Kifo cha Mustafa Kamal Ataturk laana za allah zimshukie

Kifo cha Mustafa Kamal Ataturk laana za allah zimshukie

Mustafa Kamal ataturk ni raisi wa kwanza wa Uturuki, atakumbukwa kuungana na dola za Uengereza na Ufaransa kuivunja dola ya kiislamu ya Khilafah tarehe 3 Machi 1924 , na kuigawanya dola hiyo vijinchi vidogo vidogo na kuweka vibaraka wao katika uongozi ili kuongoza kwa maslahi yao. Mmoja wa vibaraka wao akawa ni huyu Mustafa kamal aliyenzisha taifa jipya na kuliita Turkey.

Samahani kwa bahati mbaya hii unayoleta si historia, ni kama Hekaya za Abunuwasi.

Kama Mustafa Kemal Ataturk ni maarufu kwa jambo fulani ni kuzuia ugawaji wa mabaki ya Milki ya Khalifa na kuunda Uturuki wa kisasa.


1. Yale unayoita "dola ya kiislamu ya Khilafah" ilikuwa Milki ya Osmani (Ottoman Empire) iliyotawaliwa na Waturuki (Mkuu alikuwa sultani mwenye cheo cha Khalifa) na kutawala pia nchi za Waarabu (Syria, Iraki, Lebanoni, Palestina, Yemen, na Hejaz yaani sehemu ya Uarabuni). Ndani ya eneo la Uturuki ya leo takriban robo ya wananchi hawakuwa Waturuki bali Wakristo Wagiriki, Waarmenia na Waassiria.

2. Milki ya Osmani iliingia katika Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia upande wa Ujerumani ukashindwa pamoja na Ujerumani ikipigana na Urusi, Uingereza na wananchi katika sehemu zilizotafuta uhuru wao, kama Waarabu na Waarmenia.

3. Wakati wa Vita Kuu Mustafa Kemal alikuwa jenerali ya jeshi la Sultani=Khalifa alikuwa maarufu akitetea Mlangobahari ya Dardaneli dhidi ya uvamizi wa Uingereza hivyo kuzuia kukamatwa kwa mji mkuu na Uingereza.

4. Baada ya kushindwa vita Sultani=Khalifa alikubali Mkataba wa Sevres ya 1920. Kanuni za mkataba huu zililenga kugawa milki yote: Hejaz (pamoja na Makka) ilipewa uhuru, Irak na Palestina iliwekwa chini ya Shirikisho la Mataifa (league of Nations) na kukabidhiwa kwa Uingereza, Syria na Lebanoni pia chini ya Shirikisho la Mataifa na kukabidhiwa kwa Ufaransa. "Ukanda wa Milangobahari" (zone of straits") ilitengwa na kuwekwa chini usimamizi wa kimataifa moja kwa moja. Maeneo ya mashariki-kaskazini zilizokaliwa na Waarmenia yaliunganishwa na Jamhuri ya Armenia (awali ya Kirusi). Maeneo ya Wakurdi yalipangwa kuwa na mamlaka ya ndani na nafasi ya kupiga kura kuhusu uhuru. Maeneo ya magharib kabisa yaliyokaliwa na Wagiriki wengi walipewa pia mamlaka ya kujitawala na nafasi ya kupiga kura baadaye kuhusu maungano na Ugiriki. Tangu 1919 wanajeshi kutoka Ugiriki walishika tayari mji wa Smyrna (Izmir) na mazingira yake, Wafaransa na Waingereza waliingia Istanbul.

Maeneo kadhaa katika rasi ya Anatolia yalipangwa kubaki kama “Milki ya Osmani”
1567508973790.png

5. Baada ya uvamizi wa Istanbul na Uingereza na Ufaransa na kutangazwa kwa mkataba wa Sevres Mustafa Kemal aliungana na Waturuku wengine akaita “Mkutano Mkuu wa Waturuki” akatangaza serikali ya Khalifa=Sultani kuwa wasaliti akajenga jeshi jipya na kupigana na Wagiriki na Waarmenia.

