Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kinyamana,

Ukisoma postings za FMES jana utagundua na yeye hana uhakika tena. Anajiuliza maswali kama ya kwetu.

Ukiona mttu kama Mwafrika wa Kike ambay kuna wakati hawakuwa critical sana kwa Ballali ukilinganisha na mafisadi wengine. Ukiona na yeye anaanza kutilia mashaka kifo chake, jua hapo kuna tatizo kubwa sana.

Kama Ballali angelikufa naamini watu kama Mwafrika wa Kike wangealikwa kuuaga mwili wa marehemu.

Usalama wa taifa wako wapi? Balozi wetu anaenda kuimba kanisani akiliimbia gogo? Kweli nchi ya JK imefilisika kwenye kila idara.

Nakwambia wewe acha tu..... usanii wa hali ya juu hadi inatisha. Sasa hakuna ujanja tena. Usalama wa taifa wakishindwa kufanya kazi hapa basi wana JF tunaenda hadi kwenye vina vya habari kupata ukweli na kuuweka kwa hapa kwa niaba yao.
 
jamani mnatutisha! kuna gazeti moja la udaku nadhani ni risasi au sani sina uhakika niliiona mtaani leo, mbele kabisa kuna picha inayoonyesha jeneza lenye mwili wa bilali ukiwa altareni kwenye kanisa kuu la st stephen the matyrs, washington dc. tena wakasema mazishi yeke yalitumia masaa sita, mpaka watu wakachoka kufuatilia ibada.

sasa mwafrika wa kike tueleze kama nalo hili ni bonge la move.

siwezi kukataa kwa hili la mwafrika mwanamke, kwa kuwa mafisadi wa tz wanaishi mwezini, wakati sisi tunaishi hapa ardhini. mtu kuwa na 50bilioni kwenye akaunti yake, anaweza kutengeneza move moja nzuri kuliko zile za hollywood.

mh, mbesaaa

Kila kitu hapa kinatengenezwa kwa uangalifu mkubwa sana ila wanasahau kitu kimoja kuwa hawako peke yao katika hii dunia. Serikali ya Tanzania katika level ya juu kabisa inahusika na kila kitu hapa na ni swala la muda tu kabla kila kitu hakijaanza kuwageuka na kuwaaibisha.
 
Clue 3: Serikali ilipokuwa inalipia gharama za hospitali "Boston," hundi ilisema "pay to the order of...."?

hapa ndipo watu watakimbia nchi kwenye issue ya malipo ya gharama za hospitali... hii ya "Boston".....

Ninaomba tu wabunge wote wa upinzani na ccm wajiandae kwa mgongano mkubwa sana na serikali kuu katika hii issue.....

yanaendelea....
 
Kama balali hajafa basi huko kwetu huko tunaita uchuro! basi kajichuria na atakufa kiukweli sooner. Mafisadi wangekubali tu kufilisiwa na kwenda keko kuliko huu ufungwa wa kujisingizia kifo, ni kifungo zaidi ya kifungo cha gerezani.

Kweli mama,

Kuna wengi tu wanaoshangilia kwa kudhani kuwa wamempata Ballali katika hili swala kumbe na wao siku zao zinakuja karibuni ....... aibu kabisa. Afadhali kuishi maisha ya uadilifu kuliko kufikia kiwango hiki. Faida ya mapesa mengi ni nini sasa kama watu wanakuwa wanategemea kifo cha mwenzao au cha kwao binafsi ili kuishi kwa "amani, na raha mstarehe"....

grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
 
Clue 2: Nani alisema ilikuwa inatumiwa "hundi" kufanya malipo?

balali hakuwa mfanyakazi wa siri-kali hadi 'umauti' ulipomfika, so sidhani kama kulikuwa na hundi ya malipo toka kwa siri-kali. Kama alifia hospitali, lazima kuwe na kumbukumbu za kifo, na kama kafia nyumbani, nani alithibitisha kifo chake? kama kifo hakijathibitishwa kuna uwezekano kuwa wamemzika akiwa hai?
 
.....tena wakasema mazishi yeke yalitumia masaa sita, mpaka watu wakachoka kufuatilia ibada.
Mwikimbi, Kubadili 'living organism' to 'non living organism' while leaving no trace in a single day is hard work!!
 
