakini pia tunaongezea, atusaidie na sisi ambao tumepakana nao.

Bwana huyu, Lionel Dyck, yeye amekwishaaga nchi hii ya Msumbiji lakini kwenye mioyo ya wananchi mia mbili na ishirini na nane katika mji huu wa Palma, atabaki kuishi milele.

View attachment 3004740

Hawatamsahau namna alivyotumia helikopta zake kuwanusuru na midomo ya bunduki za magaidi ambao walitumwa roho za watu siku hiyo.

Siku ya maafa.

Kwao wanamwona Lionel Dyck na jeshi lake kama malaika.

Helikopta yake iliwabeba, kidogo kidogo, zamu kwa zamu, na kila mara ilipoondoka wakadhani haitokaa ikarudi tena, lakini bado ikarejea na kuwakomba watu kwenda eneo salama huko peninsula ya Afungi.

Pichani ni watalii ambao walikwama kwenye hoteli wakati wa mashambulizi ya Palma yanarindima huko nje.

View attachment 3004741

Kwa kutumia mashuka meupe wakaandika ujumbe 'HELP', na bahati wakaonekana na kuokolewa na helikopta ya DAG.

Hivyo watu hawa, ukiwajumuisha na wale wananchi wa Msumbiji 228, wanakamilisha jumla ya watu 240 waliofanikiwa kuokolewa na oparesheni ya DAG.

Sasa tukiacha kuhangaika na haya matawi ili turudi kwenye mzizi wenyewe, basi hatuna budi kuurejea ule mwaka 2012 kule Mombasa, nchini Kenya.

View attachment 3004743

Katika mwaka huo, August ya tarehe 27, siku ya Jumatatu majira ya asubuhi, sauti ya bunduki inarindima ndani ya jiji la Mombasa na kusababisha taharuki kubwa.

Kwenye zoezi hilo, zilitumwa risasi kumi na nane kwenda ubavu wa kulia (upande wa dereva) wa gari aina ya toyota hiace nyeupe iliyobeba familia nzima ndani yake.

View attachment 3004744
Risasi hizo zilikuwa zimeagizwa kitu kimoja tu, kuja na roho ya bwana Aboud Rogo aliyekuwa ameketi katika usukani. Na kweli risasi zikafanikiwa.

Aboud Rogo anafariki papo hapo, wengine wote wakibakia salama salmin mbali na mkewe, bi. Haniya, aliyeishia kupata jeraha la risasi mguuni.

View attachment 3004745

Cha kushangaza siku hiyo, bwana Rogo alikuwa yu njiani akimpeleka mkewe hospitali kwani alikuwa na maradhi, ila ajabu akaishia kupelekwa yeye hospitali akiwa marehemu.

Kifo hiki cha Rogo kinakuja muda si mrefu, takribani wiki mbili zilizopita, baada ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa Mataifa (UN) na nchi ya Marekani kwa kutuhumiwa kuwa na mahusiano na Al-shabab ya huko Somalia.

View attachment 3004746

Bwana Rogo ambaye alikuwa muumin wa itikadi kali na mmoja wa viongozi wa kikundi cha Al-hijra kinachoaminika kuwa 'wing' ya Al-shabab nchini Kenya, alinyooshewa vidole na UN kwa kusaidia Al-shabab kwenye mambo matatu:

'Funding, recruiting and logistics'.

Kwa mujibu wa UN, bwana Rogo alikuwa akiifadhili kundi hilo la kigaidi kwa michango mbalimbali ya watu, alikuwa akisaidia kutafuta vijana wa kujiunga nalo na pia alikuwa anasaidia kuwasafirisha vijana hao kufika Somalia.
View attachment 3004747

Na kifo hiki cha Rogo hakikuwa cha kwanza wala cha mwisho kwa watu waliokuwa wanafanana naye kaliba. Wote waliuawa kwa mtindo huu huu. Wanapigwa risasi na watu wasiojulikana na 'wasiokamatikana'.

View attachment 3004748

Sasa wafuasi hawa wa Rogo, kwa mujibu wa ripoti ya Nation Africa ya Kenya, ndio mabwana wanaoleta matata kule Msumbiji. Wafuasi hao walitawanyika na kusambaa maeneo mbalimbali baada ya vifo vya wakubwa wao waliowashika mkono.

Hivyo kwa maelezo haya, na yale ya kamanda Sirro kusema magaidi wale waliovuka mpaka kutoka Msumbiji na kuvamia Mtwara ni mtandao ulioanzia MKIRU (Mkuranga, Kibiti na Rufiji), yanatosha kutueleza mtandao huo haukuanzia hapa nchini.

Ulianzia huko Kenya, ukaja kwetu kisha ukaelekea Msumbiji. Kote huko unapopita, unapokelewa na wakazi ambao wengine kwa hali zao, wanashawishika kujiunga nao wakiamini ni njia ya kupambana na madhila yanayowasibu.

Watu hawa waliobeba chuki, ni rahisi kufanyiwa 'brainwashing' kwa kutumia mwamvuli wa imani. Baada ya hapo wanageuka kuwa watu wapya kabisa usiowajua.

View attachment 3004750
Wanabeba silaha kuingia ulingoni na ukikutana nao , my friend, usitegemee watakukumbuka ati wewe ulikuwa jirani yake, ulicheza naye mdako utotoni, ulikimbizana naye kwenye kombolela na kushikana kidali.

Kama bado unautaka ugali, basi tupa hiyo miguu kadiri uwezavyo, hata ukiweza kupaa angani basi wewe paa, utaenda kujiuliza uliwezaje ukiwa upo chini ya kitanda.

Mfano mzuri wa hii kesi ni vijana wawili; Nuro na Abu Dardai Jongo kule nchini Msumbiji ambao leo hii ni vinara wa mauaji katika kikundi hiki cha Ansar al-sunna.

View attachment 3004752
(Nuro Pichani)

Nuro alikuwa mfanyabiashara wa samaki hapo Cabo Delgado. Mtu poa na mcheshi. Akaja akapotea isijulikane kaenda wapi. Kuja kuonekana tena, si yule wa zamani. Anachinja watu kama utani.

View attachment 3004757

Abu Dardai Jongo yeye alikuwa na pikipiki. Alikuwa anfanya kazi ya kusafirisha watu toka mto Ruvuma mpaka Montepuez. Kitambo fulani, akaenda Macomia. Aliporejea, wenzake wanasema hakuwa tena yule Abu walokuwa wanamfahamu.

View attachment 3004759
(Abu Jongo pichani)

Haikupita muda akapotea moja kwa moja.

Tukirudi kwa jamii ya watu wanaoishi mkoa wa Pwani, mathalani Kibiti, Mkuranga na Rufiji, hamna asiyejua wengi wao hali ni dhalili. Pangu pakavu tia mchuzi.

Shughuli wanazotegemea ni kuchuma rasilimali zinazowazunguka kwa kutengeneza na kuuza mkaa, kukata na kuuza kuni na magogo ya mbao pasipo kusahau kilimo.

Hivyo watu hawa wanapokumbana na kodi kandamizi, ushuru mlima na tozo rundo kuanzia kwa maafisa wa serikali za mtaa, maafisa misitu na rasilimali mpaka polisi, huzaa chuki.

Chuki ambayo huja kuwa mtaji kwa wadhalimu.

Tunakumbuka mwaka 2013 namna gani watu wa Kibiti walifanya vurugu kubwa mpaka kufunga barabara, ikabidi IGP atoe kauli.

