Bado sijakupata vizuri ndugu....hoja yako hapa ni ipi ukiachana na mambo za kidukulilo na kudukuliwa.Eti political trap [emoji23] [emoji1787]
Waswahili hatuna kumbukumbu katika bongo zetu huwa zinafuta haraka sana
Hata kama una PhD bado kukumbuka ni zero
Walipodukuliwa wale walikuwa wanasema jamaa ni Mshamba
Mlikejeli sana
Ila mkasahau kuwa hata nyie mnadukuliwa kila leo
Hujiulizi kwanini baada ya kuomba msamaha akajiuzuru baada ya hapo?
Mjadala ufungwe hapa.Inahuzunisha kama sio kushangaza kwamba watu hawaoni kosa la Ndugai lililopelekea Rais kumnanga wazi hadi akachukia uamuzi wa kujiuzuru.
Ni kweli speaker ana nafasi ya kutumia Uhuru wake wa kutoa maoni as a normal Tanzanian. Alichokifanya alitumia Uhuru wake wa kikatiba kutoa maoni yake binafsi.
Lakini tunasahau Jambo moja kwamba kila Uhuru una mipaka yake hata Katiba inatamka wazi kuhusu haki za binadamu. Unapotoa maoni yako unapaswa kuangalia na viapo vingine ulivyoapa katika utekelezaji wa majukumu yako.
Ndugai akiwa bungeni akiwa anatekeleza majukumu yake hazuiwi kutoa maoni yake na amekuwa akifanya hivyo mathalani kwenye mambo mbalimbali hata Bandari ya Bagamoyo, kuhusu mjadala wa watoto waliopata ujauzito kurudishwa shule nk.
Tatizo linakuja pale anapotoa maoni yake nje ya bunge ingali yeye ni kiongozi wa mhimili ambao umepitisha hiyo hoja akiwa amesimamia mijadala yote halafu anaibuka nje ya bunge na kuongea namna Ile.
Sasa Rais ndio head of state, pamoja Kuna separation of powers lakini Katiba hiyohiyo inatamka Rais ni head of state maana yake Ndugai anawajibika kwa president despite ya kuwa head of one of pillars of the government.
Hapa unaweza kuelewa kwamba huwezi kuita wanahabari kumpinga boss wako maana Ndugai kama spika anakuwa mtumishi wa umma by virtue ya cheo chake.
Spika akiwa bungeni anakuwa "functus officio" hivyo haina shida Ila hawezi kuongea kumcrash boss wake nje ya bunge.
Pia kwenye chama Rais ni boss wake hivyohivyo anajikuta hawezi kumcrash Mwenyekiti wake nje ya vikao vya chama.
Kawaida ukitaka kumchallenge Mwenyekiti angepaswa kuongea kwenye vikao vya chama Tena yeye ni Mjumbe wa CC wangejadili kama hiyo anachofanya Rais anakiuka ilani ya chama.
Ndio maana wanaotaka kumchallenge Mwenyekiti huwa wanajitoa kwenye chama ndio wanaongea wanayoona wapo sawa.
Mzee Lyatonga Mrema baada ya kutokubaliana na Rais mzee Mwinyi alipoamua kumpatia mfalme wa uarabuni kitalu Cha kuwinda kule Loliondo kwa miaka 99 Mrema aliona hakubaliani na yale maamuzi ndipo alijiuzulu na akajitoa CCM ndipo akaita press conference kueleza sababu za kujiuzulu.
So in my personal view, Ndugai yawezekana ana hoja ya msingi Ila amekosea protocol ya kuwasiliana maoni yake.
Duu wewe somo la presidential Government vs parliamentary government ulielewa vizuri sana.Kwamba hujaelewa nilichoandika? Anyway nimesema kitu kinaitwa "functus officio" pia nikaongelea Uhuru wa kutoa maoni nje ya bunge una mipaka kulingana na kiapo Cha kazi yake.
Speaker anajadili mada za serikali bungeni, anatoka chama tawala anapitisha mipango ya chama chao, kwa namna yeyote hapaswi kumkosoa Rais ambaye ni boss wake na Mwenyekiti wake nje ya bunge au nje ya vikao vya chama.
Unamuona IGP au General wa Jeshi na Mkurugenzi wa usalama wa Taifa, wanaweza kuwa na maoni yao na Wana haki ya kutoa maoni Ila kulingana na kiapo Cha kazi yao na nature ya kazi yao Wana channel za kumshauri Rais Ila sio kuitisha press na kuongea hovyo.
Speaker ana nafasi ya kujadili hoja za serikali ya chama chake bungeni, hutegemei aende kinyumr na Sera ya chama chake kwa namna yeyote Ile lazima ajiondoe au afukuzwe so angetumia busara kujiondoa.
Daaah hili likitu likirudi tena kwenye uongozi mbona itakuwa shida Sana aisee
Lukuvu next PMMara paaap pia Baraza La Mawaziri limevunjwa Ummy Mwalimu waziri mkuu.
Aliharibu taswira ya nchi kimataifa, sio rahisi kurudi madarakani ataigharimu sera ya Mama ya kuifungua nchi kidiplomasia.Kwa huruma ya mama namuona Makonda akipata uteuzi wa ubunge hatimaye uwaziri.
Mkuu nchi Hii ina Mihimili mitatu, lakini Hii miwili iliyobaki yote wasimamizi wa Hii Mihimili wako under roof ya Huyo mwenzao.Kuondoka kwa ndugai kumenifanya nione mapungufu mengi sana kimfumo
1 . Hii nchi ina mhimili moja tu hizi zingine geresha
2. Hoja za mashiko hazipewi nafasi
3. Tunako elekea wimbo wa katiba mpya tutaimba wote ...muda ni mwalimu mzuri
Na hapa ndo ule ule ukweli kuwa tuna mhimili mmoja wenye nguvu kuliko mingine unadhihirika.Mkuu nchi Hii ina Mihimili mitatu, lakini Hii miwili iliyobaki yote wasimamizi wa Hii Mihimili wako under roof ya Huyo mwenzao.
1. Rais ambae ni m/kiti wa chama anapendekeza yy Jina la mtu Kuwa spika
2. Rais ambae ni mkuu wa muhimili wa Regime yy ndio anaemteua Mtu Kuwa CJ
So wote hawa wanadepend kwa hyo anaewateua
Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hv chama changu nikipendacho cha umoja kimesha sajiliwa??najiandaa kuwa Waziri tukishika hatamu hapo 2025!!Kasim Majaliwa huenda yatamkuta yaliyomkuta Joseph Sinde Warioba 1990 au John Samwel Malecela 1994
Bado sijakupata vizuri ndugu....hoja yako hapa ni ipi ukiachana na mambo za kidukulilo na kudukuliwa.
Naomba ufafanuzi wako,unajaribu kumaanisha nini yaani.
Tupa takataka kule mama sio mualifu kiasi hichoKwa huruma ya mama namuona Makonda akipata uteuzi wa ubunge hatimaye uwaziri.