Kifalsafa "kimantiki" Yesu hakutolewa Kafara. Dunia imedanganywa

Kifalsafa "kimantiki" Yesu hakutolewa Kafara. Dunia imedanganywa

Kafara ni kupoteza Jambo Fulani lenye thamani mazima. Yaani hutolipata tena. Una umefanya hivyo kwaajili ya Upendo ili upate Jambo zuri au uweka Hali ikae Sawa..
Unapaswa kuelewa vizuri alichofanya Yesu Kristo, na kwanini alifanya hivyo na kwasababu gani kafara au vizuri zaidi SADAKA ya Yesu inasemwa kuwa ilitolewa mara moja tu tofauti na kafara/sadaka nyingine.

Yesu alikufa msalabani ili kuukomboa ulimwengu. Kufa kwa ajili ya kusudio flani na sio kufa kwa uzee au ugonjwa. Manake ni kwamba aliweza kutoa kitu kikubwa zaidi ya kitu kingine, yaani uhai wake mwenyewe. Kwa vile Yesu ni Mwana wa Mungu na asiye na doa lolote, basi sadaka yake ilikuwa ya upeo wa juu kabisa na hakuna mwanadamu anaweza kufikia hata akijitolea kufa kwa ajili ya watu.

Nini kilitokea baada ya Yesu kufa msalabani. Alikwenda kuzimu (himaya ya giza na makao ya shetani). Kutokana na nguvu ya kafara alilolitoa kwa damu yake na uhai wake mwenyewe, aliweza kumnyang'anya shetani zile kamba au funguo alizokuwa anazitumia kuwatesa na kuwaangamiza wanadamu.

Kazi imekwisha au anavyosema mwenyewe; Yametimia au yamekwisha. Alipomaliza kazi hiyo kubwa na akiwa sasa na ameshanunua na kulipia haki zetu kwa damu yake, aliweza sasa kwa uwezo wa Kimungu kurudi na kuonekana katika ulimwengu wa kawaida, lakini sasa akiwa na mwili wa utukufu au hali ya kiroho. Ila kama ni kafara aliitoa na maisha yake hayakuwa tena yale yale ya kale, bali alibadilika kabisa na kwenda kwenye maisha mapya, hata baada ya kufufuka hakuishi tena maisha ya kawaida, ya kale yalikwisha kabisa sio tu kwake bali hata kwa wale aliowatolea maisha yake.
 
kujitoa kafara ni kubeba mzigo wa wengi, ili wao wawe salama, wanaume wamejitoa kafara hata kuingia sehemu hatarishi ili familia zao ziwe salama, Askari wamejitoa kafara kulinda mipakani ili taifa libaki salama

Askari wapo tayari Kujitoa Kafara kwaajili ya kulinda watu na sio kwamba wamejitoa Kafara.

Hujasikia wanajeshi wa Congo huko wanajisalimisha?

Kujitoa Kafara na kuwa tayari Kujitoa Kafara ni mambo mawili tofauti.

Mtu anaweza akawa tayari Kujitoa Kafara lakini siku ya Kafara akakimbia
 
Unapaswa kuelewa vizuri alichofanya Yesu Kristo, na kwanini alifanya hivyo na kwasababu gani kafara au vizuri zaidi SADAKA ya Yesu inasemwa kuwa ilitolewa mara moja tu tofauti na kafara/sadaka nyingine.

Yesu alikufa msalabani ili kuukomboa ulimwengu. Kufa kwa ajili ya kusudio flani na sio kufa kwa uzee au ugonjwa. Manake ni kwamba aliweza kutoa kitu kikubwa zaidi ya kitu kingine, yaani uhai wake mwenyewe. Kwa vile Yesu ni Mwana wa Mungu na asiye na doa lolote, basi sadaka yake ilikuwa ya upeo wa juu kabisa na hakuna mwanadamu anaweza kufikia hata akijitolea kufa kwa ajili ya watu.

Nini kilitokea baada ya Yesu kufa msalabani. Alikwenda kuzimu (himaya ya giza na makao ya shetani). Kutokana na nguvu ya kafara alilolitoa kwa damu yake na uhai wake mwenyewe, aliweza kumnyang'anya shetani zile kamba au funguo alizokuwa anazitumia kuwatesa na kuwaangamiza wanadamu.

Kazi imekwisha au anavyosema mwenyewe; Yametimia au yamekwisha. Alipomaliza kazi hiyo kubwa na akiwa sasa na ameshanunua na kulipia haki zetu kwa damu yake, aliweza sasa kwa uwezo wa Kimungu kurudi na kuonekana katika ulimwengu wa kawaida, lakini sasa akiwa na mwili wa utukufu au hali ya kiroho. Ila kama ni kafara aliitoa na maisha yake hayakuwa tena yale yale ya kale, bali alibadilika kabisa na kwenda kwenye maisha mapya, hata baada ya kufufuka hakuishi tena maisha ya kawaida, ya kale yalikwisha kabisa sio tu kwake bali hata kwa wale aliowatolea maisha yake.

