ππ ujue nimecheka sana ndugu yangu.
π€£π€£π€£π€£π€£π€£π€£π€£
Labda aombe Mods. π€£π€£π€£Hivi haiwezekani kufuta uzi JF?[emoji1787][emoji1787] jamaa anadhalilika kinoma
Sisi humu ni waungwana sana mbona Uzi wa Takwimu Kibu D Vs Mayele kamati ya wandewa tutakubaliana kusamehe na Uzi kuuacha baada ya kuwa mpole na kutimiza masharti yetu.Hivi haiwezekani kufuta uzi JF?[emoji1787][emoji1787] jamaa anadhalilika kinoma
Hazikai zimesimama kiongoziππAisee mwasibu balance sheet zinasemaje huko?
Acha kushupalia takwimu!Nahisi wewe utakua ndio umevuta bangi.
Katika vitu vyote umeona Ballon d'or tuu!?
Hujaona makombe ya kimataifa?
Hujaona jumla ya magoli ya timu ya taifa?
Hujaona jumla ya mataji ya timu ya klabu?
Acha kuvuta bangi ukiwa chooni tena mchana jua kali choo hakina bati.
Hujielewi unachoongea mkuu.Acha kushupalia takwimu!
Takwimu sio suluhisho la ubora wa mchezaji
Hivi hauamini Barcelona Ilikuwa Bora?
Kwani angechezea huko Napoli angefunga magoli yote hayo?
Na je unajua ratiba za mechi za timu ya Taifa la Argentina miaka ya Maradona na miaka ya Messi?
Na je akili yako ya kawaida inakuambia mchezaji akifunga anakuwa ni Bora humo uwanjani kuliko yule ambaye hajafunga?
Chukua mfano huu,
Argentina na Messi wametoa Suluhu na Chile kwa kufungana 2-2 na Messi amefunga 2 kwa mikwaju ya penalty
Argentina na Maradona wamempiga Chile 1-0 na Maradona akiweka nyavuni kwa shuti la mbali,
Kwa akili yako Nani shujaa?
Hizo takwimu unazoshupalia hazitaji mazingira ya ufungaji wa magoli
Hazitaji pressure ya mchezo
Hazitaji ubora wa kikosi na wachezaji wake
Hazitaji maufundi yaliyofanywa na mchezaji
Hazitaji aina ya kocha
Hazitaji aina ya uchezeshaji wa refa aliyohusika
Hazitaji aina ya viwanja walivyocheza
Hazitaji aina za sheria za mpira zilizohusika
Hazitaji aina za mabeki walimkaba mchezaji
Hazitaji aina ya golikipa aliyehusika!
Acha kushupalia takwimu!
Hizo takwimu zinaweza kukuambia John Boko aliwahi kuwa Bora kuliko Harry Kane
Bado unazuzuka na takwimu,Hujielewi unachoongea mkuu.
-2018 messi aliifikishaje Argentina Fainali?
-Kutokea hatua ya makundi mpaka fainali zote za Copa America messi aliifikishaje fainali Argentina?
-2022 messi alishinda magoli mawili fainali dhidi ya France ambayo sio ya Penalty ila France Mbappe alipewa penalty mbili je ulijiuliza kama Mbappe asingepata penalty mbili nani alikua anachukua ufungaji bora?
-Unaikumbuka el-classico ya kwanza messi anacheza akiwa na miaka 19 na akiwa na jezi namba 19 mgongoni aliisawazishia Barcelona huku akifunga hat trick dhidi ya mabeki bora wa Real madrid huku akiwa yeye ndio mchezaji mdogo na mchanga?
-Copa America ya 2021 kama sijakosea unajua messi kashinda magoli mangapi kuipa Argentina Copa America?
-Hivi unajua messi ndio playmaker anayeongoza kwa assist duniani?Na nadhani unajua maana ya playmaker bimaana timu haiendi bila ufundi wa huyo mtu.
-Unamfuatilia messi intermiami ana assist ngapi!?
Hujui mpira bro bora usijadili.
Messi kuifikisha Argentina fainali za Copa America alikua akifunga magoli hadi manne mechi moja peke yake.
Pia usisahau messi ni mchezaji mwenye makombe ya timu ya taifa ya under 18 mengi kuliko huyo Maradona.
Yani inaonesha toka yuko mdogo messi anakiwasha.
Itakua umeanza kufuatilia mpira juzi
Hivi takwimu zinakuja pasi na mtu kuzipambania?
Au takwimu zinaandikwa tu bro?
Usichekeshe mzee,takwimu zinakuja kwa kupambana mzee.
HAkuna beki mkubwa ambaye hajateswa na messi.
Bro mpira hujui narudia hujui mpira.Bado unazuzuka na takwimu,
Takwimu hazioneshi ubora, Ila zinaoneasha mafanikio, whether umeyapata kwa ubora wako au kubebwa na timu haizingatiwi
Unazungumzia kufika Messi kufika fainali na Argentina Mara mbili kana kwamba wachezaji wenzake kwenye timu nao hawakufika Mara mbili
Au utadhani Kama hakuna timu zingine zilizofika fainali Mara mbili ambazo hakuna mtu anaitwa Messi
Unazungumzia Messi kufunga magoli kwenye el classico akiwa na umri mdogo, kwa hio yeye alikuwa Bora kuliko Gaucho kisa tu amefunga magoli?
Magoli ni mafanikio sio ubora
Unazungumzia Messi kuwa playmaker unasahau kuwa hayo matunda ya mifumo Bora ya kisoka ambayo Maradona hajaipitia?
