Kijana usiingie kwenye ndoa kwa tumaini la kusaidiana na mkeo kifedha

Waambie hao, kazi kujifanya vidume eti usitegemee hela ya mwanamke. Sasa hela yake ina kazi gani? Kuna shemeji yangu alioa mwanamke mpambanaji, maisha yao yalivyokaa kwenye mstari akaugua kansa. Aliumwa miaka 3 mke ndio anaendesha familia na matibabu ya mume wake. Alikuja kufa lakini mpaka leo watoto anawalea vizuri sana. Sasa wewe oa mtu wa kukutegemea 100%, maisha yakigeuka ndio utajua hujui. Changua mwenza ambaye mtashirikiana kujenga familia, kuna leo na kesho. Sio maisha yanaenda mrama unaanza kusumbua watu. Hakuna atakayekujali isipokuwa mkeo na watu wa karibu. Saa nyingine hata ndugu wa damu wanaweza wasiwe na msaada wakati wa shida
 
Watu si wanafikiria maisha ni burudani tu. Maisha ni fumbo mkuu, kuoa ni mtihani unahitaji akili sana. Binafsi mi ntao mke wa mfano wa huyo shemeji yako. Hata nikifa watoto wangu wako sehemu salama coz mama yao ni strong.
 
Uzi mzur tatizo naona kama hakuna aliyeko kwenye ndoa hapa nyingi naona ni theory.

Mwanamke aliyekomaa martured, na mwanaume aliyekomaa wanaoishi Kwa heshima ya uwanauke na una ume wao tu. Nimeshuhudia ndoa mwanaume anahangaika na mke anahangaika. Sio heshima ukiwa umekaa ndani tu.

Hapo mtasumbuana.

Kile kipindi cha honeymoon kiki Isha ni mwendo wa kupambana. Uselfish wa mwanamke unakuja pale mume anapokuwa irresponsible.
 
Mkuu wewe unataka kua mkeo awe kama Bima ya afya yako hahaha.......kampuni za bima ni nyingi zingine zinatoa comprehensive insurance yoyote ikiwemo hata ya ada za watoto, tena huyu shemeji yako ana bahati wengine wanakimbia na kuolewa na wanaume wasio kua na shida kama hizo,
 
Waambie wachague wenza sio mifugo
 
Ndio.maana ya kuwa na mwenza. Mtu ambaye anakukimbia wakati wa shida hajawahi kukupenda
 
Kosa Sio la mke kosa hapo ni la mume kuoa mdangaji .
 
Bora huyo wa Masaki ujue kabisa ni wa gharama ila huyo wa bush siku akiujua mji utajua hujui.
Wanawake wengi mnapenda kudate na wanaume wenye pesa nyingi, nashangaa wanaume wenye pesa ni wachache sana, sasa sijui mnajimudu vipi, maana ni rahisi sana kukutana na mdada mwenye chura, na ni vigumu sana kukutana na mwanaume mwenye pesa nyingi Kelsea
 
Shost wambie
 
Najaribu kuunganisha ulichoandika na comment yangu nakosa kabisa mahusiano.
 
Hahaha mkuu 'never bite what you cant swallow' tafuta mke wa level yako, wakati hujampeleka mke kwenye sehemu nzuri za juu tafakali kwanza je nikikosa itakua je....... ukifikili kwamba atakusaidia yeye kwa pesa yake!!! Hiyo itakua 'own goal'
Kweli kabisa usemayo kaka ujakosea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…