Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Kifo cha David Balali: Kauli mbalimbali toka kwa watanzania

Watu walitaka mpaka Hashimu Thabiti ajue Balali kafa ndiyo wamini eeeh!

Pundit wananchi wako desparate kutafuta balozi wao mpya kwasababu wa sasa ameshindwa kazi yake
 
Mbona hakuna mwenye kusema Tanzania Daima ni ya nani?
 
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu peponi hayo masuala ya ufisadi yana muhusu yeye na mola wake

Wewe unataka mungu ampeleke fisadi peponi ili aende kuwaibia akina Nyerere? Kwi kwi kwi!!!
 
Mbona hakuna mwenye kusema Tanzania Daima ni ya nani?

Unauliza swali wakati jibu unalo? Utafiri ni mtihani wa GCSE hapa UK mwaka huu ambapo nyuma ya maswali waliweka majibu? Ingelikuwa Afrika wangetucheka sana. Inakuwaje board nzima ikafanya makosa kama hayo?
 
Kwahiyo mume wa dada yake Freeman ana dada ambaye ndio mke wa Ballali?
Kama ni hivyo kaaazi kweli kweli!
No wonder kuna unaoitwa mgogoro mzito ndani ya CHADEMA makao makuu!
Ndio haya?
 
Wewe unataka mungu ampeleke fisadi peponi ili aende kuwaibia akina Nyerere? Kwi kwi kwi!!!

kwi kwi kwi,

labda anataka aende peponi ili akachapwe viboko na Nyerere asubuhi na jioni kwa siku hamsini na sita (dont ask me why 56 days).
 
Unauliza swali wakati jibu unalo? Utafiri ni mtihani wa GCSE hapa UK mwaka huu ambapo nyuma ya maswali waliweka majibu? Ingelikuwa Afrika wangetucheka sana. Inakuwaje board nzima ikafanya makosa kama hayo?

No mambo huwa yanabadilika sometimes hata umiliki wa kampuni na usijue hadi ufanye uchunguzi!
Najua ilikuwa ya Freeman ila iyo connection ni wasiwasi tu kwasababu kutakuwa na conflict of interests hapo!
 
Sina La Kusema Huwa Nasikia Wakatoliki Wanaimba Mazikoni Ave Ave Maria Jamaa Walikuwa Wanamonita Safi Ndugu Kufika Tu Usa Jamaa Kafa What A Coinsidance?
 
Jmushi umekuwa na tabia ya kubadili sana mada hapa .Sasa hoja iliyoko si hii ambayo wewe unaulizia maswali yako .Hoja ni Yona Maro na mauza uza yake ndiyo issue hapa .TD unataka iwe issue kwa sababu ipi ? Mume ama shemeji pia havina nafasi hapa ika nafasi iko kwa hawa wanaotaka ku twist issues .
 
Naomba msamaha sana wakuu kama hoja hii iko hapa .Leo tangia kumekucha sijapitia hapa hii mail imeletwa kwangu kwa njia ya ku forward .Kuangalia nakuta ni shy ndiyo maana nikaja nayo hapa .

Mkuu Mwafrika Mke nisamehe sana Mkuu wangu.
Huyu mtoto mimi sina uhusiano naye maana naona kuna swali hapa ila nineipata mail yake nikaona nlete hapa.Haya ndiyo anayo yaeneza huku pembeni.

Hata Kenya hajawahi kufika leo anaongelea habari za US .Jamani njaa zingine hizi .Yaani nasema kama uchambuzi ndiyo huu basi mimi sitakaa nikataka kuwa mchambuzi tena .

Dont worry Lunyungu,

Nimekuelewa mkuu wangu!
 
Unauliza swali wakati jibu unalo? Utafiri ni mtihani wa GCSE hapa UK mwaka huu ambapo nyuma ya maswali waliweka majibu? Ingelikuwa Afrika wangetucheka sana. Inakuwaje board nzima ikafanya makosa kama hayo?

Mimi bado nasoma threads na posts zake taratibu sasa ili nijue nia ya maswali yake ambayo mengi ana majibu mwenyewe ni nini hasa!
 
Jmushi umekuwa na tabia ya kubadili sana mada hapa .Sasa hoja iliyoko si hii ambayo wewe unaulizia maswali yako .Hoja ni Yona Maro na mauza uza yake ndiyo issue hapa .TD unataka iwe issue kwa sababu ipi ? Mume ama shemeji pia havina nafasi hapa ika nafasi iko kwa hawa wanaotaka ku twist issues .

