Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Mkuu Mtanzania,

Heshima mbele, hapa umesema neno moja zito sana kuhusiana na this whole thing kuhusu Balali na kifo chake, sina tatizo na msimamo wako on the ishu ya kufa kwake, lakini at the same token ninajaribu ku-reason out,

Kwamba Balali, hajafa, familia yake imeamua ku-play a stint na kuwaaarifu dunia nzima kuwa amekufa, watu wa karibu na familia hiyo, ndugu wa karibu wote wa Balali na Muganda, wamekwenda huko DC, mmiliki wa Tanzania Daima ambaye naye ni ndugu wa karibu amefahamishwa kuhusu hicho kifo, serikali imefahamishwa kuhusu hicho kifo, dada yangu amefahamishwa na kualikwa kwenye msiba, juzi yamefanyika mazishi,

Sasa kama ninakuelewa vizuri, ni kwamba huu wote ni uongo uliotungwa na familia hiyo ya Balali, lakini Balali yupo na ataendelea kuishi baada ya all this?

kweli unaamini kuwa this makes a sense?

Mkuu ES,

Uzuri wa kuishi kwingi ni kuona mengi. Tuna mifano mingi tu ya watu walio fake vifo, hivyo
ni ngumu kuamini mpaka kuwe na ushahidi wa kutosha.

Mimi swali langu ni lile lile, kafia kwenye hospitali ipi? Tukishajua hospitali, mengine tutachunguza wenyewe.
 
Hapa nilichokiaona watanzania inatakiwa tuombe radhi kwa familia ya balali.

Suala la muhimu ninaloliona ni hili , Unajua assume umekaa pale counter ya CRDB au NBC na una funguo za mahali pa kutunzia pesa. Wakaja majambazi wakaamulisha uwappe kila kilichoko benki. Ukatoa baadaye wakaondoka au wakaondoka na wewe.

Mwisho wa siku wakaamua kukumalizia. Je nani atakuwa reponsible kuhakikisha haki inatendeka. Je mwenye kosa ni yule aliyekuwa na ufunguo?

Je mambo yanahisha pale tu aliyekuwa na funguo anamalizwa. Mimi nilivyoona sakata hili ni Kwamba balali alitekwa, na majambazi wakati watanzania tukishangilia, baadaye majambazi yametoa hukumu.

Suala lililoko hapa let us see kilichoko mbele yetu. Mtunza fuunguo hayupo tena na sisi hatukuweza kuliona hili.

Tuwaombe watawala wajibu maswali mawili matatu.
Je Balali alipotekwa wao walikuwa wapi?

Je kwa nini hawakufatilia mapema kulikoni atekwe?

Je kwa nini mpaka sasa watekaji wa EPA bado ni kigugumizi.
 
ES ile DVD ulituahidi mbona hatuioni?

hivi how difficult is it kupost Video kwenye Youtube?
 
A bit of otherwise thinking.

Hivi hii habari ya balali unaweza kutengeneza movie kabisa kama 24 series.
Yaani kuanzia pale alipokuwa Shirika la fedha,akaitwa na bwana uwazi na ukweli,kisha akateuliwa kuwa gavana...

Jinsi alivyokuwa akiwasadia watu fulani fulani kuchota pesa,kisha akaingia kwenye kasha then ikasemekana kalishwa sumu..mara akapotea kwenye vyombo vya habari..then ikasemekana anaumwa....mpaka kifo chake.Inawezekana all this was a planning script. ambayo sasa imetimia.

Week endi njema.
 
Mkuu GT,

Naomba nikuombe radhi mkuu, shughuli zimenitinga sana, na ni jana usiku tu ndio nimemaliza kuziangalia vipande vyote vitano, havikuwa vinne kama nilivyosema mwanzoni, nisingeweka kitu ambacho sijakiona mwenye kwanza kwa sababu what if ndani kungekuwa na something else? Maana binamu yangu mmoja aliwahi kumpa baba yangu film akamsafishie u-China kumbe hakuangalia vizuri kuwa amempa film ya watu wako uchi ikaishia kuwa aibu kubwa sana, kwa hiyo toka siku hiyo huwa ninajaribu kuwa careful mkuu,

Muda wa kuanza kuweka huko Tube sina mkuu, isipokuwa nimejaribu kuwasiliana na wenye kuweza, nia na madhumuni yangu ni kutaka iwekwe hapa JF, kwa hiyo soon itawekwa tu mkuu, au una hoja nyingine mkuu? nifahamishe tu mkuu!
 