6. Katika vita hii inayojulikana kama “Vita ya Uhuru wa Uturiki” Mustafa Kemal alifaulu kufukuza Wagiriki. Waingereza , Wafaransa na Waitalia walichoka vita wakaondoka. Urusi baada ya mapinduzi yake ya 1917 haikushiriki tena katika vita hii baada Vita Kuu. 1922 Mkataba wa Lausanne ulikubali Uturuki mpya katika mipaka yake jinsi ilivyo leo.

7. Bunge jipya likamchagua Mustafa Kemal kuwa kiongozi. Bunge likaamua kutenganisha vyeo vya Sultani na Khalifa. Usultani ulifutwa na Sultani Mehmet V. alifukuzwa nchini akahamia Italia. Shemeji yake Abdulhamid alichaguliwa na bunge kuwa khalifa mpya na mkuu wa dola, lakini bila mamlaka.

8. Baada ya miezi michache Mustafa Kemal alipata kura nyingi katika bunge kubadilisha katiba tena na kufuta pia ukhalifa. Mustafa Kemal akawa rais wa Uturuki. Abdulhamid alihamia Ufaransa alipoishi hadi mwaka 1944 akiwa mchoraji wa taswira na mtaalamu wa vipepeo. Baada ya kifo chake alizikwa Makka kwa amri wa Mfalme Saud.

9. Mustafa Kemal aliheshimiwa kama mwanzilishaji wa Uturuki wa Kisasa akapewa jina la „Baba wa Waturuki“ = Atatürk“.

10 Mustafa Kemal alichukua hatua nyingi kubadilisha Uturuki kuwa nchi ya kisasa. Aliona Uislamu kuwa sababu kubwa ya udhaifu wa taifa lake hivyo hakukataza Uislamu lakini alitenganisha serikali na dini, lakini kwa kuuunda taasisi za kusimamia misikiti zote.Alilenga kuzuia athira ya maimamu na mashehe katika shughuli za serikali. Aliwapa wanawake haki ya kupiga kura, alikataza nguo za kidini na hijabu ya wanawake.

11. Hadithi kuhusu kuzikwa kwake ni kitoto, haina msingi wowote. Mwili wake uliwekwa katika jeneza alipokufa Istanbul tarehe 10.11.1935 na kubebwa kwa manowari hadi Izmit, kutoka huko kwa treni maalumu hadi Ankara. Pale jeshi lilibeba jeneza hadi jengo la Bunge na maelfu walipita mbele yake. Mwili uliwekwa katika jeneza kubwa ya jiwe (sarcophagus) iliyokaa katika makumbusho kuu. Kwa miaka iliyofuata jengo la pekee lilijengwa kwa kutunza masalio yake na hapa yapo tangu 1953. Soma kwa undani zaidi hapa https://en.wikipedia.org/wiki/Death_and_state_funeral_of_Mustafa_Kemal_Atatürk#Transfer_to_the_capital_city
1567509017018.png

Wananchi wa Ankara jinsi alivyoaga jeneza ya Mustafa Kemal 1935
 
Kiranga...
Mimi nikukimbie wewe?

Nimefanya mijadala kwingi tena kila nikiangalia hadhira ni sura sijapatapo kuziona hata siku moja na watu wajuzi.

Nije kukukimbia wewe niko hapa nyumbani kwangu?

Nimefanya vipindi kama hivi vingi vya maswali na majibu katika radio, tv ndani na nje ya Tanzania na mimi mwenyewe ni broadcaster nitafute You Tube kuna vipindi vyangu vingi nije nikukimbie wewe unaeandika umelificha jina lako?

Sasa kaka badala ya kuonyesha umahili wako ni nini umefanya na wapi ungetumia muda huo kumuelewesha mwenye swali.., sidhani kama hili ni jukwaa la kuonyesha ni nini umefanya au umahili wako wa kufanya mambo bali ni jukwaa la kujibu na kueleza your point of view kutokana na mada husika..