Sasa Mkuu unatoa Kafara kitu Fulani alafu unauhakika utakipata kitu kilekile alichotoa Kafara. Hiyo ni KAFARA kweli?
 
KIFALSAFA "KIMANTIKI" YESU HAKUTOLEWA KAFARA. DUNIA IMEDANGANYWA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Angalizo: Mada hii inaweza isiwafae watu wote hasa watu wale wenye Itikadi na hisia Kali za kidini. Hivyo kama Taikon Master kwa kulijua Hilo, nashauri wewe kama ni wale wenye Itikadi Kali au Imani Kali Basi unaweza kupuuzia Mada hii na kuidharau ukaishia tuu hapahapa. Kuendelea kusoma itahesabika kutumia Uhuru wako kuchagua Jambo litakaloweza kukuumiza . Hivyo maumivu hayo Mimi sitahusishwa.

Tuendelee.
Tangu tukiwa watoto Wakristo tumekuwa tukifundishwa kuwa Yesu Kristo alikufa kwaajili yetu, alitolewa Kafara ili binadamu Wapate uzima na sio uzima tuu Bali uzima wa MILELE.

Yohana anatuambia hivi:
Yohana 3:16
16 “Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Aya nyingi ndani ya Biblia hasa katika vitabu vya Injili vinaeleza kuwa Yesu Kristo alikuwa ni Kafara kwaajili ya ondoleo la dhambi za wanadamu.

Waandishi wa Biblia wamejitahidi Sana kumpa Uhusika wa ajabu Yesu na kubwa zaidi ni Hilo la Kujitoa Kafara, Kufa kwaajili ya wanadamu.
Na mwisho Kabisa Kufufuka katika Wafu.

Mimi sina tatizo na Yesu Kujitoa Au kutolewa Kafara kwa Sababu wapo watu wengi waliojitoa Kafara na hata hivi Leo wapo watu wanaojitoa Kafara kwaajili ya Familia Zao na mataifa Yao.

Akili yangu inaanza Kupata shida pale ambapo Mtolewa Kafara amefufuka.

Tukio la Kufufuka kwa Yesu kama ilivyoripotiwa katika vitabu vya Injili ndilo linaloondoa dhana zima ya KAFARA ya Yesu Kristo.

Ili kitu au Jambo lisemwe limetolewa Kafara lazima lipotee na lisipatikane Tena na hakuna namna nyingine ya kulirejesha tena Jambo hilo.

Kafara ni kutoa na kupoteza Jambo la thamani Sana ili mtu apate Jambo jingine la muhimu au la thamani zaidi.
Mfano mtu anaweza kutoa Kafara Muda wake ili apate Jambo Fulani.
Kafara iliyotolewa haiwezi kurudi.

Kafara za uhai.
Unakuta mtu anatoa uhai wake kwaajili ya Familia au taifa lake. Uhai uliotolewa hauwezi kurudishwa tena. Hiyo inaitwa Kafara.

Kafara inayoweza kurudishwa haiitwi KAFARA inaweza kupewa jina jingine.

Kuna visa vya watu waliowatoa Kafara wazazi au watoto wao ili wajipatie Utajiri au vyeo. Hizo ni Kafara na zile Kafara haziwezi kurudi kamwe. Unapomtoa mzazi au mtoto Kafara haitarajiwi na haiwezekani mtoto au mzazi huyo kurudi tena. Yaani ndio umempoteza hivyo ili wewe upate utajiri au cheo Fulani. Hiyo ni KAFARA.

Tukirejea kwenye Kafara na dhabihu za wakati wa Musa. Wanyama waliokuwa wakitolewa Kafara au dhabihu ndio ilikuwa ntolee hiyo. Huwezi kumrudisha kondoo au mbuzi aliyejinjwa kwaajili ya Kafara.

Yesu alipokufa na kusulubishwa kwaajili ya wenye dhambi kama ilivyoripotiwa kwenye Injili. Ingekuwa Kafara kama angekufa Moja Kwa Moja bila ya Kufufuka tena.
Hiyo kwa kweli ingestahili kuitwa KAFARA.
Kwa sababu hapo itahesabika ni kweli kama Yesu ni mwana kipenzi cha Mungu kama alivyoripotiwa alitolewa Kafara na habari yake iliishia hapo.
Ingekuwa ni rekodi ya kueleweka kimantiki.

