Kiingereza cha Rais Samia

Kiingereza cha Rais Samia

Nimemsikiliza Hangaya, ana uwafadhali sana tena sana ukimlinga na Dr Jiwe, Dr Jiwe anaachwa mbali sana na Hangaya kwenye hii lugha.

Kama kuna mtu yeyote anabisha haya nisemayo aje kuthibitisha kwa ushaidi wa klip yake yoyote akiongea kiingereza Dr Jiwe.

Kuhusu kukosea juu ya kusema kuwa Kamala ndio mwanamke wa kwanza kugombea nafasi ya umakamu urahisi Marekani, kama mnakunbuka jiwe alisema kuwa Saddam Hussein Kuwait kipindi cha kampeni za 2015. mbele ya watanzania wenzake akiwa anaongea kiswahili kabisa.

Dr. Jiwe hakika aliufahamu udhaifu wake ndio maana hakutaka kutoka nje ya nchi hasa nchi za Ulaya na America, alifahamu atashikwa kigugumizi tu, badala yake akawa anawapekeka mama Samia na Majaliwa.

Nb. Anaepinga kuwa Dr. Jiwe hakujua kuongea lugha ya kiingereza aweke klip yake hapa.
Nina wasiwasi kuwa sababu ya Dr. Magufuli kutokwenda nje ya Africa ni kuongea kiingereza. Kwani si kuna option ya kuzungumza kiswahili akatafsiriwa?

Lakini kuna zile gadgets wanatumia kwenye mikutano ya kimataifa zinazotafsiri lugha mbalimbali.

Angeweza kutumia kimojawapo. Tena kwa uhalali wa kukitangaza kiswahili duniani na angeeleweka tu. Mbona Xi Jingpin anaongea Kichina anatafsiriwa na mkalimani na haina shida?

Kuna zaidi ya hapo.
 
Sukuma gang tupumzisheni walau kidogo jamani!!!
Hili jitu linafananisha kiingereza Cha Magu na Samia, hahaha, Magu hovyo kabisa, sukuma gang wakagawane nguo za marehemu
 
Nimemsikiliza Hangaya, ana uwafadhali sana tena sana ukimlinga na Dr Jiwe, Dr Jiwe anaachwa mbali sana na Hangaya kwenye hii lugha.

Kama kuna mtu yeyote anabisha haya nisemayo aje kuthibitisha kwa ushaidi wa klip yake yoyote akiongea kiingereza Dr Jiwe.

Kuhusu kukosea juu ya kusema kuwa Kamala ndio mwanamke wa kwanza kugombea nafasi ya umakamu urahisi Marekani, kama mnakunbuka jiwe alisema kuwa Saddam Hussein Kuwait kipindi cha kampeni za 2015. mbele ya watanzania wenzake akiwa anaongea kiswahili kabisa.

Dr. Jiwe hakika aliufahamu udhaifu wake ndio maana hakutaka kutoka nje ya nchi hasa nchi za Ulaya na America, alifahamu atashikwa kigugumizi tu, badala yake akawa anawapekeka mama Samia na Majaliwa.

Nb. Anaepinga kuwa Dr. Jiwe hakujua kuongea lugha ya kiingereza aweke klip yake hapa.
Sukuma gang bado wanaweweseka , tuwaache wakamalizie msiba na kupalilia kaburi
 
Nina wasiwasi kuwa sababu ya Dr. Magufuli kutokwenda nje ya Africa ni kuongea kiingereza. Kwani si kuna option ya kuzungumza kiswahili akatafsiriwa?

Lakini kuna zile gadgets wanatumia kwenye mikutano ya kimataifa zinazotafsiri lugha mbalimbali.

Angeweza kutumia kimojawapo. Tena kwa uhalali wa kukitangaza kiswahili duniani na angeeleweka tu. Mbona Xi Jingpin anaongea Kichina anatafsiriwa na mkalimani na haina shida?

Kuna zaidi ya hapo.
Kile kidude kwenye moyo
 
Halafu hivi ni mimi tu [maana nisije kuwa na nitpick] au mbele/ pembeni ya Kamala, Hangaya kaonekana kama hana gravitas?
Wewe ulikuwa husikilizi message ulikuwa unavizia wapi atakosea kiingereza, mie nimemsikiliza na nimemwelewa, halafu ujue siyo native speaker wa hiyo lugha.

kweli kuna makosa ya knowledge kayafanya hasa la the first woman participation.
 
Akiwa anasoma, kuna afadhali kidogo.