Na kama hio mijadala huwa ukiulizwa unaanza kutoa reference watu wakasome au kuelezea umahili wako kama vile ni kipindi cha nani zaidi nadhani huwa hutendei haki makongamano
 
Tena Hajui hata kudanganya ati venye yeye anatamka waislam 71% waliondoka kwa basic education....this man is sadist

Nimempa task asogee kwa wizara aangalie musilim wangapi walihitimu basic education

Huyu mzee angejikita kulea wajukuu badala ya kuendelea kueneza udini
Kuna siku niliwahi kumsikia muislamu 1 hivi mitaa ya riverside, nilikutana nae kwa ndugu yangu 1 hivi, alichokua anaongea hadi niliogapa jinsi watu walivyo waongo; eti hata Vatcan na Roma ( ile capital city ya Italy ) ilikuaga ya waislamu ila Wakristo wakaiteka nyara. Tukaanza mazungumzo mdogo mdogo, nilimuuliza hivi; mkuu, kwani uislamu una miaka mingapi tokea umeenza? Hilo swali likamshinda but pale pale kwa huyo ndugu yangu kulikua kumebandikwa calendar ya Kiislam, ikaonesha mwaka, then nikamuuliza swali linguine; mkuu unajua DOLA ya Rumi ilitawala dunia nkipindi gani? Swali hili nalo hakua na majibu nalo, then sasa ndio nikaanza kumpa shule mdogo mdogo hadi tukaelewana, mwishoni nikagundua kwamba amekua fed na hawa hawa kina ustaadhi KONDO. Waongo balaa.
Swali langu ambalo hua linanitatiza sana ni hili; uongo hu hua ni kwa faida ya nani? Mungu? Dini au nini? Nilidhani mcha mungu angechukia sana uongo but haiku hivyo
 
Tena Hajui hata kudanganya ati venye yeye anatamka waislam 71% waliondoka kwa basic education....this man is sadist

Nimempa task asogee kwa wizara aangalie musilim wangapi walihitimu basic education

Huyu mzee angejikita kulea wajukuu badala ya kuendelea kueneza udini
Mikocheni...
Hebu angalia na hii:

HUJUMA ZA BARAZA LA MITIHANI DHIDI YA WAISLAM - TAARIFA YA MUFTI WA BAKWATA SHEIKH SHAABAN BIN SIMBA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mohamed Said Historia, Siasa na Maendeleo Tanzania January 31, 2016 0

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: HUJUMA ZA BARAZA LA MITIHANI DHIDI YA WAISLAM
Kila sifa njema anastahiki Allah, ambaye rehema zake zimeenea katika kila kitu katika ulimwengu bila ya kujali utii ama uasi wa kitu hicho katika amri na sharia zake.
Rehema na amani zimuendee kipenzi chetu mtume Muhammad (S.A.W) kwa kuwa kiigizo chema na rehema kwa walimwengu wote.
Ndugu waandishi kwa muda mrefu waislam wamekuwa wakiilalamikia suala zima la utendaji wa serikali kuwa umekuwa wakibaguzi kwa kuwapendelea wakirsto kwa kuwapa nafasi mbalimbali muhimu serikalini na katika taasisi zake.
Ndugu waandishi na Waislam mnamo tarehe 01/ 05/2012 Baraza la mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya kidato cha Sita, matokeo hayo yaliwashtua sana wanafunzi waislam waliofanya mtihani wa elimu ya dini ya kiislam (Islamic Knowledge). Takriban asilimia 70 walifeli kwa kupata daraja F, na asilimia 30 ndio waliofaulu tu.
Katika hao waliofaulu walipata alama za juu kabisa nchi nzima ni wanafunzi saba tu ambao wamepata daraja D, kwa matokeo haya somo hili likawa somo la mwisho kwa ufaulu nchi nzima (rejea kitabu cha takwimu cha Baraza la mitihani Tanzania April 2012.
Matokeo haya yaliwashtua wazazi na walimu wa somo hili, baadhi ya wanafunzi waliamua kukata rufaa ya kutokubaliana na matokeo hayo.

