Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Acheni unafiki wenu hapa Mbowe ameongea kama mwenyekiti wa CHADEMA na aliyosema ni sahihi, kama nyie mna jipya wekeni hapa tusome sio kuwa vibaraka na makuwadi wa MAFISADI tu.
Mlitaka amsifu Kikwete kwa kwenda Japan?

Unajua huwezi kusema kama unavyosema ikiwa unajua nini kinahitajika,sio watu wanachukia ya akina Mbowe na Zitto na wenzao lakini ,kilicho muhimu ni mhimili wa hayo wanayoyasema huwa haupo ,wameyasema ya Richmond ,EPA,Buzwagi na kila siku wanakuja na jipya ,sasa nini faida ya haya kwani yanaonekana yako mengi kuliko yaliokuwa tayari yameibuliwa ,naweza kusema hizi walizonazo na walizowahi kuziibua ni silaha nzito lakini wakizitumia vibaya haziotawasaidia kitu mfano hai ni wa majeshi ya Saddam Husein walikuwa na silaha nyingi na za kisasa lakini hazikuwafaa kitu walibaki kujisifu kwenye vyombo vya habari piga tajame ,wamepigwa na silaha zao,hivyo wapinzani wataendelea kushindwa mbali ya masiri makubwa makubwa waliyonayo kuhusiana na CCM.
Huyo Balai Lama walimuibua wao na mascandali kibao ,angalia sasa maneno kutoka kwa watu wa Balali yanazidi kusema kuwa Balali hakutafuna kitu wala hahusiki na kasheshe za wizi inamaana wapinzani wanaaza kupelekwa kkwenye kona itawabidi wamtafute tena nani anahusika na mwisho itaonekana hawana msimamo kwani wanabadilika badilika kila wanaemkamata wanaambiwa sie.
Akina Lowasa wote na wenzake wamesema wameonewa inamaana kamati za kina Zitto zitatoka na majina ya watu wengine ambao wanajulikana kama kafara na ambao huishia kwenye kujiuzulu tu ,ili kuwasafisha CCM na walio ndani ya Inner circle .
Nini faida ya kumkamata fisadi ,badala ya wakwasi hawa kuibuka kwenye majukwaa kwa nini hawaendi na vielelezo vyao mahakamani na kuwashitaki mafisadi na badala yake kungojea CCM iwawajibishe hamuoni kama CCM wana hiari yao na huu ni woga wa Kikwete tu moja kwa moja angelisema mwenye ushaidi aende nao mahakamani akafungue jalada ,sio kutushutumia viongozi wetu.Tumewachagua kwa kutumia vigezo vya utendaji wao wa kazi kama mnawaona ni mafisadi na muna ushahidi wa kutosha basi elekeeni kwenye vyombo vya sheria na washitakini kama wahujumu uchumi.
Kikwete wacha kuwawajibisha viongozi na wenzako ,usiwe wewe kuwa mwenye kuwashauri waachie ngazi kwani kwa kufanya hivyo utawamaliza wote na kila siku watakuzushiya mwengine.
Akina Kabwela ,Slaa ,Kabwe wote hawa wanafahamu sheria kwa kiasi chao ikiwa wamekuwa mabingwa wa kupeleleza na kupata ushahidi basi waelekee mahakamni huko ndiko watakakokwenda kutetea ,sio kutuchafulia nchi na kutufanya tupoteze muelekeo.
 
Mwiba

Sasa wewe umefanya nini hebu twambie?
 
Mkuu ni afadhali ya kusema angalau something kuliko kunyamaza kabisa, kila kitu kina mwanzo wake hayo yote unayoyasema yanakuja, kwa sababu kumbuka waliyoyafanya haya tuliyonayo sasa ya ufisadi, walikuwa kama wewe, hawakutegmea yatakuja kubumburuka mbele ya safari,

The dataz ni kwamba majuzi Mkapa alikuwa Adis, wenyeji wake wakamletea Radio ndogo ili aweze kusikiliza Radio Tanzania, na hasa taarifa ya habari, akawafukuza nayo na kudai kuwa huwa haisikilizi maana imejaa udaku na ujinga! Huku akifoka alisema hata akiwa Tanzania huwa haisikilizi,

Sasa wewe unasema eti kina Freeman wasiseme? Unafikiri kwa nini huyu Mkapa anaigopa Radio ya nchi yake aliyowahi kuwa rais wake, hivi unafikiri kuna siku hata moja Mwalimu aliikimbia Radio Tanzania?