Wana JF,

Imefikia wakati ambapo maamuzi machungu inabidi yafanyike hapa JF na kama itawezekana kwenye media za nyumbani. Kwa zaidi ya wiki moja sasa mimi na baadhi ya wana JF hapa tumekuwa tunafanya uchunguzi kuhusu uhakika wa habari za kifo cha aliyekuwa Gavana wa benki kuu - Dr Ballali. Wakati haya yakiendelea, mimi nilizikubali na kuziamini (msisitizo zaidi kwenye imani) habari za kifo cha Ballali ambazo ziliwekwa hapa na Invisible.

Kulingana na taarifa, vyanzo vya habari, mipango ya mazishi, sala na maombi kwa marehemu ambavyo vyote viliwekwa hapa JF, imani yangu ilizidi kukua na kupelekea uamuzi wa kukubali kuwa Ballali amekufa. Hata hivyo, uchunguzi wa siri unaonyesha utata na usiri mkubwa sana kwenye ugonjwa na hatimaye kifo cha Ballali. Kila nafasi na gharama iliyotumika kupata hii habari imefikia kwenye mwisho mfu (dead end) na mchanganyo ambao haustahili kuwepo hapa.

Binafsi niliahidi kuwa nitaomba msamaha hapa JF kama itathibitishwa kwangu kuwa Ballali yuko hai. Naomba sasa niseme kuwa sina sababu ya kuthibitishiwa kuwa Ballali yuko hai ili niombe msamaha kwa kuamini kifo cha Ballali. Pamoja na kuwa sina hakika kwa sasa kuwa Ballali yuko hai, lakini pia ni vyema ikiwa wazi hapa kuwa sina hakika (na sikufanikiwa kupata uhakika kwa asilimia mia moja) kuwa Ballali amekufa. Juhudi zote za kutafuta hili na lile kuhusu kifo cha Ballali zinafikia mwisho na mlango mzito sana wa kufungua ili kujua ukweli. Na kwa hili, naomba msamaha kwa wana JF na watanzania.

Nimekuwa natumia sana neno imani (kuwa na hakika na yasioonekana) katika hii issue ya Ballali. Niliamini kifo cha Ballali na imeshindikana kupata uhakika wa kutosha kufikia hitimisho la kifo chake. Kwa hili, naomba msamaha na kusema hapa kuwa sina imani tena kuwa Ballali amekufa. Nafasi nyingi sana zilijaribu kutolewa kwa Ballali kutoa story yake kuhusu yote yaliyotokea BoT. Kwa sasa kuna mengi yamepatikana na yatawekwa hapa JF kama ilivyo kawaida ya kila miziki inayopatikana hapa JF. Ila katika hili la kifo cha Ballali, naomba niseme wazi kuwa sina imani tena kama amekufa na kwa sasa ninapinga habari zote za kifo cha Ballali.

Kama vile ambavyo nilisisitiza kutolazimisha wasomaji hapa na watanzania walio nyumbani kuamini habari za kifo cha Ballali, sitafanya kinyume chake na kulazimisha watu kutokuamini kifo chake. Ninachosema hapa ni kuwa, safari zote nilizofanya kwenda Boston na baadaye DC kwenye ibada ya mazishi hazikunipa uthibitisho wowote wa kutosha kuwa Ballali yuko hai au amekufa. Nitaacha hili kwa wasomaji na watanzania kuamua waamini lipi kuhusu kifo cha Ballali. Ninachosema hapa ni kuwa, kuna juhudi kubwa sana zinafanywa na watu wakubwa kabisa katika serikali ya Tanzania na ya hapa Marekani ili habari nzima ya Ballali ibakie kuwa utata.

Hata hivyo, ningependa kuwakumbusha wale wanaodhani kuwa kifo au kupotea kwa Ballali kutapelekea hii case kuisha wajiandae kwa safari nyingine. Inajulikana kabisa kuwa Mramba, Mgonja na viongozi wakubwa serikalini kwa pamoja au kwa nyakati tofauti waliiidhinisha malipo toka benki kuu. Iko wazi kuwa auditing ya Deloitte ilisitishwa baada ya kugundua mambo mengi ambayo serikali haikutaka yajulikane. Inafahamika kabisa kuwa wahusika wa wizi wa BoT ni wengi sana na Ballali ni kipisi tu cha mkuyu mzima. Inafahamika pia wizi wa BoT sio wa EPA peke yake, kuna mengine mengi ambayo hayajafanyiwa uchunguzi.