Naomba msamaha sana wakuu kama hoja hii iko hapa .Leo tangia kumekucha sijapitia hapa hii mail imeletwa kwangu kwa njia ya ku forward .Kuangalia nakuta ni shy ndiyo maana nikaja nayo hapa .

Mkuu Mwafrika Mke nisamehe sana Mkuu wangu.
Huyu mtoto mimi sina uhusiano naye maana naona kuna swali hapa ila nineipata mail yake nikaona nlete hapa.Haya ndiyo anayo yaeneza huku pembeni.

Hata Kenya hajawahi kufika leo anaongelea habari za US .Jamani njaa zingine hizi .Yaani nasema kama uchambuzi ndiyo huu basi mimi sitakaa nikataka kuwa mchambuzi tena .

Zote hapo juu ni comment zako!
We umeleta habari halafu unapanga itakavyojadiliwa!
Kwa hiyo si ungeifuta kabisa hiyo kauli ya Maro yenye ku suggest TD ina uhusiano na Ballali?
We na Mtanzania ndio mnanichanganya!
Sasa kinachojadiliwa hapa ni nini haswa?
Maana madai yako kuwa hoja ni ya Maro haijamaanisha kuwa hoja hizo ambazo ni contents za mjadala huu zisijadiliwe!
Ndio maana sipendi siasa na siwapendi wanasiasa!
 
Wakuu,

Naomba msifute hii thread, ni kwa ajili ya sisi tunaoamini kwamba Ballali haja. Lengo ni kujaribu kuunganisha dots pamoja na kujenga picha kubwa.

Hapa chini someni hii story ambayo naamini Anna Muganda aliisoma na kisha kuamua ku fake kifo cha Ballali.

Kama Ballali angelikufa, hii breaking news ingetangazwa na Mwanakijiji, kwanini Mwanakijiji aliamua kukaa pembeni?

Je wakuu kama akina Jasusi ambao huko nyuma wameonekana kujua mengi ya Ballali wamepotelea wapi?

Je Invisible alipata wapi habari za kwamba Ballali kafariki?

Kulingana na mimi wahusika Anna Muganda - Jasusi - Mwanakijiji - Invisible hivyo ndio habari za kifo cha Ballali zilivyosambazwa.

Poor lad Invisible, hakuelewa kwamba anaingizwa kwenye mchezo mkubwa zaidi na akaamua kututangazia umma kwi kwi kwi!!!!!

Ilikuwaje familia ya Ballali wasijue ndugu yao kafariki? Je Anna Muganda hana marafiki kazini, mitaani mpaka hii habari ya kifo cha mumewe isijulikane mpaka baada ya sikutano?

Haya endelezeni, ila kwamimi Ballali hajafariki na wakuu tunaowaamini wameamua kutudanganya hata sisi hapa JF.


Canoe widow's full confession: We faked death to clear debts and he hid next door for three years
By NATALIE CLARKE and DAVID LEIGH in Miami
Last updated at 16:17 08 December 2007


Anne Darwin: 'The lies just snowballed'

The breathtaking deceit of "back from the dead" canoeist John Darwin and his wife Anne can be revealed today.

For much of his missing five years, she says he was simply living at their home in Hartlepool ... and sharing her bed.


The 57-year-old ex-prison officer even brazenly walked along the beach near their home - his only disguise a woolly hat, a walking stick and fake limp. Yet his wife insists that their two sons were kept completely in the dark and spent five years grieving for their father.

In an astonishing interview, 55-year-old Mrs Darwin admits the couple were secretly living as husband and wife when an inquest declared him dead.

The former doctor's receptionist also knew her husband was alive and well when she cashed in a life insurance policy for £25,000 and had their £130,000 mortgage paid off by another life policy.

She said her husband plotted his disappearing act because of increasingly crippling financial debts but claims she was unaware he was actually going to carry it out - and genuinely believed he was dead after his canoe was found washed up in the North Sea.

Mrs Darwin was speaking in Miami on her way home from Panama and expects to be arrested on suspicion of fraud when she arrives back in Britain.

Cleveland police said her husband was "putting forward some sort of account" during questioning yesterday, and Mrs Darwin's claim that she was not in on his "Reggie Perrin"-style disappearance will be treated with extreme scepticism by detectives who were given 36 more hours to interview him.