View attachment 3004760

Na pia tunakumbuka namna gani tulianza kuokota miili ya watu, wakilengwa haswa wafanyakazi wa serikali mathalani watu wa serikali za mitaa na polisi.

Ilitumika nguvu kubwa kuwazima mabwana hawa. Ilibidi watu wafe, hata wale ambao ni ndugu zetu, ili wengi wetu tubaki salama.

View attachment 3004761

Lakini ni dhahiri oparesheni hii (MKIRU) haikumaliza hawa 'mabwana' wote , ndo' wengine wanakimbilia Msumbiji wanapoenda kukutana na 'locals' ambao wanaungana nao na taratibu wanaanza kukua.

Wakati huo intelijensia ya Msumbiji iko wapi? Wamelala, udenda unatiririka mpaka masikioni.

Walidharau mwiba, guu likaota tende.

Maana kabla ya kufikia shambulizi lile la kwanza la Ansar al-sunna mwaka 2017 katika mji wa Mocimboa de Praia, tayari kuna matukio matatu nyuma yalishatengeneza 'alarm' ya hatari.

View attachment 3004762

Mwaka 2015, meya wa mji wa Mocimboa de Praia alinukuliwa akisema kuna tetesi za kundi la Al-shabab ku-recruit vijana wa mji huu na kitu hiki ni hatari kwa usalama.

Kipi kilifanyika? Hamna.

Mwaka 2016, kwa kupitia 'Nacedje Community Radio', mkuu wa shule moja ndani ya jimbo hili la Cabo Delgado anasikika akilalama kupungua kwa kasi kwa idadi ya wanafunzi shuleni, wanafunzi hao wakisema shule haina tija.

View attachment 3004763

Walikuwa wanaenda wapi? Hamna anayejua.

Viongozi wa dini ya kiislamu katika maeneo kadhaa, wakaripoti kuna mafundisho ya tofauti yanayozunguka mtaani, mafundisho ambayo ni kinyume na dini ya kiislamu, mfano watu kusali wakiwa na viatu.

Nani aliyekuwa anayatoa? Hamna anayejua.

View attachment 3004765

Wanakuja kutoa macho tarehe 5, Oktoba 2017. Ansar al-sunna wanakuja katika miili yao kamili, sio story tena. Wanamwaga mvua ya vyuma kwenye vituo vitatu vya polisi na kufungua rasmi mchuano mkali ambao unadumu mpaka leo hii 2024.

View attachment 3004766

Sio story, idadi kubwa ya wahusika wa kundi hili ni watu wa hapahapa Msumbiji. Wazawa. Hawa ndo' wale wanaozungumza kireno na kimwani - lugha ya pwani ya Cabo Delgado.

Kamanda Inacio Dina, msemaji wa jeshi la polisi, alikwishalisema hili.

Na hata kwenye ile ripoti ya gazeti la serikali ya Msumbiji la tarehe 17 April 2024, majuzi tu hapa, unaona ni namna gani watu wa Msumbiji walivyotawala orodha nzima ya washukiwa wa ugaidi isipokuwa watu wawili tu ambao ni watanzania.

View attachment 3004767

Lakini zaidi ripoti ile, inaacha swali muhimu juu ya ukwasi walionao hawa Ansar al-sunna pale unaposoma maelezo ya mshukiwa Ismael Sefo Sante (23), mfanyakazi wa kampuni ya usafirishaji ya Quimenci nchini Msumbiji.

Kwa mujibu wa maelezo hayo, mshukiwa mwingine, Ally Yusuf Liwangwa au kwa jina maarufu Big Ally (47), mtanzania mfanyabiashara kutoka Dar, aliwasiliana na Ismael Sefo Sante na kumpatia 'deal' la kutafuta vijana hamsini kwa ajili ya kujiunga na kundi la Ansar al-sunna.

Deal lililoweka mezani dau la USD 15,600.

Kwa pesa za madafu ni milioni arobaini na laki tano sitini. Hapo kwenye ripoti zingine, hususani mahojiano yalofanywa na BBC Eye of Africa, mhojiwaji anasema pesa hiyo ni ya kuleta watu wawili tu kwenye kundi.

Just imagine.

View attachment 3004768

Hizi pesa zote wanatoa wapi? Kuna wanaosema ni funding toka kundi la Islamic state, lakini ni kwa maslahi gani? Wengine wanasema ni mali wanazokwapua kwenye uvamizi wao huku na kule.

Hamna anayejua maana hamna rekodi yeyote ya miamala yao. Yote haya yanafanyika kwa kificho.

Lakini swala lililo wazi hapa ni sababu ya wao kuweka makazi na kung'ang'ania hapa jimboni Cabo Delgado. Hili lina sababu nzuri na ya kusisimua kwani linatosha kwa kila 'angle'.

Kwenye ripoti ya maendeleo ya mwaka 2017, Msumbiji inaripotiwa kuwa na asilimia 46.1% ya watu wanaoishi chini ya dola moja kwa siku. Ukosefu wa ajira kwa vijana ni 41.7% na ni 25% pekee ya watu nchi nzima ndo' wanapata huduma ya umeme.

Hali ni mbaya zaidi jimbo la Cabo Delgado.

View attachment 3004769

Umaskini umekithiri kila pahali.

Watu wanautafuta mkate kwenye shughuli za uvuvi, kilimo na uchimbaji mdogo wa madini ya Ruby kwa vizazi na vizazi. Huko migodini Montepuez, vijana wengi wanajiajiri na walau wanapata chochote kitu.

Lakini baadae, katika kuongeza chumvi kwenye kidonda, serikali inawaondosha vijana hawa na mradi wanapewa kampuni kubwa ya Gemfields hivyo vijana wengi wanabakia bila ya kazi.

View attachment 3004771

Mwaka 2010, katika pwani ya mji wa Palma, inagundulikana reserve kubwa ya gesi asilia, reserve ambayo ni ya tatu kwa ukubwa barani Afrika.

Mali hiyo inavutia kampuni ya marekani, ANADARKO, ambao mwaka 2017 wanaanza kuchora mkakati wa kuhamisha watu ilikupisha mradi huu mkubwa lakini baadae kampuni ya kifaransa ya TotalEnergies inanunua hisa hii ya Anadarko kwenye uwekezaji wa gesi hapa Msumbiji kwa dola bilioni 3.

View attachment 3004773

Mradi unakuwa mikononi mwao.

Sasa rasilimali zote hizi ndani ya eneo hili, bado wananchi wanahaha kwa umaskini uliokithiri huku serikali ikiwatupa mkono.

Hapa ndo' Ansar al-sunna wanapopenyeza utambi wao. Wanashawishi watu hawa, na kama ganda la ndizi, wanawachota watu wakitumia mgongo wa imani. Vijana wanajiunga wakiamini hii ni njia sahihi ya kujikwamua.

Kwa lugha tamu ya ushawishi, wanawachota wafuasi na kukua taratibu huku macho yao yakiwa kwenye hizi rasilimali za Cabo Delgado.

Kuanzia kwenye uchumi HALALI wa gesi na madini kama vile Ruby na pia Graphite inayotumika kwenye utengenezaji wa battery za vyombo vya moto na simu za mkononi mpaka kwenye uchumi HARAMU wa pwani unaokua kwa sababu ya uingizwaji wa madawa (heroin) kutoka Asia.

View attachment 3004774

Uchumi huo unakadiriwa kuwa na thamani ya dola za kimarekani milioni mia moja.