Mkuu Dua Bravo!
 
basi mbowe si aseme tu anachojua kuliko kusema mkono wa vigogo (awataje) !! hata kama anawasuspect ! otherwise nachukulia maneno yake kama politics ! yeye pia si alivunjika mguu wiki iliyopita, au kulikuwa na mkono wa vigogo ?

Ndiyo tatizo lako wewe la kutaka kutetea hata visivyostahili kutetewa. Kifo cha Ballali kina utata mwingi sana hasa ukichukulia jinsi alivyoondoka nchini mpaka alipofariki. Inakuwaje mtu aliyewahi kushika nafasi za juu serikalini afariki dunia lakini Watanzania watangaziwe baada ya siku tano tangu kifo kitokee tena kwa kupitia gazeti binafsi? Sirikali ilifahamishwa lini kuhusu kifo cha Ballali na ni nani aliyewahamisha na kwanini waliamua kukaa kimya baada ya kufahamishwa juu ya kifo hicho? Inakuwaje mtu mkubwa kama Ballali azikwe nje ya nchi.

JK amesema kifo cha Ballali ni kazi ya Mungu, lakini bila kufafanua zaidi. Usiri mkubwa juu ya Ballali tangu alipoondoka na kama siri kali ilikuwa inajua amelazwa hospitali ipi na alikuwa anaumwa nini na kwa nini sirikali haikuweka jitihada za kumuhoji akiwa hospitalini ndizo zinazua speculation chungu nzima. Na waswahili husema, panapofuka moshi.....
 
N

JK amesema kifo cha Ballali ni kazi ya Mungu, lakini bila kufafanua zaidi. Usiri mkubwa juu ya Ballali tangu alipoondoka na kama siri kali ilikuwa inajua amelazwa hospitali ipi na alikuwa anaumwa nini na kwa nini sirikali haikuweka jitihada za kumuhoji akiwa hospitalini ndizo zinazua speculation chungu nzima. Na waswahili husema, panapofuka moshi.....

Wana JF naomba mnielimishe kitu kimoja. Kwa mtu aliyefukuzwa kazi serikalini akiwa mgonjwa mahututi katika nchi ya kigeni, kulikuwa na haja gani ya kutuma makachero kumpeleleza yeye na ndugu zake huko katika nchi ya kigeni?
 
FMES,
Visa ya Balali haijawahi kuwa "revoked." Hata ubalozi wa Marekani pale Dar ilibidi wajisahihishe kauli. Aliingia US na Diplomatic passport. Utambuzi wa hiyo ndio uliokuwa revoked. Lakini hakukuwa na uwezekano wowote kuwa Balali angechukuliwa mkeke mkeke awe deported kama wanavyowafanya marafiki zangu machinga wa Mexico wanaopatikana hawana kibali cha kuwa Marekani.
 
FMES,
Visa ya Balali haijawahi kuwa "revoked." Hata ubalozi wa Marekani pale Dar ilibidi wajisahihishe kauli. Aliingia US na Diplomatic passport. Utambuzi wa hiyo ndio uliokuwa revoked. Lakini hakukuwa na uwezekano wowote kuwa Balali angechukuliwa mkeke mkeke awe deported kama wanavyowafanya marafiki zangu machinga wa Mexico wanaopatikana hawana kibali cha kuwa Marekani.

Jasusi,

Fafanua juu ya hili maana wengi wetu tunajua visa yake ilikuwa revoked. Ila hiyo visa kuwa revoked haina maana kwamba haki ya Balali kukaa USA pia ilikuwa revoked maana inawezekana kabisa alikuwa na status nyingine pia mbali ya hii aliyoipata kwa kuwa mfanyakazi wa serikali ya TZ.
 