Her incredible account raises questions which can be determined only by police and Mrs Darwin, who has not been paid by the Daily Mail for this interview, conceded: "Yes, I know it seems too incredible to be true, but it is."


Among other astounding revelations, she said her husband:

• HID in a bedsit in the adjoining house when family and friends visited the "widow"

• WAS literally next door when his grieving sons Mark and Anthony returned from his inquest

• INSISTED Mrs Darwin put the telephone on to loudspeaker when their sons rang so he could hear their voices

• BETRAYED her by flying to America to meet a woman after an internet flirtation;

• FINALLY returned to Britain and walked into a police station because he wanted to see his sons

Revealed: The REAL reason missing canoeist John Darwin came back from the dead... he wanted to see his sons
Canoeist 'tried to buy £45,000 luxury yacht in Gibraltar after he went missing'
The charges that could put the Darwins in prison and how even the 'dead' canoeist's father admits his son was always driven by money
Mrs Darwin admits there is a real chance she will go to jail - some offences with which the couple could be charged carry a life sentence.

"I am aware that could happen and I am absolutely terrified at the prospect," she said. "I feel I have been living a kind of prison sentence for the last five years, but that's been my own private sentence and the public one will now follow."

After almost a week of lies, half truths and prevarications, Anne Darwin says she has decided to come clean and has given the Mail a noholdsbarred account of what she says has been going on these past five years.

"I suppose it became a way of life," she said. "It was very difficult, though, and I was always terrified that we would be found out. I was always on eggshells when friends and family came to stay in case someone wandered into John's room and saw him."



DEBTS AND DISAPPEARANCEAccording to Mrs Darwin, her husband began to plan his sensational disappearing act in the beginning of 2002. The couple were tens of thousands of pounds in debt, largely brought on, she says, by problems with the bedsit rental business they ran.

She says Darwin, a former teacher who had joined the prison service, also had "lots of credit cards", indicating that he was more free- spending than she would have liked.


"We were struggling to make payments and there were late payment fees and bank charges that absolutely crippled us," said Mrs Darwin, who was working then part-time in a doctor's surgery and also had a part-time admin job in the health service.

Scroll down for more ...


Caught red-handed: The photograph taken in Panama last year which proved the couple had been lying

"At that time we had about 12 houses scattered around County Durham, they were rental investments but people were slow in paying us and when we moved to Seaton Carew in December 2000 it just became too much trying to look after all the properties and both of us trying to keep full-time jobs going as well.

"I had another part-time job. We tried desperately to keep our head above water but it got increasingly difficult."


Darwin believed the only way out of the mess was for him to "die" and for his wife to cash in on the life insurance.

"John said there was only one way out of the situation, and that was to fake his death. I pleaded with him not to do it, I said it was a wrong thing to do. I honestly didn't know what he'd planned or for when."


Darwin decided on a tragedy at sea scenario. On March 21 2002, he took his red canoe out on to the sea in front of the family home and disappeared.


The sea that day was described as "like a millpond", which prompted bafflement that he could have got into difficulties. The empty canoe was found weeks later.


Although she had known his thoughts, his wife claims she genuinely believed he had died. "I suppose I didn't want to believe that he might have actually done it," she says. "I genuinely thought he had had an accident."



RETURN OF THE PRODIGAL HUSBAND

Under arrest: Police are still questioning Mr Darwin over his missing five years


Just under a year later, in February 2003, there was a knock on her door. It was Darwin. "He was an absolute mess, he was so dishevelled. I didn't even recognise him at first. It was such a shock.


"He had a beard, he was dirty, he was so thin, he looked like he'd been living rough. He smelt dreadful. When I asked him where he'd been he said it didn't matter, he was home now. He said he'd done it basically so that we didn't lose everything, which is rather ironic now.

"He had a bath, I fed him and he put some clean clothes on. I hadn't been able to part with his clothes.


"I had really thought he was dead, especially when they found the canoe and because of the state it was in.

"Now there he was, standing in front of me. Although I was pleased he was still alive, I think deep down a part of me was always angry. To think of what he put us all through. He had basically come back expecting me to forgive him."

Darwin, it turned out, was hoping that by now the insurance policy would have paid out and he and Anne would live happily ever after, albeit in a low-key, invisible kind of way.