Lakini kusema Yesu alijitoa Kafara kwaajili yetu huku akijua atafufuka au kufufuliwa ni kinyume na MSINGI wa KAFARA. Hiyo haiwezi kuitwa KAFARA.
Huo ni utapeli, ujanjaujanja ambao hata kwenye siasa za wanadamu tunaziona kila siku.

Kwenye siasa za ulaghai ni Jambo la kawaida kiongozi Fulani kutolewa Kafara na viongozi wenzake au Kujitoa Kafara kwaajili ya viongozi wenzake kwa Nje watu wanamuona alitolewa au kujitoa Kafara lakini kwa ndani kumbe ni drama, igizo ambalo watu wamepanga kumtoa au ajitoe kafara alafu baada ya muda fulani watampa cheo kingine. Au kumhamisha sehemu nyingine ya Kazi.
Au awe hafanyi Kazi lakini yupo kwenye payroll ya serikali. Huo ni utapeli, ujanjaujanja.

Kama Yesu alijua atafufuliwa au atafufuka haikuwa na maana ya Yeye kusema atajitoa uhai au mungu amemtoa mwanaume mpendwa ampendaye kwaajili ya wanadamu wakati huohuo hakumtoa Bali alimfufua na alipaa kukaa Mkono WA kuume wa Babaye.

Hivi kuna Kafara ya namna hiyo kweli?
Kafara ni kupoteza Jambo Fulani lenye thamani mazima. Yaani hutolipata tena. Una umefanya hivyo kwaajili ya Upendo ili upate Jambo zuri au uweka Hali ikae Sawa..

Mtu anakuambia Yesu katolewa Kafara au alikufa kwaajili yake alafu Muda huohuo anakuambia yupo mbinguni. Huo kama sio Mchezo wa kuchezeana akili ni kitu gani?

Yaani mtu upate uchungu wa Mtu aliyejitoa Kafara ambaye alijua atafufuka😂😂 Kweli.

Kwa minajili hiyo ni aidha Yesu alisulubishwa akafa na hakufufuka. Ili iitwe Kafara na ndio hayupo Mbinguni.
Au Yesu hakufa msalabani ila alipalizwa kama baadhi ya maandiko yanavyoripoti ikiwemo Quran.

Kwa sababu kama alifufuka Basi haikuwa Kafara.

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam

Pongezi kwa maoni yako. Lakini haimaanishi kwamba yako sahihi. Ingawa binafsi nayaheshimu
 
Hayo uliyoeleza yapo Sawa.

Tuseme Yesu ni Mungu kwa MUKTADHA WA Biblia.
Je Mungu hakumtoa Yesu Kafara? Yaani hakumpoteza Yesu kwaajili ya wanadamu?

Unajua maana ya Kafara lakini?
Au ukisikia mtu katolewa Kafara au katoa Kafara kitu au Jambo Fulani nini kinakuja kwenye Akili yako?

Kama Mungu hawezi kufa, kwa nini imeandikwa Yesu alikufa kwaajili yetu? Unamanisha hakufa?
Kwamba alidanganya?

Ikiwa Kufa kwaajili yetu ilikuwa ndio Kafara. Umuhimu wa Kafara hiyo unatoka wapi ikiwa Yesu yu hai(Yule aliyetolewa Kafara)

Ibrahim alitaka Kumtoa Isaka Kafara. Yaani kumpoteza Isaka kwaajili ya Kumpenda Mungu.
Lakini hakumtoa Kafara Isaka. Kwa sababu hakumpoteza
Nimekuelewa ila Kwa mujibu wa biblia na yohana 1---,yesu(huyo tunayemuongelea) ni muunganiko wa vitu vitatu=Mungu,Roho na Binadamu,Kwa kuwa lengo ni kumkomboa binadamu basi kilichokufa hapo ni huo ubinadamu,kilichobaki Kwa huyo yesu ni Mungu na Roho ndo vilivyofufuka basi.
 
KIFALSAFA "KIMANTIKI" YESU HAKUTOLEWA KAFARA. DUNIA IMEDANGANYWA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Angalizo: Mada hii inaweza isiwafae watu wote hasa watu wale wenye Itikadi na hisia Kali za kidini. Hivyo kama Taikon Master kwa kulijua Hilo, nashauri wewe kama ni wale wenye Itikadi Kali au Imani Kali Basi unaweza kupuuzia Mada hii na kuidharau ukaishia tuu hapahapa. Kuendelea kusoma itahesabika kutumia Uhuru wako kuchagua Jambo litakaloweza kukuumiza . Hivyo maumivu hayo Mimi sitahusishwa.

Tuendelee.
Tangu tukiwa watoto Wakristo tumekuwa tukifundishwa kuwa Yesu Kristo alikufa kwaajili yetu, alitolewa Kafara ili binadamu Wapate uzima na sio uzima tuu Bali uzima wa MILELE.

Yohana anatuambia hivi:
Yohana 3:16
16 “Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Aya nyingi ndani ya Biblia hasa katika vitabu vya Injili vinaeleza kuwa Yesu Kristo alikuwa ni Kafara kwaajili ya ondoleo la dhambi za wanadamu.

Waandishi wa Biblia wamejitahidi Sana kumpa Uhusika wa ajabu Yesu na kubwa zaidi ni Hilo la Kujitoa Kafara, Kufa kwaajili ya wanadamu.
Na mwisho Kabisa Kufufuka katika Wafu.

Mimi sina tatizo na Yesu Kujitoa Au kutolewa Kafara kwa Sababu wapo watu wengi waliojitoa Kafara na hata hivi Leo wapo watu wanaojitoa Kafara kwaajili ya Familia Zao na mataifa Yao.

Akili yangu inaanza Kupata shida pale ambapo Mtolewa Kafara amefufuka.

Tukio la Kufufuka kwa Yesu kama ilivyoripotiwa katika vitabu vya Injili ndilo linaloondoa dhana zima ya KAFARA ya Yesu Kristo.

Ili kitu au Jambo lisemwe limetolewa Kafara lazima lipotee na lisipatikane Tena na hakuna namna nyingine ya kulirejesha tena Jambo hilo.

Kafara ni kutoa na kupoteza Jambo la thamani Sana ili mtu apate Jambo jingine la muhimu au la thamani zaidi.
Mfano mtu anaweza kutoa Kafara Muda wake ili apate Jambo Fulani.
Kafara iliyotolewa haiwezi kurudi.

Kafara za uhai.
Unakuta mtu anatoa uhai wake kwaajili ya Familia au taifa lake. Uhai uliotolewa hauwezi kurudishwa tena. Hiyo inaitwa Kafara.

Kafara inayoweza kurudishwa haiitwi KAFARA inaweza kupewa jina jingine.

Kuna visa vya watu waliowatoa Kafara wazazi au watoto wao ili wajipatie Utajiri au vyeo. Hizo ni Kafara na zile Kafara haziwezi kurudi kamwe. Unapomtoa mzazi au mtoto Kafara haitarajiwi na haiwezekani mtoto au mzazi huyo kurudi tena. Yaani ndio umempoteza hivyo ili wewe upate utajiri au cheo Fulani. Hiyo ni KAFARA.

Tukirejea kwenye Kafara na dhabihu za wakati wa Musa. Wanyama waliokuwa wakitolewa Kafara au dhabihu ndio ilikuwa ntolee hiyo. Huwezi kumrudisha kondoo au mbuzi aliyejinjwa kwaajili ya Kafara.

Yesu alipokufa na kusulubishwa kwaajili ya wenye dhambi kama ilivyoripotiwa kwenye Injili. Ingekuwa Kafara kama angekufa Moja Kwa Moja bila ya Kufufuka tena.
Hiyo kwa kweli ingestahili kuitwa KAFARA.
Kwa sababu hapo itahesabika ni kweli kama Yesu ni mwana kipenzi cha Mungu kama alivyoripotiwa alitolewa Kafara na habari yake iliishia hapo.
Ingekuwa ni rekodi ya kueleweka kimantiki.

Lakini kusema Yesu alijitoa Kafara kwaajili yetu huku akijua atafufuka au kufufuliwa ni kinyume na MSINGI wa KAFARA. Hiyo haiwezi kuitwa KAFARA.
Huo ni utapeli, ujanjaujanja ambao hata kwenye siasa za wanadamu tunaziona kila siku.

Kwenye siasa za ulaghai ni Jambo la kawaida kiongozi Fulani kutolewa Kafara na viongozi wenzake au Kujitoa Kafara kwaajili ya viongozi wenzake kwa Nje watu wanamuona alitolewa au kujitoa Kafara lakini kwa ndani kumbe ni drama, igizo ambalo watu wamepanga kumtoa au ajitoe kafara alafu baada ya muda fulani watampa cheo kingine. Au kumhamisha sehemu nyingine ya Kazi.
Au awe hafanyi Kazi lakini yupo kwenye payroll ya serikali. Huo ni utapeli, ujanjaujanja.

Kama Yesu alijua atafufuliwa au atafufuka haikuwa na maana ya Yeye kusema atajitoa uhai au mungu amemtoa mwanaume mpendwa ampendaye kwaajili ya wanadamu wakati huohuo hakumtoa Bali alimfufua na alipaa kukaa Mkono WA kuume wa Babaye.

