Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Ngoja kwanza, wakati Ballali anakwenda US si alikuwa mtumishi mkubwa tu wa serikali, kwa hiyo atakuwa alipewa visa ya kidiplomasia au? wanaweza wakafuta ya kidiplomasia wakampa ya kawaida.

Money Talks!!! anaweza kuwa alihire lawyer wa nguvu na wakafight na uamuzi ukatenguliwa, sio kila mtu anayefutiwa visa anakubali kirahis rahisi tuuu.

Alafu hili la sumu, hmmmm!!!
 
Nimeonea na watu wa kampeni wa Obama na wameniambia niandike maelezo ili kuona wataweza vipi kutoa msaada ama ushauri!
Hivyo watu wasifikiri tunakaa tuu!
Wote tuko kazini kwa namna za tofauti ili Watanzania wapewe haki yao ambayo ni ukweli tupu na si vinginevyo ambapo watu kama kina MKJJ wanapata taarifa za Ballali na huku serikali ikidai haizifahamu licha ya kwamba ni serkali yenyewe iliyokuwa ikiyalipia matibabu ya Ballali!

Mkuu Jmushi

Unajua watu wanachotaka siyo process unayoitumia ni majibu yanayotakiwa tu basi.
 
Mkuu QM,

Heshima mbele mkuu, unajua as a former M-sailor, niliwahi kupata priviledge ya kwenda karibu dunia nzima isipokuwa nchi zisizozidi kama 15 tu, na nilianza safari za nje nikiwa na umri mdogo sana hata kabla ya kuwa M-sailor, kwa hiyo maneno ya Viza na za dunia ninaamini sina utata kuyaelewa,

Ninachosema ni kuwa ninaamini kuwa Marehemu alikuwa na Greren Card, kwa sababu hata enzi alizonunua ile nyumba yake kule Bethesda, asingeweza bila ya kuwa na Green Card ingawa sasa zimebadilika lakini nilipokuwa kule US na meli in the 80s ndivyo ilivyokuwa,

Ni jana tu wanyamwezi wamekamata Carlifonia watu 950, na watu 270 wamekamatwa huko nafikiri Minnesota, sasa wanasubiri kurudishwa, ninachojua ni kwamba toka baada ya September 11, huwa wanaku-deport wenyewe hawakupi tena nafasi ya kuamua mwenyewe kama zamani, na ninawajua watu wengi sana waliofanyiwa hivyo since 2001, sasa ilikuwaje hawakumfanyia Balali?

Kama alikuwa ana-contest baada ya kufutiwa ile viza, ningekuwa mtu wa kwanza kujua jinsi nilivyokuwa ninaifuatilia ile kitu mkuu, kwa sababu kuna sehemu nyingi sana ambazo zilikuwa na interest ya ile ishu, lakini ahsante kwa elimu yako ingawa bado siajridhika na majibu niliyopata so far!
 
Mkuu QM,

Heshima mbele mkuu, unajua as a former M-sailor, niliwahi kupata priviledge ya kwenda karibu dunia nzima isipokuwa nchi zisizozidi kama 15 tu, na nilianza safari za nje nikiwa na umri mdogo sana hata kabla ya kuwa M-sailor, kwa hiyo maneno ya Viza na za dunia ninaamini sina utata kuyaelewa,

Ninachosema ni kuwa ninaamini kuwa Marehemu alikuwa na Greren Card, kwa sababu hata enzi alizonunua ile nyumba yake kule Bethesda, asingeweza bila ya kuwa na Green Card ingawa sasa zimebadilika lakini nilipokuwa kule US na meli in the 80s ndivyo ilivyokuwa,

Ni jana tu wanyamwezi wamekamata Carlifonia watu 950, na watu 270 wamekamatwa huko nafikiri Minnesota, sasa wanasubiri kurudishwa, ninachojua ni kwamba toka baada ya September 11, huwa wanaku-deport wenyewe hawakupi tena nafasi ya kuamua mwenyewe kama zamani, na ninawajua watu wengi sana waliofanyiwa hivyo since 2001, sasa ilikuwaje hawakumfanyia Balali?