But she says he was upset. "He broke down and cried and said he was sorry for all the upset he'd caused.

"I wanted at that point to report everything he'd done but he threatened to say I'd been involved from the beginning. So I was trapped."


Over the next few days, there were arguments and recriminations, but the upshot was that Mrs Darwin agreed to keep her mouth shut and became complicit in the scam.

Most unfathomably of all, she agreed not to tell her two sons that their father had returned from the dead. Why? She says she did it out of love for her husband.

"My biggest mistake has been trying to protect him. It was so hard not to tell the boys. But John was adamant I mustn't tell them."

Why did he not want them to know? "Well, I suppose he didn't want them to turn him in.

"He told me just to go along with the story and not to tell anyone he was back. It was just so hard not to tell the boys but he was adamant I mustn't tell them."




INQUEST AND INSURANCE

Deceit: The Darwins' sons Anthony and Mark apparently remained oblivious that their father was alive

For the first three months after he turned up, Darwin used to "come and go" before moving back in for good.

"I always knew if he had been because I would find food missing, and if I had left any money around, he would take that too.

"John had his own key which he used to get in and out. I do not know where else he was living at that time, he never told me. I don't know if he had any transport of his own. As far as I know he didn't as he would always arrive on foot.

"Often when he was with me it was very difficult.

"Yes, we had arguments, but despite everything I still loved him.

"He lived at the house with me for three years. We lived as man and wife.

"There were a few hairy moments and I lived in fear of being found out. Most of the time I used to be frightened to even open the door.

Right away Darwin told his wife he was eager for an inquest into his demise to take place so that she could claim the life insurance. Two months later, in April 2003, a hearing was held at Hartlepool County Court.

"After John's disappearance, I had been pushing for an inquest - long before he turned up again - because I couldn't cope with it any longer and I needed to be able to get on with my life. "

Egged on by Darwin, she managed to have him declared presumed dead after persuading the coroner to make an application to the Home Office to do so without waiting the usual seven years.

"John said if we got the money from the insurance payouts and cleared our debt, we could find a way back then we could start over again. Initially I said I couldn't go through with it.

"He didn't take out life insurance policies with a view to then disappearing. We had to take out life insurance when we moved house in 2000.

"When they did finally pay out, because there was no body, the life insurance people would only pay half of it, £25,000.

"We also had a mortgage of £130,000 and that was paid off. Not having a mortgage made the burden more tolerable."

Mrs Darwin was working, and now she had a widow's pension.


TUCKED AWAY IN HIS LITTLE BEDSITIt was official - John Darwin was no longer of this world.


But on the day he was declared dead he was, his wife says, tucked away in his little bedsit within the family home.

"On the day of the inquest, John stayed at home but I didn't actually see him that day because Mark and Anthony were staying with me in the main house. He used one of the bedsits."



The Darwins owned two large adjacent houses; one the seven-bedroom family home and the other divided into 15 bedsits. The passage between the master bedroom and Darwin's bedsit was a 5ft high, 18in wide coffin-shaped hole hiden by a wardrobe with a false back and locked with a coat peg.

It was crudely boarded up with breezeblocks before the next-door house was sold.

It would have been perfectly possible for Darwin's sons to have unlocked the door and seen their father.

Once her husband had moved back in, they settled into a routine. Mr Darwin spent most of the time indoors, reading books, surfing the internet, watching daytime television and doing odd jobs about the house.


"He was used to being outdoors and he was going stir crazy trapped inside all the time. When he went out he would disguise himself sometimes by taking a walking stick and walking with a limp.

"When it was cold, he would put on a woolly hat and pull his collar upwards.

"But during the summer months he could barely get out.

"Seaton Carew was very busy at that time of the year and there were always lots of people about.

"I often had family or friends staying with me, which meant I was always walking on eggshells in case someone should catch a glimpse of John."

NINA UHAKIKA ASILIMIA 100 BALALI HAJAFA.NAANGALIA TU USANII UNAVYOFANYIKA NA WATU WANARUKIA STORI TU KWA SABABU MTU FLANI KATANGAZA JAMBO,JAMANI AMKENI NDUGU ZANGU
 
usimsahau na Lunyungu aliyekuja na bandiko la FMES kwa sahihi ya shy..

Si umeona vitu? Ameshakuja kutoa maelezo kuwa hii ni email amepokea toka kwa SHY na kumbe Shy alikopi maandishi ya FMES hapa JF.