JK amesema kifo cha Ballali ni kazi ya Mungu,

Unajua this is sad, ni kifo gani duniani ambacho sio kazi ya Mungu? Hivi huyu mkuu anaelewa kuwa haya yanayoendelea katika taifa letu yana-accomplish one thing, and one thing only nacho ni kuendelea kuishusha hadhi ya serikali yake ambayo tayari iko kwenye life support?

Ni taifa na serikali gani duniani inayoendeshwa namna hii? Gavana wa benki kuu anaondoka nchini, halafu anatumiwa watu wa kumchunguza, baadaye anafariki ghafla, serikali inajaribu kuomba kuhudhuria mazishi lakini inakataliwa, and then hata serikali yenyewe haina uhakika na kifo cha a former Gavana wake wa Benki kuu ya taifa? Halafu hata pale ilipothibitisha bado inahangaika kujisafisha kuwa haihusiki na hicho kifo?

Yaani hii serikali haisikii aibu, wala huzuni? Serikali imeshatamka kuwa Balali amefariki, lakini hadi ninapoongea wakuu wakubwa wa taifa wanatusumbua na simu ili tuwathibitishie kama ni kweli amefariki, it is very sad indeed!
 
FMES,
Visa ya Balali haijawahi kuwa "revoked." Hata ubalozi wa Marekani pale Dar ilibidi wajisahihishe kauli. Aliingia US na Diplomatic passport. Utambuzi wa hiyo ndio uliokuwa revoked. Lakini hakukuwa na uwezekano wowote kuwa Balali angechukuliwa mkeke mkeke awe deported kama wanavyowafanya marafiki zangu machinga wa Mexico wanaopatikana hawana kibali cha kuwa Marekani.

Mkuu Jasusi,

Heshima mbele mkuu, wewe ninbakuaminia kwenye hili tena 100%, ahsante mkuu kwa sababu ndio hasa nilichokitaka kujua ukweli.
 
Wana JF naomba mnielimishe kitu kimoja. Kwa mtu aliyefukuzwa kazi serikalini akiwa mgonjwa mahututi katika nchi ya kigeni, kulikuwa na haja gani ya kutuma makachero kumpeleleza yeye na ndugu zake huko katika nchi ya kigeni?

Si angewaambia FBI wakampa ulinzi? Huku nje ni kazi ya polisi kuhakikisha kila raia
hanyanyaswi na chombo chochote hasa chombo toka nje.

I hope alienda kutoa report polisi.
 
Jasusi,

Fafanua juu ya hili maana wengi wetu tunajua visa yake ilikuwa revoked. Ila hiyo visa kuwa revoked haina maana kwamba haki ya Balali kukaa USA pia ilikuwa revoked maana inawezekana kabisa alikuwa na status nyingine pia mbali ya hii aliyoipata kwa kuwa mfanyakazi wa serikali ya TZ.

Mtanzania,
Soma Tena. Kilichokuwa "revoked" ni ule utambuzi wa kuingia kwake na diplomatic passport, ambayo baada ya serikali ya Tanzania kutangaza kuwa ime"revoke" appointment yake ilikuwa null and void. Lakini kwa Ballali kuwa Marekani was never an issue. He had his residency permit which could not be revoked just because he lost his employment with the Tanzanian government. I hope huu ni ufafanuzi tosha.
 
Mtanzania,
P.S We are saying the same thing, essentially.
 
He had his residency permit which could not be revoked just because he lost his employment with the Tanzanian government. I hope huu ni ufafanuzi tosha.

Mkuu Jasusi,

Hii ndio hasa nilichokuwa ninakisema, naona sasa ukweli uko wazi kuwa kumbe tulikuwa kwenye the right track, ahsante sana mkuu kwa ufafanuzi.

Unajua kama ninavyosema kila wakati ni ukweli only ndio huwa unatusafisha hapa JF, sio logic na hoja za ubabe, ona hoja za Jasusi hapa on the ishu hazina ubabe wala nguvu, ila facts tu!!
 