View attachment 3004775

Mpenzi msomaji, mpaka kufikia hapa naweza sema haya ya nyuma yanatosha. Hata na hivyo hatuwezi kuyamaliza.

Turudi sasa mwezi July 2021, ambapo jumuiya ya SADC, Tanzania ikiwemo ndani yake, inatuma rasmi jeshi lake linaloungana na jeshi la Rwanda kuwakabili hawa Ansar al-sunna.

View attachment 3004777

Oparesheni hii inaitwa SAMIM (SADC Mission in Mozambique).

Je imefanyikaje na imefikia wapi? Na maslahi ya Rwanda yako wapi katika kuingiza jeshi lake hapa tena kwa miguu yote miwili?

Kwanini South Africa wamejitoa?

Nitakuja na uzi wa mwisho. Thanks.
Thank you very much
 
Makala murua kabisa. lakini wenye uwezo mdogo wa akili wataendelea kuishutumu dini badala ya mzizi halisi wa tatizo. Utawala mbovu wa serikali zetu na mgawanyo wa huduma usiojali wananchi, rushwa na ukandamizaji huzaa haya yote. Watu katika mazingira haya ni rahisi sana kurubuniwa na mabeberu ili tu msitulie na wao waendelee kuchota mali.
Dini inasingiziwa si hapo juzi tulisikia Gari lenye Bendera ya chama fulani ikisafirisha Wahamiaji haramu? Kweli wale ni Wahamiaji haramu au ndio hawa hawa Magaidi washenzi?
 
Makala murua kabisa. lakini wenye uwezo mdogo wa akili wataendelea kuishutumu dini badala ya mzizi halisi wa tatizo. Utawala mbovu wa serikali zetu na mgawanyo wa huduma usiojali wananchi, rushwa na ukandamizaji huzaa haya yote. Watu katika mazingira haya ni rahisi sana kurubuniwa na mabeberu ili tu msitulie na wao waendelee kuchota mali.

Dini inafuga ugaidi. Dunia nzima Waislamu ni asilimia 90 ya Ugaidi.
 
UKIWA MAKINI BILA KUFUNGAMANA NA UPANDE WOWOTE UTAGUNDUA MUANDISHI NDIO ANATENGEZENEZA PICHA YA KUHUSISHA UISLAMU NA UGAIDI ETI KISA TU ANAANDIKA ANSAR SUNNA. HIZO NDIO PROPAGANDA TUNAZOZIKATAA KWA NGUVU ZOTE.! SEHEMU TAYARI UNAONA INA RASIMALI ZA KUTOSHA KAMA GESI SASA WW UNADHANI WAZUNGU WATAWAACHA KWA AMANI.

LAZIMA WATUMIE UISLAMU KAMA KIKI KUFANIKISHA MAMBO YAO NA TAYAR WA AFRICA AKILI ZA KUFIKIRIA NI FINYU BASI WAO WANABEBA KILA AINA YA NENO WANALOLISIKIA.

SASA HAO WAISALAMU HAPO WANAUA WATU ALAFU WAO WANAPATA FAIDA GANI.?? KISHA HIYO GESI WAIPELEKE WAPI ?? ALAFU KWANN WANAOKUFA NI HAO HAO WAISLAMU WAKAZI WA MAENEO HAYO.?? HUJIULIZI PIA
???????

KUNA VITU SENSITIVES HATUWEZI KUVIANDIKA HAPA MANA MSHAZOEA KUBISHANA MTAONA PIA NI UONGO MANA NYIE MKISHA AMINI KITU NDIO HICHO HICHO HAMBADILIKI MNA VICHWA VIGUMU VYA KUKUBALI UKWELI
???
 
Wishful thinking.

Ni miaka mingapi tangu mafunzo ya JKT kwa vijana yaanze? Ni wangapi waliopitia hayo mafunzo walipata ajira? Wangapi hawakupata?

Ukiijua JKT (JWTZ) vizuri, utaacha hizi ndoto za mchana.
Ni kweli ni ndoto😀

Kwamba wao JWTZ na JKT ni special sana hapa duniani😀

Hao hao JWTZ unao wasifia ndio mambo ya panya road yametokea hapa hapa nchini tena chini ya vitoto vidogo tu na watu wazima kulazwa ndani mapema kama kuku.

Hili hili taifa ndilo yale ya kibiti yalitokea na JWTZ ikiwepo.

Rais wa nchi mchonga alinusurika kupinduliwa na hao hao JWTZ wengine kwa zaidi ya mara moja.

Wewe unafikiri hao vijana wa JKT wataendelea kuwa humble miaka yao yote huku umasikini ukiwatandika vilivyo na wanaona wakubwa wao wakitumbua tu mali na kufanya ufisadi na viongozi wa serikali huku wao wakiimbiwa uzalendo.

Unafikiri watu wanakula uzalendo etii ehhhh nakusisitiza hawa vijana sio kwamba hawawezi kufanya ila wanakosa supplier wa silaha tu maana kila sababu ya ku go against serikali wanayo hawahitaji kuambiwa na yoyote.

Ubaya au uzuri mtaani maisha kila siku yanazidi kuwa tight kwa sababu ya uongozi na hakuna mabadiliko yoyote yale.

Hata huko Msumbiji naamini kabisa walikuwepo wananchi na viongozi waliokuwa wana ongea kama wewe awali ila leo hii kiko wapi ?

Tanzania leo hii tu kuna vijana wamepotea na hawaeleweki walipoenda.

Ogopa sana mtu aliyechoka umasikini na akapata silaha huyu maana ya maisha kwake inakuwa haina uzito tena.
 
Alipohojiwa, alisema kauli hii; "Mungu, wasaidie watu wale."

Kipi kilichompelekea azungumze haya,?Alikwenda kuwasaidia,halafu anaondoka anajua fika anawaacha matatani.

Nirudie unielewe,Alikwenda kutatua tatizo,tatizo halijesha anaondoka na anawaombea Kwa Mungu.Aligundua Nini?
SteveMollel
 
Kabla ya kuendelea, turejelee kauli aliyoitoa Colonel Lionel Dyck, mkurugenzi wa jeshi binafsi la DAG ambaye mkataba wake wa kutoa msaada wa anga pale Msumbiji ulitamatika tarehe 6, April 2021.

View attachment 3004739

Alipohojiwa, alisema kauli hii; "Mungu, wasaidie watu wale."

Akimaanisha watu wa Msumbiji aliowaacha katika tabu. Tabu ambazo hakusimuliwa na mtu bali alizishuhudia yeye mwenyewe katika oparesheni yake nchini humo.

Na sisi pia tunaishi hapa. Eeh Mungu wasaidie watu wale (wa Msumbiji). Lakini pia tunaongezea, atusaidie na sisi ambao tumepakana nao.

Bwana huyu, Lionel Dyck, yeye amekwishaaga nchi hii ya Msumbiji lakini kwenye mioyo ya wananchi mia mbili na ishirini na nane katika mji huu wa Palma, atabaki kuishi milele.

View attachment 3004740

Hawatamsahau namna alivyotumia helikopta zake kuwanusuru na midomo ya bunduki za magaidi ambao walitumwa roho za watu siku hiyo.

Siku ya maafa.

Kwao wanamwona Lionel Dyck na jeshi lake kama malaika.

Helikopta yake iliwabeba, kidogo kidogo, zamu kwa zamu, na kila mara ilipoondoka wakadhani haitokaa ikarudi tena, lakini bado ikarejea na kuwakomba watu kwenda eneo salama huko peninsula ya Afungi.