Mifumo ambayo kocha anadirect timu imchezeshe nani
Usisahau Azizi Ki ni play maker Bora kabisa ambayo hayupo kwenye record za dunia
Unazungumzia Messi kufunga magoli manne kwenye mechi moja, ni yaleyale ya mifumo ambayo kocha anadirect timu imchezeshe nani
Maradona Ni kipaji asilia, ambaye alikuwa anaucheza mpira bila kubebwa na mifumo ya kisasa ya soka
Maradona hajapita kwenye academy za soka
Maradona amecheza nyakati za soka la jihadi sio soka alilocheza Messi, soka la Fair play
Maradona hajacheza soka la kisasa linalochezwa kwa pasi nyingi ambapo mchezaji unajiweka tu kwenye position upewe pasi ufunge
Maradona hajacheza timu zenye Hali ya ubora ambao unamhakikishia mchezaji kuchukua vikombe kila msimu
Maradona hajaanza soka na umri mdogo Kama Messi
Maradona hajacheza soka nyakati za maendeleo makubwa ya teknolojia za soka, Kama teknolojia zamatibabu ya mchezaji, teknolojia zachakula Cha mchezaji, teknolojia za mazoezi ya mchezaji
Nasikitika uko bize na takwimu ambazo zinaonesha mafanikio tu
Kwangu Mimi ubora ni ufundi wa kucheza mpira na ufundi wa kufunga magoli
Kuhusu takwimu kuwa mchezaji amefunga magoli mangapi hio inategemea factors nyingi Sana
Ila Maradona alikuwa mtu na nusu, ambaye kwa umashuhuri wa miguu yake, dunia ilipata kumtambua
Yaah,Bro mpira hujui narudia hujui mpira.
Messi akati anashinda makombe ya timu ya taifa under 18 alibebwa na kina nani?
Unataka kuja katika ufundi?
Basi wacha nikutajie ufundi ambao messi anao kuliko Maradona.
1)Messi ni dribbler wa dribble fupi ambae hajawahi kutokea duniani.
2)Messi ni faster dribbler kuliko dribbler yeyote ulimwenguni.
3)Messi ni mchezaji mwenye stamina na balance ya kuwekea misuli hata wachezaji watatu na asianguke.
4)Ni mchezaji ambaye ana shooting accuracy kuliko Maradona,ndio maana msimu 2019/2020 kama sijakosea aliweka rekodi ya kushinda magoli 20+ ya faulo/dead ball,rekodi ambayo haikuwahi kuwekwa na huo ni uwezo binafsi.
HUwezi mfananisha Messi na Aziz Ki we jamaa,Messi ni mchezaji ambae anaichezesha timu na anaipandisha timu na aliwahi kuhudumu nafasi tatu tofauti ndani ya wakati mmoja kipindi cha Ernesto valverde aliwahi kucheza kama CMF,AMF,LW na magoli akashinda.
Ni vigumu kuwa kiungo wa kati na ukashinda magoli mengi.
Timu ya taifa ya Argentina ilikua na kina nani bwana wewe!?
We mpira umeanza kufuatilia lini kijana?
Messi magoli anayoshinda sio ya kupewa,embu katizame clip zake,mtu anachenga mabeki wanne na kipa wake anashinda,unadhani hilo jambo dogo.
Ni skills zipi Maradona anazo na Messi hana!?
EMBU ZITAJE HAPA HIZO SKILLS.
kama ingekua kuchezeshwa na mfumo ni kifu rahisi basi kina Giroud wangekua wanabeba tuzo kila mwaka.
Au we unadhani ni kitu rahisi kuingia katika mfumo wa kocha!?
Kama messi alikua anabebwa na mfumo kwanini yeye ndio anaongoza kwa ASSIST?
Na toka lini Azizi ki akawa play maker??
Play maker ni mtu kama CHAMA AU PACOME,AZIZ KI SIO PLAYMAKER.
NILIKUULIZA UMEMFUATILIA MESSI HUKO INTERMIAMI ANACHOKIFANYA!?
[emoji115][emoji115][emoji115][emoji115]Embu kamfuatilie.
Messi kabla hajaenda Barcelona alionekana akiwa na kipaji huko kwao Buenos aires tena anakichafua balaa.
Uwe na heshima aisee usimfananishe messi na Maradona, kama unadhani academy inamkuza mchezaji bila kipaji basi hata wewe ungeenda uone kama utafaulu kuwa mchezaji bora.
Hiyo Argentina ukimtoa messi unaona pengo kubwa kabisa hili hapa linaonekana.
YANGA MTOE AZIZ KI UONE KAMA HAITACHEZA NA KUSHINDA.
Barcelona toka messi aondoke kila mtu alikiri moyo wa barcelona umeondoka na timu ikazorota.
Narudia kukwambia takwimu haziji pasi na kupambana.
Kama unadhani timu inambeba mchezaji asiye na kipaji basi kina Giroud wangekua na ballon dor.
Kama academy inambeba mchezaji asiye na kipaji basi kila mtu angekua mchezaji.
Uzi tutaufunga siku ya sherehe za Aziz Ki kukabidhiwa kiatu chake cha dhahabu cha mfungaji Bora wa msimu huu wa 2024.Sisi humu ni waungwana sana mbona Uzi wa Takwimu Kibu D Vs Mayele kamati ya wandewa tutakubaliana kusamehe na Uzi kuuacha baada ya kuwa mpole na kutimiza masharti yetu.
Na huu tungeutelekeza angekubali kuwa alibumbwa na kuomba radhi ila Cha kusikitisha ndugu Mwasibu licha ya wazee wenye hekima wakina Tate Mkuu na Dr Matola PhD kumsihi atulie bado akawa anashusha matusi kwa wachangiaji ,kejeli pamoja na dislikes. Sasa Wandewa tukaona jamaa inabidi aendelee kupigwa spana bila kupoa mpaka akubali masharti
GB 64 tumetowaa Police tumempa na laki moja apunguze machungu.