Aliyeiandika hii arcticle yaani Mkulu Wangu Ngurumo, ni mtu ninayemuheshimu sana kwa sababu huwa hachanganyi maneno wala hana mchezo, lakini ninakubaliana naye na pia kutofautiana naye kuwa kwa dataz nilizonazo aliyehusika na "one on one" ni mwingine,

lakini huenda huyu anayemsema ndiye the originator, lakini facilitator ni mwingine kabisa, yaani "mzee wa mbeya" Mkuu wangu Mtanzania upo hapo?
 
Aliyeiandika hii arcticle yaani Mkulu Wangu Ngurumo, ni mtu ninayemuheshimu sana kwa sababu huwa hachanganyi maneno wala hana mchezo, lakini ninakubaliana naye na pia kutofautiana naye kuwa kwa dataz nilizonazo aliyehusika na "one on one" ni mwingine,

lakini huenda huyu anayemsema ndiye the originator, lakini facilitator ni mwingine kabisa, yaani "mzee wa mbeya" Mkuu wangu Mtanzania upo hapo?

Mkulu naomba utuwekee angalau vijihint
 
there is nothing but speculations....
who is sure that balali was given sumu?
who is sure that balali was even sick when he was in the US?
who is sure that balali died/ did not died on may 16( or 18 ...which ever)?

if anybody knows with a certinity, then they should give us facts with proof and not 'i will not mention the name' crap
 
Mkuu GT,

Naomba nikuombe radhi mkuu, shughuli zimenitinga sana, na ni jana usiku tu ndio nimemaliza kuziangalia vipande vyote vitano, havikuwa vinne kama nilivyosema mwanzoni, nisingeweka kitu ambacho sijakiona mwenye kwanza kwa sababu what if ndani kungekuwa na something else? Maana binamu yangu mmoja aliwahi kumpa baba yangu film akamsafishie u-China kumbe hakuangalia vizuri kuwa amempa film ya watu wako uchi ikaishia kuwa aibu kubwa sana, kwa hiyo toka siku hiyo huwa ninajaribu kuwa careful mkuu,

Muda wa kuanza kuweka huko Tube sina mkuu, isipokuwa nimejaribu kuwasiliana na wenye kuweza, nia na madhumuni yangu ni kutaka iwekwe hapa JF, kwa hiyo soon itawekwa tu mkuu, au una hoja nyingine mkuu? nifahamishe tu mkuu!

naona inakaribia wiki..hivi si unajyo kwenye CD hiyo Video? kwa nini usiende kwenye internet cafe waambie wakuwekee kwenye Youtube au google video


Ni free na hauchajiwi...
 
Nimetoa hint ya kutosha hapo, wakati mwingine na sisi tujaribu kufikiri na kutafuta pia, tuache uvivu, ninamtafuta Ngurumo sasa hivi ili ku-compare notes kwanza!
 
naona inakaribia wiki..hivi si unajyo kwenye CD hiyo Video? kwa nini usiende kwenye internet cafe waambie wakuwekee kwenye Youtube au google video

Ni free na hauchajiwi...

Mkuu GT,

Nia ni kuiweka hapa JF, kuna wanaoweza kufanya hivyo na watafanya hivi karibuni, kwa wale walioniomba copy naomba kusema hivi, siwezi kuirusha hewani ikakufikia sasa jaribu kufikiri kabla ya kunitumia ujumbe!
 
Huu mtandao ni mnene sana na nilitabiri wana JF kutegwa!
Kila ninalotabiri ndugu zangu sijui kwanini hutokea!
Sasa hapa ni mwendo wa rumours after rumours hadi watu wachoke...Inawezekana nia ni kuwachosha watu kwa mi information isiyokuwa na kichwa wala miguu na kuwa throw out of the real point..Ikishindikana then tujaribu kusije kukatokea watu watakaoipelekea JF kufungwa kwasababu hilo halitazima moto..Bali kuuchochea!
 