Kama alikuwa ana-contest baada ya kufutiwa ile viza, ningekuwa mtu wa kwanza kujua jinsi nilivyokuwa ninaifuatilia ile kitu mkuu, kwa sababu kuna sehemu nyingi sana ambazo zilikuwa na interest ya ile ishu, lakini ahsante kwa elimu yako ingawa bado siajridhika na majibu niliyopata so far!

FMES

Nakubaliana nawe kuwa Balalli alikuwa Raia wa nchi mbili, marekani na Tanzania(In other words alikuwa anavunja sheria ya Tanzania). Ukirejea kauli ya Jefrey Salais wa Ubalozi wa Marekani hapa Tanzania mara baada ya kifo cha Ballali alisema kwamba walimfutia visa kwa sababu class yake ya visa aliipata kama mtumishi mwandamizi wa serikali lakini bado alikuwa na haki ya kuishi Marekani. Alikwepa kujibu kama Ballali ana uraia wa marekani au la. Alikwepa kujibu swali la green card. Kauli yake aliiitoa juu ya visa tu. Na ameiweka kama mtego, ila bado wawe na uhuru baadaye wakibanwa sana kukiri kuwa Balalli alikuwa na green card. Je, Ballali alikuwa mercenary?

Asha
 
FMES anamaanisha aliyemuua Ballali ni Apson Mwang'onda Mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa.

Mkuu heshima mbele, nimesema hivi nitaiomba serikali inipe nafasi nimhoji ninayemhisi ndio nitasema ni wazi nani, so far bado nasubiri majibu, ila hii yako kali sana mkuu, damn!

Lakini when the time is right nitasema waziii! Huwa hakuna haraka si unakumbuka barua ya Butiku kwa mkapa!
 
Balozi wa Marekani nchini, Bw. Mark Green amesema kuwa serikali ya nchi yake haijaombwa na Serikali ya Tanzania kumrudisha nchini aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Balali.

Alisema kwa kiasi kikubwa, hatua kama hizo zitategemea maamuzi yatakayochukuliwa na Serikali ya Tanzania kuhusiana na jambo hilo.

Hata hivyo, alisema wao wako tayari kumsaidia Rais Jakaya Kikwete kushughulikia ombi litakalofanikisha utekelezaji wa azma hiyo kama ipo.

Bw. Green alikuwa akijibu maswali ya wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari ofisini kwake ambapo aliwaita kuzungumzia ujio wa Rais George Bush nchini mwezi ujao.

Alipoulizwa mahali alipo hivi sasa Dk. Balali huko Marekani, Balozi huyo alijibu kwamba hajui na kuongeza kwamba sheria za Marekani hazimruhusu kutangaza nyendo na mahali walipo watu wanaoishi Marekani.

Kuhusu uwezekano wa kurudishwa nchini fedha zinazodaiwa kuchotwa BoT endapo sehemu yake imehifadhiwa kwenye mabenki ya Marekani, alisema kwa kuzingatia sheria za nchini mwake, fedha kama hizo zitafuatiliwa na hata kama zilipitia katika mkondo wa benki za Marekani.

Alisema suala la kurudishwa kwa fedha (kama zipo), kama ilivyo katika kumrejesha Balali, kwa kiasi kikubwa pia litategemea maamuzi ya Serikali ya Tanzania.

Aidha, kuhusu habari zilizozagaa kuwa Dk. Balali alipatiwa uraia wa Marekani kwa njia ya Green Card, alisema kuwa mtu yeyote anayeomba viza maana yake siyo raia wa Marekani na kwamba Balali aliomba viza miaka miwili iliyopita kwa wadhifa aliokuwa nao kama Gavana wa BoT.

Alisema, juhudi za Rais Kikwete kuhusu mapambano dhidi ya Rushwa ni miongoni mwa mambo ambayo Rais Bush atayazungumzia akiwa nchini.

Tanzania ni miongoni mwa nchi tano za Afrika ambazo zitatembelewa na Rais George Bush wa Marekani mwezi ujao. Nchi zingine ni Rwanda, Benin, Ghana na Liberia.
  • SOURCE: Nipashe
~

Huu mjadala pia uzingatie swali ni kwanini serikali haikuona umuhimu wa kuwapa ushirikiano wamarekani ili waweze kumleta Ballali kama walivyokuwa wakitaka kufanya!
Wale wanaofikiri presha hii hatukuianza zamani wanajidanganya na bado wanaendelea kufanya hivyo!
 