Waislam kupitia Taasisi mbali mbali za kiislam walimuandikia katibu mkuu wa wizara ya elimu na mafunzo ya ufundi kumuomba aunde tume huru kuchunguza matokeo ya somo husika.
Kufuatia malalamiko hayo ya baadhi ya taasisi za dini, baraza la mitihani liliyatazama matokeo hayo na kugundua pia walikosea na hivyo Baraza la mitihani likaidhinisha kutolewa matokeo mapya kwa somo hilo.

Mabadiliko hayo ya matokeo ufaulu kwa wanafunzi wale wale ambao awali walifeli kwa asilimia 70, sasa yakabadilika na ufaulu ukaongezeka kwa zaidi ya asilimia 70.
Kwa namna yoyote ile itakavyokuwa dosari kubwa kama hii ni kashfa kubwa kwa Baraza la mitihani Tanzania na Serikali kwa ujumla.
Na kwa kutilia maanani muundo na historia ya utendaji wa wa baraza la mitihani la Tanzania kama nilivyoanza kuelezea, Waisla wanayokila sababu ya kuamini
kwamba matokeo haya ni uthibitisho tosha wa hujuma ambazo wanafunzi wa kiislam walikuwa wakifanyiwa kwa muda mrefu.

Na hii inatupa picha kwamba dosari hizi zilizotokea kwenye somo la maarifa ya kiislam, haziishii kwenye somo hili, bali uchunguzi ukifanyika kwa masomo yote waliofanya wanafunzi wa kiislam itadhihirika kwamba hila na dhulma kama hizi zinafanyika katika masomo mengine.
Kimsingi kwa dhulma hii waliyoifanya baraza la mitihani dhini ya wanafunzi wa kiislam, Bakwata na waislam wote kwa ujumla wamepoteza imani na baraza la mitihani la Tanzania na hasa katibu mtendaji wake .
Bakwata, linawapongeza na kuwaunga mkono Taasisi zote za kiislam nchini kwa jitihada ya kuligundua hili na hatua walizozichukuwa dhidi ya baraza la mitihani na kuhufahamisha umma wa kiislam juu ya kadhia hii.