Asante Kamanda kwenye hili!
 
kwi kwi kwi,

labda anataka aende peponi ili akachapwe viboko na Nyerere asubuhi na jioni kwa siku hamsini na sita (dont ask me why 56 days).

Mie naomba aende AHERA na huko amkute Dito na wavalishwe gauni kama la Adolf Hitler. Kila siku asubuhu wanachora saba na kutumbukiziwamo nanasi...
Huko wamsubiri Mugabe na wale viongozi wa Burma (Mynmar).
 
•
Mwili wa Balali kuchomwa moto leo

*Heshima kutolewa Kanisa la Mtakatifu Stephen
*Ratiba yaonesha ndugu wa karibu tu kuhudhuria

Na Joseph Lugendo

ALIYEKUWA Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Dkt. Daudi Ballali anazikwa leo mjini Washington DC, Marekani na huenda mwili wake ukachomwa moto kwa mujibu wa taratibu za makaburi anakozikwa.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha kuaminika kutoka nchini humo, mwili wa marehemu uliohifadhiwa kwenye nyumba ya maziko ya De-Vol iliyoko mjini humo unatarajiwa kuagwa leo saa 4 asubuhi kwa saa za Marekani katika Kanisa Kuu la St.Stephen Martyr 2436 Pennsylvania Ave,NW Washington, DC 20037.

Heshima za mwisho zitatolewa kanisani hapo baada ya misa na zitahusisha ndugu jamaa na marafiki wa karibu tu na sio hadhara ya mtu yeyote anayetaka kushiriki.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Bw.Ombeni Sefue ataongoza waombolezaji kutoa heshima hizo akifuatiwa na watumishi wa Idara mbalimbali alizowahi kutumikia marehemu Ballali alipokuwa akifanyakazi kwenye Shirika la Fedha Duniani (IMF), ndugu zake waliowasili Marekani siku chache zilizopita na Watanzania wachache wanaoishi Washington DC.

Baada heshima za mwisho mwili huo utapelekwa katika makaburi ya Wakatoliki ya Get of Heaven eneo la Silver Spring, MD. Hata hivyo haijajulikana kama mwili huo utachomwa moto ama utazikwa kiafrika kwa kuteremshwa kaburini kwasababu huduma zote mbili zinakubalika katika makaburi hayo.

Ikiwa atachomwa moto, majivu yake hayataruhusiwa kugawanywa bali yatateremshwa kaburini kwa mujibu wa taratibu za kikatoliki.

Wakati huo huo chanzo chetu kingine kilichokarubu na familia hiyo hapa nchini kilidokeza kwamba mazishi hayo yamesababisha mgawanyiko na mvutano mkubwa ndani ya familia yake.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, mvutano huo sasa umeigawa familia hiyo katika makundi makuu mawili yanayopingana.

Mvutano huo umesababishwa na kutokubaliana kulikojitokeza baina ya makundi hayo ya familia juu ya mahali anapopaswa kuzikwa Dkt. Ballali.

Mtoa habari wetu alisema upande unaoongozwa na mke wa marehemu Bi Anna Muganda ulitaka Dkt. Ballali azikwe nchini Marekani alikofia wakati upande wa ndugu zake walitaka mwili wa marehemu urejeshwe nchini kwa maziko.

Akizungumza kwa simu na Majira jana jioni, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Patrick Mombo, alisema amezungumza na Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani lakini nao haukuwa na habari zozote juu ya mazishi ya Dkt. Ballali.

"Nimezungumza na Balozi, alikuwa akielekea ofisini lakini hakuwa na taarifa zozote za mazishi, sasa hivi kule ni asubuhi, nikipata taarifa yoyote nitakueleza," alisema Balozi Mombo.

Juzi Serikali katika nyakati tofauti ilitoa taarifa rasmi za kifo cha Dkt. Ballali kilichotokea Ijumaa ya wiki iliyopita Mei 16, mwaka huu.

Katika taarifa iliyotolewa na Ikulu, Rais Jakaya Kikwete alielezea masikitiko yake juu ya kifo hicho na kuelekeza kuwa taarifa zaidi juu ya mazishi yake zitatokana na uamuzi wa familia yake.

Kwa upande wa BoT, Ofisa Uhusiano Mwandamizi, Bw. Emmanueli Mwero naye alitoa taarifa ya kuthibitisha kifo hicho na kuahidi kutoa taarifa za mara kwa mara juu ya kitakachokuwa kikiendelea.