Hivi kuna Kafara ya namna hiyo kweli?
Kafara ni kupoteza Jambo Fulani lenye thamani mazima. Yaani hutolipata tena. Una umefanya hivyo kwaajili ya Upendo ili upate Jambo zuri au uweka Hali ikae Sawa..

Mtu anakuambia Yesu katolewa Kafara au alikufa kwaajili yake alafu Muda huohuo anakuambia yupo mbinguni. Huo kama sio Mchezo wa kuchezeana akili ni kitu gani?

Yaani mtu upate uchungu wa Mtu aliyejitoa Kafara ambaye alijua atafufuka😂😂 Kweli.

Kwa minajili hiyo ni aidha Yesu alisulubishwa akafa na hakufufuka. Ili iitwe Kafara na ndio hayupo Mbinguni.
Au Yesu hakufa msalabani ila alipalizwa kama baadhi ya maandiko yanavyoripoti ikiwemo Quran.

Kwa sababu kama alifufuka Basi haikuwa Kafara.

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Sijadoma yote ila kati ya uongo mkubwa wazungu wamefanikiwa kutuhadaa, na wanapiga hela ndefu sana bila hustle ni dini. Dini zote duniani zimeanzishwa na wao na makao makuu yapo kwenye nchi husika. Na sadaka na zaka zote zinaenda kwao, yesu manabii sijui kina nani nikama kina mkandamizaji wanavyotufanyia leo, miaka 500 mbele utasikia kina zumaridi wanasomwa kweny bibilia ya wakati huo
 
Unapaswa kuelewa vizuri alichofanya Yesu Kristo, na kwanini alifanya hivyo na kwasababu gani kafara au vizuri zaidi SADAKA ya Yesu inasemwa kuwa ilitolewa mara moja tu tofauti na kafara/sadaka nyingine.

Yesu alikufa msalabani ili kuukomboa ulimwengu. Kufa kwa ajili ya kusudio flani na sio kufa kwa uzee au ugonjwa. Manake ni kwamba aliweza kutoa kitu kikubwa zaidi ya kitu kingine, yaani uhai wake mwenyewe. Kwa vile Yesu ni Mwana wa Mungu na asiye na doa lolote, basi sadaka yake ilikuwa ya upeo wa juu kabisa na hakuna mwanadamu anaweza kufikia hata akijitolea kufa kwa ajili ya watu.

Nini kilitokea baada ya Yesu kufa msalabani. Alikwenda kuzimu (himaya ya giza na makao ya shetani). Kutokana na nguvu ya kafara alilolitoa kwa damu yake na uhai wake mwenyewe, aliweza kumnyang'anya shetani zile kamba au funguo alizokuwa anazitumia kuwatesa na kuwaangamiza wanadamu.

Kazi imekwisha au anavyosema mwenyewe; Yametimia au yamekwisha. Alipomaliza kazi hiyo kubwa na akiwa sasa na ameshanunua na kulipia haki zetu kwa damu yake, aliweza sasa kwa uwezo wa Kimungu kurudi na kuonekana katika ulimwengu wa kawaida, lakini sasa akiwa na mwili wa utukufu au hali ya kiroho. Ila kama ni kafara aliitoa na maisha yake hayakuwa tena yale yale ya kale, bali alibadilika kabisa na kwenda kwenye maisha mapya, hata baada ya kufufuka hakuishi tena maisha ya kawaida, ya kale yalikwisha kabisa sio tu kwake bali hata kwa wale aliowatolea maisha yake.
Qyesu aliuawa kwa sababu alienda kinyume na mafundisho ya kiyahudi, wala hakufia mtu yeyote
 
Leta hoja acha taarabu kama za ccm
Siwezi kukupa hoja yoyote wewe ambaye umekaririshwa ujinga wa Madrassa na ukanielewa.. Umefundishwa kupinga ufufuko wa Yesu na ndio msingi wa Imani yako.. Sasa hivi mimi ntakupa hoja gani unielewe.. Ila narudia Tena.. Habari za Yesu ni bora mkaachana nazo tu kwa sababu hamumuwezi huyo.. Na hata mkileta mawazo yenu na mafundisho yenu hayatabadili ukweli kuwa Yesu ndio njia Ukweli na Uzima.. Na kwake Kila goti litapigwa..
 
1 Wakorintho 15:55-57 – Ewe mauti, u wapi ushindi wako? Ewe mauti, u wapi uchungu wako? Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati. Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Lile tukio la Yesu lilibeba mambo mawili kwa wakati mmoja kwa maana ya kifo chake kilikuwa dhabihu ya upatanisho, na ufufuo wake ulikuwa uthibitisho wa ushindi wake dhidi ya mauti na dhambi.