Sheikh Ponda Issa Ponda akiomba dua kabla ya kuanza kwa maandamano dhidi ya NECTA
Tunarudia baraza tunawapongeza taasisi zote za kiislam na tunasema katika hili Bakwata tuko nyuma yao kwani kauli yao ndio kauli yetu.
Bakwata, inamshangaa Katibu mtendaji wa Baraza la mitihani (Necta) Dk. Joyce Ndalichako, kwa kauli yake aliyoitoa kupitia vyombo mbali mbali vya habari vya jana tarehe 5/06/2012, akisema hakuna hujuma na mitihani inasahihishwa na walimu wenye sifa,wanachaguliwa na na wakuu wa shule zao, walimu wenye uzoofu na kuna mfumo wa usahihishaji aliohuita “Conveyor Belt”.
Bakwata inasema hapa tatizo la msingi sio mitihani kusahihishwa na walimu wenye sifa,na nani anawachagua walimu hao wenye sifa au huo mfumo wa
usahihishaji, tatizo la msingi hapa ni kufelishwa kwa makusudi kwa wanafunzi wetu wa kiislam katika somo husika, wakati nakala za mitihani yao (Scripts) zinaonyesha wamefaulu.
Bakwata, tunahoji kwanini tatizo hili la huo mfumo (Conveyor Belt) litokee mwaka huu, mbona matokeo ya mwaka jana waislam hawakulalamika na kulikuwa hakuna dosari kama za mwaka huu iweje itokee mwaka huu, wakati mfumo ni ule ule?
Bakwata, tunaamini waislam katika hili tumehujumiwa na waislam hawajaridhishwa na majibu ya Dk. Ndalichako, aliyoyatoa kupitia vyombo vya habari vya hapa nchini.
Hiyo mifumo ya usahihishaji sio maneno matakatifu kwamba haiwezi kuchezewa kutokana hila za binadamu ni mifumo iliyowekwa na binadamu, na binadamu huyohuyo anaweza kuibadilishabadilisha vyovyote anavyotaka.
Sisi kama Bakwata,tunaamini ili kurudisha imani ya waislam dhidi ya Baraza la mitihani tunataka mambo yafuatayo yafanyike,
· Tume huru iundwe la kuchunguza Baraza la mitihani la Tanzania na utendaji wake wa kazi kwa kipindi cha miaka kumi iliyopita.
· Katibu mkuu wa baraza la mitihani (Necta) ajiuzulu mara moja ili kulinda heshima ya serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Baraza la Mitihani.
· Watendaji wakuu wa kitengo cha mitihani na wanaohusika na mfumo wa kompyuta ya Baraza la mitihani nao wawajibishwe mara moja.
· Hatua za kisheria na kinidhamu zichukuliwe dhidi ya watumishi wa baraza la mitihani watakaothibitika kuhusika na kashfa hii.
· Muundo wa baraza la mitihani uzingatie uwiano wa kidini, kitendo cha chombo nyeti kama hiki kujazana watu wa dini moja kunaliondolea baraza la mitihani sura ya kitaifa, kwani takwimu zinaonyesha makatibu wakuu watendaji na manaibu katibu wakuu wamekuwa wakristo na wenyevyiti wa baraza hilo ni wakristo tangu lilipoanzishwa mwaka 1973, mpaka hii leo na takwimu tunazo.
· Pia tunaiyomba Serikali iwape nafasi wanafunzi wote ambao baada ya matokeo yao kubadilishwa wamekuwa na sifa za kujiunga na vyuo vikuu waruhusiwe kuomba mikopo bodi ya mikopo, tunalisema hili kutokana na muda wa kuomba mikopo kwa wanafunzi wanaotaka kujiunga na elimu ya juu kwisha.
Suala la Sensa ya watu na makazi.
Kama tunavyojua kwa mwaka huu wa 2012, kuna zoezi la sense ya watu na makazi ambayo inatarajiwa kufanyika kuanzia mwezi wa nane, 2012, na kutoka na upotoshaji ulioenea kwenye vyombo vya habari hapa nchini, kalenda iliyochapichwa na ofisi ya waziri mkuu, imetoa takwimu zinazoonyesha idadi ya watanzania ni milioni 43 ambapo kwa mujibu wa dini zao wakristo ni asilimia 52, waislam asilimia 32 na dini zingine ni asilimia 16.
Bakwata tunalaani kitendo hiki na tunasema takwimu hizi sio sahihi na zinapotosha wananchi, hii ni kwa sababu katika sense zilizofanyika hivi karibuni ikiwemo sense ya mwaka 2002 kipengele kinachobainisha dini za watanzania kiliondolewa.
Kwakuwa taarifa hizi zinaonekana kwenye kalenda zinazoonyesha zimetayarishwa na ofisi ya waziri mkuu, tunaitaka serikali kurudisha kipengele kinachobainisha dini za watanzania katika sense ya mwaka huu ili ukweli ujulikane na kuondoa kabisa sintofahamu hii.
SUALA LA MGOGORO WA HIVI KARIBUNI ZANZIBAR
Ndugu waandishi wa habri naamini nyinyi nyote kama waandishi wa habari mnajua au mmesikia vurugu zilizohusisha imani za dini zilizotokea visiwani humo na kutokana na taarifa nyingi za vyombao vya habari zilizokuwa zikitolewa tangu mgogogro huu uanze kuna kila dalili za kuchukuliwa hatua za haraka haraka na katika mazingira haya wale wote waliohusika na vurugu hizi wasijulikane tena na watu wasio na hatia wakahusishwa na hali ikawa mbaya zaidi kwa hivy o kutokana na kadhia yote hiyo na yote yaliyosemwa na makundi mbalimbali ya waisla na wasiokuwa waislam Sisi kama Bakwata tunasema yafuatayo:
Kwanza tunalaani kitendo cha uvunjifu wa amani uliotokea Zanzibar na tunaamini waliofanya vurugu zote zile sio waislam bali ni wahuni tu.
Pili tunasema Wazanzibar, wasikilizwe kwa yale ambayo wanayapigia kelele kama malalamiko yao yapo katika muungano Serikali haina budi kuyasikiliza
yale yote yanayolalamikiwa na kuyarekebisha, kwani Muungano sio qur- an useme kilichomo humo hakiwezi kurekebishika.
Tatu iundwe tume huru yenye wajumbe kutoka pande zote, makanisa, Serikali na UAMSHO ili zichunguzwe tuhuma hizi kwa undani zaidi maana kwa kweli athari zinaweza zikawa za muda mrefu kwani zinapandikiza kutoaminiana baina ya Wazanzibar hasa wakristo na waislam jambo ambalo halikuwepo hapo kabla na yoyote takae bainika kuwa na hatia sheria ichukue mkondo wake bila ya kujali wadhifa alionao katika chama, dini ama Serikali.
Mwisho tunamuomba Allah atupe Imani ya kweli katika nchi yetu na kama kuna fisadi na adui Allah amdhalilishe hapahapa Duniani, amen.
Wabillah Tawfiq.
Sheikh Issah Bin Shaabani Simba.
Sheikh Mkuu na Muft wa Tanzania
 