Unajua this is sad, ni kifo gani duniani ambacho sio kazi ya Mungu? Hivi huyu mkuu anaelewa kuwa haya yanayoendelea katika taifa letu yana-accomplish one thing, and one thing only nacho ni kuendelea kuishusha hadhi ya serikali yake ambayo tayari iko kwenye life support?

Ni taifa na serikali gani duniani inayoendeshwa namna hii? Gavana wa benki kuu anaondoka nchini, halafu anatumiwa watu wa kumchunguza, baadaye anafariki ghafla, serikali inajaribu kuomba kuhudhuria mazishi lakini inakataliwa, and then hata serikali yenyewe haina uhakika na kifo cha a former Gavana wake wa Benki kuu ya taifa? Halafu hata pale ilipothibitisha bado inahangaika kujisafisha kuwa haihusiki na hicho kifo?

..HUUU HAUKUWA WAKATI MUAFAKA KWA SERIKALI KUTOA KAULI YOYOTE YA KUKANUSHA KUHUSIKA NA MAUWAJI YA BALALI...MEMBE AMEONESHA UDHAIFU MKUBWA SANA KWENYE HILI........MAZINGIRA YALIYOPO HAYAKUPASA KUONGEA KWA KUKANUSHA...INGETOSHA TU KAMA ANGEWAJIBU WAANDISHI KWA KUTOA POLE KWA FAMILIA NA WOTE WALIOGUSWA..MENGINE ASINGEYAONGELEA..

..KWA HILI IMEONESHA AKILI YA MEMBE NA JK ZINAFANANA....YAANI WATU WANAOONGEA ALAFU NDIO WANAFIKIRI..SIJUI WANAITWAJE WATU WA HIVI!!!....MAANA UTAGUNDUA KAULI YA JK PIA NI YA KUTAPATAPA .KWA KUSEMA ...NI KAZI YA MUNGU!!!!....KWANI MWENYE MAMLAKA YA ROHO ZETU SI ANAJULIKANA NI MOLA!!....ANGEWEZA KUONGEA KIVINGINE..

KWA KAULI HIZI BASI NA HALI YA MAMBO ILIVYOKUA HADI ANAFARIKI..UKIFANYA UCHAMBUZI WA HARAKA UTABAKIA NA JIBU MOJA NALO NI; KIFO CHA BALALI SI CHA KAWAIDA!
 
Jamani yaelekea Balali amekufa kweli. Ishu hapa si kafa au hajafa. Ishu ya kujadiliwa hapa iwe ni pesa zetu je nazo zimekufa? Kweli hatuna jinsi tutakavyo zirudisha kwa ku convict waizi hawa? Kama kweli Kalishwa sumu basi hata wanaotafuta ushahidi watapata maana hakuna siri katika damu ya mtu. Kaini alijaribu kufanya kile kile kwa nduguye Abel lakini ukweli ulibaki wazi. Lakini kama kafa natural death basi tumeliwa kama tusipokuwa macho, ingawa naamini kufa kwa mtu mmoja hakuwezi kubadilisha ushahidi.
 
FMES,
Visa ya Balali haijawahi kuwa "revoked." Hata ubalozi wa Marekani pale Dar ilibidi wajisahihishe kauli. Aliingia US na Diplomatic passport. Utambuzi wa hiyo ndio uliokuwa revoked. Lakini hakukuwa na uwezekano wowote kuwa Balali angechukuliwa mkeke mkeke awe deported kama wanavyowafanya marafiki zangu machinga wa Mexico wanaopatikana hawana kibali cha kuwa Marekani.

Jasusi unasema Ubalozi ndio unabidi ujisahihishe, nimezimia mi confidence yako ile mbaya. Lakini nadhani umekosea kwa sababu naamini ubalozi haujakosea na nadhani wao wana make sense zaidi.