Kitendo tu cha kumwaga damu tayari ni dhabihu hiyo ila kifo ni unyang'anyi wa yale yote ambayo yalikua yanamilikiwa na kile kilichotolewa kafara vibaki kwa mwenye kuifanya hiyo kafara (umiliki kamili).

Na ukiangalia Yesu alifanya hivyo kwa maana ya kufa pia alikufa kwahiyo hii tayari inamaanisha ule umiliki kamili ulipatikana kwa maana hata kafara ambazo umezizungumzia wewe hapo juu ni mauaji ya lazima na si ya kihatima kwahiyo Kila kafara iliyowahi kutolewa huwa inakufa tena baada ya ule muda wa hatima ya kifo chake kufikia na wakati huu unapofikia ile kafara iliyofanyika huwa inapoteza nguvu kwa maana ile mitetemo ya aliyetolewa kafara inakua tayari imeshafutwa kwenye ulimwengu(hapa ili uelewe vizuri chukulia mfano wa unapofuta file kwenye laptop yako, linaelekea kwenye recycle bin, ni kwamba halionekani pale ambapo lilikuwepo lakini lipo na kama recycle bin ingekua inahifadhi hizo files kwa muda fulani na baadae ile automatic deletion inatokea permanently basi ingekua ni sawa na asili ya kafara).

Kwahiyo Yesu angekufa tu bila kufufuka basi upatanisho pekee ndio ungekua umetimilizwa ila ule ushindi kamili dhidi ya dhambi na mauti ungekosekana, lakini pia hata kafara yake isingekua ya milele kwa maana kuna nyakati ile mitetemo yake ingefutwa kwenye uso wa Dunia ila kile kitendo cha ufufuo kinamaanisha ile mitetemo yake ipo na itaendelea kuwepo siku zote na hii ndio maana halisi ya ondoleo la dhambi na uzima wa milele.

All in all kifo na ufufuo wa Yesu ni moja ya mafumbo makuu yaliyomo ndani ya biblia, na hata kuzaliwa kwake pia ni fimbo lakini pia ni majibu ya maswali mengi ya agano la kale hasa kile kitabu cha Mwanzo.

Ndio maana Mimi huwa nawaambia watu ya kwamba biblia yote imeishia mwanzo moja hadi sita.

NB: kitendo cha kutumika kwaajiri ya hatima ya mtu au watu wengine kwa namna ya kafara au namna nyingine yoyote yenye kutia upofu upande wako wa kiroho kiasi cha kukufanya ushindwe kutimiza hatima yako ya kiMungu iliyofanya uwe hapa duniani huo tayari ni udhaifu na wala hakuna uhuisho kwa watu wadhaifu, na njia ya kuifanya mitetemo ya mtu fulani iendelee kubaki duniani ni uhuisho, kwahiyo Yesu alijiondoa kwenye huu mtego ili akupe wokovu kamili na wamilele.

Umefafanua vizuri sana.
Robert Heriel Mtibeli una la kujifunza hapa.
 
Askari wapo tayari Kujitoa Kafara kwaajili ya kulinda watu na sio kwamba wamejitoa Kafara.

Hujasikia wanajeshi wa Congo huko wanajisalimisha?

Kujitoa Kafara na kuwa tayari Kujitoa Kafara ni mambo mawili tofauti.

Mtu anaweza akawa tayari Kujitoa Kafara lakini siku ya Kafara akakimbia
kwani unafikiri kafara ya Yesu ilitakiwa kufanyika vipi? je unaamini kafara inafanyika juu ya mwili na sio roho?
 
1 Wakorintho 15:55-57 – Ewe mauti, u wapi ushindi wako? Ewe mauti, u wapi uchungu wako? Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati. Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Lile tukio la Yesu lilibeba mambo mawili kwa wakati mmoja kwa maana ya kifo chake kilikuwa dhabihu ya upatanisho, na ufufuo wake ulikuwa uthibitisho wa ushindi wake dhidi ya mauti na dhambi.

Kitendo tu cha kumwaga damu tayari ni dhabihu hiyo ila kifo ni unyang'anyi wa yale yote ambayo yalikua yanamilikiwa na kile kilichotolewa kafara vibaki kwa mwenye kuifanya hiyo kafara (umiliki kamili).