Kupotea au kufa kwa Ballali sio mwisho wa huu mchezo na hii movie. Kwa sasa ndio mwanzo sehemu ya pili ya hii series inaandaliwa na wengine wote kwa kuanzia na mzee wa kula nyasi (Mramba), Mgonja na wenzake wajiandae kwa sehemu ya pili ambayo ndio kwa sasa wametia mafuta kwenye moto.

Huu ni mwanzo tu.....

Mwafrika wa Kike,

Kwanza ninakuvulia kofia (sina kofia, ila naivua kama ishara) kwa kazi yako nzuri.

Mimi pia sikuamini kwamba Ballali amekufa, kama ambavyo sikuamini kwamba Osama Ben Laden ndiye aliyehusika na the "controlled demolition" (sio terrorist attack) ya World Trade Centre, Pentagon, etc. Kuna conspiracy kubwa sana, na hii si theory, it is practical. Lakini kama ulivyosema, kuna utata mkubwa.

Kwa upande mmoja wa shilingi (kwa kuwa mahesabu "yao" bado hayajakaa vizuri), ninaamini kwamba Ballali hajafa, ila, mbinu zinafanyika tuamini kwamba amefariki, hususan kwa kupitia "mainstream media" ya Bongo. Bahati mbaya hakuna "underground media" other than JF, kwa hiyo, hata hao wa "udaku" hawawezi kufanya tathmini ya kina na kubaini ukweli.

Kwa upande mwingine, ninaamini kwamba "kifo" cha Ballali kimeletwa ili kuzima kesi ya ufisadi uliokithiri hapa nchini. Ballali ndiye shahidi mkuu kwenye kesi hiyo.

Jambo moja kubwa la kutatanisha ni uvumi kwamba Ballali ni raia wa Marekani. Kama hili ni kweli, ninashindwa kuamini kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliweza kumteua raia wa Marekani kuwa Gavana wa Benki Kuu, kazi ambayo ni nyeti mno?!!! Kulikoni?

Utata utata utata!

Bado kuna utata mwingine, maswali bado ni mengi... suala la Serikali kuhusishwa na maziko ya Ballali, suala la Serikali "kushauriwa" na familia ya "marehemu" kabla ya habari za kifo chake kutangazwa rasmi... Utata utata utata!

./Mwana wa Haki!
 
balali hakuwa mfanyakazi wa siri-kali tangu hadi 'umauti' ulipomfika, so sidhani kama kulikuwa na hundi ya malipo toka kwa siri-kali. Kama alifia hospitali, lazima kuwe na kumbukumbu za kifo, na kama kafia nyumbani, nani alithibitisha kifo chake? kama kifo hakijathibitishwa kuna uwezekano kuwa wamemzika akiwa hai?

nani alisema balali hakuwa mfanya kazi wa serikali mpaka umauti unamfika?
 
nani alisema balali hakuwa mfanya kazi wa serikali mpaka umauti unamfika?

si alifukuzwa ajira yake ya udalali pale BOT, au nalo lilikuwa changa la macho. Maana siku hizi hakuna kuingia ndani au kukaa nje unaweza umbuka hivi hiiivi, ilobaki ni kukaa mguu mmoja ndani mwingine nje.
 
Narudia kauli yangu ya awali ktk threads nyengine kuhusu kifo cha balali.
"nilipokuwa mtoto ilikuwa ni rahisi kudanganywa, ila sasa nimekua na sidanganyiki kama mtoto"
Ilipita mwezi hapa since Mzee mwanakijiji aliposema kuwa anahisi Balali amefariki, baadae serikali kwa pupa ikaspeculate news kuwa kafa. Nikajisemea moyoni kuwa serikali imekurupukia hoja za JF. Na ukiangalia mwenendo wa mazishi na speculations zake inatia shaka.