Anayeamini kuwa aliyefanya hivi ni ni RA ameuzwa na hajakaa chini kufikiri. Ngojeni wengine tutakapoandika ndipo dots zitakapounganishwa. Katika kutafuta majibu naomba niwape clue mbili:

a. Ni nani sources za habari za Ballali, ugonjwa wake, sumu, kifo, n.k
b. What if the misinformation of Tanzania haikuanza wiki iliyopita au baada ya Ballali kuondoka?


sasa hivi lengo ni kuhamisha kidole toka kwa mhusika mwenyewe na kukielekeza kwa mtu mwenye jina baya. Nilipokuwa mdogo tuliishi jirani na jamaa mmoja ambaye alijulikana kuwa ni mwizi. Lakini huyo jamaa pia alikuwa ni mjenzi. Sasa alikuwa anaiba na kujenga au anapopewa nafasi ya kujenga anaiba pia cement nk na kujenga kwake.

Sasa sisi tukafikiria kwanini tusimpe huyu jamaa ujenzi wa nyumba yetu? Tulipompa ujenzi na kumsimamia kutwa nzima wizi mtaani ulipungua. Lakini siku moja tukiwa kwenye kumwaga zege kutwa nzima na makarai yale... tunarudi mtaani (tulikokuwa tunajenga ni kama maili 3 hivi toka kibanda cha zamani) basi mtaani walipomuona jamaa watu wakaanza kumpigia kelele kuwa amewaibia mchana huo. Hilo lisingewezekana kwani karibu watu 20 walikuwa naye kwenye ujenzi wetu.

Lakini wakajitokeza hadi mashahidi kuwa walimuona huko. Ni baada ya hekima ya wazee ndipo ilipogundulika kuwa mwizi alikuwa ni mtu mwingine mtaani hapo ambaye alikuwa anatumia "sifa mbaya" ya fundi wetu kujitajirisha na yeye akijua kuwa akiiba atakayelaumiwa ni "mwizi anayejulikana".

so, in this case kuna jaribio la kumfanya RA ndiye mwizi wao!! na mwizi mwenyewe anaendelea na mikutano, yuko Bubu, na hakuna mtu atakayethubutu kuandika kichwa hicho cha habari bila kutiwa kashkash.
 
Wale waliokuwa wakifurahishana kuwa tusahau kuhusu kifo cha Ballali kwasababu alikuwa huru na haikuwepo haja ya kuwa shaidi wa kwanza ama mtuhumiwa ama "A key suspect" kama walivyosema wanasheria wetu then wajiulize upya?
Wakina MKJJ kujaribu kufunika ukweli na kudhalilisha wengine kwa maneno ya kejeli kuwa tunaota!
Sasa hawa wanasheria ambao we think the same nao wanaota?