Siongelei kuamini, naongelea fact.
Quran ina contradictions.
Hii ni fact, si imani.
Ukisema imeandikwa Kiarabu, siielewi, hiyo nayo ni contradiction.
Itakuwaje Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote aachie habari zake ziandikwe kwenye lugha inayoeleweka na watu fulani tu, na wengine wasizielewe vizuri?
Contradictions!
Zipo njia mbili tu zakukujibu wewe juu yahii hoja yako..
1-,wewe ulitaka Quran iwe katika Lugha Gani?
2-Kiarabu ndio lugha pekee inayofanyiwa Research mpaka sasa ikiwa na sifa ya kwamba ikibadilika herufi moja tu ktk sentensi either kwa kuandikwa au kwakutamkwa basi maana nzima yahiyo sentensi inabadilika..hivyo kwasifa hii inaifanya Kiarabu kua lugha pana zaidi na yenye kueleweka zaidi!
Allah anasema "Tumeiteremsha Quran katika lugha ya kiarabu Ili mpate kuielewa(kuifahamu")
 
Zipo njia mbili tu zakukujibu wewe juu yahii hoja yako..
1-,wewe ulitaka Quran iwe katika Lugha Gani?
2-Kiarabu ndio lugha pekee inayofanyiwa Research mpaka sasa ikiwa na sifa ya kwamba ikibadilika herufi moja tu ktk sentensi either kwa kuandikwa au kwakutamkwa basi maana nzima yahiyo sentensi inabadilika..hivyo kwasifa hii inaifanya Kiarabu kua lugha pana zaidi na yenye kueleweka zaidi!
Allah anasema "Tumeiteremsha Quran katika lugha ya kiarabu Ili mpate kuielewa(kuifahamu")
Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wotw na upendo wote, ahitaji au atumie lugha ya watu fulani kueneza neno lake kwa watu wenye lugha nyingi tofauti, na hivyo kuweka kikwazo cha tafsiri kwa watu wengi sana?

Kwa nini hakuweka habari zake kwenye DNA ya kila mtu anapozaliwa, ili kila mtu ajue habari za Mungu bila kusoma kitabu, kwa kuwa kitabu kitazaa maswali kuhusu tafsiri, watu walioandika, siasa, utamaduni, tafsiri etc.

Mungu wenu alishindwa kuweka habari zake kwenye DNA ya kila mtu?
 