Pichani ni watalii ambao walikwama kwenye hoteli wakati wa mashambulizi ya Palma yanarindima huko nje.

View attachment 3004741

Kwa kutumia mashuka meupe wakaandika ujumbe 'HELP', na bahati wakaonekana na kuokolewa na helikopta ya DAG.

Hivyo watu hawa, ukiwajumuisha na wale wananchi wa Msumbiji 228, wanakamilisha jumla ya watu 240 waliofanikiwa kuokolewa na oparesheni ya DAG.

Sasa tukiacha kuhangaika na haya matawi ili turudi kwenye mzizi wenyewe, basi hatuna budi kuurejea ule mwaka 2012 kule Mombasa, nchini Kenya.

View attachment 3004743

Katika mwaka huo, August ya tarehe 27, siku ya Jumatatu majira ya asubuhi, sauti ya bunduki inarindima ndani ya jiji la Mombasa na kusababisha taharuki kubwa.

Kwenye zoezi hilo, zilitumwa risasi kumi na nane kwenda ubavu wa kulia (upande wa dereva) wa gari aina ya toyota hiace nyeupe iliyobeba familia nzima ndani yake.

View attachment 3004744
Risasi hizo zilikuwa zimeagizwa kitu kimoja tu, kuja na roho ya bwana Aboud Rogo aliyekuwa ameketi katika usukani. Na kweli risasi zikafanikiwa.

Aboud Rogo anafariki papo hapo, wengine wote wakibakia salama salmin mbali na mkewe, bi. Haniya, aliyeishia kupata jeraha la risasi mguuni.

View attachment 3004745

Cha kushangaza siku hiyo, bwana Rogo alikuwa yu njiani akimpeleka mkewe hospitali kwani alikuwa na maradhi, ila ajabu akaishia kupelekwa yeye hospitali akiwa marehemu.

Kifo hiki cha Rogo kinakuja muda si mrefu, takribani wiki mbili zilizopita, baada ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa Mataifa (UN) na nchi ya Marekani kwa kutuhumiwa kuwa na mahusiano na Al-shabab ya huko Somalia.

View attachment 3004746

Bwana Rogo ambaye alikuwa muumin wa itikadi kali na mmoja wa viongozi wa kikundi cha Al-hijra kinachoaminika kuwa 'wing' ya Al-shabab nchini Kenya, alinyooshewa vidole na UN kwa kusaidia Al-shabab kwenye mambo matatu:

'Funding, recruiting and logistics'.

Kwa mujibu wa UN, bwana Rogo alikuwa akiifadhili kundi hilo la kigaidi kwa michango mbalimbali ya watu, alikuwa akisaidia kutafuta vijana wa kujiunga nalo na pia alikuwa anasaidia kuwasafirisha vijana hao kufika Somalia.
View attachment 3004747

Na kifo hiki cha Rogo hakikuwa cha kwanza wala cha mwisho kwa watu waliokuwa wanafanana naye kaliba. Wote waliuawa kwa mtindo huu huu. Wanapigwa risasi na watu wasiojulikana na 'wasiokamatikana'.

View attachment 3004748

Sasa wafuasi hawa wa Rogo, kwa mujibu wa ripoti ya Nation Africa ya Kenya, ndio mabwana wanaoleta matata kule Msumbiji. Wafuasi hao walitawanyika na kusambaa maeneo mbalimbali baada ya vifo vya wakubwa wao waliowashika mkono.

Hivyo kwa maelezo haya, na yale ya kamanda Sirro kusema magaidi wale waliovuka mpaka kutoka Msumbiji na kuvamia Mtwara ni mtandao ulioanzia MKIRU (Mkuranga, Kibiti na Rufiji), yanatosha kutueleza mtandao huo haukuanzia hapa nchini.

Ulianzia huko Kenya, ukaja kwetu kisha ukaelekea Msumbiji. Kote huko unapopita, unapokelewa na wakazi ambao wengine kwa hali zao, wanashawishika kujiunga nao wakiamini ni njia ya kupambana na madhila yanayowasibu.

Watu hawa waliobeba chuki, ni rahisi kufanyiwa 'brainwashing' kwa kutumia mwamvuli wa imani. Baada ya hapo wanageuka kuwa watu wapya kabisa usiowajua.

View attachment 3004750
Wanabeba silaha kuingia ulingoni na ukikutana nao , my friend, usitegemee watakukumbuka ati wewe ulikuwa jirani yake, ulicheza naye mdako utotoni, ulikimbizana naye kwenye kombolela na kushikana kidali.

Kama bado unautaka ugali, basi tupa hiyo miguu kadiri uwezavyo, hata ukiweza kupaa angani basi wewe paa, utaenda kujiuliza uliwezaje ukiwa upo chini ya kitanda.

Mfano mzuri wa hii kesi ni vijana wawili; Nuro na Abu Dardai Jongo kule nchini Msumbiji ambao leo hii ni vinara wa mauaji katika kikundi hiki cha Ansar al-sunna.

View attachment 3004752
(Nuro Pichani)

Nuro alikuwa mfanyabiashara wa samaki hapo Cabo Delgado. Mtu poa na mcheshi. Akaja akapotea isijulikane kaenda wapi. Kuja kuonekana tena, si yule wa zamani. Anachinja watu kama utani.

View attachment 3004757

Abu Dardai Jongo yeye alikuwa na pikipiki. Alikuwa anfanya kazi ya kusafirisha watu toka mto Ruvuma mpaka Montepuez. Kitambo fulani, akaenda Macomia. Aliporejea, wenzake wanasema hakuwa tena yule Abu walokuwa wanamfahamu.

View attachment 3004759
(Abu Jongo pichani)

Haikupita muda akapotea moja kwa moja.

Tukirudi kwa jamii ya watu wanaoishi mkoa wa Pwani, mathalani Kibiti, Mkuranga na Rufiji, hamna asiyejua wengi wao hali ni dhalili. Pangu pakavu tia mchuzi.

Shughuli wanazotegemea ni kuchuma rasilimali zinazowazunguka kwa kutengeneza na kuuza mkaa, kukata na kuuza kuni na magogo ya mbao pasipo kusahau kilimo.

Hivyo watu hawa wanapokumbana na kodi kandamizi, ushuru mlima na tozo rundo kuanzia kwa maafisa wa serikali za mtaa, maafisa misitu na rasilimali mpaka polisi, huzaa chuki.

Chuki ambayo huja kuwa mtaji kwa wadhalimu.

Tunakumbuka mwaka 2013 namna gani watu wa Kibiti walifanya vurugu kubwa mpaka kufunga barabara, ikabidi IGP atoe kauli.

View attachment 3004760

Na pia tunakumbuka namna gani tulianza kuokota miili ya watu, wakilengwa haswa wafanyakazi wa serikali mathalani watu wa serikali za mitaa na polisi.

Ilitumika nguvu kubwa kuwazima mabwana hawa. Ilibidi watu wafe, hata wale ambao ni ndugu zetu, ili wengi wetu tubaki salama.

View attachment 3004761

Lakini ni dhahiri oparesheni hii (MKIRU) haikumaliza hawa 'mabwana' wote , ndo' wengine wanakimbilia Msumbiji wanapoenda kukutana na 'locals' ambao wanaungana nao na taratibu wanaanza kukua.

Wakati huo intelijensia ya Msumbiji iko wapi? Wamelala, udenda unatiririka mpaka masikioni.

Walidharau mwiba, guu likaota tende.

