Tanzania ni nchi inayofuata Utawala wa Sheria, ni Nchi ya kidemokrasia, Viongozi wetu wana amini katika haki na usawa.
Kuna matukio yanatokea, yanaumiza saana, yanasikitisha saana, tukio la kuuwawa kikatili kwa mtoto Asimwe Novart tena mhusika akiwa ni baba mzazi ambaye alipaswa kuwa mlinzi wa huyu Malaika, kea kweli kuna muda unatamani Sheria ziwekwe pembeni na maumivu aliyopitia huyu mtoto wapitie hao wote waliohusika kukatisha uhai wa huyu Malaika.
Fikiria wakati Asimwe Novart akiwa anahitaji msaada mbele ya Wanaume katili, hakuweza hata kujitetea zaidi ya macho ya huruma alionyesha kuomba huruma kwa Wanaume hawa katili, Alihitaji upendo wa baba, lakini baba alimuangamiza.
Inauma, inaumiza kuona hawa watu waliotenda unyama huu, kwa sababu ya Tanzania kuwa nchi ya Utawala wa Sheria wanapelekwa mahakamani tena kwa gari, Kuna muda unatamani ungekuwa na whisk ushudie ule ukatili waliotenda wakitendewa wao waexperience maumivu aliyopitia Asimwe Novart.
Pumzika kwa Amani Asimwe Novart
Mwenyezi Mungu ibariki Tanzania
Mwenyezi Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan