Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kijiwe kitafungwa kwa kuandika kwamba aliyemuua Ballali ni Rostam Aziz?

Gazeti linaweza kufungiwa lakini sio JF. Ukifungia JF leo, zitakuja zingine 20.

Mimi siamini hii habari ya sumu kwamba ni kweli. Wewe utalishwa sumu, ukimbilie USA, ukae miezi tisa, hakuna hata daktari mmoja ambaye anaweza kusimama na kusema wazi kwamba umelishwa sumu?

Hata KGB walipotaka kumuua yule jamaa wa Ukraine bado ilijulikana, hata Polonium 210 ya UK bado ilijulikana, sasa hii sumu ya gavana wetu ni sumu gani hiyo?

Hili suala la sumu mimi nililipinga toka mwanzoni na sasa ndio natapata sababu kubwa za kulipinga. Sumu ilikuwa ni sababu ya Ballali kutoroka TZ na kupotelea kimoja USA wakati wanaandaa mipango mingine.

Kuna kampeni kubwa ya kuwadanganya Watanzania juu ya hili jambo la Ballali.

Mkuu umelonga,

Inamaana wanataka kutuambia kwamba hii sumu ilikuwa Calculated?

Ondoeni Uzushii huuuu, JF sio ya Majungu.
 
mawazo huru hayana bei! ila mawazo ya upotoshaji huwa yananunulika. Watu hawanunui watu wenye mawazo huru wananunua wanaoweza kupotosha watu. Na wewe una bei.

Very strong(maneno ya FMES)

Kamanda MKJJ, hapa umekata mzizi wa fitina
 
Very strong(maneno ya FMES)

Kamanda MKJJ, hapa umekata mzizi wa fitina

Kibunango wewe ni mwana CCM unayezidi kumvutia MKJJ upande wenu ili kuwachonganisha upinzani zaidi!
Upinzani ulikuwa na imani kubwa na MKJJ na sasa watetezi wake nihawa ccm kina Kibunango na wengine wenye taarifa kama kina Field Marshall!
Msilete siasa za kulambishana pipi kijiti hapa!
Etu subirini naleta news!
Hivi hamuwaonei huruma watanzania kweli?
 
MKJJ hii ni mara ya mwisho nakuomba urudi upande wa wazalendo ili imani yao kwako irudi! Mafisadi walijua una ushawishi mkubwa! Lakini hawakujua kuna kina JMushi Narudia tena...RUDI KAMBINI MKUU USIJE UAKANGUKA KIFO KIBAYA CHA IMANI YA SIASA ZETU AMBAYO TULIKUWA NAYO KWAKO WAKATI UKIWA UPANDE WA WAZALENDO!

Mkuu wangu Mushi, huwa hapa forum tunasema hivi, kama huelewi jambo basi uliza kabla ya kukurupuka maana yanayoendelea kwa nyuma hujui kama unavyooonyesha hapa na hayo maneno against mkuu MMJ, kuna tunaojua mkuu and I mean it!
 
Mkuu wangu Mushi, huwa hapa forum tunasema hivi, kama huelewi jambo basi uliza kabla ya kukurupuka maana yanayoendelea kwa nyuma hujui kama unavyooonyesha hapa na hayo maneno against mkuu MMJ, kuna tunaojua mkuu adn I mean it!

Nakubali kuna namna wewe na wengineo mnavyomjua!
Na mimi simjui kihivyo ila nilkuwa mshabiki mkubwa sana wa MKJJ!
Na bado nina kaimani nilikokabakiza..Integemea na karata zake atakaovyozicheza!
Lakini ajue imani ya wananchi kwake imetetereka! Hilo asibishe!
Mimi ni ushauri wangu tu wa bure!
Mimi pia ni shabiki wa Zitto..Lakini bado nina ushauri wangu binafsi!
Kuweni makini ndugu zangu...Mkumbatie siasa za wazalendo kuanzia mwanzo hadi mwisho!
Tunajua hata MKJJ akishawahi kukiri kuwa walifuatwa na mafisadi ili waiuze jf..Hatujui mambo yaliishia vipi lakini naamini jf bado kuna walioko upande wa Wazalendo na kuna wale ambao wameshatetereka na JMushi yuko hapa kuwapa tahadhari ili waikoe ile imani iliyobakia!
 
Mkuu mimi nilipolifuatilia hili kule State Department, niliambiwa kuwa Balali ana Green Card ambayo ni valid, nikaambiwa tulichomfutia ni viza tu kama ofisa wa serikali kutoka executive branch,

na bongo sasa hivi ninawajua viongozi wetu wengi kwenye sekta mbali mbali wanamiliki hizo Green Card, na ambao huenda US kwa siri sana kuzi-activate na kuna mpaka wenye pass kabisa za huko, sasa hili limekaaaje wakuu?

Mmojawapo Masha, tena anayetakiwa kutulindia wizara yetu ya mambo ya ndani. Tanzania sijui tutafungwa magoli mpaka lini?

Mkuu ES, ili clue yako nzito, wacha niendelee kukuna kichwa ila ni kama jina linakuja.

Clues za Mwanakijiji zinafunga kamba kuliko kufungua, sio za kuzifuata.

Hii ya RA ni kama alivyosema Mwanakijiji, kwasababu kila mtu anajua yeye jambazi basi kila jambo atasingiziwa yeye.
 
Mmojawapo Masha, tena anayetakiwa kutulindia wizara yetu ya mambo ya ndani. Tanzania sijui tutafungwa magoli mpaka lini?

Mkuu ES, ili clue yako nzito, wacha niendelee kukuna kichwa ila ni kama jina linakuja.

Clues za Mwanakijiji zinafunga kamba kuliko kufungua, sio za kuzifuata.

Hii ya RA ni kama alivyosema Mwanakijiji, kwasababu kila mtu anajua yeye jambazi basi kila jambo atasingiziwa yeye.

Hivi Masha naye anyo green card? duh! by the way Rita Mlaki naye anayo permanent residence UK
 
Ukiwa na green card hauhitaji visa!
Na green Card ili iendelee kuwa valid kama ukiwa nje ya nchi ni lazima urudi marekani at least mara moja kwa mwaka!
So hata kama alikuwa na green card..Then bado tutailaumu serikali kwasababu ndio imani kuwa walikuwa na mpango mchafu itaongezeka!

Jmushi,

Katika watu wagumu niliowahi kukutana nao humu JF ni kama unaongoza. Sijui ni mgumu wa kuelewa au mgumu wa kubadilika (joke) kwi kwi kwi!!!!

Pamoja na kuwa na green card lakini huenda kwa kazi aliyokuwa nayo ilikuwa inamruhusu kuwa na visa special ambayo huenda ina nguvu kubwa kuliko hiyo green card. Anaweza kuwa alikuwa anaingia USA kama VIP kitu ambacho asingeliweza kufanya akiwa na hiyo green card.

Mimi naamini Ballali ana uraia wa USA, angalieni vizuri nasema ana na wala sio alikuwa kwi kwi kwi!!!!

Kuna wengine toka UK pia wanaongoza TZ wakiwa na green cards za UK.
 
Naona sasa JF imekuwa sehemu ya mipasho.. Where are we going? Hayo maneno mnarushiana kati ya MKJJ , FMES na Jmushi. Naona sasa tuwaachie muendeleee na mipasho
 
Naona sasa JF imekuwa sehemu ya mipasho.. Where are we going? Hayo maneno mnarushiana kati ya MKJJ , FMES na Jmushi. Naona sasa tuwaachie muendeleee na mipasho

Mzimu wa Ballali(Joke)
 
Mbowe atoa kauli nzito kifo cha Ballali

na Lucy Ngowi
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amesema kifo cha aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), Daudi Ballali kina mkono wa baadhi ya vigogo wa serikali, kwa sababu alikuwa shahidi muhimu katika vita ya ufisadi.

Mbowe ambaye anakuwa kiongozi wa kwanza kutoa kauli hiyo nzito, alisema hayo wakati alipokuwa akizungumza na wakazi wa Mtaa wa Ufipa, pamoja na waandishi wa habari katika Makao Makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Alisema kuna kitendawili kinachotegwa sasa na baadhi ya vigogo wa Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kwa kuwa Ballali alikuwa shahidi muhimu sana katika vita ya ufisadi aliyodai kufanywa na chama tawala.

Mbowe alisema, tangu Ballali alipoondoka nchini Agosti, mwaka jana, vyombo vyote vya habari viliandika vikidai gavana huyo wa zamani ana ushahidi wa kina kuhusu ubadhirifu wa pesa za BoT, matokeo yake Rais Jakaya Kikwete alitengua uteuzi wake na kuunda kamati ya kuchunguza ufisadi huo.

Mwenyekiti huyo wa CHADEMA alisisitiza kuwa, Ballali hakula peke yake, bali alikula na baadhi ya viongozi waandamizi wa serikali ya awamu ya tatu na ya nne na kuongeza kuwa, hata baadhi ya fedha zilizotumika wakati wa kampeni ya mgombea wa CCM, zilitokana na fedha za EPA.

“Kuteketea kwa Ballali, tutaamini kuna mkono mchafu wa baadhi ya viongozi wa serikali, kwa sababu ni shahidi muhimu katika vita ya ufisadi. Wasifikiri kufa kwa Ballali, ndiyo mwisho wa mapambano, lakini nawaambia ndiyo kwanza vita ya ufisadi itapamba moto.

“Ufisadi na mchezo mchafu wa CCM, umewatesa watoto wetu, wazazi wetu na sasa basi, tutapambana hadi watakapouana wote waishe. Wamemuua Ballali, Amina Chifupa wataendelea kuuana,” alisema mwenyekiti huyo.

Amina alikuwa Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), aliyefariki mwaka jana baada ya kuugua ghafla, na kifo chake kuzua gumzo nchini kutokana na msimamo wake wa kutaka kutaja majina ya wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya.

Kwa mujibu wa Mbowe, katika pesa zilizoibwa BoT, pesa pekee zinazochunguzwa ni fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), lakini tuhuma za ubadhirifu na wizi wa BoT hazikuwa za akaunti hiyo peke yake.

“EPA ni sehemu tu, pesa nyingine hazijaundiwa tume. Tunamwambia Rais Kikwete, utawala wake kwa miaka miwili iliyobakia utakuwa ni wa kuunda tume tu. Wamemwondoa Ballali kwa sababu ndani ya Ballali, kuna mambo mengi yaliyofichika,” alisisitiza.

Alisema BoT ni benki ya serikali, hivyo pesa zinazohifadhiwa ni kodi za Watanzania na ili ziweze kuchukuliwa, lazima mamlaka itoke serikalini.

Mwenyekiti huyo alisema, aliyekuwa Waziri wa Fedha awamu ya tatu, Basil Mramba na Katibu Mkuu, Grey Mgonja, wanahusika katika wizi huo wa BoT kwa kuwa walimwidhinisha Ballali, alipe pesa mbalimbali zilizokuwa zinatoka bila mpangilio, lakini mpaka sasa hawajaguswa.

“Tunataka Mramba, Mgonja watueleze ukweli kuhusiana na ubadhirifu uliokuwa unafanywa BoT,” alisema mwenyekiti huyo.

Alisema anamshangaa Rais Kikwete kuunda tume nyingine iliyomhusisha Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika na Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hosea ilhali serikali imeficha ripoti ya awali.

Awali, mwenyekiti huyo alizindua tawi la CHADEMA Mtaa wa Ufipa, Kinondoni na kusema kuwa, huo ni mkakati wa uzinduaji wa matawi ya chama chake katika Jiji la Dar es Salaam.

Alionya kuwa, kamwe tawi hilo lisiwe la CHADEMA tu, bali liwe kwa nia ya kuwatetea wananchi wote katika eneo hilo. Pia lisiwabague wanachama wa vyama vingine vya siasa.

“Viongozi wa CHADEMA na tawi la Ufipa, msiwe wa kwanza kuhujumu wanachama wa vyama vingine vya siasa, bali muwe kimbilio la wote wenye matatizo katika mtaa huo,” alisema Mbowe.

Ballali alifariki dunia Mei 16 nchini Marekani na kuzikwa juzi katika makaburi ya Wakatoliki ya Gate of Heaven, Silver Spring, nchini humo, ambako watu maarufu walihudhuria mazishi yake, akiwemo Balozi wa Tanzania nchini humo, Ombeni Sefue.

Ballali amekuwa akiripotiwa kuugua kwa muda mrefu, lakini muda wote serikali haijawahi kutaja ugonjwa uliokuwa ukimsumbua na hospitali aliyokuwa akipata matibabu.

Hata alipofariki, serikali haikuwahi kutangaza kifo chake hadi gazeti hili lilipoibua taarifa hiyo siku tano baadaye.
 
Sasa mkuu huoni kuwa profile ya kesi ya huyu mkuu ilikuwa ni too big kwao US kutom-deport? Maaaana ninakumbuka kuwa Kurt Waldheim yula m-Austria, walipomshitukia tu kuwa ana noma, wanyamwezi kwanza walimfukuza na kumpiga marufuku kuingia tena US kama raia lakini walisema wazi kuwa hawawezi kumzuia kuingia US kama rais wa Austria,

Sasa iweje hii ya Balali wakamuachia tu hivi hivi aishi huko bila viza ambayo tayari walishaitangaza kuwa wameifuta? Wakati wabunge wetu wa upinzani walikuwa tayari wameitwa huko Congress na kutema wazi sumu nzima ya Balali hapa bongo? Na jinsi tulivyokuwa tukumuhitaji sana kulisaidia taifa letu kwa uchunguzi wa EPA ambao wao wenyewe wanyamwezi waliushinikiza ufanyike?

Naomba shule zaidi hapa wakuu!

FMES
Huwa kuna 90 days period yakuondoka nchini baada yakufutiwa visa/green card.

Sasa basi, kama Ballali alifutiwa visa kama inavyodaiwa, basi alikuwa na hizo siku 90 kufungasha virago.

Na kama Ballali ali-contest (assuming) ufutiwaji wa visa yake, basi huenda alipewa temporary stay wakati kesi yake inashughulikiwa na uhamiaji. Na kumbuka kesi kama hii inaweza kuchukua hata mwaka na zaidi. Na muda wote huo anakuwa safe from deportation.

All in all, hata kama visa ikifutwa, kuna uwezekano mkubwa wa mfutiwaji kuendelea kuminya. Kwa sababu, uhamiaji huwa hawana muda na resource za kutosha kumfuatilia kila mtu aliyekuwa nje ya status. Ndio maana kuna over 2m illegal immigrants in the U.S.
 
Naona sasa JF imekuwa sehemu ya mipasho.. Where are we going? Hayo maneno mnarushiana kati ya MKJJ , FMES na Jmushi. Naona sasa tuwaachie muendeleee na mipasho

mpasho unaweza kukugeukia w.o!
 
Nimeonea na watu wa kampeni wa Obama na wameniambia niandike maelezo ili kuona wataweza vipi kutoa msaada ama ushauri!
Hivyo watu wasifikiri tunakaa tuu!
Wote tuko kazini kwa namna za tofauti ili Watanzania wapewe haki yao ambayo ni ukweli tupu na si vinginevyo ambapo watu kama kina MKJJ wanapata taarifa za Ballali na huku serikali ikidai haizifahamu licha ya kwamba ni serkali yenyewe iliyokuwa ikiyalipia matibabu ya Ballali!
 
Anayeamini kuwa aliyefanya hivi ni ni RA ameuzwa na hajakaa chini kufikiri. Ngojeni wengine tutakapoandika ndipo dots zitakapounganishwa. Katika kutafuta majibu naomba niwape clue mbili:

a. Ni nani sources za habari za Ballali, ugonjwa wake, sumu, kifo, n.k
b. What if the misinformation of Tanzania haikuanza wiki iliyopita au baada ya Ballali kuondoka?


sasa hivi lengo ni kuhamisha kidole toka kwa mhusika mwenyewe na kukielekeza kwa mtu mwenye jina baya. Nilipokuwa mdogo tuliishi jirani na jamaa mmoja ambaye alijulikana kuwa ni mwizi. Lakini huyo jamaa pia alikuwa ni mjenzi. Sasa alikuwa anaiba na kujenga au anapopewa nafasi ya kujenga anaiba pia cement nk na kujenga kwake.