Watu mbalimbali waliotoa maoni juu ya kifo hicho, licha ya kuitaka Serikali kufanya uchunguzi ili kupata taarifa zaidi pia walipendekeza mwili wake uletwe nchini kwa ajili ya mazishi.

Hata hivyo, kinyume na mtazamo huo wa wananchi, taarifa nyingine zisizo rasmi zilidai kuwa, Dkt. Ballali, enzi za uhai wake alipendekeza kama akifa, mwili wake usiletwe nchini.

Taarifa hizo zilidai kwamba mazishi rasmi ya Dkt. Balali yanatarajiwa kufanyika leo nchini Marekani.

Wakati huo huo serikali imelaumiwa kwa kupiga chenga msiba wa gavana huyo hasa ambaye ndani ya moyo wake alikuwa na taarifa muhimu kuhusu yaliyojiri katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

"Huyu alikuwa ni mtu muhimu hivyo serikali haikupswa kukaa kimya...kwa kweli hili limetusikitisha sana," alisema Kiongozi wa Upinzani Bungeni na Mbunge wa CUF, Bw. Hamad Rashid Mohamed, alipozungumza na gazeti hili.

Alisema walitegemea serikali ingetoa tamko hasa kwa kuzingatia kuwa gavana anateuliwa na Rais, hivyo hilo ni jukumu la serikali kuueleza umma kuhusu yaliyotokea badala ya kuiachia taasisi.

Bw. Rashid alisema hata kama serikali haikuona umuhimu wa kuwapatia taarifa wananchi basi ilistahili kuwaeleza jinsi ilivyosikitishwa na kifo chake hasa kwa kuzingatia kuwa kimetokea katika kipindi muhimu na uchunguzi ya 'madudu' yaliyotokea ndani ya akaunti ya EPA ukiwa unaendelea.

Alisisitiza kuwa Dkt. Ballali alikuwa na taarifa muhimu kuhusu EPA, hivyo serikali ilipaswa kutolea taarifa kifo hicho. "Watanzania walipaswa kuambiwa tangu kuugua kwake hadi kufariki," alisisitiza.

Alisema inawezekana ameacha wosia na nyaraka mbalimbali hivyo ameitaka serikali kuunda tume ya kuchunguza kifo chake. Ameshauri tume itakayoundwa itoke miongoni mwa wabunge.
 
Slaa: Tume ichunguze kifo cha Daudi Ballali




na Mwandishi Wetu



KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amependekeza kuundwa kwa tume huru ya kimataifa itakayochunguza mazingira ya kifo cha Gavana wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Daudi Ballali.

Akizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa ambaye ni Mbunge wa Karatu, alisema umuhimu wa kuundwa kwa tume hiyo unatokana na utata uliozingira habari zote zinazomhusu Ballali tangu alipoondoka hapa nchini Agosti mwaka jana.

Dk. Slaa, mwanasiasa aliyeibua tuhuma kadhaa dhidi ya Ballali, na mmoja wa wanasiasa waliokuwa mstari wa mbele kutaka kurejeshwa nchini, ili aje kujibu tuhuma mbalimbali zilizokuwa zikimkabili, ikiwa ni pamoja na kusaidia uchunguzi wa wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya BoT, alisema kifo chake kabla ya kukamilika kwa suala hilo, ni pigo kubwa.

'‘Tunaiomba serikali iunde tume ya kimataifa ili ukweli ujulikane. Huyu ni mtu mkubwa, ana siri nyingi za taifa. Anahusishwa na ufisadi. Hatuwezi tukaliacha suala hili likaachwa hivi hivi tu.

'‘Kama serikali imeficha ugonjwa, hospitali na hata hicho kifo ambacho taarifa zake zimepatikana baada ya siku nne, tunataka tume huru iundwe ihusishe majaji na watu wenye heshima katika jamii ya kimataifa," alisema Slaa.

Mwanasiasa huyo ambaye ndiye aliyesoma orodha ya mafisadi mwaka jana na kuibua mwamko wa kipekee katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi, alirejea kauli aliyopata kuisema siku zilizopita kuhusu Ballali na umuhimu wake wa kumrejesha hapa nchini wakati akiwa hai.