Kwa nini Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wotw na upendo wote, ahitaji au atumie lugha ya watu fulani kueneza neno lake kwa watu wenye lugha nyingi tofauti, na hivyo kuweka kikwazo cha tafsiri kwa watu wengi sana?
Kwa nini hakuweka habari zake kwenye DNA ya kila mtu anapozaliwa, ili kila mtu ajue habari za Mungu bila kusoma kitabu, kwa kuwa kitabu kitazaa maswali kuhusu tafsiri, watu walioandika, siasa, utamaduni, tafsiri etc.
Mungu wenu alishindwa kuweka habari zake kwenye DNA ya kila mtu?
Katika Uumbaji wake Allah ameweka dalili zilizowazi katika kila kiumbe..ili kumfanya kiumbe atambue uwepo na ukubwa wake yeye Allah...Hiyo DNA unayoizungumzia hapa Kama ungetulia kidogo kiasi cha dakika5 ukajiuliza ni nani aliyekuwekea hiyo DNA ktk mwili wako tena ikiwa imepangiliwa kwa ufundi na ustadi wa hali ya juu basi ingetosha kabisa wewe kuamini uwepo wa mueza vyote na mwenye nguvu kuliko vyote.. !
Lakin ukishindwa kumtambua kwa uwepo wake kupitia viumbe vyake ikiwemo hiyo DNA unayoizungumzia basi inakubidi urudi ktk maneno yake yaliyoteremshiwa mitume na manabii (vitabu vyake) ili upate kukumbuka na kutafakari!
Hivyo basi lengo la kuwepo wa hivyo vitabu nikumkubusha mwanadamu ajitambue na amtambue Mola wake Mlezi!
Waswahili wanasema Elimu bila daftari hupotea bila Habari!
 
Katika Uumbaji wake Allah ameweka dalili zilizowazi katika kila kiumbe..ili kumfanya kiumbe atambue uwepo na ukubwa wake yeye Allah...Hiyo DNA unayoizungumzia hapa Kama ungetulia kidogo kiasi cha dakika5 ukajiuliza ni nani aliyekuwekea hiyo DNA ktk mwili wako tena ikiwa imepangiliwa kwa ufundi na ustadi wa hali ya juu basi ingetosha kabisa wewe kuamini uwepo wa mueza vyote na mwenye nguvu kuliko vyote.. !
Lakin ukishindwa kumtambua kwa uwepo wake kupitia viumbe vyake ikiwemo hiyo DNA unayoizungumzia basi inakubidi urudi ktk maneno yake yaliyoteremshiwa mitume na manabii (vitabu vyake) ili upate kukumbuka na kutafakari!
Hivyo basi lengo la kuwepo wa hivyo vitabu nikumkubusha mwanadamu ajitambue na amtambue Mola wake Mlezi!
Waswahili wanasema Elimu bila daftari hupotea bila Habari!

Hujajibu swali nililokuuliza, na ulilojibu sijakuuliza.

Kwa nini huyo Mungu wako hakuweka habari zake zote kwenye DNA tusihitaji vitabu na migogiro ya kiutamaduni na tafsiri kati ya lugha tofauti?

Hujajibu swali hili.
 
Hujajibu swali nililokuuliza, na ulilojibu sijakuuliza.
Kwa nini huyo Mungu wako hakuweka habari zake zote kwenye DNA tusihitaji vitabu na migogiro ya kiutamaduni na tafsiri kati ya lugha tofauti?
Hujajibu swali hili.
Hiyo DNA ni KITABU tosha kutoka kwake Allah..sasa kitumie kumjua yeye...maana yeye ndie aliekuwekea DNA!
 
Zipo njia mbili tu zakukujibu wewe juu yahii hoja yako..
1-,wewe ulitaka Quran iwe katika Lugha Gani?
2-Kiarabu ndio lugha pekee inayofanyiwa Research mpaka sasa ikiwa na sifa ya kwamba ikibadilika herufi moja tu ktk sentensi either kwa kuandikwa au kwakutamkwa basi maana nzima yahiyo sentensi inabadilika..hivyo kwasifa hii inaifanya Kiarabu kua lugha pana zaidi na yenye kueleweka zaidi!
Allah anasema "Tumeiteremsha Quran katika lugha ya kiarabu Ili mpate kuielewa(kuifahamu")
Huyo mungu alishusha tourati, zabur na Injil katika lugha gani?
 