Maana kabla ya kufikia shambulizi lile la kwanza la Ansar al-sunna mwaka 2017 katika mji wa Mocimboa de Praia, tayari kuna matukio matatu nyuma yalishatengeneza 'alarm' ya hatari.

View attachment 3004762

Mwaka 2015, meya wa mji wa Mocimboa de Praia alinukuliwa akisema kuna tetesi za kundi la Al-shabab ku-recruit vijana wa mji huu na kitu hiki ni hatari kwa usalama.

Kipi kilifanyika? Hamna.

Mwaka 2016, kwa kupitia 'Nacedje Community Radio', mkuu wa shule moja ndani ya jimbo hili la Cabo Delgado anasikika akilalama kupungua kwa kasi kwa idadi ya wanafunzi shuleni, wanafunzi hao wakisema shule haina tija.

View attachment 3004763

Walikuwa wanaenda wapi? Hamna anayejua.

Viongozi wa dini ya kiislamu katika maeneo kadhaa, wakaripoti kuna mafundisho ya tofauti yanayozunguka mtaani, mafundisho ambayo ni kinyume na dini ya kiislamu, mfano watu kusali wakiwa na viatu.

Nani aliyekuwa anayatoa? Hamna anayejua.

View attachment 3004765

Wanakuja kutoa macho tarehe 5, Oktoba 2017. Ansar al-sunna wanakuja katika miili yao kamili, sio story tena. Wanamwaga mvua ya vyuma kwenye vituo vitatu vya polisi na kufungua rasmi mchuano mkali ambao unadumu mpaka leo hii 2024.

View attachment 3004766

Sio story, idadi kubwa ya wahusika wa kundi hili ni watu wa hapahapa Msumbiji. Wazawa. Hawa ndo' wale wanaozungumza kireno na kimwani - lugha ya pwani ya Cabo Delgado.

Kamanda Inacio Dina, msemaji wa jeshi la polisi, alikwishalisema hili.

Na hata kwenye ile ripoti ya gazeti la serikali ya Msumbiji la tarehe 17 April 2024, majuzi tu hapa, unaona ni namna gani watu wa Msumbiji walivyotawala orodha nzima ya washukiwa wa ugaidi isipokuwa watu wawili tu ambao ni watanzania.

View attachment 3004767

Lakini zaidi ripoti ile, inaacha swali muhimu juu ya ukwasi walionao hawa Ansar al-sunna pale unaposoma maelezo ya mshukiwa Ismael Sefo Sante (23), mfanyakazi wa kampuni ya usafirishaji ya Quimenci nchini Msumbiji.

Kwa mujibu wa maelezo hayo, mshukiwa mwingine, Ally Yusuf Liwangwa au kwa jina maarufu Big Ally (47), mtanzania mfanyabiashara kutoka Dar, aliwasiliana na Ismael Sefo Sante na kumpatia 'deal' la kutafuta vijana hamsini kwa ajili ya kujiunga na kundi la Ansar al-sunna.

Deal lililoweka mezani dau la USD 15,600.

Kwa pesa za madafu ni milioni arobaini na laki tano sitini. Hapo kwenye ripoti zingine, hususani mahojiano yalofanywa na BBC Eye of Africa, mhojiwaji anasema pesa hiyo ni ya kuleta watu wawili tu kwenye kundi.

Just imagine.

View attachment 3004768

Hizi pesa zote wanatoa wapi? Kuna wanaosema ni funding toka kundi la Islamic state, lakini ni kwa maslahi gani? Wengine wanasema ni mali wanazokwapua kwenye uvamizi wao huku na kule.

Hamna anayejua maana hamna rekodi yeyote ya miamala yao. Yote haya yanafanyika kwa kificho.

Lakini swala lililo wazi hapa ni sababu ya wao kuweka makazi na kung'ang'ania hapa jimboni Cabo Delgado. Hili lina sababu nzuri na ya kusisimua kwani linatosha kwa kila 'angle'.

Kwenye ripoti ya maendeleo ya mwaka 2017, Msumbiji inaripotiwa kuwa na asilimia 46.1% ya watu wanaoishi chini ya dola moja kwa siku. Ukosefu wa ajira kwa vijana ni 41.7% na ni 25% pekee ya watu nchi nzima ndo' wanapata huduma ya umeme.

Hali ni mbaya zaidi jimbo la Cabo Delgado.

View attachment 3004769

Umaskini umekithiri kila pahali.

Watu wanautafuta mkate kwenye shughuli za uvuvi, kilimo na uchimbaji mdogo wa madini ya Ruby kwa vizazi na vizazi. Huko migodini Montepuez, vijana wengi wanajiajiri na walau wanapata chochote kitu.

Lakini baadae, katika kuongeza chumvi kwenye kidonda, serikali inawaondosha vijana hawa na mradi wanapewa kampuni kubwa ya Gemfields hivyo vijana wengi wanabakia bila ya kazi.

View attachment 3004771

Mwaka 2010, katika pwani ya mji wa Palma, inagundulikana reserve kubwa ya gesi asilia, reserve ambayo ni ya tatu kwa ukubwa barani Afrika.

Mali hiyo inavutia kampuni ya marekani, ANADARKO, ambao mwaka 2017 wanaanza kuchora mkakati wa kuhamisha watu ilikupisha mradi huu mkubwa lakini baadae kampuni ya kifaransa ya TotalEnergies inanunua hisa hii ya Anadarko kwenye uwekezaji wa gesi hapa Msumbiji kwa dola bilioni 3.

View attachment 3004773

Mradi unakuwa mikononi mwao.

Sasa rasilimali zote hizi ndani ya eneo hili, bado wananchi wanahaha kwa umaskini uliokithiri huku serikali ikiwatupa mkono.

Hapa ndo' Ansar al-sunna wanapopenyeza utambi wao. Wanashawishi watu hawa, na kama ganda la ndizi, wanawachota watu wakitumia mgongo wa imani. Vijana wanajiunga wakiamini hii ni njia sahihi ya kujikwamua.

Kwa lugha tamu ya ushawishi, wanawachota wafuasi na kukua taratibu huku macho yao yakiwa kwenye hizi rasilimali za Cabo Delgado.

Kuanzia kwenye uchumi HALALI wa gesi na madini kama vile Ruby na pia Graphite inayotumika kwenye utengenezaji wa battery za vyombo vya moto na simu za mkononi mpaka kwenye uchumi HARAMU wa pwani unaokua kwa sababu ya uingizwaji wa madawa (heroin) kutoka Asia.

View attachment 3004774

Uchumi huo unakadiriwa kuwa na thamani ya dola za kimarekani milioni mia moja.

View attachment 3004775

Mpenzi msomaji, mpaka kufikia hapa naweza sema haya ya nyuma yanatosha. Hata na hivyo hatuwezi kuyamaliza.

Turudi sasa mwezi July 2021, ambapo jumuiya ya SADC, Tanzania ikiwemo ndani yake, inatuma rasmi jeshi lake linaloungana na jeshi la Rwanda kuwakabili hawa Ansar al-sunna.

View attachment 3004777

Oparesheni hii inaitwa SAMIM (SADC Mission in Mozambique).

Je imefanyikaje na imefikia wapi? Na maslahi ya Rwanda yako wapi katika kuingiza jeshi lake hapa tena kwa miguu yote miwili?

Kwanini South Africa wamejitoa?