Yes Indeed as long as I don't need FBI waniambie kuwa Ballali ni Marehemu..

Kikwete, kwa nini Ballali?

ban_tahariri.jpg



KAMA kuna jambo lililotushangaza kwa Rais Jakaya Kikwete tangu alipoingia madarakani, ni kumpa kisogo aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali, tangu alipoanza kuugua, alipolazwa hospitalini hadi alipofariki dunia Ijumaa wiki iliyopita.
Si kawaida ya rais wetu kufanya kitendo kama hiki. Tunavyomjua sisi wa Tanzania Daima Jumapili, ni mtu anayewajali Watanzania wake, hasa wanapokuwa katika matatizo, bila kujali kama walimkosea yeye au serikali yake.
Maswali wanayojiuliza Watanzania wengi kwa sasa baada ya kupatikana kwa taarifa za kifo cha Dk. Ballali, ndiyo tunayojiuliza hata sisi, ingawa hatupati majibu. Tunajua wapo wanaoweza kuyajibu lakini kwa makusudi wameamua kukaa kimya.
Ukimya wao huo, ndio uliotufanya tufikirie mbali zaidi hadi kumfikia Rais Kikwete, ambaye ingawa ameonyesha kutenda tofauti na kawaida yake katika hili la Dk. Ballali, lakini tunaamini anaweza kuwaambia Watanzania sababu iliyomfanya yeye na serikali yake kujiweka mbali katika kipindi chote kigumu cha kuugua hadi kufariki dunia kwa Dk. Ballali.
Tunaamini kuwa kifo cha Dk. Ballali, iwe kilitokea kwa mipango ya watu fulani au kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu, kinamuweka Rais Kikwete katika wakati mgumu, kwa sababu kadhaa, kubwa ikiwa kushindwa kwa serikali na timu aliyoiunda kuchunguza wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Aidha, picha waliyonayo sasa Watanzania dhidi ya Rais Kikwete, inazusha maswali mengi, likiwamo la kama huruma yake ni kwa Watanzania wote au wapo baadhi ambao hawaonei huruma hata wanapokuwa katika hatari ya kufa.
Picha hii inajitokeza kutokana na mlolongo wa matukio yasiyo kuwa ya kawaida aliyoyafanya dhidi ya Dk. Ballali.
Tangu aingie madarakani, Rais Kikwete amejiwekea rekodi ya kutokataa barua za kujiuzulu za wasaidizi wake.
Mifano ya hali hii ni kukubali kwake kujiuzulu kwa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, marehemu Ditopile Mzuzuri, aliyekuwa waziri mkuu, Edward Lowassa, ambaye aliachia ngazi pamoja na mawaziri wawili, Nazir Karamagi na Ibrahim Msabaha, na hivi karibuni, Andrew Chenge.
Hawa wote waliandika barua za kujiuzulu baada ya kuandamwa na kashfa, kila mmoja kwa namna yake. Lakini kwa Dk. Ballali haikuwa hivyo, alikataa barua yake ya kujiuzulu baada ya kutolewa kwa taarifa ya uchunguzi wa kashfa ya EPA na siku chache baadaye alimtimua kazi.
Jambo jingine linaloleta utata ni kutopatikana kwa taarifa za kama Rais Kikwete alikwenda kumjulia hali Dk. Ballali wakati akiwa kitandani huko Marekani, akiugulia ugonjwa uliomuua. Rekodi zilizopo zinaonyesha kuwa Rais Kikwete ni mwepesi kwenda kuwajulia hali watu wanaomgusa wanapokuwa wagonjwa au kuhudhuria mazishi yao.
Alifanya hivyo kwa marehemu Amina Chifupa, alipokuwa amelazwa katika Hospitali ya Lugalo na alikwenda Muhimbili kuwajulia hali waandishi wa habari wa MwanaHalisi, Saed Kubenea na Ndimara Tegambwage, walipojeruhiwa wakiwa kazini, bila kujali kama watu hao ni wakosoaji wakubwa wa serikali yake.
Kwa Dk. Ballali haya yote hakuyafanya. Kwa roho ya ubinadamu ya kawaida sisi tunadhani ipo sababu ya kutokea kwa yote haya ambayo sasa yamezua picha tofauti kabisa miongoni mwa jamii ya Watanzania. Tunaamini kuwa Rais Kikwete anatambua Dk. Ballali alikuwa ni mmoja wa washirika wake wa karibu kikazi hadi alipougua na kwenda Marekani kutibiwa, hivyo kwa roho ya kibinadamu, anaweza kuwaeleza Watanzania walau kwa ufupi sababu ya ukimya wake kwa Ballali. Tunaamini rais anaweza kufanya hivyo kwa kumbukumbu tuliyonayo kutoka kwa swahiba wake, Lowassa, ambaye baada ya kulazimika kujiuzulu, rais alitumia mkutano wake na wazee wa Dar es Salaam kueleza jinsi alivyoumizwa na kujiuzulu huko kwa Lowassa, bila kuwajali watu wangemfikiliaje! Tunaomba afanye hivyo na kwa Dk. Ballali.
 