Lakini akiwa anaongea kutoka kichwani ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa], anapata shida sana.

Yaani Magu na Hangaya walichaguana wote wakiwa weupe kwenye hiyo lugha pendwa.

Muangalie na msikilize kwenye video hapo chini. Yale ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa] kwenye karatasi, anapata shida kuyaongea.

Anajiuma uma tu. Hajiamini. Mpaka hata taarifa za ukweli [facts] anazikosea.

Uchaguzi mkuu wa Marekani wa 2020 haukuwa uchaguzi wa kwanza wa nchi hiyo kuwa na mwanamke kama mgombea umakamu wa Rais.

Wakati Geraldine Ferraro anagombea kwenye tiketi moja na Walter Mondale, Hangaya alikuwa wapi?

Wakati Sarah Palin anagombea na John McCain, Hangaya alikuwa wapi?

Au alitaka kusema kuwa 2020 ndo mara ya kwanza kwa mwanamke kuwa katika tiketi iliyoshinda uchaguzi lakini akajiuma uma na akakosea hizo basic facts?

Halafu, ni ‘the United States and Tanzania have enjoyed excellent relations [siyo relation], for the last [past sounds much better] 60 years’.

Halafu kuna watu wanadai eti Hangaya yuko vizuri kwenye Kiingereza 🤣. Ama kweli hii lugha ni janga la kitaifa.

Maana mtu yeyote aijuaye vizuri hiyo lugha hawezi kusema eti Hangaya yuko vizuri.

Hangaya na Magu labda wanapishana kwenye lafudhi tu. Magu alikuwa na lafudhi nzito/ nene zaidi. Hangaya ya kwake si nzito kivile, hivyo kuonekana kama vile anaimudu, kumbe wapi!

Kwenye sintaksia, semantiki, sarufi, kunyambua vitenzi, n.k., hawapishani sana. Wote mulemule tu.


Toa upuuzi wako hapa,kwani yeye ni Muingereza au Mmarekani? Mbona anaongea vizuri tu? Hii ndio shida kuu ya wabongo kama wewe. Unataka aongee kama wenye lugha halafu iweje? Au kwa kuwa umeishi Marekani hivyo unataka kila mtu aongee kama wao?
 
Kwangu lugha maridhawa si tatizo sana kwa sababu Umombo si lugha yetu mama, nakwazika sana Rais yoyote akiwemo Samia kuanza kukandia viongozi waliopita wakati ni viongozi waliotokana na chama kilekile kiitwacho chama tawala...

Sijui hawaelewi kuwa unapomponda Rais aliyepita ni sawa kabisa na kukiponda chama chao wenyewe na sera ama ilani zake...
Kama angekuwa wa awamu tofauti tungesema pengine ana haki ya kurekebisha yaliyokosewa...Sasa huyu na kampeni alifanya na mwenzake kama ishara ya maono ya pamoja anapokuja kuyageuka mwenzake anapokosa power hiyo si sawa, ni indicator ya kukosa integrity na uaminifu ambayo sidhani kama yeye yupo hivyo
 
Akiwa anasoma, kuna afadhali kidogo.

Lakini akiwa anaongea kutoka kichwani ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa], anapata shida sana.

Yaani Magu na Hangaya walichaguana wote wakiwa weupe kwenye hiyo lugha pendwa.

Muangalie na msikilize kwenye video hapo chini. Yale ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa] kwenye karatasi, anapata shida kuyaongea.

Anajiuma uma tu. Hajiamini. Mpaka hata taarifa za ukweli [facts] anazikosea.

Uchaguzi mkuu wa Marekani wa 2020 haukuwa uchaguzi wa kwanza wa nchi hiyo kuwa na mwanamke kama mgombea umakamu wa Rais.

Wakati Geraldine Ferraro anagombea kwenye tiketi moja na Walter Mondale, Hangaya alikuwa wapi?

Wakati Sarah Palin anagombea na John McCain, Hangaya alikuwa wapi?

Au alitaka kusema kuwa 2020 ndo mara ya kwanza kwa mwanamke kuwa katika tiketi iliyoshinda uchaguzi lakini akajiuma uma na akakosea hizo basic facts?

Halafu, ni ‘the United States and Tanzania have enjoyed excellent relations [siyo relation], for the last [past sounds much better] 60 years’.

Halafu kuna watu wanadai eti Hangaya yuko vizuri kwenye Kiingereza 🤣. Ama kweli hii lugha ni janga la kitaifa.