Nitakuja na uzi wa mwisho. Thanks.
Ukichunguza kwa umakini Sana utagundua kwamba yale maeneo karibia yote yenye vurugu kule Msumbiji yana historia kongwe sana kuhusiana na suala la vurugu za kisiasa, hata kabla ya Taifa hilo la Msumbiji halijapata uhuru wake kutoka kwa mkoloni wao Ureno. Kambi nyingi sana za Makundi ya kisiasa ya Wapigania Uhuru wa nchi hiyo ya Msumbiji ziliwekwa katika ukanda huo wa Kaskazini mwa nchi hiyo, maeneo ambayo hadi leo hii bado yanaendelea kukumbwa na vurugu. Makundi ya Wapigania Uhuru ya vyama vya Siasa vya FRELIMO na RENAMO vilikuwa na Kambi zao nyingi za wazi na za siri kubwa ktk maeneo hayo yenye vurugu kwa sasa. Baada ya kufanikisha suala la kuuangusha utawala wa mkoloni wao Ureno, maeneo hayo tayari yalikuwa yamevurugwa vibaya sana na vita vya ukombozi, miundombinu yote ya kujenga uchumi kama vile viwanda viliharabiwa kabisa na mapigano ya vita.
Mbaya zaidi, hata chama cha Siasa cha FRELIMO kilipofanikiwa kushika madaraka ktk nchi hiyo ya Msumbiji, haikukishirikisha Chama cha RENAMO ktk kuitawala nchi hiyo ya Msumbiji, badala yake vyama hivyo viligawanyika na kuwa vyama vinavyohasimiana, vikapigana vita tena wao kwa wao ili kugombea kupata udhibiti wa madaraka ktk nchi hiyo, hatimaye Chama cha RENAMO kilizidiwa nguvu na kushindwa vita. Chama cha FRELIMO kutokana na msaada mkubwa waliopata kutoka kwa Mwl. J. K. Nyerere na CCM yake, walifanikiwa kuhodhi na kudhibiti mamlaka na madaraka yote ya nchi hiyo ya Msumbiji, na RENAMO kikawa Chama kikuu cha Upinzani dhidi ya FRELIMO.
Mbaya zaidi tena, utawala wa FRELIMO ulikichukulia Chama cha RENAMO kama Kundi la Waasi wala siyo Chama cha Siasa, Matokeo yake Wanachama na Wapiganaji wa RENAMO wakakimbilia msituni na kuweka Kambi zao nyingi za Siri kwenye huo Upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Serikali ya Msumbiji Kama ililitelekeza kabisa kwa muda mrefu eneo hilo lililopo Kaskazini mwa nchi hiyo kwa sababu ililiona kama eneo lenye maficho ya Waasi wa RENAMO, hata huduma za kijamii zilikuwa duni sana kwenye maeneo hayo. Wananchi wengi wa upande huo wa Kaskazini mwa nchi waliona kama Serikali ya Msumbiji imewatenga na haikuwa inawajali. Serikali ilijichimbia mizizi kwenye eneo la Kusini mwa nchi hiyo ya Msumbiji na kuigawa nchi ktk mapande mawili ya Kaskazini na Kusini. Serikali hiyo ya Msumbiji ilirudi tena kwa kasi upande wa Kaskazini mwa nchi hiyo baada ya Ugunduzi wa Nishati ya Gesi kwenye maeneo hayo ya Kaskazini, hapo ndipo ukawa mwanzo mpya wa kuibuka kwa Vurugu hizi zinazoendelea hivi sasa ktk eneo hilo la Kaskazini mwa nchi hiyo ya Msumbiji.

Suala la Dini au Udini ktk vurugu hizo za huko Msumbiji linatumika tu na wahusika kama "SCAPEGOAT" ili kuweza kupata msaada wa kijeshi na wa silaha za kupigania vita dhidi ya maadui zao.
 
Alipohojiwa, alisema kauli hii; "Mungu, wasaidie watu wale."

Kipi kilichompelekea azungumze haya,?Alikwenda kuwasaidia,halafu anaondoka anajua fika anawaacha matatani.

Nirudie unielewe,Alikwenda kutatua tatizo,tatizo halijesha anaondoka na anawaombea Kwa Mungu.Aligundua Nini?
SteveMollel
Alikwenda kutatua tatizo gani hasa huko Msumbiji??
Shida kubwa Sana tuliyonayo sisi Watu weusi ni kwamba huwa hatupendi kabisa kufanya tafiti za kina ili kubaini kiini hasa cha Migogoro ya kibinadamu inayoliandama bara hili la Afrika. Ni lazima tuwe tunafanya utafiti wa kina ili tujue viini au vyanzo halisi vinavyosababisha Migogoro (root cause) ili tuweze kutatua Migogoro hiyo inayotuandama ktk nchi zetu hizi miaka nenda rudi.

Je, Unajua ni kwa Nini huyo mzungu (mkaburu) pamoja na wenzake walikuwepo kwenye eneo hilo lenye machimbo ya gesi huko Jimboni Cabo Delgado nchini Msumbiji wakiwa na silaha za kijeshi ikiwamo na hiyo helikopta ya kijeshi aliyotumia katikà kufanya uokoaji wa hao Watu??? Unazijua sababu???
 
Kabla ya kuendelea, turejelee kauli aliyoitoa Colonel Lionel Dyck, mkurugenzi wa jeshi binafsi la DAG ambaye mkataba wake wa kutoa msaada wa anga pale Msumbiji ulitamatika tarehe 6, April 2021.

View attachment 3004739

Alipohojiwa, alisema kauli hii; "Mungu, wasaidie watu wale."

Akimaanisha watu wa Msumbiji aliowaacha katika tabu. Tabu ambazo hakusimuliwa na mtu bali alizishuhudia yeye mwenyewe katika oparesheni yake nchini humo.

Na sisi pia tunaishi hapa. Eeh Mungu wasaidie watu wale (wa Msumbiji). Lakini pia tunaongezea, atusaidie na sisi ambao tumepakana nao.

Bwana huyu, Lionel Dyck, yeye amekwishaaga nchi hii ya Msumbiji lakini kwenye mioyo ya wananchi mia mbili na ishirini na nane katika mji huu wa Palma, atabaki kuishi milele.

View attachment 3004740

Hawatamsahau namna alivyotumia helikopta zake kuwanusuru na midomo ya bunduki za magaidi ambao walitumwa roho za watu siku hiyo.

Siku ya maafa.

Kwao wanamwona Lionel Dyck na jeshi lake kama malaika.

Helikopta yake iliwabeba, kidogo kidogo, zamu kwa zamu, na kila mara ilipoondoka wakadhani haitokaa ikarudi tena, lakini bado ikarejea na kuwakomba watu kwenda eneo salama huko peninsula ya Afungi.

Pichani ni watalii ambao walikwama kwenye hoteli wakati wa mashambulizi ya Palma yanarindima huko nje.

View attachment 3004741

Kwa kutumia mashuka meupe wakaandika ujumbe 'HELP', na bahati wakaonekana na kuokolewa na helikopta ya DAG.

Hivyo watu hawa, ukiwajumuisha na wale wananchi wa Msumbiji 228, wanakamilisha jumla ya watu 240 waliofanikiwa kuokolewa na oparesheni ya DAG.

Sasa tukiacha kuhangaika na haya matawi ili turudi kwenye mzizi wenyewe, basi hatuna budi kuurejea ule mwaka 2012 kule Mombasa, nchini Kenya.

View attachment 3004743

Katika mwaka huo, August ya tarehe 27, siku ya Jumatatu majira ya asubuhi, sauti ya bunduki inarindima ndani ya jiji la Mombasa na kusababisha taharuki kubwa.