Balali ana duel citizenship sasa mnataka niamini kuwa amekufaaaaa??? Serikali ya ki-secomedy
 
huu ni utata sana, unaweza kukuta hata MAREHEMU alihudhuria kwenye MSIBA/MAZISHI yake!
 
kwa kawaida Paka ni kiumbe mpole anayeishi na watu ndani ya nyumba.
Paka huyo huyo ukimfungia ndani ukaanza kumpiga akakosa pa kutokea utaona makucha yake.

Watanzania tumefungiwa ndani ya giza nene na siri-kali yetu.

Kwanza siri-kali kwa kutumia wizara ya fedha na BOT wametuibia fedha zetu nyingi sana.

Pili wanajitahidi kwa nguvu za fedha zetu kuficha wezi.

Tatu wanatumia fedha zetu kututukana na kutupa lugha za kebehi majibu ya kimatusi na kutuona hamnazo.

Umauti-plastic surgery wa Balali unaonyesha uuwaji wa siri-kali kwa raia wake. Haijawahi kutokea ktk historia mtu mwenye aliyekuwa na wadhifa kama ule kuzikwa na watu wasiojulikana. Kwani kila ambaye nimejaribu kuongea nae ama kwa simu ama kwa mdomo awe karibu ndugu, au balozi wa tz usa hakuna mwenye jibu huyu balali amefariki au la.

Balali yu hai anaishi sehemu isiyojulikana ama anasura nyingine.

Wakati umefika wa kurudisha siri-kali serikalini. Tugeuzi hiki chungu mpaka tuujue ukweli.

Kikwete alipokuja usa kwenye mkutano wa sullivan kati ya dec 11 to 13 alikutana na balali kwa sirikubwa sana. wakati huo Balali alikuwa akiishi kati ya dc na Maryland alikuwa mzima wa afya.

Paka anataka kujitetea.
Bila kwenda ikulu kwa hasira na kudai haki yetu sioni ushindi.
Amani haiji ila kwa ncha ya upanga.
Hakuna maendeleo yalifikiwa kwa kubembelezana.
 
Kweli Hiki Kifo Ni Utata Na Hata Mimi Sijaamini Kwamba Kilitokea, Kwa Sababu Kila Mtu (reliable Sources) Walikuwa Wanaleta Habari Tofauti Kwa Sababu Mpaka Leo Hii Sijui Balali Alifia State Gani? Ukiangalia Habari Za Kifo Chake Sijafahamu Alifia State Au City Gani Kwa Sababu Ndugu Zake Na Serikali Zilitoa Location Tofauti. Na Mpaka Sasa Sijamuona Fmes Na Wenzake Kuongelea Hii Thread, Hopeful Atakuja Na Habari. Na Nilishasema Kwamba Jinsi Jamaa Alivyo Controversial The Least Ambacho Ndugu Zake Wangefanya Ni Kuuonyesha Mwili Kwa Watanzania Woote Na Mwili Ungerudishwa Bongo Watu Waone, Lakini Jinsi Walivyofanya Ni Kuyeyushana Tuu Na Uongo Mtupu. Lakini Ipo Siku Ukweli Utajulikana Tuu
 
Kwenye thread moja niliuliza.... msimamo wa Anna Muganada kwenye hili swala zima uko wapi(Tangu tuhuma zimeanza mpaka kufukuzwa kazi kwa Ballali?
Lol, MwK ina maana Ballali alienda kwa wakwe wake wa zamani kufanyiwa plastic surgery?
 
Admin, pls sticky this thread so that whomever visit JF (including Mafisadi) iwe kifungua kinywa chao kwa mshangao!!
 
[QUOTE=MaMkwe;Aseme nini? Anatafuta umaarufu tu wa kisiasa. Wenzie tunamlilia ndugu yetu yeye anataka kuleta mzaha. Hivi hawa wanasiasa wa Bongo hawajui kifo?

HIVI UNAJUA KWAMBA MBOWE ANA DISTANCE RELATIONSHIP NA LATE GOV.MAANA GOV. MARRIED TO ANNA MUGANDA,WHO IS J.MUGANDA,FORMELY WITH VOA,WHO MARRIED TO FREEMAN SISTER...do a research utaona.just a lil bit of info.amani
 
Back
Top Bottom