Kijana afanya utani wa kutaka kumuua Rais Magufuli, aambuliwa kifungo cha miaka 2 jela

Kijana afanya utani wa kutaka kumuua Rais Magufuli, aambuliwa kifungo cha miaka 2 jela

Ni vema kusoma alama za nyakati, huu si wakati wa kufanya masihara.
Itabidi niwe makini nikiwa nasoma vichwa vya habari vya magazeti,maana huwa kunakuwaga na kaubishani flani hivi ka hoja kutokana na habari zilivyoandikwa.

Sema Mara nyingi huwa nabishanaga kuhusu kabumbu hivyo sijawahi kuathirika[emoji4]
 
Akajifunze kwanza maana miaka miwili sawa sawa na mwaka mmoja si haba
 
Nani alimrecord? Kiongozi anaejitutumua kujifanya mwamba always huwa waoga sana
Alikosea sana
Unadiriki kusema quote "ALIKUA ANAFANYA UTANI KUSEMA ATAMUUA RAIS" wewe ni mtetezi wake ??, kitu gani kimekuongoza hadi ku hitimisha kua alikua anafanya utani ilhali yeye mhusika amwkiri mahakamani ? Usijitoe ufahamu ndugu issues zinazongusa Rasi ni nyeti kuliko unavyofikiri, na unadiriki kusema ”SIJAONA KOSA LA KUMFANYA AFUNGWE MIAKA MIWILI" Unajua sheria zinasemaje kwa mtu anaetishia kuua ?
Narudia tena Sijaona Kosa hapo, nimetoa mifano michache ya hicho unachokiita sheria, Hivi unajua iKila raia ana haki sawa mbele ya sheria ?, hao askari walioua na huyu aliyetania kwamba ataua, nani ana kosa linalostahiri adhabu ?, huyo kijana amekiri kwamba alisema hayo maneno wewe unataka kulazimisha kwamba amekiri alitaka kumuu, !!, wewe ni mtetezi wa wapangaji wa Ikulu ?, naamini unajaribu kujifanya mwehu ilhali una akili timamu, huyo malaika wenu mnamtetea ili mteuliwe ?, wengine mko mbali sana sio rahisi kuonwa, Kijana mmoja raia wa Argentina alimfyatulia risasi Papa John Paul ll mwaka 1984 lakini Papa aliamuru huyo kijana aachiwe huru !!
 
Ni kosa kisheria jamani, hata wewe ukitishwa kuuawa nenda kashtaki.Mimi nimewahi kumshtaki mtu kwa kunitamkia kwamba ataniua ila badae nikamuonea huruma sikwenda mahakamani mpaka kesi ikafutwa. Pamoja na hayo Rais ni nembo ya Taifa unatishia vipi kumuua hata kama unatania.

Tuache ushabiki wa kijinga.
Yule alietishia kumuua Lissu yuko wap? Na Yule alomtishia NAPE yuko wap?
 
Kwa hiyo alimaanisha kumuua rais au ukweli unaoufahamu wewe ni upi?

Vyovyote iwavyo point yangu ni kuwa watu wausome utawala uliopo na kujua waende nao vipi.
Binafsi yangu nime kuelewa dada.
 
Unadiriki kusema quote "ALIKUA ANAFANYA UTANI KUSEMA ATAMUUA RAIS" wewe ni mtetezi wake ??, kitu gani kimekuongoza hadi ku hitimisha kua alikua anafanya utani ilhali yeye mhusika amwkiri mahakamani ? Usijitoe ufahamu ndugu issues zinazongusa Rasi ni nyeti kuliko unavyofikiri, na unadiriki kusema ”SIJAONA KOSA LA KUMFANYA AFUNGWE MIAKA MIWILI" Unajua sheria zinasemaje kwa mtu anaetishia kuua ?
Wangapi wametishia kuua hadharan na hapajafungwa wala kukamatwa...!!!? Wangapi wameua wazi kabisa Kwa raia wasio na kosa na je wamekamatwa au kufungwa hata tu siku moja? Iweje Kwa mtu aliesema tena kijiweni "ANATANIA" hafu afungwe...!!?? Duuh
 
Coaster2015,
Kwa mujibu wa sheria, hao askari unaosema wameua, na huyo kijana aliyetishia kuua, yote hayo ni makosa na yana hukumu zake kwa mujibu wa sheria na kanuni za adhabu, usihitimishe kwa kusema "SIJAONA KOSA HAPO" inawezekana wewe hujaona kosa kulingana na Elimu yako.
 
Hiki cheti changu chenye degeree inabidi kifutwe. Mimi miaka yote najua nembo ya taifa ni hii
ngao.jpeg
 
Wangapi wametishia kuua hadharan na hapajafungwa wala kukamatwa...!!!? Wangapi wameua wazi kabisa Kwa raia wasio na kosa na je wamekamatwa au kufungwa hata tu siku moja? Iweje Kwa mtu aliesema tena kijiweni "ANATANIA" hafu afungwe...!!?? Duuh
Ukiua ni kosa na lina adhabu zake, ukitishia kuua ni kosa na lina adhabu zake, sasa hao ambao wametishia kuua na ambao waliua lakini hawajafungwa hilo ni swali ambalo wewe na mimi hatuna majibu, lakini haiondoi ukweli kuwa ni kosa
 
Kwa ulinz wa yule mwamba ata isis wanaweza kushughulishwa vyakutosha sembuse uyu mnyaturu mzalendo uyu wangempima tu akili ukute ana ziro IQ au msongo wa mawazo anahitaji matibabu sio kumpiga mvua
 
Katenda kosa tarehe 26/nov Leo tarehe 4/12 na hukumu tayari imeshatoka!!! Pongezi kubwa kwa Mahakama kwa kuendesha kesi ushaidi kukamilika na kutoa hukumu ndani ya wiki moja toka mshtakiwa kutenda kosa.Mahakama nyingine nchini kote ziige mfano huu maana kuna ndg, rafiki, jamaa zetu wengi sana wapo mahabusu bila kujua hatma ya mashtaka yao.
elewa hajaisumbua mahakama kwa kukiri kosa, huyo kashindwa maisha tu bora akale bure jela, atakuwa gereza gani nimuwekee na bili ya maziwa
 
Ni kosa kisheria jamani, hata wewe ukitishwa kuuawa nenda kashtaki.Mimi nimewahi kumshtaki mtu kwa kunitamkia kwamba ataniua ila badae nikamuonea huruma sikwenda mahakamani mpaka kesi ikafutwa. Pamoja na hayo Rais ni nembo ya Taifa unatishia vipi kumuua hata kama unatania.

Tuache ushabiki wa kijinga.
Yule aliyendika na kutishia hadharani kwamba atamuua Lisu yuko wapi?

Tunataka jibu
 
Ila huyu kijana hajipendi,ama alikua kalewa bangi au pombe
 
Mwambieni His Excellency Dr. John Pombe Magufuli amsamehe huyo kijana. Alikosea.
 
Back
Top Bottom