Kijana unayejitafuta kimaisha, katika utafutaji wako Zanzibar iweke namba moja

Kijana unayejitafuta kimaisha, katika utafutaji wako Zanzibar iweke namba moja

Mkuu kwa unyenyekevu mkubwa naomba uniambie ni sehemu gani Zanzibar wanalipa hichi kiasi naweza weka bondi baadhi ya vitu vya mjomba nikadandia gari hata kesho kutwa. I have to support my people at home, and where I work, I earn only 4,000 per day.
Hiyo buku 4 kwa hapa kwetu ni bei ya supu ya samaki na chapati mbili. Hujaiona mchana bado
 
Uzi Mzuri, Nimepanga Nikimaliza Chuo Niende Zanzibar, Lakini Ninajiulizaa Nitafanya kazi ipi !? Maana Nina Usikivu Hafifu "Hearing Loss" Though Mimi Si Mtu wa Kuchagua Kazi Na Nimeshafanya kazi G1 Security.,
Mungu Anisaidie.
 
Washkaji walishanitonya kitambo Zanzibar ujenzi raia wanakamata 15 per day, Ukijikunja miezi mitatu Milioni unakuwa umeisogelea. Sema nauli ya kunitoa huku karagwe hadi Zanzibar ndio mtiti bado naitafuta.
Huko Zanzibar una wadau tayari wako huko? Yaani ukitoka huko Karagwe una sehemu ukifika na kuanza kazi? Kama ndio nitakutumia nauli
 
Mku muwe mna waambia na exactly maeneo ya kwenda pia msisahau gharama za maisha zanzibar
pia kazi zimekua za shida sana siku hizi kwani wanyamwezi wamemwagika kwa wingi sana huezi amini saiv hata kazi ya kupakua saruji mpaka utoe hongo mambo huku si rahisi hata kidogo
 
Acha utani mkuu . Kwahiyo Breakfast na lunch kwa mtu ambaye anajibana sana inaweza kuwa inamkosti kiasi gani kwa Siku?.
Elf 6 ukijibana sana yani hapo hata matunda huli

Ukiweka na dina mtu mmoja hapo kama buku 9 hiv. Yani hapo chakula na maji bas. Sisi tuko wawili geto usiku tunakula chakula cha kupika
Unga nusu na robo 1500
Samaki wa buku jero wawili 3000
Nyanya mbili 400
Kitunguu 200
Hoho 200
Karoti 200
Ndimu 200
jumla 5900

DONGOA GETO LA WATU WAWILI USIKU TU.
 
Hiyo kitu niliiona, ni fursa kubwa. Hoteli za huko chupa hizi za maji ni nyingi sana, ni suala la kwenda tu kuchukua.
Thats opportunity machupa mengi mnoo ya plastiki. Napambania niweze kupata mashine ya kusaga unga hizi. Huku chupa zenye thaman ni zile ndogo mana wamama wanazitumia kuwekea juisi za matunda. Naweka picha muda mfupi ujao
 
Mku muwe mna waambia na exactly maeneo ya kwenda pia msisahau gharama za maisha zanzibar
pia kazi zimekua za shida sana siku hizi kwani wanyamwezi wamemwagika kwa wingi sana huezi amini saiv hata kazi ya kupakua saruji mpaka utoe hongo mambo huku si rahisi hata kidogo
We simpe M tembea, paje, jambian mpaka michamvi mpaka Nungwi huko. Ina mana umekosa hata trainee ya kufanya uendane na soko la huku?. Watu wanatoka Mwanza wanakuja wanatoboa eti waunguja hawana kazi za kufanya. Juzi kuna waunguja waligoma zege wanataka elfu 30 kila mtu wakaja wabara kwa elfu 20 wakalipiga wakasepa zao.

Kuna sehem Bwejuu inaitwa kwa Lila, hapo kuna waha wengi kuliko wazanzibar wenyewe na wote wanaishi kwa kazi za kishkaji shkaji tu. Nakupa namba za Maduga anataka saidia fundi jambiani
 
We simpe M tembea, paje, jambian mpaka michamvi mpaka Nungwi huko. Ina mana umekosa hata trainee ya kufanya uendane na soko la huku?. Watu wanatoka Mwanza wanakuja wanatoboa eti waunguja hawana kazi za kufanya. Juzi kuna waunguja waligoma zege wanataka elfu 30 kila mtu wakaja wabara kwa elfu 20 wakalipiga wakasepa zao.

Kuna sehem Bwejuu inaitwa kwa Lila, hapo kuna waha wengi kuliko wazanzibar wenyewe na wote wanaishi kwa kazi za kishkaji shkaji tu. Nakupa namba za Maduga anataka saidia fundi jambiani
nipe namba nimcheki mkuu
 
Mkuu, ni jambo jema kama ungedadavua hizo gharama
Zanzibar fursa kubwa ni ujenzi plus utalii.Hizi shughuli zimebeba mnyororo mkubwa sana wa kiuchumi.

Shughuli nyingi za ujenzi hufanyika shamba. Paje, Nungwi na Kiwengwa ndiyo shamba kubwa kwa Unguja na pia ndizo vitovu vikubwa vya utalii.

Watu wengi hutoka mjini na kuja kufanya shughuli zao shamba.Kawaida kibarua hulipwa tsh 15000-20000 kwa kutwa wakati fundi hulipwa tsh 30000-50000 kwa kutwa.

Nauli plus msosi huwa ndiyo kikwazo hasa kwa kibarua, fundi huwa hapati kikwazo sana.Minimum nauli ni tsh 5000 kwenda na kurudi na msosi ukijibana ni tsh 5000 kwa siku.