Huyo mungu alishusha tourati, zabur na Injil katika lugha gani?
Hivyo vyote vimeshushwa kwa kabila ya Bani-Israel!Tourat ilikua katk lugha ya Bani-Israel sambamba na Zaburi..injiel ilikua ktk lugha la kiiberania hii nilugha miongoni mwa makabila ya kizazi cha Israel (Bani-Israel)!
 
Hivyo vyote vimeshushwa kwa kabila ya Bani-Israel!Tourat ilikua katk lugha ya Bani-Israel sambamba na Zaburi..injiel ilikua ktk lugha la kiiberania hii nilugha miongoni mwa makabila ya kizazi cha Israel (Bani-Israel)!
Kwa hiyo hizo lugha ya bani israel ina mapungufu hadi mungu akabadili mawazo akaamua sasa ashushe kitabu chake kwa kiarabu?
 
Kwa hiyo hizo lugha ya bani israel ina mapungufu hadi mungu akabadili mawazo akaamua sasa ashushe kitabu chake kwa kiarabu?
Swali zuri sana umewaza vyema kabsa mkuu..na nitakujibu kama ifatavyo!
Quran imekuja kwa Mtume Muhammad ikiwa yeye ni Muarabu hivyo ufunuo wake hauwezi kua ktk lugha nyingine zaidi ya kiarabu kama vile Yesu alivyopewa kitabu ktk lugha yake yakiiberania nasi katka lugha ya kiarabu!hapo sawa tumeelewana mkuu?
Pia Quran imekuja kwa kiarabu kwasababu ndio muongozo wa ulimwengu mzima na ili kitabu kiweze kutumika ulimwengu mzima bila kuleta mchanganyano lazima itumike lugha moja ambayo haiwezi kubadilishwa na kuchezewa na watu hivyo kupoteza maana halisi ya ujumbe wa Mungu..na kwahapa kiarabu kimefaulu!..bila shaka mwenyewe umejiona jinsi vitabu vingine vilivyobadilishwa kwa lengo lakutafsiri na mwisho wasiku kitabu kikapoteza uhalisia wake..Leo hii tourat au injiil unayoisoma wewe siyo ile ile halisi waliopewa Musa na Issa(Yesu)!nahii nikutokana na udhaifu wa lugha!Biblia yako hiyohiyo unayoitumia ukiienda Nayo China huwezi kumsomea mchina andiko na akakuelewa au yeye akusomee andiko kutoka kwenye biblia yake ukaelewa!sasa swali lina kuja kati yenu ni nani anayesoma Andiko lakweli?lakin hiyo ni tofauti na Quran kua katka lugha yakiarabu kwanza Quran imebaki ktk uhalisia wake,na ugumu wakuchezea lugha hii imeifanya Quran isiweze kubadilishwa...,Hivyo hata ukienda China na Quran yako ukamsomea mchina anajua nakuelewa hiyo ni Quran imesomwa nayeye akikusomea pia wewe unajua amesema nini..na hii ndio maana Quran nikitabu cha watu wote!
Hivyo kama Quran ingekua ktk lugha nyingine kwanza isingeweza kueleweka na pili ingekua imeshatiwa mikono na watu hivyo kupoteza uhalisia wake!na ukijaribu kutunga Quran yakwako watu watajua hiyo ni fake!na hii ni tofauti na biblia hujui ni Agano lipi ndio sahihi maana kila kukicha unasikia "New testament" au kujua ni Biblia ipi ndio sahii kati ya yenye vitabu Vingi na yenye vitabu vichache!
 
Ninahitaji Quran kama ukumbusho wangu na ndio maana Quran pia inaitwa UKUMBUSHO!
Ukiandika DNA inatosha, halafu ukaandika unahitaji Quran kama ukumbusho wako, ume ji contradict halafu hata hujui kwamba ume ji contradict.
 
Back
Top Bottom