Serikali inaficha ukweli – Wanasheria

na Mwandishi Wetu



BAADHI ya wanasheria wameshangazwa na usiri wa serikali kuhusu kuugua hadi kufa kwa aliyekuwa Gavana wa Benki ya Tanzania (BoT), Dk. Daudi Ballali.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima Jumapili mwishoni mwa wiki, wanasheria hao walisema lazima serikali inaficha jambo kuhusu Dk. Ballali.
Mmoja wa wanasheria hao, Mabere Marando, alitoa lawama kuhusu ukimya wa serikali, katika kuugua hadi kufariki dunia kwa Dk. Ballali, na kuongeza kwamba kutawafaidisha watuhumiwa wa wizi wa fedha katika akaunti ya malipo ya madeni ya nje (EPA), uliofanyika BoT.
"Nimesikitishwa sana na kifo cha Dk. Ballali, alikuwa Mtanzania mwenzetu. Lakini kinachosikitisha zaidi ni ukweli kwamba kifo chake kitaathiri sana uchunguzi wa wizi wa fedha za EPA.
"Ukimya wa serikali kuhusu kuugua hadi kufa kwa Dk. Ballali, unashangaza, ni wazi kuwa kuna jambo inaficha, kwa sababu haiwezekani isijue mahali alipo gavana wake wakati ilikuwa ikimlipia sehemu ya gharama za matibabu kama tulivyoelezwa na gavana wa sasa," alisema Marando.
Alieleza zaidi kuwa kitendo cha tume iliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete, kuchunguza tuhuma hizo kutomuhoji Dk. Ballali hadi mauti yalipomkuta, nacho kinashangaza, kwa sababu alipaswa kuhojiwa kwanza, kwani alikuwa shahidi muhimu katika kesi hiyo.
Mwanasheria mwingine wa serikali aliyeomba jina lake lihifadhiwe, alizungumzia suala hilo na kusema ni jambo la ajabu kwa timu inayochunguza kashfa ya EPA kutomuhoji Dk. Ballali hadi anakufa.
"Huyu alikuwa ‘key' katika uchunguzi huu, timu ya rais ilipaswa kumuhoji mapema kabisa, inashangaza kusikia mpaka anakufa hakuwahi kuhojiwa na serikali inasema haimtafuti.
"…Huu uchunguzi unaofanywa ni lazima utiliwe shaka na mjuzi yeyote wa mambo ya kisheria. Uchunguzi unaofanywa ni kama mchezo fulani hivi! "Na hapa wa kushakiwa kwanza ni serikali, haijulikani inaficha nini kuhusu huyu ndugu yetu, kwa sababu tangu alipougua mpaka anakufa, habari zake zimekuwa siri kubwa," alisema na kuongeza kwamba, ni ajabu kwa serikali kutokujua alipo mtuhumiwa wa wizi wa mabilioni ya shilingi. Alisema, hata taarifa zilizotolewa kuwa amefutiwa hati ya kuishi Marekani ziliongeza mashaka, kwa sababu alitakiwa kuondoka nchini humo baada ya kutotambuliwa, lakini hadi anakufa alikuwa huko. Aidha, aliwataka Watanzania kuihoji serikali kwa nini ilifanya siri matatizo ya kuugua hadi kufa kwa Dk. Ballali, na kuongeza kwamba Marekani inatakiwa kutoa taarifa za uchunguzi wa kifo chake ili wananchi wajue, kwa kuwa ni haki yao kufanya hivyo.

Kati ya hayo niliyo highlight hapo juu ambayo wanasheria hao wameyasema kuna ambalo sijawahi kulizungumzia hapa jf?

Sikusema kuwa itakuwa vipi serikali imlipie Ballali gharama za matibabu halafu isijue kilichomsibu?
Bilii zote za matibabu serikali ni lazima inazo na inajua everything!
Wanajidahi kuwa hawajui...Fool me once..Shame on you..Fool me twice shame on me.
 
there is nothing but speculations....
who is sure that balali was given sumu?
who is sure that balali was even sick when he was in the US?
who is sure that balali died/ did not died on may 16( or 18 ...which ever)?

if anybody knows with a certinity, then they should give us facts with proof and not 'i will not mention the name' crap

[FONT="Comic Sans M[B][B]gaijin,

In his resignation letter to the president, Balali mentioned sickness as a major factor that has forced him to resign.[/B][/B]S"][/FONT]
 
there is nothing but speculations....
who is sure that balali was given sumu?
who is sure that balali was even sick when he was in the US?
who is sure that balali died/ did not died on may 16( or 18 ...which ever)?

if anybody knows with a certinity, then they should give us facts with proof and not 'i will not mention the name' crap

We unaongea lugha ya kigeni hapa. Nakuelewa kwa mbali ni kama lugha ya Mantiki. Kama nimepatia, basi hatuongei hiyo lugha hapa. Ni sawa na kumwongelesha Mhabeshi Kidachi. Hatokuelewa!

Wazungu waliobobea kwenye elimu za Sayansi wanaamini Elvis Presley kajificha na Tupac. Itakuwa sisi wenye asili ya imani za Kichawi Chawi na kuamini yasiyo thibitika?

Ili tuelewane na hiyo lugha yako ya kigeni, kwanza tupe Kamusi ya Mantiki-Kiswahili au Logic-English Dictionary!
 
Ndio maana wa Kenya huwa wakituita wa Tanzania kuwa waswahili maneno mengi.....sasa ndio ime click in my mind
 
Back
Top Bottom