Inaeleweka Mburushi kafanya kweli lakini alitumia aina gani ya sumu??????

Pia inaelekea sumu yenyewe ama ilikosewa kwani ilitakiwa imuue Ballali mapema au kutokana na jamaa kuwa na afya nzuri haikufanya kazi mapema kama ilivyodhaniwa au kwa kuwa alikuwa hospitali ya hali ya juu labda matibabu yalisaidia kuchelewesha kufa kwake.

Kama kweli alipewa sumu, waliompa sumu naona walikuwa na wasi wasi mkubwa na kuanza kuulizana mbona hafi kulikoni?
 
Duh hizi habari ndefu sana!!!
Bubu nadhani ingekuwa jambo zuri kama maoni ya wasomaji ungekuwa unayaacha, mwenye kutaka kuyasoma aende kwenye website husika...ni wazo tu.
 
Mkuu heshima mbele, nimesema hivi nitaiomba serikali inipe nafasi nimhoji ninayemhisi ndio nitasema ni wazi nani, so far bado nasubiri majibu, ila hii yako kali sana mkuu, damn!

Lakini when the time is right nitasema waziii! Huwa hakuna haraka si unakumbuka barua ya Butiku kwa mkapa!

Wewe FMES unataka ruhusa umhoji mtuhumiwa? Akikuzidi nguvu huko utasema nini? Utaishia kuminywa ....... maaana ndio lugha yao wanayotumia.
 
Leo kwenye F1 mambo yasio tabirika yametokea

Kibunago,

Weusi na sisi kwa ubaguzi ndio wenyewe, tulikuwa hatujui formula one lakini baada ya mweusi mwenzetu (Hamilton) kuanza kupeta huko basi wote tumekuwa wapenzi nikiwemo na mimi.

Kijana wetu kashinda leo huko Monaco ndio maana Kibunango hakujizuia kutuma hiyo kwenye thread ambayo haihusiki na michezo.
 
Halafu kuna mtu anayejua kama Zitto hakuulizia hii issue alipoletwa na State Department?
Nani asiyejua Issue hii ya Ballali ni issue ambayo karibia kila Mtanzania ana njaa kali ya kujua something?
Nani asiyejua kuwa STATE DEPARTMENT NDIO JIKONI KWENYEWE KUHUSIANA NA ISSUE NZIMA YA CHAKULA CHA HABARI ZA BALALI?
The ONLY THING ambayo ni ngumu kuamini ni uwepo wa mtu mwenye njaa jikoni na halafu asidokoe walau tunyango tuwili tutatu kujidai kuwa anapima kama kimeiva?
Kwanini na sisi tusipate walau mchuzi na kinyango cha kurumangia?
 
Baada ya kuendeleza libeneke kwenye madai yangu kuwa Kikwete amekataa kumrudisha Ballali na yeye kuwa aware na rumours hizo..Alisisitiza kuwa tuendelee kuwa wavumilivu na tuachane na rumours ambazo si za kweli kwani Ballali atakufa muda si mrefu kwa mapenzi ya Mungu.
Hivyo basi uvumilivu wetu uliokuwa ukisapotiwa na wengi hapa JF umepelekea matokeo haya ambayo ni watu wale wale wa jf waliokuwa wakimtetea Mh Rais ndio wenye information za mtu ambaye Mh Rais alikuwa hataki hata kumsikia!