Na ukiangalia Yesu alifanya hivyo kwa maana ya kufa pia alikufa kwahiyo hii tayari inamaanisha ule umiliki kamili ulipatikana kwa maana hata kafara ambazo umezizungumzia wewe hapo juu ni mauaji ya lazima na si ya kihatima kwahiyo Kila kafara iliyowahi kutolewa huwa inakufa tena baada ya ule muda wa hatima ya kifo chake kufikia na wakati huu unapofikia ile kafara iliyofanyika huwa inapoteza nguvu kwa maana ile mitetemo ya aliyetolewa kafara inakua tayari imeshafutwa kwenye ulimwengu(hapa ili uelewe vizuri chukulia mfano wa unapofuta file kwenye laptop yako, linaelekea kwenye recycle bin, ni kwamba halionekani pale ambapo lilikuwepo lakini lipo na kama recycle bin ingekua inahifadhi hizo files kwa muda fulani na baadae ile automatic deletion inatokea permanently basi ingekua ni sawa na asili ya kafara).

Kwahiyo Yesu angekufa tu bila kufufuka basi upatanisho pekee ndio ungekua umetimilizwa ila ule ushindi kamili dhidi ya dhambi na mauti ungekosekana, lakini pia hata kafara yake isingekua ya milele kwa maana kuna nyakati ile mitetemo yake ingefutwa kwenye uso wa Dunia ila kile kitendo cha ufufuo kinamaanisha ile mitetemo yake ipo na itaendelea kuwepo siku zote na hii ndio maana halisi ya ondoleo la dhambi na uzima wa milele.

All in all kifo na ufufuo wa Yesu ni moja ya mafumbo makuu yaliyomo ndani ya biblia, na hata kuzaliwa kwake pia ni fimbo lakini pia ni majibu ya maswali mengi ya agano la kale hasa kile kitabu cha Mwanzo.

Ndio maana Mimi huwa nawaambia watu ya kwamba biblia yote imeishia mwanzo moja hadi sita.

NB: kitendo cha kutumika kwaajiri ya hatima ya mtu au watu wengine kwa namna ya kafara au namna nyingine yoyote yenye kutia upofu upande wako wa kiroho kiasi cha kukufanya ushindwe kutimiza hatima yako ya kiMungu iliyofanya uwe hapa duniani huo tayari ni udhaifu na wala hakuna uhuisho kwa watu wadhaifu, na njia ya kuifanya mitetemo ya mtu fulani iendelee kubaki duniani ni uhuisho, kwahiyo Yesu alijiondoa kwenye huu mtego ili akupe wokovu kamili na wamilele.
Ubarikiwe sana
 
KIFALSAFA "KIMANTIKI" YESU HAKUTOLEWA KAFARA. DUNIA IMEDANGANYWA.

Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli

Angalizo: Mada hii inaweza isiwafae watu wote hasa watu wale wenye Itikadi na hisia Kali za kidini. Hivyo kama Taikon Master kwa kulijua Hilo, nashauri wewe kama ni wale wenye Itikadi Kali au Imani Kali Basi unaweza kupuuzia Mada hii na kuidharau ukaishia tuu hapahapa. Kuendelea kusoma itahesabika kutumia Uhuru wako kuchagua Jambo litakaloweza kukuumiza . Hivyo maumivu hayo Mimi sitahusishwa.

Tuendelee.
Tangu tukiwa watoto Wakristo tumekuwa tukifundishwa kuwa Yesu Kristo alikufa kwaajili yetu, alitolewa Kafara ili binadamu Wapate uzima na sio uzima tuu Bali uzima wa MILELE.

Yohana anatuambia hivi:
Yohana 3:16
16 “Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu kiasi cha kumtoa Mwanae pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.

Aya nyingi ndani ya Biblia hasa katika vitabu vya Injili vinaeleza kuwa Yesu Kristo alikuwa ni Kafara kwaajili ya ondoleo la dhambi za wanadamu.

Waandishi wa Biblia wamejitahidi Sana kumpa Uhusika wa ajabu Yesu na kubwa zaidi ni Hilo la Kujitoa Kafara, Kufa kwaajili ya wanadamu.
Na mwisho Kabisa Kufufuka katika Wafu.

Mimi sina tatizo na Yesu Kujitoa Au kutolewa Kafara kwa Sababu wapo watu wengi waliojitoa Kafara na hata hivi Leo wapo watu wanaojitoa Kafara kwaajili ya Familia Zao na mataifa Yao.

Akili yangu inaanza Kupata shida pale ambapo Mtolewa Kafara amefufuka.

Tukio la Kufufuka kwa Yesu kama ilivyoripotiwa katika vitabu vya Injili ndilo linaloondoa dhana zima ya KAFARA ya Yesu Kristo.

Ili kitu au Jambo lisemwe limetolewa Kafara lazima lipotee na lisipatikane Tena na hakuna namna nyingine ya kulirejesha tena Jambo hilo.