Former BOT Governor’s Termination Invalidates U.S. Visa


Press Release

Embassy of the United States
Dar-es-Salaam.Tanzania
January 16, 2008

The Tanzanian government recently inquired about the visa status of Mr. Daudi Ballali, the former Bank of Tanzania governor, in light of his recent termination. The United States Government has informed the Tanzanian government that it is revoking Mr. Ballali's visa because he no longer represents Tanzania.

Mr. Ballali visa was issued in his capacity as a representative of the Tanzania government. Simply put, because of the termination of his service, he no longer represents the government and is no longer eligible for his current non-immigrant visa status.


(Habari kamili: http://tanzania.usembassy.gov/pr_01162008.html)

Nasema wana make sense zaidi kwa sababu Diplomatic Passport na Visa ni vitu viwili tofauti ambavyo Ubalozi hauwezi kujichanganya kusema kimoja wakimaanisha kingine. Na kama wangekuwa wana maanisha Diplomatic Passport haitambuliwi hiyo isinge sema lolote kuhusu immigration status yake. Balozi ali hint kwamba Mzee yuko illegal aliposema hawagongi kila mlango kutafuta illegal aliens.

Kwa hiyo Visa Status yake ilitenguliwa.
 
Jasusi unasema Ubalozi ndio unabidi ujisahihishe, nimezimia mi confidence yako ile mbaya. Lakini nadhani umekosea kwa sababu naamini ubalozi haujakosea na nadhani wao wana make sense zaidi.

Former BOT Governor’s Termination Invalidates U.S. Visa


Press Release

Embassy of the United States
Dar-es-Salaam.Tanzania
January 16, 2008

The Tanzanian government recently inquired about the visa status of Mr. Daudi Ballali, the former Bank of Tanzania governor, in light of his recent termination. The United States Government has informed the Tanzanian government that it is revoking Mr. Ballali's visa because he no longer represents Tanzania.

Mr. Ballali visa was issued in his capacity as a representative of the Tanzania government. Simply put, because of the termination of his service, he no longer represents the government and is no longer eligible for his current non-immigrant visa status.


(Habari kamili: http://tanzania.usembassy.gov/pr_01162008.html)

Nasema wana make sense zaidi kwa sababu Diplomatic Passport na Visa ni vitu viwili tofauti ambavyo Ubalozi hauwezi kujichanganya kusema kimoja wakimaanisha kingine. Na kama wangekuwa wana maanisha Diplomatic Passport haitambuliwi hiyo isinge sema lolote kuhusu immigration status yake. Balozi ali hint kwamba Mzee yuko illegal aliposema hawagongi kila mlango kutafuta illegal aliens.

Kwa hiyo Visa Status yake ilitenguliwa.

Kuhani Mkuu,

Nafikiri wote wawili mko sahihi. Jasusi huwa anaandika kwa ufupi sana ila maana yeke ni hiyo hiyo kwamba visa ambayo ilikuwa kwenye diplomatic passport ndio ilikuwa revoked kwasababu alikuwa hana sifa tena ya kuwa na visa ya namna hiyo.

Kitu ambacho ubalozi hawakusema ni juu ya status zingine za Ballali huko USA. Kama ana green card au uraia basi hizo status hazikuguswa kwenye hiyo statement.

Serikali ilikuwa na miezi kama tisa ya kumrudisha Ballali nyumbani lakini hawakufanya hivyo, hapo ndipo mwanzo wa matatizo yote.
 
Hii issue ya suala la status la marehemu kweli linachanganya.

Kwa uelewo wangu, hauwezi ku-hold more than one viza in the U.S. Sasa iliwezekana vipi kwa marehemu ku-hold some sort of a visa, yet kuwa U.S. GC holder?

GC is an 'immigrant visa', while all other visa are categorized as 'non-immigrant visa.' Na once mtu aki-upgade to immigrant visa (GC), then the other non-immigrant visa aliyokuwa nayo inakuwa automatically dissolved.

Kwa hiyo kama Ballali alikuwa na GC, then hakuwa na haja ya yeye kuwa na U.S.visa ya aina nyingine yeyote.