Hapo bado kodi ya chumba plus umeme coz maji sehemu nyingi ni bure na wana msemo wao 'maji ni ya Mungu'!Viburudisho kama bando ni muhimu coz hizi kazi zinategemea sana mawasiliano!

Kupitia mchanganuo huo hapo juu, unaweza kuona jinsi kujichanga kunavyokuwa na changamoto zake (siyo kama haiwezekeni)hasa kwa kibarua.

Ukibahatika kazi za mjini ambazo huwa chache minimum msosi plus nauli ni tsh 5000 ukijibana.Pia ukibahatika japo (ni ngumu kupata) site za kulala, pia husaidia kujibana, mara nyingi hizi site kama ni kubwa hulindwa na vikosi.

Unatakiwa ufanye nini?? (kibarua)

1) Chukua chumba shamba bei huanzia 50000-100000.

2) Punguza (piga ndefu) kula na kunywa maji plus juisi na energy. Utaweza?? Kazi zako zinategemea nguvu kwa asilimia 100%

3) Vumilia kwa muda mpaka ukiwa fundi coz ukiweka nia ni muda mfupi kwani faida utakayokuwa nayo fundi wako atakuelekeza kwa vitendo zaidi .

Kama kichwa ni chepesi ndani ya miezi mitatu mpaka sita utakuwa umeiva iwe kwenye tofali, mbao,chuma,tiles,umeme n.k, hakuna notisi ni vitendo tu! Fundi kwa 30000-50000 kwa siku una uwezo wa kufanya chochote!
 
Zanzibar fursa kubwa ni ujenzi plus utalii.Hizi shughuli zimebeba mnyororo mkubwa sana wa kiuchumi.

Shughuli nyingi za ujenzi hufanyika shamba. Paje, Nungwi na Kiwengwa ndiyo shamba kubwa kwa Unguja na pia ndizo vitovu vikubwa vya utalii.

Watu wengi hutoka mjini na kuja kufanya shughuli zao shamba.Kawaida kibarua hulipwa tsh 15000-20000 kwa kutwa wakati fundi hulipwa tsh 30000-50000 kwa kutwa.

Nauli plus msosi huwa ndiyo kikwazo hasa kwa kibarua, fundi huwa hapati kikwazo sana.Minimum nauli ni tsh 5000 kwenda na kurudi na msosi ukijibana ni tsh 5000 kwa siku.

Hapo bado kodi ya chumba plus umeme coz maji sehemu nyingi ni bure na wana msemo wao 'maji ni ya Mungu'!Viburudisho kama bando ni muhimu coz hizi kazi zinategemea sana mawasiliano!

Kupitia mchanganuo huo hapo juu, unaweza kuona jinsi kujichanga kunavyokuwa na changamoto zake (siyo kama haiwezekeni)hasa kwa kibarua.

Ukibahatika kazi za mjini ambazo huwa chache minimum msosi plus nauli ni tsh 5000 ukijibana.Pia ukibahatika japo (ni ngumu kupata) site za kulala, pia husaidia kujibana, mara nyingi hizi site kama ni kubwa hulindwa na vikosi.

Unatakiwa ufanye nini?? (kibarua)

1) Chukua chumba shamba bei huanzia 50000-100000.

2) Punguza (piga ndefu) kula na kunywa maji plus juisi na energy. Utaweza?? Kazi zako zinategemea nguvu kwa asilimia 100%

3) Vumilia kwa muda mpaka ukiwa fundi coz ukiweka nia ni muda mfupi kwani faida utakayokuwa nayo fundi wako atakuelekeza kwa vitendo zaidi .

Kama kichwa ni chepesi ndani ya miezi mitatu mpaka sita utakuwa umeiva iwe kwenye tofali, mbao,chuma,tiles,umeme n.k, hakuna notisi ni vitendo tu! Fundi kwa 30000-50000 kwa siku una uwezo wa kufanya chochote!
Your explanation is very deep. You covered everything man.
Kama kichwa ni chepesi ndani ya miezi mitatu mpaka sita utakuwa umeiva iwe kwenye tofali, mbao,chuma,tiles,umeme n.k, hakuna notisi ni vitendo tu! Fundi kwa 30000-50000 kwa siku una uwezo wa kufanya chochote!
To be honest, ningependelea zaidi kuwa fundi chuma, tiles au mbao mkuu ila hasahasa fundi chuma. Kuhusu chakula na sehemu ya kulala vimo ndani uwezo wangu.

Una connection yoyote ya mafundi chuma au tiles mkuu?.
 
Elf 6 ukijibana sana yani hapo hata matunda huli

Ukiweka na dina mtu mmoja hapo kama buku 9 hiv. Yani hapo chakula na maji bas. Sisi tuko wawili geto usiku tunakula chakula cha kupika
Unga nusu na robo 1500
Samaki wa buku jero wawili 3000
Nyanya mbili 400
Kitunguu 200
Hoho 200
Karoti 200
Ndimu 200
jumla 5900

DONGOA GETO LA WATU WAWILI USIKU TU.
Mkuu there are times I go up to three months without eating any fruit, whether it's a banana, an orange, or anything else. Kuhusu msosi vijijini tulikuwa tunakula ugali na chumvi kwa hiyo hizo hoho, karoti, ndimu siwezi kuziweka kwenye bajeti kabisa.

Mpango mzima niambie chapati mbili na chai ni kiasi gani 😀😀😀.
 
Back
Top Bottom