Kafara ni kutoa na kupoteza Jambo la thamani Sana ili mtu apate Jambo jingine la muhimu au la thamani zaidi.
Mfano mtu anaweza kutoa Kafara Muda wake ili apate Jambo Fulani.
Kafara iliyotolewa haiwezi kurudi.

Kafara za uhai.
Unakuta mtu anatoa uhai wake kwaajili ya Familia au taifa lake. Uhai uliotolewa hauwezi kurudishwa tena. Hiyo inaitwa Kafara.

Kafara inayoweza kurudishwa haiitwi KAFARA inaweza kupewa jina jingine.

Kuna visa vya watu waliowatoa Kafara wazazi au watoto wao ili wajipatie Utajiri au vyeo. Hizo ni Kafara na zile Kafara haziwezi kurudi kamwe. Unapomtoa mzazi au mtoto Kafara haitarajiwi na haiwezekani mtoto au mzazi huyo kurudi tena. Yaani ndio umempoteza hivyo ili wewe upate utajiri au cheo Fulani. Hiyo ni KAFARA.

Tukirejea kwenye Kafara na dhabihu za wakati wa Musa. Wanyama waliokuwa wakitolewa Kafara au dhabihu ndio ilikuwa ntolee hiyo. Huwezi kumrudisha kondoo au mbuzi aliyejinjwa kwaajili ya Kafara.

Yesu alipokufa na kusulubishwa kwaajili ya wenye dhambi kama ilivyoripotiwa kwenye Injili. Ingekuwa Kafara kama angekufa Moja Kwa Moja bila ya Kufufuka tena.
Hiyo kwa kweli ingestahili kuitwa KAFARA.
Kwa sababu hapo itahesabika ni kweli kama Yesu ni mwana kipenzi cha Mungu kama alivyoripotiwa alitolewa Kafara na habari yake iliishia hapo.
Ingekuwa ni rekodi ya kueleweka kimantiki.

Lakini kusema Yesu alijitoa Kafara kwaajili yetu huku akijua atafufuka au kufufuliwa ni kinyume na MSINGI wa KAFARA. Hiyo haiwezi kuitwa KAFARA.
Huo ni utapeli, ujanjaujanja ambao hata kwenye siasa za wanadamu tunaziona kila siku.

Kwenye siasa za ulaghai ni Jambo la kawaida kiongozi Fulani kutolewa Kafara na viongozi wenzake au Kujitoa Kafara kwaajili ya viongozi wenzake kwa Nje watu wanamuona alitolewa au kujitoa Kafara lakini kwa ndani kumbe ni drama, igizo ambalo watu wamepanga kumtoa au ajitoe kafara alafu baada ya muda fulani watampa cheo kingine. Au kumhamisha sehemu nyingine ya Kazi.
Au awe hafanyi Kazi lakini yupo kwenye payroll ya serikali. Huo ni utapeli, ujanjaujanja.

Kama Yesu alijua atafufuliwa au atafufuka haikuwa na maana ya Yeye kusema atajitoa uhai au mungu amemtoa mwanaume mpendwa ampendaye kwaajili ya wanadamu wakati huohuo hakumtoa Bali alimfufua na alipaa kukaa Mkono WA kuume wa Babaye.

Hivi kuna Kafara ya namna hiyo kweli?
Kafara ni kupoteza Jambo Fulani lenye thamani mazima. Yaani hutolipata tena. Una umefanya hivyo kwaajili ya Upendo ili upate Jambo zuri au uweka Hali ikae Sawa..

Mtu anakuambia Yesu katolewa Kafara au alikufa kwaajili yake alafu Muda huohuo anakuambia yupo mbinguni. Huo kama sio Mchezo wa kuchezeana akili ni kitu gani?

Yaani mtu upate uchungu wa Mtu aliyejitoa Kafara ambaye alijua atafufuka😂😂 Kweli.

Kwa minajili hiyo ni aidha Yesu alisulubishwa akafa na hakufufuka. Ili iitwe Kafara na ndio hayupo Mbinguni.
Au Yesu hakufa msalabani ila alipalizwa kama baadhi ya maandiko yanavyoripoti ikiwemo Quran.

Kwa sababu kama alifufuka Basi haikuwa Kafara.

Robert Heriel
Taikon Master
Kwa sasa Dar es salaam
Afadhali wavaa kobazi wao wanajua mtu wao alikufa wala hakufufuka na hatakaa afufuke wala hakupaa mbinguni amezikwa kama wengine na kaburi lake lipo hadi leo linaitwa alkaaba ila wanaamini siku ya kiama watakutana naye huko atakusanya umati wake.
 
Back
Top Bottom