Kifo cha ghafla cha Mfugale sawa na Prof. Chachage: Kuna viashiria vyote vya kupewa sumu. Serikali ichunguze

Kifo cha ghafla cha Mfugale sawa na Prof. Chachage: Kuna viashiria vyote vya kupewa sumu. Serikali ichunguze

Mimi sitaki kutilia shaka sababu nimeshuhudia watu kufariki ghafla tu tena sana mtu mzima mara anajisikia vibaya anapoteza maisha. Shida yangu moja tu kwa yule sijui katibu mkuu aliyekuwa anasimulia tukio. Kwa mujibu wa maelezo yake kajisikia vibaya akamwambia nenda ofisini kapumzike kikao kiendelee baadae akasema ngoja nikamwangali kaenda kamkuta kwenye kitu ila wazi hali yake sio nzuri akauliza wasaidizi kimetokea nini wakasema aliomba tu AC iongezwe iwe baridi basi akakaa mpaka alivyokuja na kumkuta.
Kuna mahali mmoja alisema according to him ... ngoja nimfuate na nitarudi naye hapa kwenye kikao ...... kwa hali hiyo kulikuwa na tuhuma ambazo late alitakiwa kujibu.....

Anyway mmesema afya yake alikuwa imedorora ukiongeza na hayo ya kikao lazima moyo ushindwe kuhimili.

Ameondoka ni nini kitafuata, muda utaongea.
 
Yaani unasema kabisa kuwa ni wazi amepewa sumu halafu unahitisha kwa kuomba uchunguzi?! We jamaa uko sawa upstairs!
Hauelewi kuwa kazi ya uchunguzi ni kuweka mambo kuwa wazi, sasa kama wewe unasema “ni wazi” tayari, unataka kuchunguza nini!
 
Umeeleza VIZURI ila naongeza uyu bwana sio maskini familia wanashindwa vipi kufanya uchunguzi binafsi wa ndugu yao hata KWA kupeleka mwili kenya ,ili mwisho wa siku waje na majibu mazuri , kwamba kama alitendewa Jambo baya wanafikili watapata majibu sahii,

Wafiwa poleni lakini pia yawabidi jiongeza , ili mpate chanzo au tatizo lililosababisha kifo chake , aliopokua wanasema hawajui tatizo Sasa mnashindwa vipi jiongeza kufanya uchunguzi binafsi wa marehem KWA kutumia watu Wengine nje ya tz
Ni kupoteza nguvu na kuongeza uchungu. Huwezi ishinda serikali kwa namna yoyote ile
 
Mwaka jana kuna watu wengi sana walikufa kwa covid-19 eneo ninaloishi. Kuna wakati mwanafunzi wangu aligua covid-19 nikaandika hapa kuwa huenda na mimi ni mhanga, watu wengi wakanitoa wakanipa moyo na kunishrui nitumie nyungu! Mungu ni mkuua alininususru, na namshukuru sana kwa hilo.

Covid-19 huwa haiui mtu kwa siku moja au mbili tu; inachukua muda wa kuanzia siku nane na kuendelea, kwani huanza na homa kabla ya mapafu kuanza kubana. Ile homa inaweza kuchukua siku nne au tano hivi kabla mapafu hayajaanza kubana; baada ya mapafua kuanza kubana inachukua si chini ya siku nne za mtu kuishi akiwa anahema sana kabla hajashindwa kabisa kupumua. Kwa mtu anayeugua ghafla siku moja na kufa siku hiyo hiyo au baada ya siku mbili tatu tu ujue siyo Covid-19, kuna kingine zaidi.

Data zilizotolewa na madakatari waliofanya urtafiti wa kupima ni muda gani mwili unaweza kuhimiri covid-19 umeonyesha kuwa siku za chini ni nane hadi siku 37; paper yao iko hapa

SAWA.
Mengi uliyoandika ni sahihi. Lakini ushuhuda wako hauna msingi wowote katika kuondoa uwezekano wa COVID-19 kuhusika.

Na hayo uliyoeleza, siyo kwamba ndio sehemu kamilifu ya matatizo yanayoambatana na COVID-19; kwa sababu bado kuna mengi yasiyofahamika juu ya ugonjwa wenyewe; na ukichukulia kwamba siyo wagonjwa wote ni lazima waonyeshe dalili hizo na kwa nyakati hizo ulizotaja wewe.