Kwenye zoezi hilo, zilitumwa risasi kumi na nane kwenda ubavu wa kulia (upande wa dereva) wa gari aina ya toyota hiace nyeupe iliyobeba familia nzima ndani yake.

View attachment 3004744
Risasi hizo zilikuwa zimeagizwa kitu kimoja tu, kuja na roho ya bwana Aboud Rogo aliyekuwa ameketi katika usukani. Na kweli risasi zikafanikiwa.

Aboud Rogo anafariki papo hapo, wengine wote wakibakia salama salmin mbali na mkewe, bi. Haniya, aliyeishia kupata jeraha la risasi mguuni.

View attachment 3004745

Cha kushangaza siku hiyo, bwana Rogo alikuwa yu njiani akimpeleka mkewe hospitali kwani alikuwa na maradhi, ila ajabu akaishia kupelekwa yeye hospitali akiwa marehemu.

Kifo hiki cha Rogo kinakuja muda si mrefu, takribani wiki mbili zilizopita, baada ya kuwekewa vikwazo na Umoja wa Mataifa (UN) na nchi ya Marekani kwa kutuhumiwa kuwa na mahusiano na Al-shabab ya huko Somalia.

View attachment 3004746

Bwana Rogo ambaye alikuwa muumin wa itikadi kali na mmoja wa viongozi wa kikundi cha Al-hijra kinachoaminika kuwa 'wing' ya Al-shabab nchini Kenya, alinyooshewa vidole na UN kwa kusaidia Al-shabab kwenye mambo matatu:

'Funding, recruiting and logistics'.

Kwa mujibu wa UN, bwana Rogo alikuwa akiifadhili kundi hilo la kigaidi kwa michango mbalimbali ya watu, alikuwa akisaidia kutafuta vijana wa kujiunga nalo na pia alikuwa anasaidia kuwasafirisha vijana hao kufika Somalia.
View attachment 3004747

Na kifo hiki cha Rogo hakikuwa cha kwanza wala cha mwisho kwa watu waliokuwa wanafanana naye kaliba. Wote waliuawa kwa mtindo huu huu. Wanapigwa risasi na watu wasiojulikana na 'wasiokamatikana'.

View attachment 3004748

Sasa wafuasi hawa wa Rogo, kwa mujibu wa ripoti ya Nation Africa ya Kenya, ndio mabwana wanaoleta matata kule Msumbiji. Wafuasi hao walitawanyika na kusambaa maeneo mbalimbali baada ya vifo vya wakubwa wao waliowashika mkono.

Hivyo kwa maelezo haya, na yale ya kamanda Sirro kusema magaidi wale waliovuka mpaka kutoka Msumbiji na kuvamia Mtwara ni mtandao ulioanzia MKIRU (Mkuranga, Kibiti na Rufiji), yanatosha kutueleza mtandao huo haukuanzia hapa nchini.

Ulianzia huko Kenya, ukaja kwetu kisha ukaelekea Msumbiji. Kote huko unapopita, unapokelewa na wakazi ambao wengine kwa hali zao, wanashawishika kujiunga nao wakiamini ni njia ya kupambana na madhila yanayowasibu.

Watu hawa waliobeba chuki, ni rahisi kufanyiwa 'brainwashing' kwa kutumia mwamvuli wa imani. Baada ya hapo wanageuka kuwa watu wapya kabisa usiowajua.

View attachment 3004750
Wanabeba silaha kuingia ulingoni na ukikutana nao , my friend, usitegemee watakukumbuka ati wewe ulikuwa jirani yake, ulicheza naye mdako utotoni, ulikimbizana naye kwenye kombolela na kushikana kidali.

Kama bado unautaka ugali, basi tupa hiyo miguu kadiri uwezavyo, hata ukiweza kupaa angani basi wewe paa, utaenda kujiuliza uliwezaje ukiwa upo chini ya kitanda.

Mfano mzuri wa hii kesi ni vijana wawili; Nuro na Abu Dardai Jongo kule nchini Msumbiji ambao leo hii ni vinara wa mauaji katika kikundi hiki cha Ansar al-sunna.

View attachment 3004752
(Nuro Pichani)

Nuro alikuwa mfanyabiashara wa samaki hapo Cabo Delgado. Mtu poa na mcheshi. Akaja akapotea isijulikane kaenda wapi. Kuja kuonekana tena, si yule wa zamani. Anachinja watu kama utani.

View attachment 3004757

Abu Dardai Jongo yeye alikuwa na pikipiki. Alikuwa anfanya kazi ya kusafirisha watu toka mto Ruvuma mpaka Montepuez. Kitambo fulani, akaenda Macomia. Aliporejea, wenzake wanasema hakuwa tena yule Abu walokuwa wanamfahamu.

View attachment 3004759
(Abu Jongo pichani)

Haikupita muda akapotea moja kwa moja.

Tukirudi kwa jamii ya watu wanaoishi mkoa wa Pwani, mathalani Kibiti, Mkuranga na Rufiji, hamna asiyejua wengi wao hali ni dhalili. Pangu pakavu tia mchuzi.

Shughuli wanazotegemea ni kuchuma rasilimali zinazowazunguka kwa kutengeneza na kuuza mkaa, kukata na kuuza kuni na magogo ya mbao pasipo kusahau kilimo.

Hivyo watu hawa wanapokumbana na kodi kandamizi, ushuru mlima na tozo rundo kuanzia kwa maafisa wa serikali za mtaa, maafisa misitu na rasilimali mpaka polisi, huzaa chuki.

Chuki ambayo huja kuwa mtaji kwa wadhalimu.

Tunakumbuka mwaka 2013 namna gani watu wa Kibiti walifanya vurugu kubwa mpaka kufunga barabara, ikabidi IGP atoe kauli.

View attachment 3004760

Na pia tunakumbuka namna gani tulianza kuokota miili ya watu, wakilengwa haswa wafanyakazi wa serikali mathalani watu wa serikali za mitaa na polisi.

Ilitumika nguvu kubwa kuwazima mabwana hawa. Ilibidi watu wafe, hata wale ambao ni ndugu zetu, ili wengi wetu tubaki salama.

View attachment 3004761

Lakini ni dhahiri oparesheni hii (MKIRU) haikumaliza hawa 'mabwana' wote , ndo' wengine wanakimbilia Msumbiji wanapoenda kukutana na 'locals' ambao wanaungana nao na taratibu wanaanza kukua.

Wakati huo intelijensia ya Msumbiji iko wapi? Wamelala, udenda unatiririka mpaka masikioni.

Walidharau mwiba, guu likaota tende.

Maana kabla ya kufikia shambulizi lile la kwanza la Ansar al-sunna mwaka 2017 katika mji wa Mocimboa de Praia, tayari kuna matukio matatu nyuma yalishatengeneza 'alarm' ya hatari.

View attachment 3004762

Mwaka 2015, meya wa mji wa Mocimboa de Praia alinukuliwa akisema kuna tetesi za kundi la Al-shabab ku-recruit vijana wa mji huu na kitu hiki ni hatari kwa usalama.

Kipi kilifanyika? Hamna.

Mwaka 2016, kwa kupitia 'Nacedje Community Radio', mkuu wa shule moja ndani ya jimbo hili la Cabo Delgado anasikika akilalama kupungua kwa kasi kwa idadi ya wanafunzi shuleni, wanafunzi hao wakisema shule haina tija.

View attachment 3004763

Walikuwa wanaenda wapi? Hamna anayejua.