Sasa kama ubalozi wa U.S. waliishu statement ya ku-revoke visa ya Ballali iliyokuwa stamped kwenye passport, then we know one thing for sure .....hakuwa GC holder. Kwa sababu, GC haiwi stamped kwenye passport......ila inatengenezewa ki-ID card chake.

By the way, mtu huwezi kuwa raia wa nchi fulani halafu yet ukawa na visa ya nchi hiyo. For what? I mean, visa is used merely for entry permit. Sasa kama wewe ni raia, then why would you need a visa to enter your own country? It just doesn't make any sense!
 
Kuhani Mkuu,

Nafikiri wote wawili mko sahihi. Jasusi huwa anaandika kwa ufupi sana ila maana yeke ni hiyo hiyo kwamba visa ambayo ilikuwa kwenye diplomatic passport ndio ilikuwa revoked kwasababu alikuwa hana sifa tena ya kuwa na visa ya namna hiyo.

Kitu ambacho ubalozi hawakusema ni juu ya status zingine za Ballali huko USA. Kama ana green card au uraia basi hizo status hazikuguswa kwenye hiyo statement.

Bonge la pointi. Lakini kuna development nyingine zilitokea baada ya hiyo statement.

Kwenye Uraia hakuna utata. Balozi Green alitangaza Jumatatu iliyopita kwamba Ballali sio raia wa US. (Kumbuka, japo hayuko Homeland Security, Balozi Green ana faili la Uraia/ US Visa status ya kila Mtanzania aliyerekodiwa. Na status ambazo sio kanjanja lazima zirekodiwe. Kwa hiyo kwenye Uraia hakuna utata. Mzee alikuwa M-Bongo.

Kwenye Diplomatic Visa, sio kweli kwamba Jasusi yuko sahihi. Kitu kama "Diplomatic Visa" hakihitajiki. Hivyo ndivyo Balozi Green alisema: Ukiwa na Visa/Uraia tayari, huhitaji Visa nyingine yeyote. Ballali asingeweza kupewa Visa nyingine (mmeiita 'diplomatic Visa') kama tayari ana Permant Resident/Uraia. 'Diplomatic Visa' hicho kitu sidhani kama kipo. Na kama kipo, Balozi Green asingesema kwamba haiihitajiki Visa ya ziada.

Na hata Green Card pia hakuwa nayo. Ubalozi wa US uliulizwa, "kama mmetengua Visa yake kwa nini hamumtimui?" Akajibu "sisi hatuendi mlango kwa mlango tunatafuta illegal aliens." Kumbuka, Balozi hapo anaongea akijua vizuri sana Visa status ya Ballali. Ina maana anatuambia Mzee alikuwa illegal. Lakini hiyo ni inference ambayo mimi nina i draw. The more conclusive evidence ni kwamba US walisema wamempa Billlali "non-immigrant Visa." Kama alikuwa na Green Card, yaani "Immigrant Visa," utapewaje tena "non-immigrant Visa" wakati huo huo?

Wakati anakufa Mzee Ballali hakuwa na Uraia, wala Green Card, wala Visa yoyote ile. Hakuna la zaidi.
 
Mimi hapa tu mkishaanza kuchanganya majina ndio huwa ninachoka wakati wote hapa tunajua tayari nani ni nani, ishu iko very clear, hakuna hapa wa kuweza kushindana na Jasusi on hii ishu, alichosema ndio mwanzo na mwisho,

Tufike mahali tukubali kuwa tulikuwa hatujui kinachoendelea, kama ni serikali ya US hawana lolote hao nao ni mtandao tu!, huwezi waaamini on anything, viza ya mtu inapokuwa revoked huko Us unaondoka hapo hapo siku hizi toka September 11, tunawajua wengi waliorudi hapo hapo, hasa kule Texas, yaani Dallas.

Wakuu kuna mengi ya ku-deal na ishu ya Balali, zaidi ya hili swali aliyelianzisha ni mimi, na nimeridhika na majibu ya Jasusi.
 
Back
Top Bottom