Ulijua kwamba Mfugale kabla hajafariki hakuwa na baadhi ya dalili hizo, hata kama alikuwa halalamiki juu yake? Siyo watu wote huonyesha dalili hizo ulizotaja kwa ukubwa wa kuwatia hofu na kuanza kutafuta msaada, hasa ukichukulia tabia za watu wengi kujihisi kuwa miili yao ni imara. Wanasubiri hadi hali iwe ngumu zaidi kabla ya kutafuta msaada.

Kinachozungumziwa hapa ni kutojua ni nini hasa kinaweza kuwa kimesababisha au kimechangia kifo cha Mfugale. Ni kazi ndogo sana sasa kupima na kujua kama marehemu alikuwa na COVID-19 au hapana.

Hii ni hatua moja ya kujaribu kutambua sababu za kifo cha ghafla.
 
Ni kupoteza nguvu na kuongeza uchungu. Huwezi ishinda serikali kwa namna yoyote ile
"Huwezi ishinda serikali"(?)
Kwa vile serikali hizi ni za kidhalimu, na wananchi wake mmejiweka tayari kukubali kwamba hamuwezi kuishinda serikali hata kama serikali hiyo inawafanyia udhalimu! Inawanyima haki zenu.

Hii ni taabu sana ya kuwa na raia wenye mawazo kama haya.
 
Umeeleza VIZURI ila naongeza uyu bwana sio maskini familia wanashindwa vipi kufanya uchunguzi binafsi wa ndugu yao hata KWA kupeleka mwili kenya ,ili mwisho wa siku waje na majibu mazuri , kwamba kama alitendewa Jambo baya wanafikili watapata majibu sahii,

Wafiwa poleni lakini pia yawabidi jiongeza , ili mpate chanzo au tatizo lililosababisha kifo chake , aliopokua wanasema hawajui tatizo Sasa mnashindwa vipi jiongeza kufanya uchunguzi binafsi wa marehem KWA kutumia watu Wengine nje ya tz
Si lazima kupeleka mwili nje ya nchi, uchunguzi unafanyika hapa hapa, ikilazimu kwa msaada wa wataalam toka nje; au hata sampuli kupelekwa nje.

Kama wao kama ndugu hawajaridhishwa na maelezo ya sababu za kifo cha ndugu yao, wanayo haki ya wao kutafuta ukweli.
 
Habari wana JF.

Leo nimefuatilia live wakati Eng. Mfugale anaagwa Dar. Kwa maelezo machache ya familia, idara na wizara ni wazi kabisa Eng. Mfugale alipewa sumu.

Wito wangu kwa Serikali ifanye uchunguzi wa kina kwa kutumia vyombo na njia zote. Kwa sababu bado hajazikwa nafasi ya uchunguzi wa kina bado ipo.

Kifo cha Eng. Mfugale kimefanana kabisa na kifo cha Prof. Chachage pale Kibaha kwenye kikao.

Nina sababu nyingi za kwanini nasema hivyo, nachelea ziandika hapa kwa sababu inaweza ishia toa hints zangu (taaluma na kazi yangu). Nimefunzwa vyema maeneo hayayalehayale (sitaki toa codes).

Pia nilifuatilia vyema issues za Prof. Chachage, Dr. Mwakyembe, Dr. Omary A. Juma kwa kutaja wachache.

NB: Pia nipo JF kitambo sana; wauaji au serikali wanaweza kuja na hoja mufilisi ya ugeni wa akaunti yangu. Hii ipo kimkakati na hii ndiyo chapisho langu la kwanza.

Best Regards;
Uviko 19 in 2021.
Mwendazake je?
 
Moderator uzushi kama huu mnaacha wa nini?

Au mnaona mama ni mpole ndio maana mnaacha habari kama hizi ambazo zinaweza kuligawa taifa?

Hebu futeni huu ujinga
 
Halafu haijawahi kuelezwa wapi uchunguzi ulifikia wala mtuhumiwa ni nano na kwanini hajakamatwa. Na huyo ndio makam mwenyekeiti, wengine je
Ni uongo,mangula hakupewa sumu,wanasema yule mbilikimo eti alimpa sumu,,sasa mangula akaamua kusimamia harusi ya mbilikimo ili kuwahakikushia kua ile habari ni fake.
Pili makonda,hakumpiga mitama warioba,,ilikuwa ni fake news,,warioba mwenyewe alikiri kuwa makonda alikuwa akijaribu kumlinda warioba..
 