Maana mtu yeyote aijuaye vizuri hiyo lugha hawezi kusema eti Hangaya yuko vizuri.

Hangaya na Magu labda wanapishana kwenye lafudhi tu. Magu alikuwa na lafudhi nzito/ nene zaidi. Hangaya ya kwake si nzito kivile, hivyo kuonekana kama vile anaimudu, kumbe wapi!

Kwenye sintaksia, semantiki, sarufi, kunyambua vitenzi, n.k., hawapishani sana. Wote mulemule tu.


Hivi lugha ya Kiingereza ina uzito gani katika vigezo vya kuwa Rais wa Tanzania? Jee, hiki ni kitu kweli cha kutupotezea usingizi : eti Magufuli na Samia wanapishana kwenye lafudhi tu lakini wote hawakimudu Kimombo! Afadhali lugha inayozungumziwa ingekuwa Kiswahili, kwani Rais inabidi awe mfano kwenye lugha ya Taifa. Mtanzania una mengi ya kuwazia kuhusu kujikwamua kwenye changamoto za kiuchumi na kijamii, zaidi ya kujadili Kiingereza cha Rais wako. Hoja hii haina tija kwenye maslahi ya Mtanzania. Kama mmoja wao anakimanya kimombo zaidi ya mwenzie, so what?
 
Nina wasiwasi kuwa sababu ya Dr. Magufuli kutokwenda nje ya Africa ni kuongea kiingereza. Kwani si kuna option ya kuzungumza kiswahili akatafsiriwa?

Lakini kuna zile gadgets wanatumia kwenye mikutano ya kimataifa zinazotafsiri lugha mbalimbali.

Angeweza kutumia kimojawapo. Tena kwa uhalali wa kukitangaza kiswahili duniani na angeeleweka tu. Mbona Xi Jingpin anaongea Kichina anatafsiriwa na mkalimani na haina shida?

Kuna zaidi ya hapo.
Sifa zile za Dr Jiwe yaani hicho kitu hakutaka kabisa, hakutaka hata kidogo kudhalilisha nafsi yake. na kwa kufanya hivyo pia watu ambao walikuwa wanahoji elimu yake wangeendelea mkunyanyasa kupitia udhaifu wa kuto jua kuongea kiingereza.

Nb. Pamoja na yote yatupasa tujue kwamba kuongea kiingereza sio ishara kuwa upo juu kielimu.
 
Inakwenda kusikojulikana..
Hapana. The state is finally back from ruthless hijackers and mercenaries.
Ilipo sasa hivi kama wananchi tunaweza kupaza sauti na tukasikilizwa si kuuliwa.

Tusiruhusu ipitilize kusikojulikana!!
 
Hapana.

Fluency haihusiani na kusoma vilivyoandikwa.

Ni kwamba hana lafudhi nzito/ nene. Hicho ndicho kinachomfanya aonekane ana afadhali.

Lakini maneno mengi sana yanampa shida kuyatamka.

Hata yale maneno ya kawaida ya hiyo lugha hawezi kuyatamka vizuri.

Ukimwandikia neno kama ‘xylophone’ au ‘discombobulation’, anaweza kupoteza fahamu akijaribu kuyatamka.
Sasa utamfananisha na jiwe?si afadhali yeye kuliko jiwe aliyekua anajifungia chumbani anaogopa kusafiri
 
Nb. Pamoja na yote yatupasa tujue kwamba kuongea kiingereza sio ishara kuwa upo juu kielimu.
Nadhani iangalie kwenye taswira hizi:
1. Elimu inayoeleweka bila ufaulu wa kukariri.
2. Uwezo binafsi wa mtu kujenga hoja na kujieleza!
3. Maandalizi (mazoezi) binafsi

NB: Huko tuliko tujiandae kikamilifu ku encounter international situations. Dunia ni kijiji. Wengi wanaomsema SSH wanapata shida hizo hizo hata wakikutana na Wachina, Indians, Russians ambao si native English speakers.
 
Akisoma anakuwa fluent kidogo, kuwa mtu wa pwani kunamfanya aweze kusoma vizuri.

Yale ya kutoa kichwani ni mweupe pe! Kama mimi tu😋
Tatizo ni maandalizi... Na kukosa mtiririko wa hoja!
Na mtu akiwa hivyo haijalishi anatumia lugha gani!
 
Sioni kama ni tatizo kubwa sio mother tongue yao JPM na Samia sio lazima waongee fluently.

Mfumo wetu wa elimu wa zamani kiingereza hakikupewa nafasi kubwa hata uwe na PHD hauwezi ongea fluent English.