Wazee hiki ni kipande cha hotuba ya Mh Rais kuhusiana na
uchunguzi wa Akaunti ya EPA
Ndugu Wananchi;
Jambo la tatu ambalo nimepanga kuliongelea leo ni hili suala la ukaguzi wa Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje na hatua zinazoendelea kuchukuliwa baada ya taarifa ya ukaguzi kutolewa.

Ndugu Watanzania wenzangu;
Kwa mara nyingine tena nawapongeza na kuwashukuru wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young kwa kazi nzuri waliyoifanya na kutoa taarifa ya kina kuhusu matatizo yahusuyo matumizi ya fedha za Akaunti hiyo. Nawashukuru pia Watanzania wenzangu kwa kuunga mkono hatua tulizochukua na tunazoendelea kuchukua kuhusu suala la Benki Kuu. Hata hivyo, nasikitishwa na taarifa ninazozipata kuhusu kuwepo uvumi mwingi unaoenezwa na baadhi yetu kuhusu suala hili. Baadhi ya uvumi huo umekuwa unapotosha ukweli na kuwachanganya wananchi. Napenda kutumia nafasi hii kuwaomba wanaoeneza uvumi na uongo kuacha kufanya hivyo. Aidha, nawasihi wananchi wawe watulivu na wavumilivu.
Napenda kuwahakikishia kuwa, Serikali inayo dhamira ya dhati ya kulifuatilia suala hili mpaka mwisho wake ujulikane. Mwisho ambao utakuwa na maslahi kwa taifa letu. Pamoja na yote yatakayofanywa, tunataka kuhakikisha kuwa fedha zilizolipwa kinyume cha utaratibu zinarudishwa. Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wenzake, yaani Mkuu wa Jeshi la Polisi na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU wameanza kuchukua hatua. Nimewataka watoe taarifa kwa wananchi mara kwa mara kadri inavyowezekana pamoja na haja ya kuwa waangalifu kutokutoa mengi yahusuyo uchunguzi wanaoufanya ili ushahidi usiharibike.
Nawaomba Watanzania wenzangu tuwe na subira. Naamini kazi hii itakamilika ndani ya kipindi cha miezi sita tuliyowapa. Napenda kurudia ombi la Serikali kwa wananchi wenye taarifa zitakazosaidia katika uchunguzi na hatua katika suala hili waisaidie kamati yetu
 
Ufunuo mpya:Ballali aliungama ukweli kashfa ya EPA

Habari Zinazoshabihiana
• Kikwete ashtushwa kifo cha Ballali 24.05.2008 [Soma]
• ...Mdogo wake afichua wosia mwingine 25.05.2008 [Soma]
• ...Watanzania washtushwa usiri wa kifo chake 22.05.2008 [Soma]

*Majira Jumapili lanasa alichokisema
*Serikali ya Kikwete yasubiri kuumbuka

Na Hassan Abbas

ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Dkt. Daud Ballali, kabla ya kufikwa na mauti yake nchini Marekani, aliungama 'dhambi' yake kuu ya kuhusishwa na kashfa ya ufisadi kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), gazeti hili linawathibitishia Watanzania.

Katika ungamo hilo, Ballali (65), aliyekuwa akichukuliwa kuwa mmoja wa watuhumiwa na mashahidi wakuu wanaoweza kueleza nani hasa walikuwa nyuma ya ufisadi huo, imebainika alitaja moja kwa moja mhusika, ungamo ambalo sasa baada ya kifo chake, linaiacha Serikali ya CCM kuwa ndiye mtuhumiwa mkuu.

Kwa mujibu wa nyaraka ambazo gazeti hili limezipata kutoka vyanzo vya kuaminika na maelezo ya siri yaliyotolewa na baadhi ya ndugu zake, Ballali amekufa akiwa ameinyooshea kidole Serikali kuwa ndiyo inayohusika na fedha za EPA zilizochotwa BoT, kauli inayoonesha kuwa yeye alikuwa akipokea tu maagizo ya kuziidhinisha.

Ungamo la kwanza la Ballali katika fumbo kuu la ufisadi huo, uchunguzi wetu umebaini, alilifanya katika mahojiano yake na wakaguzi wa Deloitte & Touche, ambao ndio wa kwanza kuibua kashfa ya EPA kabla ya wakaguzi wengine wa Ernst&Young kuhitimisha.