Kama imefanyika ataitoa huyo daktari au jopo la madaktari waliofanya......kama kuna sampuli zimechukuliwa kwenda kwingineko itabidi wasubiri hayo majibu ili kukamilisha ripoti yao, sawasawa?

Hayo maelezo yako sasa yaunganishe na hoja yangu ile ya msingi, refa wao na uwanja wao… utatokaje?
 
Mimi sitaki kutilia shaka sababu nimeshuhudia watu kufariki ghafla tu tena sana mtu mzima mara anajisikia vibaya anapoteza maisha. Shida yangu moja tu kwa yule sijui katibu mkuu aliyekuwa anasimulia tukio. Kwa mujibu wa maelezo yake kajisikia vibaya akamwambia nenda ofisini kapumzike kikao kiendelee baadae akasema ngoja nikamwangali kaenda kamkuta kwenye kitu ila wazi hali yake sio nzuri akauliza wasaidizi kimetokea nini wakasema aliomba tu AC iongezwe iwe baridi basi akakaa mpaka alivyokuja na kumkuta.

Tuseme yote ni kweli ila hivi mtu kasema najisikia vibaya utamwambia nenda ofisini na wasaidizi walichofanya kuongeza AC sio mara moja kuandaa usafiri kumpeleka Hosp au kuita huduma ya kwanza bila kusubiri mpaka katibu mkuu aje ndio aratibu magari hivi kweli goverment city hakuna hata first aid clinic?

Kwa hapo kuna uzembe mkubwa sana katika ku deal na emergency case sisemi watu hawafariki lakini kuwe na hatua za haraka za kujitosheleza unaweza kuokoa maisha ya mtu yoyote. Kwenye hili haliko sawa na sio kwa marehemu tu kwa wafanyakazi wote linaweza kutokea.
Kwa sasa,na korona hii,mtu akisema ansjisikia vibaya,hapo hapo wahisha hospital chap chap,,ukichelewa tu,,kwa heri
 
Habari wana JF.

Leo nimefuatilia live wakati Eng. Mfugale anaagwa Dar. Kwa maelezo machache ya familia, idara na wizara ni wazi kabisa Eng. Mfugale alipewa sumu.

Wito wangu kwa Serikali ifanye uchunguzi wa kina kwa kutumia vyombo na njia zote. Kwa sababu bado hajazikwa nafasi ya uchunguzi wa kina bado ipo.

Kifo cha Eng. Mfugale kimefanana kabisa na kifo cha Prof. Chachage pale Kibaha kwenye kikao.

Nina sababu nyingi za kwanini nasema hivyo, nachelea ziandika hapa kwa sababu inaweza ishia toa hints zangu (taaluma na kazi yangu). Nimefunzwa vyema maeneo hayayalehayale (sitaki toa codes).

Pia nilifuatilia vyema issues za Prof. Chachage, Dr. Mwakyembe, Dr. Omary A. Juma kwa kutaja wachache.

NB: Pia nipo JF kitambo sana; wauaji au serikali wanaweza kuja na hoja mufilisi ya ugeni wa akaunti yangu. Hii ipo kimkakati na hii ndiyo chapisho langu la kwanza.

Best Regards;
Uviko 19 in 2021.
Mpwa unazungumzia kifo cha Mfugale au unajizungumzia wewe?? Umeanza vyema sana na hii iko wazi na kuna Uzi mwingine kama huu hapa hapa JF ila sasa kuanza kujisifia wewe mwenyewe, hapa umechemka!
 
Hayo maelezo yako sasa yaunganishe na hoja yangu ile ya msingi, refa wao na uwanja wao… utatokaje?
Hata wataalamu wanaweza kwenda chaka kubainisha sababu hasa ya kifo, wakati mwingine kifo kinabaki kuwa fumbo....
 
Kifo kipo tu kila mtu atakufa, mbona wakifa watu wa kawaida (pangu pakavu) huwezi kusikia habari za namna hiyo?

Au wenye pesa na mamlaka wao hawatakiwi kufa?
 
Hata wataalamu wanaweza kwenda chaka kubainisha sababu hasa ya kifo, wakati mwingine kifo kinabaki kuwa fumbo....

Ni fumbo kwa kuwa tu kinakuja bila taarifa, ila baada ya hapo ni lazima sababu ijulikane.
 
Back
Top Bottom