Kijana baada ya kumaliza masomo yako mjini ni wakati wa kurudi nyumbani kijijini, wazazi wako wanakungoja

Kijana baada ya kumaliza masomo yako mjini ni wakati wa kurudi nyumbani kijijini, wazazi wako wanakungoja

aise,
muwe mnatuma kweli basi hiyo sukari, sio tena nyie ndio mnawapiga vizinga wazazi dah!

nikiwa mjini siku zingine hapo nyuma,
nimemsika dada moja muhitimu wa chuo kikuu hapo mjini, amehitimu miaka 4 iliyopita yuko nyumbani hana cha kufanya ,

siku hiyo,
akawa anabishana na mamake mzazi kwa uchungu sana,
na akamwambia mamake kwamba amechoka kua housegirl wa nyumbani kwao dah! ilinishangaza sana kwakweli...

nikajiuliza hivi kama familia hii ingekua na mashamba pangekua na mabishano ya aina hii kweli ?
huenda angeambiwa kabishane na shamba maana sasa mama atafanyaje?🐒
Na wazazi wakamgeuza house girl badala wamtafutie kitu cha kujishugulisha.

Ajira ni changamoto
 
Na wazazi wakamgeuza house girl badala wamtafutie kitu cha kujishugulisha.

Ajira ni changamoto
sure,
yupo kaka yangu mkali sana,
kijana wake hakufaulu kidato cha nne, kijana amechunga sana ng'ombe na nguruwe za nyumbani kwao,

mimi na yeye hatukonana kitambo kidogo,
majuzi nimekutana nae mjini, kwanza kabadilika sana na ametakata vizuri sana,

nikamuuliza kulikoni mjini, unafanya nini? akanijibu hua kila baada ya wiki moja anakuja mjini naleta nguruwe wazima na kuwauza...

nikamuhoji biashara ikoje lakini,
akasema sio mbaya na ndio maana kila wiki niko mjini ingawa wanyama hao si wengi sana huko vijijini tunapoenda kuwanunua kwasasa,

akanieleza kua safari hii amekuja na nguruwe wenye jumla ya kilo294,
na kila kilo ya nguruwe nauza elfu10...

sikutaka kuuliza zaidi,
ila kwa nilivyopima maelezo yake ni kwamba anatengeneza pesa mingi sana kwa mwezi mara 3 au 4 ya mwenye mshahara wa laki6 au 7 kwa mwezi,

gentleman,
hii si fursa ya kuchangamkia kabisa kuondokana na unyonge wa kiuchumi 🐒
 
Wazazi wa vijana wengi wa leo wanafanya maombi na kuwaombea vijana wao sana kila lililo jema wafanikiwe katika maisha yao, hakuna mzazi alie nyuma kwenye hili kwasababu mambo yamebadilika sana sasahivi...

Lakini vijana wengi wamedinda kabisa kurudi nyumba vijijini kwao, licha yakua wameshamaliza masomo miaka mingi imepita sasa, lakini bado wamekomaa tu mijini.

Ndiyo, wanawasiliana na wazazi wao vizuri tu kwamba hawajambo wanaendelea vizuri na maisha mjini,

Ila cha kushangaza vizinga vya hapa na pale kwa vijana hawa kwa wazazi wao huko vijijini haviishi, kila mara kijana akipiga simu nyumbani kijijini kwa wazazi, basi ujue amekwama anapiga kizinga cha kuomba chochote kitu kwa mama au baba kwaajili ya kujikimu kimaisha huko mjini wanako randaranda bila uelekeo tangu wamemaliza masomo miaka zaidi 8 au 10 iliyopita lakini ajira bilabila...

Baadhi ya wazazi wamebadili hata namna ya kuwaombea watoto wao, na sasa wanawombea vijana warudi vijijini kwao kwani viwanja walivyowatengea wajenge nyumba na mashamba vipo salama na vinawasubiri ..,

Rudini nyumbani kumenoga friends ladies and gentlemen,

Au mpaka ianzishwe kampeni ya, ewe kijana mzururaji mjini, rudi nyumbani kijijini kumenoga?