Siku hizi English medium ndio zinasaidia kuwa fluent sababu watoto wanajua kirahisi zaidi.

Tunamjudge kiongozi wetu kwa vigezo muhimu vipaumbele ktk policies,Diplomacies etc sio kiingereza.
Acha visingizio vya kijinga, kiingereza ni lugha rasmi ya taifa kama kilivyo kiswahili, kiingereza hakitumiki serikalini kwa hiari bali kinatumika kisheria, maneno ya wanasiasa weka pembeni.
 
Akiwa anasoma, kuna afadhali kidogo.

Lakini akiwa anaongea kutoka kichwani ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa], anapata shida sana.

Yaani Magu na Hangaya walichaguana wote wakiwa weupe kwenye hiyo lugha pendwa.

Muangalie na msikilize kwenye video hapo chini. Yale ambayo hayajaandikwa [hajaandikiwa] kwenye karatasi, anapata shida kuyaongea.

Anajiuma uma tu. Hajiamini. Mpaka hata taarifa za ukweli [facts] anazikosea.

Uchaguzi mkuu wa Marekani wa 2020 haukuwa uchaguzi wa kwanza wa nchi hiyo kuwa na mwanamke kama mgombea umakamu wa Rais.

Wakati Geraldine Ferraro anagombea kwenye tiketi moja na Walter Mondale, Hangaya alikuwa wapi?

Wakati Sarah Palin anagombea na John McCain, Hangaya alikuwa wapi?

Au alitaka kusema kuwa 2020 ndo mara ya kwanza kwa mwanamke kuwa katika tiketi iliyoshinda uchaguzi lakini akajiuma uma na akakosea hizo basic facts?

Halafu, ni ‘the United States and Tanzania have enjoyed excellent relations [siyo relation], for the last [past sounds much better] 60 years’.

Halafu kuna watu wanadai eti Hangaya yuko vizuri kwenye Kiingereza 🤣. Ama kweli hii lugha ni janga la kitaifa.

Maana mtu yeyote aijuaye vizuri hiyo lugha hawezi kusema eti Hangaya yuko vizuri.

Hangaya na Magu labda wanapishana kwenye lafudhi tu. Magu alikuwa na lafudhi nzito/ nene zaidi. Hangaya ya kwake si nzito kivile, hivyo kuonekana kama vile anaimudu, kumbe wapi!

Kwenye sintaksia, semantiki, sarufi, kunyambua vitenzi, n.k., hawapishani sana. Wote mulemule tu.


naona anasoma wala hatowi kichwani.Kwa maelezo yako yanamhusu pia muandaaji.
 
Meko hata kiswahili tu aliondoka kinampiga chenga:

MBWA anaita UMBWA
 
Nadhani iangalie kwenye taswira hizi:
1. Elimu inayoeleweka bila ufaulu wa kukariri.
2. Uwezo binafsi wa mtu kujenga hoja na kujieleza!
3. Maandalizi (mazoezi) binafsi

NB: Huko tuliko tujiandae kikamilifu ku encounter international situations. Dunia ni kijiji. Wengi wanaomsema SSH wanapata shida hizo hizo hata wakikutana na Wachina, Indians, Russians ambao si native English speakers.
Ni kweli kabisa mkuu, lakini hapa nilikuwa najaribu kuongea ili watu wafahamu kwamba unaweza kuongea sana kiingereza, kiarab au hata kichina na kifaransa sio kwababu umesoma sana, isipokuwa isipokuwa umekaa sana nchi ambazo wanaongea sana hizo lugha.

Nina mfano, Kuna rafiki yangu mmoja sikuwa juwa kuwa yupo vizuri kiasi kile katika uongeaji wa kiingereza, na ni kwa vile hakuwa muongeaji wa kiingereza bila sababu kama kaka na dada zangu wa kihaya..

Sasa Kuna siku tukuwa na orally interview jamaa alitelemsha ngeli ya hatari bahati nzuri interview hiyo ilikuwa adharani, wote tuliokuwa tunashiriki tulikuwepo yaani mwenzako anahojiwa unaona na unasikia.

Baada ya hapo tukamuuliza ndugu yetu hii kitu umeingia nayo kutoka wapi!!? (Jamaa ni muislam) watania wakasema dua hizo huyo ni shehe. Ila uhalisia jamaa alikaa Zambia Lusaka, baba yake akiwa anafanya kazi TAZARA
 
Back
Top Bottom