'‘Nilipata kusema huko nyuma, na leo narejea tena kulisema hili kwamba, iwapo Ballali atakufa kabla ya hajarejeshwa nchini kujibu tuhuma za ufisadi ndani ya BoT na hata kabla hajahojiwa na Kamati ya Mwanasheria Mkuu inayochunguza kashfa ya EPA, basi damu yake itakuwa juu ya serikali," alisema Slaa.

Alisema mwenendo mzima wa namna serikali na Rais Jakaya Kikwete walivyolishughulikia suala zima la Ballali, kuanzia kuondoka kwake kwenda nje kwa matibabu, kulazwa na baadaye kufa, ni jambo linalotia shaka na kuibua maswali mengi.

Mwanasiasa huyo alisema anaamini haiwezekani Ballali, ambaye ugavana wake ulitenguliwa na si kufukuzwa, aende nje kwa matibabu na alazwe pasipo serikali kupitia Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Marekani, kujua mahali aliko.

Alisema anaamini kwamba gharama zote za matibabu ya Ballali zilibebwa na serikali, kwani hata baada ya uteuzi wake wa ugavana kutenguliwa, aliendelea kubakia kuwa mtumishi wa serikali.

'‘Hiki kiini macho cha serikali kudai eti hawajui alikokuwa amelazwa na anakoishi Ballali, ni ushahidi wa wazi kwamba serikali ilikuwa inaficha jambo.

'‘Walikuwa wakijua aliko, na walifanya hivyo wakijua kwamba iwapo angerejea angeweza kutoa siri kwa kuwataja wahusika wengi, na hivyo kuleta mtikisiko mkubwa serikalini," alisema Dk. Slaa.

Aliilaumu serikali kwa kutoa taarifa nyingi zinazokinzana kila mara waandishi wa habari walipokuwa wakifanya juhudi kubwa katika kufuatilia alikokuwa gavana huyo wa zamani wa BoT.

Alisema uamuzi wa serikali kukaa kimya kwa muda mrefu pasipo kutoa taarifa hata baada ya Ballali kufa, ni ushahidi mwingine wa namna ilivyokuwa ikishikwa na kigugumizi kuhusu suala hilo.

'‘Ninachosema hapa ni kwamba, wakati serikali inapotoa majibu yenye utata na yenye kupingana, haijawahi kusimama na kusema aliyeondoka ni mtu wetu, Mtanzania mwenzetu. Ni kwa nini serikali ilikuwa haifuatilii? Kwa nini ubalozi haukufuatilia? Unaweza kuona namna serikali inavyojaribu kuficha jambo," alisema Dk. Slaa.

Alisema ni jambo la ajabu kwamba, maofisa wa ubalozi wamekuwa wakifuatilia kwa karibu kila mara Watanzania wanapokwenda India kwa matibabu ya moyo, tena kwa watu wa kawaida kabisa na hivyo kuzua maswali ni kwa nini kwa Ballali hali ilikuwa ni tofauti.

Kama hiyo haitoshi, Dk. Slaa alieleza kushangazwa na kifo cha Ballali ambacho kimetokea siku chache tu baada ya kuwapo kwa taarifa za makachero kutumwa kumfuatilia nchini Marekani.

'‘Ni jambo lisiloeleweka sawa sawa na linalopaswa kutolewa maelezo. Haiwezekani tunasikia makachero wamekwenda kumfuata na siku chache baadaye kupitia katika mtandao tunaambiwa amefariki na kisha siku chache baadaye inatangazwa rasmi amekufa. Nini kimemuua? Serikali itujibu," alisema.

Alisema huko nyuma na hata katika mtandao kulikuwa na taarifa za mtu huyo kuwekewa sumu, jambo ambalo serikali pamoja na kutakiwa kulitolea ufafanuzi ilikaa kimya.

Alieleza kushangazwa kwake pia na hatua ya Kamati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali inayochunguza Kashfa ya EPA, kuwahoji watuhumiwa wengine na wamiliki wa kampuni 22, huku ikimuacha shahidi muhimu Ballali, katika muda wote wa miezi karibu mitano ya kazi yao.

'‘Ni kwa nini wanahojiwa akina Jeetu Patel na wengine wa makampuni 22, na hawa watu hawakuteremka BoT kama Roho Mtakatifu. Ninaamini Ballali angekuwapo angeeleza siri hizo," alisema Dk. Slaa.
 
Back
Top Bottom