Msione aibu bana eti kisa tu wadogo zako na wale rafiki zako walioishia darasa la saba wana majumba na magari ya maana kijijini na wewe mwenye shahada hata hueleweki dah 🐒

Una maoni gani kuhusu hili ndugu mdau?

Mungu Ibariki Tanzania
Mwenyewe ulishindwa kurudi kijijini kwenu ukajisali kuwa chawa wa CCM mjini.
 
Wazazi wa vijana wengi wa leo wanafanya maombi na kuwaombea vijana wao sana kila lililo jema wafanikiwe katika maisha yao, hakuna mzazi alie nyuma kwenye hili kwasababu mambo yamebadilika sana sasahivi...

Lakini vijana wengi wamedinda kabisa kurudi nyumba vijijini kwao, licha yakua wameshamaliza masomo miaka mingi imepita sasa, lakini bado wamekomaa tu mijini.

Ndiyo, wanawasiliana na wazazi wao vizuri tu kwamba hawajambo wanaendelea vizuri na maisha mjini,

Ila cha kushangaza vizinga vya hapa na pale kwa vijana hawa kwa wazazi wao huko vijijini haviishi, kila mara kijana akipiga simu nyumbani kijijini kwa wazazi, basi ujue amekwama anapiga kizinga cha kuomba chochote kitu kwa mama au baba kwaajili ya kujikimu kimaisha huko mjini wanako randaranda bila uelekeo tangu wamemaliza masomo miaka zaidi 8 au 10 iliyopita lakini ajira bilabila...

Baadhi ya wazazi wamebadili hata namna ya kuwaombea watoto wao, na sasa wanawombea vijana warudi vijijini kwao kwani viwanja walivyowatengea wajenge nyumba na mashamba vipo salama na vinawasubiri ..,

Rudini nyumbani kumenoga friends ladies and gentlemen,

Au mpaka ianzishwe kampeni ya, ewe kijana mzururaji mjini, rudi nyumbani kijijini kumenoga?

Msione aibu bana eti kisa tu wadogo zako na wale rafiki zako walioishia darasa la saba wana majumba na magari ya maana kijijini na wewe mwenye shahada hata hueleweki dah 🐒

Una maoni gani kuhusu hili ndugu mdau?

Mungu Ibariki Tanzan
Halafu
 
mmeng'ang'ana town ndugu akikupigia simu na kukujulisha yupo po mjini leo, anataka aje akutembelee, unamruka utadhani anakudai dah 🤣

visingizio kibao,
mara ooh nimesafiri kidogo, ntakupigia baadae, mara ooh niko bize ntakucheki subiri kidogo

kumbe geto lako la mjini ni vichekesho na aibu na tayari una 20yrs uko town,

wakati anaekupigia ni bwanamdogo tu ulimuacha shule ya msingi na aliishia hapo hapo, anakwambia kaja kufunga mzigo kwajili ya duka lake 🤣
Aiseeee mkuu ulivyoandika hapa kuna watu haya ndo maisha yao halisi yaani umepiga panapouma...🤣

Nimekumbuka miaka hiyo ya nyuma nilikuwa nimemaliza tu chuo nikakaza nibaki mjini aisee nilipigika ile mbaya, siku moja mshua kanipigia simu ananiambia unafanya nini huko si urudi tu nyumbani....

Nilikuwa mpole balaa huku moyoni nikijisemea daah mshua kajuaje hali ninayopitia ile sijakaa vizuri nikaona muamala wa 200k ya nauli na matumizi madogo! MAISHA HAYA YAACHE TU😀😀
 
Aiseeee mkuu ulivyoandika hapa kuna watu haya ndo maisha yao halisi yaani umepiga panapouma...🤣

Nimekumbuka miaka hiyo ya nyuma nilikuwa nimemaliza tu chuo nikakaza nibaki mjini aisee nilipigika ile mbaya, siku moja mshua kanipigia simu ananiambia unafanya nini huko si urudi tu nyumbani....