Viongozi wa dini ya kiislamu katika maeneo kadhaa, wakaripoti kuna mafundisho ya tofauti yanayozunguka mtaani, mafundisho ambayo ni kinyume na dini ya kiislamu, mfano watu kusali wakiwa na viatu.

Nani aliyekuwa anayatoa? Hamna anayejua.

View attachment 3004765

Wanakuja kutoa macho tarehe 5, Oktoba 2017. Ansar al-sunna wanakuja katika miili yao kamili, sio story tena. Wanamwaga mvua ya vyuma kwenye vituo vitatu vya polisi na kufungua rasmi mchuano mkali ambao unadumu mpaka leo hii 2024.

View attachment 3004766

Sio story, idadi kubwa ya wahusika wa kundi hili ni watu wa hapahapa Msumbiji. Wazawa. Hawa ndo' wale wanaozungumza kireno na kimwani - lugha ya pwani ya Cabo Delgado.

Kamanda Inacio Dina, msemaji wa jeshi la polisi, alikwishalisema hili.

Na hata kwenye ile ripoti ya gazeti la serikali ya Msumbiji la tarehe 17 April 2024, majuzi tu hapa, unaona ni namna gani watu wa Msumbiji walivyotawala orodha nzima ya washukiwa wa ugaidi isipokuwa watu wawili tu ambao ni watanzania.

View attachment 3004767

Lakini zaidi ripoti ile, inaacha swali muhimu juu ya ukwasi walionao hawa Ansar al-sunna pale unaposoma maelezo ya mshukiwa Ismael Sefo Sante (23), mfanyakazi wa kampuni ya usafirishaji ya Quimenci nchini Msumbiji.

Kwa mujibu wa maelezo hayo, mshukiwa mwingine, Ally Yusuf Liwangwa au kwa jina maarufu Big Ally (47), mtanzania mfanyabiashara kutoka Dar, aliwasiliana na Ismael Sefo Sante na kumpatia 'deal' la kutafuta vijana hamsini kwa ajili ya kujiunga na kundi la Ansar al-sunna.

Deal lililoweka mezani dau la USD 15,600.

Kwa pesa za madafu ni milioni arobaini na laki tano sitini. Hapo kwenye ripoti zingine, hususani mahojiano yalofanywa na BBC Eye of Africa, mhojiwaji anasema pesa hiyo ni ya kuleta watu wawili tu kwenye kundi.

Just imagine.

View attachment 3004768

Hizi pesa zote wanatoa wapi? Kuna wanaosema ni funding toka kundi la Islamic state, lakini ni kwa maslahi gani? Wengine wanasema ni mali wanazokwapua kwenye uvamizi wao huku na kule.

Hamna anayejua maana hamna rekodi yeyote ya miamala yao. Yote haya yanafanyika kwa kificho.

Lakini swala lililo wazi hapa ni sababu ya wao kuweka makazi na kung'ang'ania hapa jimboni Cabo Delgado. Hili lina sababu nzuri na ya kusisimua kwani linatosha kwa kila 'angle'.

Kwenye ripoti ya maendeleo ya mwaka 2017, Msumbiji inaripotiwa kuwa na asilimia 46.1% ya watu wanaoishi chini ya dola moja kwa siku. Ukosefu wa ajira kwa vijana ni 41.7% na ni 25% pekee ya watu nchi nzima ndo' wanapata huduma ya umeme.

Hali ni mbaya zaidi jimbo la Cabo Delgado.

View attachment 3004769

Umaskini umekithiri kila pahali.

Watu wanautafuta mkate kwenye shughuli za uvuvi, kilimo na uchimbaji mdogo wa madini ya Ruby kwa vizazi na vizazi. Huko migodini Montepuez, vijana wengi wanajiajiri na walau wanapata chochote kitu.

Lakini baadae, katika kuongeza chumvi kwenye kidonda, serikali inawaondosha vijana hawa na mradi wanapewa kampuni kubwa ya Gemfields hivyo vijana wengi wanabakia bila ya kazi.

View attachment 3004771

Mwaka 2010, katika pwani ya mji wa Palma, inagundulikana reserve kubwa ya gesi asilia, reserve ambayo ni ya tatu kwa ukubwa barani Afrika.

Mali hiyo inavutia kampuni ya marekani, ANADARKO, ambao mwaka 2017 wanaanza kuchora mkakati wa kuhamisha watu ilikupisha mradi huu mkubwa lakini baadae kampuni ya kifaransa ya TotalEnergies inanunua hisa hii ya Anadarko kwenye uwekezaji wa gesi hapa Msumbiji kwa dola bilioni 3.

View attachment 3004773

Mradi unakuwa mikononi mwao.

Sasa rasilimali zote hizi ndani ya eneo hili, bado wananchi wanahaha kwa umaskini uliokithiri huku serikali ikiwatupa mkono.

Hapa ndo' Ansar al-sunna wanapopenyeza utambi wao. Wanashawishi watu hawa, na kama ganda la ndizi, wanawachota watu wakitumia mgongo wa imani. Vijana wanajiunga wakiamini hii ni njia sahihi ya kujikwamua.

Kwa lugha tamu ya ushawishi, wanawachota wafuasi na kukua taratibu huku macho yao yakiwa kwenye hizi rasilimali za Cabo Delgado.

Kuanzia kwenye uchumi HALALI wa gesi na madini kama vile Ruby na pia Graphite inayotumika kwenye utengenezaji wa battery za vyombo vya moto na simu za mkononi mpaka kwenye uchumi HARAMU wa pwani unaokua kwa sababu ya uingizwaji wa madawa (heroin) kutoka Asia.

View attachment 3004774

Uchumi huo unakadiriwa kuwa na thamani ya dola za kimarekani milioni mia moja.

View attachment 3004775

Mpenzi msomaji, mpaka kufikia hapa naweza sema haya ya nyuma yanatosha. Hata na hivyo hatuwezi kuyamaliza.

Turudi sasa mwezi July 2021, ambapo jumuiya ya SADC, Tanzania ikiwemo ndani yake, inatuma rasmi jeshi lake linaloungana na jeshi la Rwanda kuwakabili hawa Ansar al-sunna.

View attachment 3004777

Oparesheni hii inaitwa SAMIM (SADC Mission in Mozambique).

Je imefanyikaje na imefikia wapi? Na maslahi ya Rwanda yako wapi katika kuingiza jeshi lake hapa tena kwa miguu yote miwili?

Kwanini South Africa wamejitoa?

Nitakuja na uzi wa mwisho. Thanks.
Ok 👍
 
Alikwenda kutatua tatizo gani hasa huko Msumbiji??
Shida kubwa Sana tuliyonayo sisi Watu weusi ni kwamba huwa hatupendi kabisa kufanya tafiti za kina ili kubaini kiini hasa cha Migogoro ya kibinadamu inayoliandama bara hili la Afrika. Ni lazima tuwe tunafanya utafiti wa kina ili tujue viini au vyanzo halisi vinavyosababisha Migogoro (root cause) ili tuweze kutatua Migogoro hiyo inayotuandama ktk nchi zetu hizi miaka nenda rudi.

Je, Unajua ni kwa Nini huyo mzungu (mkaburu) pamoja na wenzake walikuwepo kwenye eneo hilo lenye machimbo ya gesi huko Jimboni Cabo Delgado nchini Msumbiji wakiwa na silaha za kijeshi ikiwamo na hiyo helikopta ya kijeshi aliyotumia katikà kufanya uokoaji wa hao Watu??? Unazijua sababu???
Tusaidie kw faida ya wengi
 
Back
Top Bottom