Katika mahojiano yake na Ballali ya Septemba 8 na 9, 2006, Mkurugenzi Mwandamizi wa Ukaguzi wa Kampuni ya Deloitte, Bw. Samuole Sithole kutoka Afrika Kusini, aliyesafiri rasmi kuja nchini kumbana Ballali, ndiye aliyefanikiwa kupata ungamo la Gavana huyo.

Nyaraka zinaonesha kuwa siku ya kwanza ya mahojiano hayo, Ballali alifanikiwa, hata baada ya kubanwa sana, kuificha siri kuu iliyojificha juu ya wahusika halisi wa ufisadi wa EPA ambapo kampuni zipatazo nane zilipitishiwa kijanja kiasi cha sh. bilioni 133.

Hata hivyo, akitumia utaalamu na umahiri wake wa kuhoji watuhumiwa ambao ni wataalamu wa masuala ya fedha na uchumi waliokumbwa na kashfa mbalimbali, Jumamosi ya Septemba 9, Bw. Sithole aliweza kupata kile alichokitaka kutoka kwa Ballali ambaye alifanya ungamo ambalo hadi anakufa, alikuwa anaangalia uwezekano wa kulifafanua zaidi, ili jamii iujue ukweli.

Ballali katika mahojiano hayo, aliitaka Serikali moja kwa moja, kupitia Wizara ya Fedha kuwa ndiyo inayojua kuhusu suala la malipo ya EPA.

Katika ungamo hilo pia Ballali alikwenda mbali zaidi kwa kuwafahamisha wachunguzi hao kuwa ni Serikali pia ambayo inaweza na inapaswa kutoa risiti za kuthibitisha matumizi ya pesa hizo.

Serikali kupitia kwa aliyekuwa Waziri wa Fedha, Zakia Meghji iliwahi kuuma maneno kwa kuzikana fedha hizo lakini baadaye ilieleza kuwa zilitumika kwa matumizi 'mahsusi yenye maslahi ya taifa.'

Duru za siasa zinazihusisha fedha hizo na kampeni za CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, ingawa karibu viongozi wote waandamizi wa chama hicho akiwemo Katibu Mkuu mstaafu, Bw. Phillip Mangulla waliwahi kukanusha walipoulizwa na gazeti hili wakidai kuwa chama hicho kina miradi, wafadhili na wanachama wanaokifanya kijitosheleze.

Hata hivyo wiki hii tena, siku chache baada ya kufariki dunia, ungamo hilo la Ballali limepata nguvu baada ya mmoja wa wanafamilia wake wa karibu aliyezungumza na Majira Jumapili Dar es Salaam kwa sharti la kutotajwa jina, kufichua kuwa katika siku zote alizopata kumsikia marehemu akizungumza na watu wake wa karibu enzi za uhai wake, alikuwa akisononeka sana kuhusishwa na ufisadi huo na alipanga kuyasema yote.

"Alikuwa akiufuatilia mjadala wote, alikuwa mvumilivu sana, lakini alishajipanga kusema ukweli wote," kilidokeza chanzo hicho.

Akaongeza: "Alikuwa akitaka kusikia kauli ya mtu mmoja muhimu sana, ninyi pia mtakuwa mnamjua, kama mtu huyo angekuwa akitoa kauli za kuonekana kumkandamiza, basi naye alikuwa tayari kusema ukweli wote kwamba kuna waliohusika kuchukua fedha za EPA.

Lakini alisita baada ya mtu huyo kila ninyi (waandishi wa habari) mlipokuwa mkimbana, akawa haongei mengi kuhusu hilo. " Hakutaka kufafanua mtu huyo ni nani.


Source:
http://www.majira.co.tz/kurasa.php?soma=tanzania&habariNamba=6753
 
...nimemuangalia Sasa Hivi Membe Akikanusha Kuhusika Kwao Na Kumuuwa Bilali ..anavyojiuma Uma ...hadi Anatia Huruma ...sikuona Mantiki Ya Kujitutumua Vile Kama Kweli Anajua ..hawakumuuwa.......
 
Back
Top Bottom