Nilikuwa mpole balaa huku moyoni nikijisemea daah mshua kajuaje hali ninayopitia ile sijakaa vizuri nikaona muamala wa 200k ya nauli na matumizi madogo! MAISHA HAYA YAACHE TU😀😀
unaona sasa,
sasa hivi unakula maisha kijijini saaaafi, na ukitaka kuja kula bata mjini unakuja tu bila mbambamba yoyote lakini una uhakika wa kila kitu..

ni kujipanga, kuamua na kuthubutu tu maisha unatoboa maisha 👊👊👊💪
 
unaona sasa,
sasa hivi unakula maisha kijijini saaaafi, na ukitaka kuja kula bata mjini unakuja tu bila mbambamba yoyote lakini una uhakika wa kila kitu..

ni kujipanga, kuamua na kuthubutu tu maisha unatoboa maisha 👊👊👊💪
Haha😂 nilishatoka huko kwa sasa nipo ndani jiji moja hivi kubwa, hicho ni kipindi cha miaka kama 6 nyuma hahaha.....
 
unaona sasa,
sasa hivi unakula maisha kijijini saaaafi, na ukitaka kuja kula bata mjini unakuja tu bila mbambamba yoyote lakini una uhakika wa kila kitu..

ni kujipanga, kuamua na kuthubutu tu maisha unatoboa maisha 👊👊👊💪
Haya mambo yapo na wala sio utani, vijana waache kung'ang'ania mjini kama pamewashinda.

Unakuta kijana hana kazi ya kueleweka anashinda anazurula tu, kodi anadaiwa kila siku ni kumpiga chenga mwenye nyumba inafika hatua anaondoka saa 11 asubuhi kurudi saa 8 usiku ili wasigongane na mother house.

Kingine ambacho ni aibu mtu upo mjini lakini ukipigiwa simu na ndugu, jamaa na marafiki kuwa tumefika mjini tuje walau tukusalimie unabaki kutoa sababu za uongo tu kumbe hutak wajue maisha unayoishi kwa vile yanatia huzuni...

Mwisho:VIJANA BADILIKENI ACHENI KUNG'ANG'ANIA MJINI TZ MAPORI NI MENGI NA KUNA FURSA KIBAO.
 
Haya mambo yapo na wala sio utani, vijana waache kung'ang'ania mjini kama pamewashinda.

Unakuta kijana hana kazi ya kueleweka anashinda anazurula tu, kodi anadaiwa kila siku ni kumpiga chenga mwenye nyumba inafika hatua anaondoka saa 11 asubuhi kurudi saa 8 usiku ili wasigongane na mother house.

Kingine ambacho ni aibu mtu upo mjini lakini ukipigiwa simu na ndugu, jamaa na marafiki kuwa tumefika mjini tuje walau tukusalimie unabaki kutoa sababu za uongo tu kumbe hutak wajue maisha unayoishi kwa vile yanatia huzuni...

Mwisho:VIJANA BADILIKENI ACHENI KUNG'ANG'ANIA MJINI TZ MAPORI NI MENGI NA KUNA FURSA KIBAO.
huo ni ukweli kabisa gentleman,

kuna kijana wa darasa la saba7 tu wa hapo kijijini kwetu, kila wiki analeta mjini wanyama aina ya nguruwe kati ya 10-15 kutoka mkoani, anaondoka na kati ya milioni3-4. Just imagine hata 25 hajafika...

kijana anazurura kuwanunua hao mifugo huko kijijini anawakusanya pamoja wenzake wanawakusanya wanajaza Lori la kukodi wanaleta mzigo town within 2 to 3days anarudi kijijini..

lakin kuna jamaa anaisubiri laki6 yenye makato kibao for 30days na mwingine hana kabisa hata hiyo 🐒
 
Back
Top Bottom