Sasa sisi tukafikiria kwanini tusimpe huyu jamaa ujenzi wa nyumba yetu? Tulipompa ujenzi na kumsimamia kutwa nzima wizi mtaani ulipungua. Lakini siku moja tukiwa kwenye kumwaga zege kutwa nzima na makarai yale... tunarudi mtaani (tulikokuwa tunajenga ni kama maili 3 hivi toka kibanda cha zamani) basi mtaani walipomuona jamaa watu wakaanza kumpigia kelele kuwa amewaibia mchana huo. Hilo lisingewezekana kwani karibu watu 20 walikuwa naye kwenye ujenzi wetu.

Lakini wakajitokeza hadi mashahidi kuwa walimuona huko. Ni baada ya hekima ya wazee ndipo ilipogundulika kuwa mwizi alikuwa ni mtu mwingine mtaani hapo ambaye alikuwa anatumia "sifa mbaya" ya fundi wetu kujitajirisha na yeye akijua kuwa akiiba atakayelaumiwa ni "mwizi anayejulikana".

so, in this case kuna jaribio la kumfanya RA ndiye mwizi wao!! na mwizi mwenyewe anaendelea na mikutano, yuko Bubu, na hakuna mtu atakayethubutu kuandika kichwa hicho cha habari bila kutiwa kashkash.

Mwanakijiji anamaanisha aliyemuua Balalli ni Benjamini William Mkapa. FMES anamaanisha aliyemuua Ballali ni Apson Mwang'onda Mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa. Ansebert Ngurumo anamaanisha aliyemuua Ballali ni Rostam Aziz. Halafu mwingine aliyesema yule Mkurugenzi wa Sasa wa Usalama wa Taifa Rashid Othaman yeye alishangaa kumkuta Balalli bado yu hai. BM na AM lao moja. RA na RO lao moja. Je, hapa palikuwa na uswahiba wa kuua na kuzika? Inawezekana wote hapa mnazungumza lugha moja ila mwanzo wenu ni tofauti. Inawezekana Balalli aliuwawa na Apson, kwa maelekezo ya Mkapa yaliyoratibiwa na Rostam na kufuatiliwa na Rashid kuona kama yametekelezwa. Hakuna wakili wa Marekani ambapo Balalli amekula kiapo autueleze ukweli?

Asha
 
Serikali inaficha ukweli – Wanasheria

na Mwandishi Wetu

BAADHI ya wanasheria wameshangazwa na usiri wa serikali kuhusu kuugua hadi kufa kwa aliyekuwa Gavana wa Benki ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima Jumapili mwishoni mwa wiki, wanasheria hao walisema lazima serikali inaficha jambo kuhusu Dk. Ballali.

Mmoja wa wanasheria hao, Mabere Marando, alitoa lawama kuhusu ukimya wa serikali, katika kuugua hadi kufariki dunia kwa Dk. Ballali, na kuongeza kwamba kutawafaidisha watuhumiwa wa wizi wa fedha katika akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA), uliofanyika BoT.

"Nimesikitishwa sana na kifo cha Dk. Ballali, alikuwa Mtanzania mwenzetu. Lakini kinachosikitisha zaidi ni ukweli kwamba kifo chake kitaathiri sana uchunguzi wa wizi wa fedha za EPA.

"Ukimya wa serikali kuhusu kuugua hadi kufa kwa Dk. Ballali, unashangaza, ni wazi kuwa kuna jambo inaficha, kwa sababu haiwezekani isijue mahali alipo gavana wake wakati ilikuwa ikimlipia sehemu ya gharama za matibabu kama tulivyoelezwa na gavana wa sasa," alisema Marando.

Alieleza zaidi kuwa kitendo cha tume iliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, kuchunguza tuhuma hizo kutomuhoji Dk. Ballali hadi mauti yalipomkuta, nacho kinashangaza, kwa sababu alipaswa kuhojiwa kwanza, kwani alikuwa shahidi muhimu katika kesi hiyo.

Mwanasheria mwingine wa serikali aliyeomba jina lake lihifadhiwe, alizungumzia suala hilo na kusema ni jambo la ajabu kwa timu inayochunguza kashfa ya EPA kutomuhoji Dk. Ballali hadi anakufa.

"Huyu alikuwa ‘key' katika uchunguzi huu, timu ya rais ilipaswa kumuhoji mapema kabisa, inashangaza kusikia mpaka anakufa hakuwahi kuhojiwa na serikali inasema haimtafuti.

"…Huu uchunguzi unaofanywa ni lazima utiliwe shaka na mjuzi yeyote wa mambo ya kisheria. Uchunguzi unaofanywa ni kama mchezo fulani hivi! "Na hapa wa kushakiwa kwanza ni serikali, haijulikani inaficha nini kuhusu huyu ndugu yetu, kwa sababu tangu alipougua mpaka anakufa, habari zake zimekuwa siri kubwa," alisema na kuongeza kwamba, ni ajabu kwa serikali kutokujua alipo mtuhumiwa wa wizi wa mabilioni ya shilingi.

Alisema, hata taarifa zilizotolewa kuwa amefutiwa hati ya kuishi Marekani ziliongeza mashaka, kwa sababu alitakiwa kuondoka nchini humo baada ya kutotambuliwa, lakini hadi anakufa alikuwa huko.

Aidha, aliwataka Watanzania kuihoji serikali kwa nini ilifanya siri matatizo ya kuugua hadi kufa kwa Dk. Ballali, na kuongeza kwamba Marekani inatakiwa kutoa taarifa za uchunguzi wa kifo chake ili wananchi wajue, kwa kuwa ni haki yao kufanya hivyo.
 
Mwanakijiji anamaanisha aliyemuua Balalli ni Benjamini William Mkapa. FMES anamaanisha aliyemuua Ballali ni Apson Mwang'onda Mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa. Ansebert Ngurumo anamaanisha aliyemuua Ballali ni Rostam Aziz. Halafu mwingine aliyesema yule Mkurugenzi wa Sasa wa Usalama wa Taifa Rashid Othaman yeye alishangaa kumkuta Balalli bado yu hai. BM na AM lao moja. RA na RO lao moja. Je, hapa palikuwa na uswahiba wa kuua na kuzika? Inawezekana wote hapa mnazungumza lugha moja ila mwanzo wenu ni tofauti. Inawezekana Balalli aliuwawa na Apson, kwa maelekezo ya Mkapa yaliyoratibiwa na Rostam na kufuatiliwa na Rashid kuona kama yametekelezwa. Hakuna wakili wa Marekani ambapo Balalli amekula kiapo autueleze ukweli?

Asha

Mmmmmhhhh!!!! Dadangu hiyo ya kwako kali.
 
Mwanakijiji anamaanisha aliyemuua Balalli ni Benjamini William Mkapa. FMES anamaanisha aliyemuua Ballali ni Apson Mwang'onda Mkurugenzi wa zamani wa Usalama wa Taifa. Ansebert Ngurumo anamaanisha aliyemuua Ballali ni Rostam Aziz. Halafu mwingine aliyesema yule Mkurugenzi wa Sasa wa Usalama wa Taifa Rashid Othaman yeye alishangaa kumkuta Balalli bado yu hai. BM na AM lao moja. RA na RO lao moja. Je, hapa palikuwa na uswahiba wa kuua na kuzika? Inawezekana wote hapa mnazungumza lugha moja ila mwanzo wenu ni tofauti. Inawezekana Balalli aliuwawa na Apson, kwa maelekezo ya Mkapa yaliyoratibiwa na Rostam na kufuatiliwa na Rashid kuona kama yametekelezwa. Hakuna wakili wa Marekani ambapo Balalli amekula kiapo autueleze ukweli?

Asha

Ukiombwa ushahidi utatoa?
 
Back
Top Bottom